Ubunge Tarime: Wagombea, Kampeni na Uchaguzi

Ubunge Tarime: Wagombea, Kampeni na Uchaguzi

Status
Not open for further replies.
Invisible,

Hakuna sababu yoyote ya kupiga watu. Kama Mtikila anaongea hayo maneno, si wachukue video na kupeleka mahakamani?

Vyama vya upinzani vikianza kupiga watu, CCM wataishia kupiga mara kumi. Watakaodhurika ni watu wa kawaida na ambao wanachotaka ni amani na maendeleo kwenye nchi yao. Kwa nchi maskini kama TZ ni rahisi mno kwa matajiri na wanasiasa kuwanunua vijana ili wapige wabaya wao. Je tunataka ujinga kama huo?


Mtanzania unajuaje kuwa ni "vyama vya upinzani" ndio vimeanza "kupiga watu" badala ya hawa watu wenyewe kubebeshwa lawama hizo.
 
Si tulishasikia Mbowe mwenyewe alikimbizwa kwa mawe hukohuko Tarime? Hawa hawajatumwa na CCM wala CHADEMA, labda kuna zaidi

Hapana mleta habari kutupasha kwa mbwembwe kuwa Mtikila yamemkuta hayo baada ya kuhutubia kuwa Mbowe na Chadema ndio waliomuua Wangwe. Hapo by implication hao watakuwa ni mashabiki wa Chadema,,,
 
Unajua kwa nchi za Kiafrika ukiwa chama cha upinzani, kitu kimoja ambacho ni muhimu ku avoid ni kufanya vurugu. CHADEMA inatakiwa wawe wanaongoza kupiga kelele za kuonewa na wala sio wao kuongoza kufanya vurugu.

Kwanini umechukulia kuwa ni chama kimefanya vurugu na siyo wahuni wachache?
 
Mtikila; aliyetoa maneno kuwahusisha watu na kifo bila uthibitisho; polisi waliosikiliza na kuombwa wamkamate wakashindwa; na wananchi waliomshambulia mtikila, wote ni wahalifu na washughulkikiwe ipasavyo.
lakini ukijumuisha na yaliyotokea Kiteto, utaanza kuona taratibu Tanzania is drifting towards siasa za shari
 
Kwanini umechukulia kuwa ni chama kimefanya vurugu na siyo wahuni wachache?

Mzee Mwanakijiji,

Hutakiwi kuwa genius kujua hilo katika mtililiko huu. Ni sawa na kule Kiteto wala hatukutakiwa kuwa genius kujua vijana wa CCM walipiga viongozi wa CHADEMA.
 
Haya ndiyo matatizo ya Mtikila, kwanini hakuacha Polisi wafanye kazi yao? I see, Mengi naye anamuunganisha kama mwanasiasa vile? Kaazi kwelikweli

teh teh teh
Na EPA nayo waachiwe akina wazee wa kuzuia rushwa,polisi na mahakam,ama unasema je?? kwi kwi kwi

Hapa nataka kusema hivi mtu yeyote anayeona kumechezwa ndivyo sivyo ana haki ya kusema lolote na yule anayeona hakutendewa haki anachukua mkondo wa sheria.

Sasa kama sheria yenyewe ndio ya mkononi si balaa hili.

Kumbe siku CHADEMA watakapo chukua nchi na MBOWE tukamwita majina mengi mfano FISADI,MHUNI,kumbe tutapigwa MAWE.kazi kweli kweli

NA yule kaka wa MAREHEMU kwenye ufunguzi wa kampeni mbona yeye hawajampa kipigo ama bado wanamuwinda??
 
Mzee Mwanakijiji,

Hutakiwi kuwa genius kujua hilo katika mtililiko huu. Ni sawa na kule Kiteto wala hatukutakiwa kuwa genius kujua vijana wa CCM walipiga viongozi wa CHADEMA.

inawezekana ni "vijana wa CCM" au "Vijana wa Chadema" lakini tunajuaje kuwa ni party sanctioned violence? Kwanini vijana hawa wasiwe wahalifu na wakashikwa kama wahalifu wengine. Hili la kumwajibisha mtu kwa vitendo vyake kwanini ni gumu?

Hivi unaamini kuwa Chadema ndio kiliamuru vijana hawa wampige mawe Mtikila?
 
...Kumbe siku CHADEMA watakapo chukua nchi na MBOWE tukamwita majina mengi mfano FISADI,MHUNI,kumbe tutapigwa MAWE.kazi kweli kweli...

mkipigwa mawe itakuwa ni kutokana na wahalifu; na wahalifu hawana sababu.
 
inawezekana ni "vijana wa CCM" au "Vijana wa Chadema" lakini tunajuaje kuwa ni party sanctioned violence? Kwanini vijana hawa wasiwe wahalifu na wakashikwa kama wahalifu wengine. Hili la kumwajibisha mtu kwa vitendo vyake kwanini ni gumu?

Hivi unaamini kuwa Chadema ndio kiliamuru vijana hawa wampige mawe Mtikila?

Mzee Mwanakijiji,

I hope unaelewa siasa. Kama unaelewa basi utajua siasa si mahakamani.

Leo FIFA wamewaadhibu Croatia kwa chants za Monkey dhidi ya mchezaji wa UK, kwanini wasiwaajibishe hao waliokuwa wanatoa hayo maneno ya kashfa badala ya kuiadhibu nchi? Chama cha siasa kinakuwa judged sio kwa matendo ya viongozi wake tu bali hata matendo ya washabiki wao.

I hope hizi vurugu hazitaishia kwa watu wasio na hatia.

Kwenye vurugu vyama vya mabavu kama CCM ndio huneemeka. Kama kiongozi wa chama cha siasa TZ haelewi hilo, hafai kuwa kwenye siasa.
 
Yule mchungaji matata anayeitwa Mtikila, hivi pundwe amepelekwa hospitali kulazwa na kushonwa nyuzi baada ya kupigwa mawe na wananchi wenye hasira. Mtikila alipata dhahama hiyo baada ya kuhutubia kuwa Mbowe na CHADEMA yake ndio waliomuua Chacha Wangwe.

.......ndiyohiyo

Uganga njaa mwingine ni hatari kweli kweli.

Hivi huyu fake pastor atamaliza kampeni salama huko Tarime?
 
Hapana mleta habari kutupasha kwa mbwembwe kuwa Mtikila yamemkuta hayo baada ya kuhutubia kuwa Mbowe na Chadema ndio waliomuua Wangwe. Hapo by implication hao watakuwa ni mashabiki wa Chadema,,,
Basi hizi ni siasa za kitoto I may say. Pamoja na kuwa Mtikila anaweza kutofautiana nao CHADEMA sioni sababu ya wao kufurahia yeye kupigwa mawe.

Shame on their bones (whomever celebrates Mtikila's stoning).

🙁
 
Basi hizi ni siasa za kitoto I may say. Pamoja na kuwa Mtikila anaweza kutofautiana nao CHADEMA sioni sababu ya wao kufurahia yeye kupigwa mawe.

Shame on their bones (whomever celebrates Mtikila's stoning).

🙁

I do! He should stop poking his nose in other people's businesses.
 
mkipigwa mawe itakuwa ni kutokana na wahalifu; na wahalifu hawana sababu.

Kumbe umekubali kua kamanda wa POLISI ni GENIUS kwa kupeleka polisi wengi sehemu hiyo.Sasa ulikua unalalamika nini kuhusu polisi kuongezeka??

Kamanda ongeza watu huko wakakamate WAHALIFU maana inaonekana FFU hawatoshi ,400 kwa wilaya nzima ni wachache sana.
 
Mzee Mwanakijiji,

I hope unaelewa siasa. Kama unaelewa basi utajua siasa si mahakamani.

Naielewa siasa vizuri sana, na siasa has to involve the courts. Siasa na mahakama zinakuwa ni kama mtu na mkwe wake, mmoja lazima amuheshimu mwenzie lakini lazima wahusiane kwani mmoja kaoa kutoka kwa mwingine.

I hope hizi vurugu hazitaishia kwa watu wasio na hatia.
Kwa kadiri ya kwamba vyombo vya usalama vinaona hili ni suala la kisiasa vitafiia huko. Hili ni suala la uhalifu.

Kwenye vurugu vyama vya mabavu kama CCM ndio huneemeka. Kama kiongozi wa chama cha siasa TZ haelewi hilo, hafai kuwa kwenye siasa.

Sifikiri kama hivyo ni kweli; kwenye vurugu vyama vya mabavu au vinavyofumbia macho vurugu na uvunjwaji wa sheria ndivyo huannguka. Chama chochote kinachocheza na damu za watu kitaungwa na watu hao hao kwani damu yao haitamwagika bure.
 
Hold on a minute; riots na vitu kama hivyo siyo suala la watu wa Tarime tu. Vinatokea sehemu nyingi duniani na ndio maana tunakuwa na Polisi.

a. Mtu anayevunja sheria ni mhalifu. Period hakuna udhuru wa Chama wala siasa katika hilo. Kama hawa watu wamempiga mawe hakuna cha kudai ni wana Chadema au wana CCM; hawa ni wahalifu na sheria ichukue mkondo wake.

b. Kama Mtikila alikuwa anaeneza habari hizo na kudai kwa uthabiti kuwa x,y,z wamemuua Wangwe na kueneza habari hizo ili kupanda chuki miongoni mwa wananchi au kuchezea hisia zao hilo linaweza kuwa kwenye uhuru wa maoni. Lakini tukijiuliza kama angesema Makamba, Kikwete na Msekwa wamemuua Mbatia mnafikiri kweli Polisi wangeacha asambaze habari hizo au angetiwa pingu kwa "uchochezi"?

Sasa kama habari hii kuwa "Wananchi walipandwa na hasira na kuwaomba polisi wamkamate kwa kufanya uchochezi lakini polisi wakamuacha aendelee kusema na kugawa makaratasi yenye maneno yake kuwa Mbowe, Mengi, Ndesa, Slaa, Mnyika na Zitto ndio waliopanga na kumuua Chacha Wangwe kwa kutuma vijana wamchome Kisu na baadaye kumpiga na nyundo. Hapo ndipo wananchi wakamgeukia na kumpiga mawe" Ni kweli, tunajiuliza sasa Polisi waliomwagwa huko ni wa nini?

c. NI kutokuwa makini kuwawajibisha CHadema au mtu mwingine yeyote kwa vitendo vya watu wenye akili na utashi wao. Kila mtu lazima ajifunze kubebeshwa mzigo wake yeye mwenyewe. Kwanini mzigo huu wa watu kupiga watu wengine mawe wabebeshwe Chadema au CCM for that matter? Kwanini wasibebeshwe wahalifu wenyewe na kuwajibishwa.

Kama aliyechochea watu hao hasira kwa maneno yake ni Mtikila kwanini Mtikila asiwajibishwe kwa kuchochea hasira za watu namna hiyo kwa maneno ya kichochezi?

Kama Polisi walikuwepo na waliona uchochezi unaodaiwa kufanywa na Mtikila kwanini wao wenyewe wasiwajibishwe kwa hilo. Kama watadai ni uhuru wa maoni, hebu mtu athubutu huko Tarime aanza kusambaza vipeperushi kuwa CCM, Kikwete na Makamba walipanga njama za kumuua Wangwe wakaajiri wauaji kutoka Afrika ya Kusini ambao walistage accidenti na mmoja wa watu waliosimimamia operesheni hiyo ni Mbunge maarufu wa Chama hicho akishirikiana na Kamishna mmoja wa Polisi. Na ya kuwa yule daktari mpya wa Mkoa wa Dodoma aliletwa pale kwa ajili ya kuficha ushahidi kwani ilikuwa ni siku chache tu tangu afike Dodoma ndiyo kifo cha Wangwe kilitokea. Mtu huyo aeneze uvumi huu kwa kugawa makatarasi kwenye kampeni na muone kama Msekwa na Jeshi zima la Polisi halitashuka Tarime.

Tusiwe na haraka ya kuhukumu watu wengine kwa makosa ya wengine. Kila mtu abebeshwe mzigo wake yeye mwenyewe.

On the other hand, kwanini watu hawa wa wafanye kitu kana kwamba wanamtetea Mbowe na Chadema huko Tarime?

if b) second para applies then he deserved it!
 
Lakini KITETO CCM ndio waliwapiga CHADEMA na sio wahuni wachache.Kazi kweli kweli

Kiteto viongozi wa Chadema walipigwa wakiwa mikononi mwa Polisi na siyo CCM; lakini viongozi wa CCM walikuwa na mazungumzo na Polisi hao na hivyo kuonekana kutoka baraka zao. Je kuna dalili yoyote kuwa viongozi wa Chadema walicoordinate mapigo haya ya mawe? Je kuna wakati wowote wananchi walitaka Polisi waingilie kati?
 
Kumbe umekubali kua kamanda wa POLISI ni GENIUS kwa kupeleka polisi wengi sehemu hiyo.Sasa ulikua unalalamika nini kuhusu polisi kuongezeka??

Kamanda ongeza watu huko wakakamate WAHALIFU maana inaonekana FFU hawatoshi ,400 kwa wilaya nzima ni wachache sana.


Unaniwekea maneno tena, ni wapi mimi nililalamika kuhusu Polisi kuongezeka Tarime?
 
Mzee Mwanakijiji,

Hutakiwi kuwa genius kujua hilo katika mtililiko huu. Ni sawa na kule Kiteto wala hatukutakiwa kuwa genius kujua vijana wa CCM walipiga viongozi wa CHADEMA.

Mtanzania mie si mwana CCM wala CHADEMA, lakini maneno aliyoongea Mtikila na kugawa yale makaratasi yamenistua sana. Nafkiri hata wanaCCM wengi yamewastua, au mwezetu? Yale yale ya Simba Vs Yanga?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom