Ubunge Tarime: Wagombea, Kampeni na Uchaguzi

Ubunge Tarime: Wagombea, Kampeni na Uchaguzi

Status
Not open for further replies.
Mwananchi

MWENYEKITI wa Chama cha Democratic Party (DP), Mchungaji Christopher Mtikila jana alidai kuwa waliomjeruhi juzi ni wanachama wa Chadema, lakini jana kada mmoja wa CCM na wanachama wanne wa DP walifikishwa mahakamani kwa kosa la kumshambulia mwanaiasa huyo matata.

Mtikila, ambaye anasifika kwa kutoa tuhuma nzito dhidi ya mtu yeyote bila ya woga, alitunguliwa kichwani na jiwe wakati akitoa tuhuma kuwa Chadema inahusika katika mauaji ya mbunge wa zamani wa Tarime, Chacha Wangwe, wakati akihutubia mkutano wa hadhara. Shambulizi hilo lilisababisha Mtikila kukimbizwa hospitalini ambako alishondwa nyuzi saba kichwani.

Akizungumza na waandishi wa habari hotelini jana Mtikila alisema baada ya kupatiwa matibabu na kwenda kituo cha polisi alikuta watu tofauti wamekamatwa kuhusika na shambulio hilo baada ya kubaini kuwa wengi wao ni wafuasi wa chama chake.

''Kama nilivyoeleza jana, hawa polisi wanataka kuvuruga kesi yangu kwa lengo la kuilinda Chadema," alisema Mtikila. "Walionipiga mawe si hao waliokamatwa. Ninawajua, mmoja sawa, lakini wengine sio. Wamekamata wanachama wangu na sasa wanataka kunifanya kuamini kuwa wanachama wangu wamehusika.''

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa jana na Kamanda wa Oparesheni Maalum, Venance Tossi watu waliohusika na kufanya shambulio hilo la mawe katika mkutano huo ni Musa Petro (4, Afidhi Stanislaus, Mwita Chacha, Mwita Kyaongo pamoja na Selema William.

Kuhusu madai ya Mtikila kuwa waliokamatwa si wale waliohusika na shambulio hilo, Kamanda Tossi alisema anachoamini yeye ni kuwa waliokamatwa ndio waliohusika na tukio hilo.

''Wamekamatwa jana katika eneo la tukio, na leo wamefikishwa mahakamani, sasa kama waliokamatwa sio wenyewe hilo ni suala lake Mtikila,'' alieleza na kisha akakata simu.

Habari zaidi zimeeleza kuwa Musa Petro, ambaye ni mmoja wa watu waliokamatwa, ametambuliaka kuwa ni balozi wa nyumba kumi wa CCM na kwamba wengine waliobaki ni wanachama wa DP inayoongozwa na mchungaji huyo wa kanisa la ufufuo.

Watu watano wanaosadikiwa kumshambulia Mchungaji Mtikila wamefikishwa mahakamani jana katika kesi namba TAR /IR/ 3419 /08.

Wakati watu watano wakifikishwa kortini kwa tuhuma za kumshambulia Mtikila, wananchi wameelezea kipigo hicho kuwa ni fundisho kwa wanasiasa ambao wameshindwa kunadi sera za vyama vyao na badala yake kuchochea mgawanyiko kwa kutumia kifo cha aliyekuwa mbunge wao Chacha Wangwe.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti jana, baadhi ya wananchi waliozungumza na Mwananchi walisema kuwa sababu iliyomfanya Mtikila apigwe na jiwe na kujeruhiwa kichwani ni sawa na ile iliyomfanya Dk. Sengondo Mvungi wa chama cha NCCR-Mageuzi kushambuliwa.

Mmoja wa wakazi wa mji wa Tarime, Ambrosi Wantaigwa alisema kuzungumza suala la kifo katika ajenda ya uchaguzi kumekuwa kukiwaumiza wananchi wa Tarime na hivyo kuwataka wanasiasa kuepuka jambo hilo.

''Hili ni jambo linaloumiza sana kama serikali ilishatangaza awali kuwa ni ajali, familia haikuridhika nayo ikaitisha watalaam wake na kufanya uchunguzi na kudhihirika kuwa ni ajali, unawezaje kusimama jukwaani kututangazia mambo kama hayo. Kama unadhani unao ushahidi, jukwaa si mahala pake, peleka polisi,'' alieleza.

Naye Mchungaji Nicodemas alisema kuwa Mtikila akiwa mchungaji mwenzake alitenda kosa ambalo kimantiki linapingana na maandiko matakatifu, kwa vile kwa kauli zake zinapanda mbegu za chuki na uchochezi.


''Kabla ya kutamka hayo alipaswa kujiuliza kwanza mara mbili, kwa sababu wananchi wa Tarime bado wana uchungu wa kifo cha mbunge wao ambaye walimpenda sana.Ukishindwa kutofautisha jambo, kama biblia inavyoeleza kuwa kila jambo kwa wakati wake, basi hayo ndiyo matokeo yake,'' alieleza mchungaji huyo.

My Take:

Usiharakishe kuhukumu na kubebesha watu lawama.
 
Mmoja wa wakazi wa mji wa Tarime, Ambrosi Wantaigwa alisema kuzungumza suala la kifo katika ajenda ya uchaguzi kumekuwa kukiwaumiza wananchi wa Tarime na hivyo kuwataka wanasiasa kuepuka jambo hilo.

Call me anything you want, lakini ninawa-support wananchi waliompa kipigo Mtikila, tena kwa 100% Yes I love it, a clear message kwa serikali na wanasiasa wote bongo, kuwa play with wananchi at your own risk,

Wananchi wa Tarime, wamepoteza mbunge wao katika mazingara ya kusadikika, serikali inawayeyusha na hadithi za chekechea, Mtikila ni agent wa mafisadi that is the bottomline, leo anakuja kuwachezea wananchi na siasa za Bulicheka? Who is Mtikila anyways? Hii political platform anapewa na nani? Nani anayemlipia kwenda huko Tarime?

Enough is enough! Majuzi tumesoma hapa kuwa yule Mzee, alifungwa miaka mitano kwa kushikwa na hela za rushwa alizopewa na Hosea, great story then how did Nyeri get out of prison wakati alishikwa na bunduki akiwa amefanya ujambazi tena wa wazi na sio mara moja? Kina Lowassa na wenzake mbona wanapeta tu kama kawa, eti utawala wa sheria na haki? Where? uko wapi huo utawala? Utawala wa haki ulikuwa wapi kwa kesi ya Ditopile?

The time comes, kwamba kama watawala wetu hawana a built in political system ya kutathmini kinachoendelea katika maisha ya kawaida ya wananchi wao, this should be their wake up call, kwamba wananchi wamechoka na ujinga, huyu si ndiye Mtikila aliyekuwa akiwahamasa wananchi kuwapiga magabacholi? Sasa mkuki kwa nguruwe tu, kama unapenda haki, then ungeuliza how come Mtikila akitukana viongozi wa CCM anashikwa na kuwekwa ndani, lakini akiwatukana wa Chadema hashikiwi wala kuwekwa popote? So much kwa haki na sheria!

Ninarudia tena kuwa wananchi wa Tarime, hapo tupo ukurasa mmoja, hawa wanasiasa ushwara ni kuwapa vipigo, na akitokea another goi goi politician huko Tarime piga tena kisawa sawa, wananchi walianza na kuwazomea sasa wamehamia kwenye kipigo, saaafi sana kama watawala hawasikii hizi mesaage, then wananchi wahamie kwenye another tactic lakini the message ni very clear hapa enough is enough!
 
Mida si mirefu kampeni za CCM kijiji cha nyamongo uliko mgodi wa barrick zimezomewa na vijana wa kazi...wenye uchungu na ardhi yao....wanasema CCM ndio imemuuzia barrick kwa miaka 100 mgodi huo...better not to wear any thing that show barrick symbol on your shirt...

U never know what will happen when crazy mgombea like mtikila say barrick are the one who pay for the death of that chacha wangwe...(dont qoute me am jst thinking..)
So its worse most of wagombea are using jazba ya watu wa tarime kwa faida zao za kisiasa...ukiwapandikiza kitu they react hapo hapo....no time to think we will think laiter..

Nafikiri ikifika tarehe 2 hivi watu waaze kuondoka eneo hili hasa wale ambao walikatia vitambulisho maeneo ya mbali na nyamongo,tarime,kimakorere etc nikiwa na maana ya musoma,buda,na kwingine...if u dont belong here and ur are not living in the camp jst gate annual leave and go home...anything can happen.
 
Nakulilia Tanzania. Wachangiaji wote nawaomba baada ya kuandika maoni yako bonyeza kwanza "PREVIEW POST" usome uliyoyaandika na kuyatathmini kisha ufanye masahihisho kama kuna ulazima halafu ndio ubonyeze "SUBMIT REPLY". Kwa nini nasema hivi ?

Kama binadamu tuna tabia ya kukurupuka hasa tunapokabiliana na yale ambaye ama hatukubaliani nayo au hayatufurahishi. Kwenye blog kama hii unaweza ukajivua nguo bila kujua kwa kukimbilia kuandika yale ambayo kama tu ungetulia kidogo, ungeweza kuyajengea hoja tofauti. Wakati mwingine afadhali hata usubiri kidogo kwa kujiuliza - hivi kweli hii habari inawezekana katika mazingira haya. Hisia tu inatosha kukusukuma kujiumbua na watu wakaamini ndivyo ulivyo na wengine wakakudharau hata wasichukulie maanani unalojaribu kutetea ama kupinga.

Toka hii post imetoka nimejiuliza mambo mengi tu. DP haijaweza kushinda uchaguzi wowote kwa ngazi yoyote toka isajiliwe. Kitu gani kimemtuma Rev. Mtikila Tarime, mtu ambaye hata kufanikisha mambo ya binafsi anakopa, je, fedha za kwenda Tarime kapata wapi. Ana mvuto gani kwa Chadema kwa mfano mpaka wanachadema waache kuhudhuria mkutano wa Chadema waende kumsikiliza na kumponda mawe.

Upinzani kwa ujumla unachafuliwa kila kukicha na watu aina ya Rev. Mtikila. Toka mfumo wa vyama vingi uanze, watu aina ya Mtikila, wamefanya uma wa watanzania usiwe na imani na upinzani. Imefikia kwamba hata anapotokeza mtu makini na kuanza kupambana na status quo, wengi wetu tunambeza na tunashindwa kutambua mchango wake muhimu kwa vile tu tumembatiza jina mpinzani.

Sasa hivi tunaendekeza ujinga mwingine kwamba upinzani wa kweli utatokana tu ndani ya CCM pamoja na kwamba kila siku CCM inazoa uozo hadi uozo. Mtu yeyote anayeishi kwenye huu uozo tuko tayari kumpokea kama shujaa kama atatoswa bila kujali uchafu anaotoka nao huko na tutampakata pamoja na uvundo wote wa miaka nenda rudi.

Watanzania, watu mahiri tunao lakini tumeamua kutowapa ushirikiano kwa sababu wengi tumevaa miwani mieusi na tunachoweza kuona ni ubwabwa, kanga, vijisenti na kila aina ya makombo tunayotupiwa na MAISADI wa CCM.
Amkeni wananchi, achaneni na malimbukeni yanajitokeza humu kutetea maovu ya watawala wetu. Kama unaweza kukubali kudanganywa kwa miaka 40 basi kubali wewe zezeta au ndio sote tu mazezeta?

Kwa mwendo wa sasa ni kwamba kila baada ya miaka kumi tunapata kiongozi ovyo kuliko aliyemtangulia. Kwa uchungu nduzu zangu tufikirie huyo atakayemfuata JK kwa mtindo huu, si ndio itakuwa balaa maanake sasa hivi tayari anapikwa. Ukipanda uozo utavuna uozo.
 
Nashindwa kuelewa ni nini kinafanyika maana kama sikosei nadhani mtikila hana mgombea ktk hiki kinyang'anyiro sasa haya maneno anayoyaongea yanamsaidia nini au yanajenga nini ktk chama cha DP,hakika hizi njaa zitatuua
 
Kama hana mgombea na alienda tu kuchafua huko Tarime basi waliombonda walikosea:

WALITAKIWA KUMBONDA MPAKA AFE!
 
Kama hana mgombea na alienda tu kuchafua huko Tarime basi waliombonda walikosea:

WALITAKIWA KUMBONDA MPAKA AFE!

Wachangiaji wote nawaomba baada ya kuandika maoni yako bonyeza kwanza "PREVIEW POST" usome uliyoyaandika na kuyatathmini kisha ufanye masahihisho kama kuna ulazima halafu ndio ubonyeze "SUBMIT REPLY".

DP wana mgombea wake na ni Mchungaji vilevile, Mtikila yupo huko kumnadi mgombea wa chama chake....
 
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif][/FONT]
Vurugu Tarime, risasi zarushwa
Similar Stories
close.gif
•Mdogo wa Wangwe aihama CHADEMA 09.09.2008 [More] •Osama azua tafrani msibani 01.08.2008 [More] •Mauaji Tarime: Diwani atiwa mbaroni 02.09.2008 [More]
Na Mwandishi wetu, Tarime

TARIME kunawaka moto. Baada ya Mchungaji Christopher Mtikila kujeruhiwa kwa mawe juzi katika mkutano wa hadhara Tarime Mjini, jana jioni watu wanaodhaniwa ni wa vyama vya upinzani walivamia kwenye kituo cha kuuza mafuta kinachomilikiwa na mgombea wa CCM, wakarusha risasi na kupora pesa.

Wavamizi hao ambao inaanimika walifanya hivyo kwa sababu za kisiasa, walivamia kwa bunduki katika kituo hicho kinachomilikiwa na Peter Zacharia, ambaye anagonbea udiwani kwa tiketi ya CCM jana mida ya saa moja jioni katika eneo la Mugumu.

Mkuu wa Wilaya ya Tarime, Edward Olelenga amethibitisha kutokea kwa uvamizi huo alipozungumza na mwandishi wa habari hizi leo asubuhi na kusema kwamba ameanzisha operesheni kali kuwasaka wahalifu hao popote pale watakapokuwa wamejichimbia.

Mkuu huyo wa wilaya amesema kwamba zaidi ya shilingi milioni moja inasadikiwa zimeporwa katika tukio hilo la kutisha ambapo mwanamke mmoja aliyekuwa akiuza mafuta kwenye kituo hicho alitishwa kwa kupigwa na kitako cha bunduki kichwani kabla hajaporwa pesa hiyo.

Watu walioshuudia tukio hilo wamesema kwamba hali ilikuwa inatisha hasa baada ya askari wa Kituo Kikuu cha Mugumu kuanza kurusha risasi wakisaidiana na wale wanaolinda Benki ya NMB Mugumu katika kujaribu kuwadhibiti watu hao.

Mkuu huyo wa wilaya amesema polisi wanamsaka mtu mmoja aitwaye Chonchori ambaye wavamizi hao walimtaja wakati wakimlazimisha mwanamke huyo kwenye kituo cha mafuta awape pesa ambazo bado thamani yake halisi haijafahamika.

Kaimu Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mara, Steve Buyuya amethibitsha kutokea kwa uvamizi huo na kusema kwamba anasubiri taarifa kamili kutoka kwa Mkuu wa Polisi wa Wilaya ili hatua zaidi zichukuliwe wakati uchunguzi ukiendelea.

Kumekuwepo na upinzani mkali wa kisiasa kati ya mgombea udiwani huyo na wenzake wa vyama vya upinzani ambapo wamekuwa wakidai kwamba ana kiburi cha pesa na mambo mengine mbalimbali ikiwemo kutowajali wapiga kura wa Tarime Mjini.

Katika kuonyesha kwamba Tarime hapatoshi, mkutano wa hadhara uliokuwa ukihutubiwa na viongozi wa CCM kumnadi mgombea wao jana uliingia mushkeli baada ya watu kuuvamia kwa mawe na kupelekea watu wanne kutiwa mbaroni na polisi.

Mkutano huo ulikuwa unafanyika katika eneo la Nyamongo karibu na Mgodi wa North Mara ambapo baada ya mgombea ubunge wa CCM, Christopher Kangowe kuanza kuhutubia, watu wasiojulikana walianza kurusha mawe wakidai kwamba serikali ya CCM iliwapa mgodi Wazungu na kuwaacha wenyeji wakiwa maskini.

Kutokana na hali hiyo ya machafuko, mkutano huo wa hadhara haukufanyika kama ilivyopangwa ilibidi ufanyike kwa wasiwasi na kumalizika mapema kabla ya muda wake. Ulihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa CCM akiwemo Mbunge Ole Sendeka na Tambwe Hizza.

Wakati huohuo, Katibu Mkuu wa CCM, Yusuf Makamba leo anakwenda kumpa pole Mchungaji Mtikila ambaye anaugulia maumivu katika hoteli ya Skylodge alipofikia, baada ya kupigwa mawe juzi na watu wanaosadikiwa kwamba ni mashabiki wa vyama vya siasa.

Mtikila alibamizwa na jiwe kisogoni na kuachia kipaza sauti, kabla ya kudondoka jukwaami alipokuwa akihutubia wananchi ambako ilidaiwa wananchi hao walichukizwa na kauli yake ya kwamba Chadema ndio walimuua Chacha Wangwe na kwamba Rais Kikwete alimkumbatia Ditopile ambaye alikuwa muuaji.

Source: DarLeo-Gazeti lako la kila siku jioni

My take:
Ni uungwana huo bwana Yusufu Makamba, hata kama lengo likiwa ni ku-score more points kwenye kampeni hizi.
 
Vurugu Tarime, risasi zarushwa
Similar Stories
close.gif
•Mdogo wa Wangwe aihama CHADEMA 09.09.2008 [More] •Osama azua tafrani msibani 01.08.2008 [More] •Mauaji Tarime: Diwani atiwa mbaroni 02.09.2008 [More]
Na Mwandishi wetu, Tarime

TARIME kunawaka moto. Baada ya Mchungaji Christopher Mtikila kujeruhiwa kwa mawe juzi katika mkutano wa hadhara Tarime Mjini, jana jioni watu wanaodhaniwa ni wa vyama vya upinzani walivamia kwenye kituo cha kuuza mafuta kinachomilikiwa na mgombea wa CCM, wakarusha risasi na kupora pesa.

Wavamizi hao ambao inaanimika walifanya hivyo kwa sababu za kisiasa, walivamia kwa bunduki katika kituo hicho kinachomilikiwa na Peter Zacharia, ambaye anagonbea udiwani kwa tiketi ya CCM jana mida ya saa moja jioni katika eneo la Mugumu.

Mkuu wa Wilaya ya Tarime, Edward Olelenga amethibitisha kutokea kwa uvamizi huo alipozungumza na mwandishi wa habari hizi leo asubuhi na kusema kwamba ameanzisha operesheni kali kuwasaka wahalifu hao popote pale watakapokuwa wamejichimbia.

Mkuu huyo wa wilaya amesema kwamba zaidi ya shilingi milioni moja inasadikiwa zimeporwa katika tukio hilo la kutisha ambapo mwanamke mmoja aliyekuwa akiuza mafuta kwenye kituo hicho alitishwa kwa kupigwa na kitako cha bunduki kichwani kabla hajaporwa pesa hiyo.

Watu walioshuudia tukio hilo wamesema kwamba hali ilikuwa inatisha hasa baada ya askari wa Kituo Kikuu cha Mugumu kuanza kurusha risasi wakisaidiana na wale wanaolinda Benki ya NMB Mugumu katika kujaribu kuwadhibiti watu hao.

Mkuu huyo wa wilaya amesema polisi wanamsaka mtu mmoja aitwaye Chonchori ambaye wavamizi hao walimtaja wakati wakimlazimisha mwanamke huyo kwenye kituo cha mafuta awape pesa ambazo bado thamani yake halisi haijafahamika.

Kaimu Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mara, Steve Buyuya amethibitsha kutokea kwa uvamizi huo na kusema kwamba anasubiri taarifa kamili kutoka kwa Mkuu wa Polisi wa Wilaya ili hatua zaidi zichukuliwe wakati uchunguzi ukiendelea.

Kumekuwepo na upinzani mkali wa kisiasa kati ya mgombea udiwani huyo na wenzake wa vyama vya upinzani ambapo wamekuwa wakidai kwamba ana kiburi cha pesa na mambo mengine mbalimbali ikiwemo kutowajali wapiga kura wa Tarime Mjini.

Katika kuonyesha kwamba Tarime hapatoshi, mkutano wa hadhara uliokuwa ukihutubiwa na viongozi wa CCM kumnadi mgombea wao jana uliingia mushkeli baada ya watu kuuvamia kwa mawe na kupelekea watu wanne kutiwa mbaroni na polisi.

Mkutano huo ulikuwa unafanyika katika eneo la Nyamongo karibu na Mgodi wa North Mara ambapo baada ya mgombea ubunge wa CCM, Christopher Kangowe kuanza kuhutubia, watu wasiojulikana walianza kurusha mawe wakidai kwamba serikali ya CCM iliwapa mgodi Wazungu na kuwaacha wenyeji wakiwa maskini.

Kutokana na hali hiyo ya machafuko, mkutano huo wa hadhara haukufanyika kama ilivyopangwa ilibidi ufanyike kwa wasiwasi na kumalizika mapema kabla ya muda wake. Ulihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa CCM akiwemo Mbunge Ole Sendeka na Tambwe Hizza.

Wakati huohuo, Katibu Mkuu wa CCM, Yusuf Makamba leo anakwenda kumpa pole Mchungaji Mtikila ambaye anaugulia maumivu katika hoteli ya Skylodge alipofikia, baada ya kupigwa mawe juzi na watu wanaosadikiwa kwamba ni mashabiki wa vyama vya siasa.

Mtikila alibamizwa na jiwe kisogoni na kuachia kipaza sauti, kabla ya kudondoka jukwaami alipokuwa akihutubia wananchi ambako ilidaiwa wananchi hao walichukizwa na kauli yake ya kwamba Chadema ndio walimuua Chacha Wangwe na kwamba Rais Kikwete alimkumbatia Ditopile ambaye alikuwa muuaji.

Source: DarLeo-Gazeti lako la kila siku jioni

My take:
Ni uungwana huo bwana Yusufu Makamba, hata kama lengo likiwa ni ku-score more points kwenye kampeni hizi.

Kwanini awe muungwana kwa mwanasiasa wa DP na kuwa na kiburi pamoja madharau na unyanyasaji kwa wananchi?

Unajuwa tafsiri ya siasa kwa wazee wetu hawa viongozi ni tofauti na dunia yetu ya sasa iliko na inakoelekea.

Ni kama matatizo yake na Nape huko ccm na akadai kuwa amefungiwa mbinguni na duniani...Sasa hiyo ni kauli dhidi ya kijana na kada maarufu wa chama chake...Vipi kuhusu wananchi wa kawaida?

We seriously need change..Na kama kina Makamba hawaoni dalili hizo na kuamua kushiriki kikamilifu kwenye mabadiliko haya..Basi asishangazwe pale historia itakapomgeuka.
 
Ama kweli tunao waandishi. Hivi ujambazi unaofanyika wilayani Serengeti unahusishwaje na uchaguzi Tarime ? Vyombo vya habari vinapaswa kuwa makini sana na hawa wanaojiita waandishi wa habari. Wakati wa matukio yaliyofuatia taarifa za Mbowe kutimuliwa kwa marungu huko Tarime, nilishangaa mwalimu mmoja wa shule ya msingi ambaye hajapata mafunzo yoyote ya uandishi alipotajwa kama katibu wa Mara press club. Ujambazi kwenye vituo vya mafuta haujaanza leo au jana mkoani Mara. Hivi wahariri wetu wanafanya kazi gani?
 
Ama kweli tunao waandishi. Hivi ujambazi unaofanyika wilayani Serengeti unahusishwaje na uchaguzi Tarime ? Vyombo vya habari vinapaswa kuwa makini sana na hawa wanaojiita waandishi wa habari. Wakati wa matukio yaliyofuatia taarifa za Mbowe kutimuliwa kwa marungu huko Tarime, nilishangaa mwalimu mmoja wa shule ya msingi ambaye hajapata mafunzo yoyote ya uandishi alipotajwa kama katibu wa Mara press club. Ujambazi kwenye vituo vya mafuta haujaanza leo au jana mkoani Mara. Hivi wahariri wetu wanafanya kazi gani?

Gagnija sifagilii uandishi wa wengi wa waandishi wetu lakini tukio hili si la kulidharau hata kiodogo.
Kumbuka kuwa FFU wako wengi huko na mapolisi wa kumwagwa...Hivyo kusema tu ni tukio la ujambazi na huku jeshi lote hilo la ulinzi na usalama likiwa limetanda na pia kuhudumiwa na mwenye kituo hicho kilichovamiwa(Zakaria)bila kujiuliza maswali muhimu then utakuwa mvivu wa kufikiri.
Sasa kama hali inakuwa hivyo wakati kuna ulinzi mkubwa...Then hali inakuwa vipi wakati kuna polisi na ulinzi wa kawaida?
Wao wamezoea kukaa huko Dar na Dodoma na kubwata mi amri tu...Sasa wanaenda huko mtaani kuomba kura lakini wanaenda na vitisho kama vile wao wamezaliwa kuwa watwana na watawala...Yani wanaendeleza DYNASTY.
Na usije ukashangazwa machafuko makubwa yakatokea huko kama ccm wataendeleza siasa kama hizi wanazozifanya...Wananchi wanataka sera na si vitisho na unyanyasaji...Kama wanaamini mbunge wao kauwawa..then muwe makini sana.
 
Ama kweli tunao waandishi. Hivi ujambazi unaofanyika wilayani Serengeti unahusishwaje na uchaguzi Tarime ? Vyombo vya habari vinapaswa kuwa makini sana na hawa wanaojiita waandishi wa habari. Wakati wa matukio yaliyofuatia taarifa za Mbowe kutimuliwa kwa marungu huko Tarime, nilishangaa mwalimu mmoja wa shule ya msingi ambaye hajapata mafunzo yoyote ya uandishi alipotajwa kama katibu wa Mara press club. Ujambazi kwenye vituo vya mafuta haujaanza leo au jana mkoani Mara. Hivi wahariri wetu wanafanya kazi gani?

Kweli kabisa Gagnija,

Yaani tukio linatokea Serengeti (mugumu) na waandishi wa habari wanasema kuwa limetokea Tarime na huku wakisema kuwa mkuu wa wilaya ya Tarime amethibitisha kutokea kwa tukio hilo.

Hata kama tukikubali kinafiki kuwa mugumu iko Tarime, wizi wa kwenye kituo cha mafuta hauwezi kuhusishwa na siasa za Tarime hata kidogo. Ujambazi ni sehemu ya maisha siku hizi kwa vile polisi wako bize kufanya kampeni za siasa badala ya kulinda raia na mali zao.

Haya niliyasema sana wakati wa msiba wa Wangwe na sasa ukweli zaidi unazidi kujitokeza.

Mhariri wa Dar Leo asubirie simu yangu muda si mfupi kwa kuchapisha habari ya uongo na upuuzi kama hii.
 
Lakini kwanini akina SLaa na wengineo wanaotajwa na Mtikila kuwa ndio waliopanga mauaji ya Wangwe hawachukui hatua za kisheria?Na hapa by "hatua za kisheria" simaanishi kwenda kushtaki polisi bali kumpeleka mahakamani moja kwa moja?Slaa na wenzake walipotoa list of shame,watajwa walitishia kwenda mahakamani na hawakwenda,na hivyo kututhibitishia kwamba tuhuma zote dhidi yao zilikuwa za kweli.Wakati mwingine kukaa kimya unapotuhumiwa kunaweza kumpa jeuri mtoa tuhuma kuendelea kumwaga tuhuma zaidi.Unadhani leo Mtikila angediriki kuongea hayo iwapo akina Slaa wangechukua hatu mara baada ya ile press conference ya kuwatuhumu na mauaji ya Wangwe?Kipigo alichopata kinaweza kuwa solution ya muda mfupi tu lakini ukweli ni kwamba huyu mtu alipaswa apandishwe kizimbani kuthibitisha tuhuma zake.

Ndugu yangu mahakama inachukua mda mrefu sana,ni kupoteza mda.Huyu Mtikila anatumiwa na mafisadi ambao tuhuma zingine za wazi kabisa kama Richmond zimeshatolewa maamuzi na kamati ya uchunguzi ya bunge,lakini mpaka sasa hakuna kinachoendelea.Sasa Dr Slaa na ufahamu wake wa hali ya juu aende mahakamani kumshitaki beneficially wa ufisadi huoni ni kupoteza mda na kumpa credibilty ya bure mwanasiasa mbagaizaji?
Yeye anafahamu taratibu za mashtaka ya jinai kwa nini asipeleke majina hayo ya akina Mbowe kwa IGP badala yake akaongelee kwenye jukwaa la siasa?Kuhusu mwembeyanga,hali ni tofauti Dr Slaa alianzia bungeni,lakini mafisadi wakatumia uwezo wa PM Lowassa kublock hoja.Baada ya hapo Dr Slaa akaamua kuwapelekea wananchi wapime wenyewe maamuzi ya kupiga kura baada ya vishawishi yanavyozalisha ufisadi na hali ngumu ya maisha.
 
Mushi,
You're missing something. Ujambazi umefanyika Mugumu wilayani Serengeti, Polisi wamemwagwa Tarime kuteka jimbo. Sitashangaa nikisikia kuwa Mugumu sasa hivi haina askari wa kutosha kwani wengi wamepelekwa Tarime.
 
Ben,

Hapo ndipo ninapowashangaa CHADEMA, badala ya kukubali ukweli kwanini mwenyekiti wenu hajaenda Tarime mnaanza kuja na hadithi za Abunuwas kibao.

Sawa endeleeni kujidanganya, ila tu wengine hamuwezi kutudanganya kama mnavyojidanganya kwenye lile la wabunge wa kuteuliwa.
Mkuu Mtanzania
Inaelekea unajua alichopanga Makamba,mbona unamng'ang'ania sana Mh.Mbowe aende huko?Maana sijaona mantiki ya kumpeleka Mwenyekiti wa chama wakati kuna timu kabambe inayoendesha kampeni kwa ufanisi mkubwa.Kwa taarifa yako njama chafu za Makamba zinajulikana,yule anaweza kufanya uchafu wowote bila kujali athari kwa taifa lake.CCM kama chama kimepuuza kutumia political strategist kimeamua kutmia propoganda cheap za akina Mkamba type.CHADEMA kina political strategist wanafanya mambo kwa mpangilio maalum bila kukurupuka.
 
Ama kweli tunao waandishi. Hivi ujambazi unaofanyika wilayani Serengeti unahusishwaje na uchaguzi Tarime ? Vyombo vya habari vinapaswa kuwa makini sana na hawa wanaojiita waandishi wa habari. Wakati wa matukio yaliyofuatia taarifa za Mbowe kutimuliwa kwa marungu huko Tarime, nilishangaa mwalimu mmoja wa shule ya msingi ambaye hajapata mafunzo yoyote ya uandishi alipotajwa kama katibu wa Mara press club. Ujambazi kwenye vituo vya mafuta haujaanza leo au jana mkoani Mara. Hivi wahariri wetu wanafanya kazi gani?

Ndio maana wanaambiwa wakasome.....lakini wenyewe wanaishia kuwa wakali kwa kuonekana wanadharauliwa. Lakini tatizo jingine kubwa ni maslahi binafsi kwanza ya umma baadaye, siku hizi ni watanzania wachache kweli wanaoweza kukataa kupokea chochote(pesa) ili atimize lolote kwa ajili ya manufaa ya mtoaji pesa, sio kwenye siasa, hospitalini, mahakamani, TRA, manispaa na kadhalika.
 
Yule mchungaji matata anayeitwa Mtikila, hivi pundwe amepelekwa hospitali kulazwa na kushonwa nyuzi baada ya kupigwa mawe na wananchi wenye hasira. Mtikila alipata dhahama hiyo baada ya kuhutubia kuwa Mbowe na CHADEMA yake ndio waliomuua Chacha Wangwe.

.......ndiyohiyo



Mtikila kupigwa mawe kajitakia mwenyewe,kwani mtu huyo kazi yake kila anapoongea ni kuchochea tu vurugu sijawahi kumsikia akielezea vizuri chama chake kina mikakati ipi endapo kitapewa uongozi wa kisiasa,yeye ni mkosoaji tu wa mambo na mtoa shutuma.He spends a lot of his time in courts as if he is a freedom fighter,let him now face the music.
 
Katika bandiko hili ndugu Mtanzania alisimama sana kuwalaumum Chadema bila ya ushahidi wa maneno yake .Leo Mktikila polisi wanasema kwapigwa na wafuasi wake na wana CCM na Chadema hajakamatwa wala kutajwa hata mmoja .Mtanzania unasemaje kuhusu hili ?
 
Katika bandiko hili ndugu Mtanzania alisimama sana kuwalaumum Chadema bila ya ushahidi wa maneno yake .Leo Mktikila polisi wanasema kwapigwa na wafuasi wake na wana CCM na Chadema hajakamatwa wala kutajwa hata mmoja .Mtanzania unasemaje kuhusu hili ?


Yawezekana nayo imepikwa,kama ya mbowe ilipikwa ktk vyombo vya habari vingi tena kwa masaa kadhaa tu hii itashindikana nini kupikwa?

Harafu nahoja nyingine Kama kweli polisi wametumwa kukipa ushindi ccm kwanini hawakutumia hii advantage ya kupigwa mtikila kukamata wafuasi wa chadema mvua?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom