Ubunge Tarime: Wagombea, Kampeni na Uchaguzi

Status
Not open for further replies.

Duuuu???? kaaazi kweli kweli,
Mkuu Gembe kama hiyo ndiyo your take kutoka katika habari hiyo kweli naamini bado tuna safari ndefu sana kujikwamua!

Anyway, Kudos Chadema na hongera Mbowe kwa ushujaa ulio uonyesha kukanyaga Tarime na kukatilia mbali tantaralila zote kwamba huwezi kanayaga tarime, mara ukifika utapigwa, mbona kinyume chake umepokelewa kama shujaa?? Mungu awatie shime wote wapambanaji! inshalah tutashinda.
 
Sasa sijui watu kama akina Mtanzania waliotaka kupotosha tangu mwanzo sasa watasemaje?
 
katika hali ya kushangaza yusuf makamba aliingia mitini wakati mabalozi wanipotembelea Tarime kujionea kampeni za uchaguzi zinavyondeshwa...
swali: je tatizo ni lile lile la kutokujua kingereza au kulikuwa na nini mpaka awakimbie? nisaidieni...
 
Ochu,
Tatizo haliwezi kuwa kiingereza. Balozi alisema amelazimika kwenda Tarime baada ya kila siku kuwa anasoma habari zinazoonyesha kuwa mambo huko yanakwenda sivyo. Makamba ni mhusika mkuu wa hayo yanayotokea huko hivyo alichokimbia ni maswali ya balozi huyo. Usisahau, viongozi wetu ni waoga sana wanapokuwa na hawa wakuu toka nchi tunazoita wahisani.
 
Tatizo sio kiingereza, kwani mabalozi wengine suala la kiswahili kwao sio ishu. Makamba kuwakimbia jamaa hawa ni ile ya hali ya kuona niitawaeleza nini 'wafadhiri' hawa wanielewa hasa kwa kuwa hawa hawaitegemei Habari Leo kutoa habari. makamba na chama chake wamekuwa ndo watu muhimu sana katika kuleta fujo hapa tarime. Mbaya zaidi hata wasaidizi wakuu wa rais, mawaziri wamekuwa ni mashabiki na wacochezi wakubwa wa vurugu hizi.

UELEWA WA MTANZANIA HAUWEZI KUPIMWA KWA KUJUA LUGHA YA KIGENI
 
katika hali ya kushangaza yusuf makamba aliingia mitini wakati mabalozi wanipotembelea Tarime kujionea kampeni za uchaguzi zinavyondeshwa...
swali: je tatizo ni lile lile la kutokujua kingereza au kulikuwa na nini mpaka awakimbie? nisaidieni...

Wakati mwingine Polisi kumtambua mhalifu haisumbui, mhalifu akishamuona polisi naye akijui kishafanya matukio mengi ya uhalifu, mhalifu huyu akimuona polisi lazima akimbie. Hivyo usishangae alijihisi ni mhalifu mbele yao.
 


Mkuu nadhani ni vyote, Kiingereza na kutojua atajibu nini.....viongozi wetu bwana! nakumbuka Dr Juma Ngasongwa kuna siku alikutana na mabalozi wa EU wakati yeye ni waziri wa biashara na viwanda, aliulizwa nini kifanyike kuongeza uzalishaji...alijibu nadhani tukipata vijenereta vitasidia sana kutatua shida ya umeme vijijini...I just turned the TV to channel 5 kuendelea na zecomedy enzi hizo. Makamba ni shida zaidi maana hana ufahamu na lugha ni tatizo, sasa angeongea nini jamani?

Ushi
 
katika hali ya kushangaza yusuf makamba aliingia mitini wakati mabalozi wanipotembelea Tarime kujionea kampeni za uchaguzi zinavyondeshwa...
swali: je tatizo ni lile lile la kutokujua kingereza au kulikuwa na nini mpaka awakimbie? nisaidieni...

Kwanini isiwe aliwakimbia kwasababu mabalozi hawajui Kiswahili? Hatua ya kwanza ya kujikomboa kikweli kweli ni kuanza kuthamini vilivyo vyako.
 
katika hali ya kushangaza yusuf makamba aliingia mitini wakati mabalozi wanipotembelea tarime kujionea kampeni za uchaguzi zinavyondeshwa...
Swali: Je tatizo ni lile lile la kutokujua kingereza au kulikuwa na nini mpaka awakimbie? Nisaidieni...


tatizo ni kwamba makamba kiingereza hakipandi ni lini umeshasikia anaongea na mgeni wa nje na lini amesafiri nje labda alipokuwa anaumwa, tofauti kabisa na mangula.
 
Kwanini isiwe aliwakimbia kwasababu mabalozi hawajui Kiswahili? Hatua ya kwanza ya kujikomboa kikweli kweli ni kuanza kuthamini vilivyo vyako.

tupewe sababu ya kukimbia basi ili tuache speculations...
 
Duh hii kali mimi naona cha kwanza Lugha cha pili ni yeye anahusika moja kwa moja na vulugu zile.
 
Kwanini isiwe aliwakimbia kwasababu mabalozi hawajui Kiswahili? Hatua ya kwanza ya kujikomboa kikweli kweli ni kuanza kuthamini vilivyo vyako.

Pamoja ya kwamba kiswahili ndiyo lugha yetu na inapasa tujivunie lakini kwa mtu ambaye anataka public office kujua lugha za kigeni siyo tu ni muhimu bali ni lazima walau kiingereza.
Hao mabalozi labda kwavile wako Tanzania muda mrefu kidogo wanaweza wakawa wanajuajua kiswahili.Wale ambao hawajamaliza hata mwezi?Lakini ndiyo tuseme Makamba hatoweza kusafiri kwenda nje ya nchi bila ya kuwa na mkalimani?Kuna vyama marafiki huwa wanaalikana,Makamba hawezi kwenda kuwapokea mpaka awe na Mkalimani?
Kisa najivunia kiswahili changu.Hayo mambo waachieni warusi na wachina,hayo ni mataifa makubwa ati lakini hivi vinchi vyetu ombaomba lazima tukazane kuzijua hizi lugha za mnaowaita wafadhili!
 
tatizo ni kwamba makamba kiingereza hakipandi ni lini umeshasikia anaongea na mgeni wa nje na lini amesafiri nje labda alipokuwa anaumwa, tofauti kabisa na mangula.

Kama kiongozi wa chama nadhani kujua kiingereza si ishu angeweza kuongea hata kupitia mkalimani.Na pia sitaki kuamini kuwa hajui kimombo ukizingatia umri alio nao na kama alipitia shule ze misheni kama anavyosema mwenyewe.
 
Kama kiongozi wa chama nadhani kujua kiingereza si ishu angeweza kuongea hata kupitia mkalimani.Na pia sitaki kuamini kuwa hajui kimombo ukizingatia umri alio nao na kama alipitia shule ze misheni kama anavyosema mwenyewe.

Hii kali kumbe umri ulikienda na kimombo kina panda? will try it with my grandpa!!
 

Unajuaje hata hao mabalozi wote wanajua Kiingereza? Requirement mojawapo kwa nchi mbalimbali kwa mabalozi wanaokuja Tanzania ni pamoja na kujua Kiswahili ingawaje sio lazima sana.

Point hapo ilikuwa mna uhakika gani kwamba hao mabalozi hawajui Kiswahili? Pia kama
Makamba hajui Kiingereza angeweza kutumia mkalimani bila tatizo lolote.

Tatizo la TZ ni uwezo wa viongozi wetu kuongoza na wala sio tatizo la kushindwa kuongea Kiingereza.

Utajivunia Kiswahili wakati unakimbilia kiingereza kabla hata ya kujua huyo wa upande wa pili anajua kiswahili au la?

Ni muhimu sana kujua lugha lakini sio kwa maana mnayotaka kuionyesha kwenye mjadala huu.
 
Jamani, wakati Makamba anamjibu mgombea wa Chadema aliyetaka wafanye mdahalo kwa Kiingereza alisema yeye si maimuna? Sa mbona mnamzushia babu wa watu kuwa Kiingereza akipandi?
Mwenyewe alishasema kuwa asingeweza kukutna nao kwa sababu yuko busy na kampeni na ratiba yake haikuonyesha kuwa anakutana na mabalozi siku hiyo!!!!!
 
Yes, the problem is not English but is "what to explain to them once they will need him to comment how the campaign is going?
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…