Magabe Kibiti
JF-Expert Member
- Jan 20, 2008
- 292
- 2
Good question. Unajua Kiswahili saa ingine kigumu.
yaani nimepitia kamusi zote zinazopatikana kwenye mtandao na sikupata hili neno sasa ikabidi tu niulize jamii inisaidie.
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Good question. Unajua Kiswahili saa ingine kigumu.
Taarifa zilizothibitika kutoka Tarime zinaeleza kuwa wananchi wanne wa Tarime wanaosadikiwa kuwa wafuasi wa CHADEMA wamejeruhiwa vibaya kwa kukatwa mapanga na watu wawili kwa sababu zinazoweza kuwa za kisiasa.
Taarifa zinaeleza kuwa watu hao wanne walikuwa eneo amabapo helkopta inayotumiwa na CHADEMA katika kampeni za ubunge na udiwani ilikuwa inasubiria kutua.Wakati wananchi na wafuasi wa CHADEMA wakiwa wanasubiri kuwasili kwa viongozi wa chama chao,ilitokea gari ambapo walishuka watu wawili wakiwa na mapanga na ghafla wakawavamia watu hao kwa kuwakatakata kwa mapanga.
Akithibitisha kuwahudumia watu hao hospitalini, daktari (jina ninalo) amethibitisha na kueleza kuwa mmoja wa majeruhi ameshonwa nyuzi kumi na tisa (19) kwa nje.Hakutaja idadi ya nyuzi alizoshonwa kwa ndani.
Hali hii inajitokeza zikiwa zimebaki siku tatu tu wanatarime watumie haki yao kikatiba kumchagua mwakilishi wao.
halisi said:HATARI:
KUna taarifa za watu watatu kukatwa na mapanga mbele ya polisi Tarime na watuhumiwa kutoroshwa na gari la kiraia linalojulikana. Polisi badala ya kushughulikia watuhumiwa, wakakimbia na gari lao.
Saa moja baadaye uongozi wa polisi unafika eneo la tukio na wakati wanaendelea kukagua, gari lililowatorosha watuhumiwa linafika, na wananchi wanapiga kelele kusema hilo! Hilo!, linageuza na kukimbia, mkuu wa polisi anaamuri gari la polisi liwafukuze, dereva wa polisi anacheka na kukaidi amri ya bosi wake. GAri linatokomea na polisi wanaendelea kubaki walipo.
MAONI:
-Hii ni hatari na matokeo yake huenda kukazuka mauaji ya kutisha.
-Jimbo moja lisiwe mwanzo wa maafa kwa Watanzania
-JK lazima atoe tamko la kukemea na kuwaambia watu wake waache UJINGA
yaani nimepitia kamusi zote zinazopatikana kwenye mtandao na sikupata hili neno sasa ikabidi tu niulize jamii inisaidie.
yaani nimepitia kamusi zote zinazopatikana kwenye mtandao na sikupata hili neno sasa ikabidi tu niulize jamii inisaidie.
yaani nimepitia kamusi zote zinazopatikana kwenye mtandao na sikupata hili neno sasa ikabidi tu niulize jamii inisaidie.
Angalieni matumizi ya Lugha waungwana...Alidhamiria kusema "kumuenzi" maana neno "Hedhi" lina maana tofauti,na hapo mahali si pake
Ku Enzi na hedhi ni tofauti Enzi ni tofauti neno enzi kama kweli ni kweli na hedhi ni ile tu ya kuzuga zuga na mtimanyogo fulani maana unalazimika kusema hivyo BILA kusema hivyo inamaana hutopata unachokitafuta.
ILI ni weke bayana CHADEMA wana mhedhi CHACHA ama wanamuenzi.?Maana nimeona Mbowe akitumia neno hilo sana ktk kampeni zake.
Jamani, hedhi si ni zile "siku" za akina first lady au?
Matumizi ya Helikopta ktk kampeni za chama hayawezi kuwa na sifa nzuri ya aina yoyote ile zaidi ya ku prove kuwa ndivyo tulivyo.. Kwanza ni aibu kubwa kwa kiongozi kusema barabara mbovu wakati wananchi wako unaotafutra kura zao, barabara hizo ndio maisha yao ya kila siku..Ulichotakiwa wewe kama kiongozi kupelekwa muswada bungeni ioli kwanza upate kuwaambia wananchi jinsi ulivyotetea ujenzi wa barabara hizo..Pia zingatieni kwamba tatizo la viongozi kushindwa kufika sehemu hizo ni moja ya sababu kubwa ambayo inaweza kupitisha miswada kama hiyo maanake ndio kula yenu. Kwa mtazamo wowote ule wewe ni mshindi kwa wananchi wako. Focus ya kampeni siku zote huwa ni wananchi sio swala la kufikiria viongozi.
Leo hii ya kuwafuata wananchi na helikopta utadhani unawapelekea misaada ya chakula na dawa kumbe ni kampeni za chama...Nooo guys mnaharibu nyotre Chadema na CCM..
Wakuu wangu Chadema kusema kweli haya ni makosa niliyasema ktk uchaguzi uliopita na nitaendelea kupinga matumizi ya Helikopta kwani viongozi mashujaa wote toka kina Washington hadi Castro waliepuka sana kuonyesha tofauti zaoi na wananchi wa sehemu hizo. Kama kulikuwa na Umuhimun wa kutumia helikopta basi mgeenda hadi Musoma kisha mkachukua mabus ama magari madogo, pikipiki na kadhalika mkipitia vijijini ambapo wananchi wangeweza kuwaona mkipita na bendera zenu zikipepea kuelekea Tarime...
Na maandalizi ya msafara yangetakiwa kufanywa mapema kiasi kwamba wananchi wa vijiji vyote vinavyounganisha Musoma na Tarime wangekuwa na taarifa ya msafara huo..Trust me, hii ndio njia nzuri ya kujitangaza...
Hamuwezi kuamini lakini nakumbuka vizuri sana wakati mwalimu Nyerere alipotembelea Kibara, wilaya ya Mwibara kati ya mwaka 1966 au 67, hiyo kumbukumbu nimeibeba hadi leo hii..Nakumbuka vizuri tukiwa peku peku tukifukuzia magari ya serikali kwa miguu hadi makao makuu ya chama. Sura za wananchi na mpasuko wa roho bado nauona kama vile ilikuwa jana tu..Na sababu kubwa niliyokuja gundua ni kwamba ilikuwa mara yangu ya kwanza na pengine the only chance ya kumuona kiongozi wangu (Nyerere)..
Pamoja na yote haya najua kama hata sisi raia ndivyo tulivyo kwani kuiona Helikopta ni bora na maajabu zaidi kwetu kuliko kumwona kiongozi mwenyewe!..Ni ushindi wa mazingaombwe!
Kwa wale wanaotetea matumizi ya helikopta kwa sababu barabara ni mbovu.
Mbona tunawalaumu waheshimiwa wabunge na mabosi serikalini wanapokazania kuwa ni lazima wanunuliwe mishangingi kwa sababu hiyo hiyo, yaani barabara hazipitiki? Hivi toka tuanze kuwanunulia hiyo migari, hizo fedha zingewekezwa kwenye hizo barabara si angalau leo wengi wao wangekosa kisingizio. Sisi ni watu wa bling. Na helikopta kama yalivyo hayo mashangingi ni bling pia. Na wote tunajijua tunavyopenda cheini zetu za dhahabu, hata kama bado tunakaa katika chumba cha kupanga!
Mpaka leo sijasikia jambo la maana linalozungumziwa kuhusu mwananchi wa Tarime kutoka pande zote zinazogombania uchaguzi huu. Wamebaki kutambiana na kuonyeshana ubabe. Sera ni kama za Sarah Palin, ku-appeal to the lcd wakati matatizo ya mwananchi yanafagiliwa chini ya jamvi. Lakini hamna cha kushangaza kwa sababu fundamentally wote ni wale wale. Wakiingia hao wengine nao wataendeleza libeneke kama kazi!
Huu utafiti umefanywa na Thomas Ngawaiya
Na Godfrey Lutego
Uchaguzi mdogo wa mbunge na Diwani wa jimbo la Tarime mkoani Mara unafanyika kesho huku ushindani mkubwa ukiwa kati ya mgombea wa chama tawala, CCM, Bw. Christopher Kangoye nawa chama cha upinzani, CHADEMA, Bw. Charles Mwera.
......
Kwa mujibu wa tathmini iliyofanywa na Taasisi ya Utawala bora na Maendeleo Tanzania (CEGODETA), CCM ina nafasi kubwa ya kutwaa jimbo hilo kwa ushindi wa asilimia 65 ikifuatiwa na CHADEMA iliyokuwa inalishikilia inayopewa nafasi ya kupata asilimia 35 na vyama vinavyobaki vinatarajiwa kupata asilimia 5.
.....
Hata hivyo, tathmini hiyo inatofautiana kidogo na tathmini iliyotolewa na gazeti moja likikariri wanaodaiwa kuwa wananchi wa Tarime kuwa CHADEMA itaendelea kutetea jimbo hilo kwa ushindi wa asilimia 50 huku CCM ikipata asilimia 45 na vyama vingine vilivyobaki asilimia 5.
Mkuu Mugabe
Kumbuka Ngawaiya alikuwa zamani TLP akaasi na kurudi CCM kwa hiyo utafiti alio ufanya sijui yupo Tarime au kwa kuwauliza Makamba,Msekwa na Komba?
Amefanya utafiti akiwa na majibu tayari....