Ubunge Tarime: Wagombea, Kampeni na Uchaguzi

Ubunge Tarime: Wagombea, Kampeni na Uchaguzi

Status
Not open for further replies.
Uchaguzi huu umetufundisha mengi sana:





ii) Tumefika turning point, kwa maana kwamba katika kila sehemu kuna watu wenye kutaka kuona haki inawepo. Tarime kulikuwa na majaribio mengi ya kutaka kubadilisha matokeo, lakini kuna baadhi ya watendaji ndani ya Halmashauri ya Tarime ambao walikuwa wanafanya kazi kwa niaba ya Tume walikataa kata, wakisema kuwa haki lazima itendeke. Hii ina maana kuwa kuna watendaji katika serikali hii ya ovyo ya CCM ambao kwa kweli wapo tayari kusimamia haki hata kama kufanya hivyo italeta matatizo kwenye vibarua vyao. Ni hatua ya namna hii iliyowezesha vyama vya upinzania huko Zambia, Malawi, na hata Kenya. Bila kuwa na watu wenye uchu wa haki ndani ya vyombo vya dola, itakuwa ngumu kuishinda CCM. Kwa sababu hiyo nachukua nafasi hii kuwashukuru sana watendaji mbalimbali wa Tume ya Uchaguzi huko Tarime waliohakikisha kuwa wanashinda majaribu na mashinikizo ya akina Makamba na kuhakikisha wana mtangaza mshindi kama walivyoamua wananchi.

iii) Tunawashukuru wana JF kwa changamoto na nasaha zenu, ambazo kwa kweli zimekuwa zinatusaidia sana kujifunza. Matokeo ya Tarime yametuchochea kufanya kazi ya siasa, na katika siku chache zijazo mtashuhudia viongozi wa chadema wakisambaa mikoani kwa ajili ya kazi ya kukisimika chama katika nyoyo za watanzania.





Vi) Mwisho, niseme kwamba uchaguzi huu unaashiria mwisho wa siasa za ujanjaujanja. Siasa za akina Tambwe, Makamba na Akwilombe hazitawasaidia huko tuendako. Huko tuendako kinachotakiwa ni umakini, ukweli na uwezo. Blabla, longolongo na uongo unaoenezwa na akina Tambwe hauna tija. Anayeendelea kuwadanganya CCM kwamba umahiri wa kusema uongo ndio ushujaa katika siasa anawadanganya, na wajiandae kuumbuka zaidi huko tuendako. Kwa kuwasaidia, katika kujipanga upya, wawafukuze au wawape kazi nyingine akina Tambwe, Akwilombe na Makamba.



Bara-bara! Umefanya vyema ku-acknowledge na kuwashukuru hawa wanaojitoa mhanga kuinusuru nchi hii. Ukombozi waja, pengine mapema kuliko inavyotabiriwa.



.
 
Wana ccm wenzako wengi wamekimbia forum kuanzia jana mkuu, Msekwa na wengine walikimbia toka Tarime kabla hata matokeo hayajatangazwa rasmi na msimamizi wa uchaguzi. Anyway, ingawa huu ni ushindi mmoja tu kati ya viti vingi sana bungeni, ni vizuri ijulikane hapa kuwa wana-Tarime wamefanya la muhimu sana kwa demokrasia Tanzania.

Labda watanzania wengi sasa watajifunza hapa na kusema NO pale ambapo mambo yanakuwa yamewafikia shingoni huku ccm na mafisadi kama jambazi hili la Tarime - Zakaria wakiwaonyesha vipesa pesa vya wizi.

Mkuu MwK. Demokrasia sio kushindwa kwa CCM na Upinzani kushinda; Bali ni mwananchi kumchagua anayempenda bila kubughudhiwa.

Kidumu Chama Cha Mapinduzi

Kidumu Chama Tawala.
 
Hata kuaga wenyeji wao hawakuwaaga. Kushindwa kubaya hasa ukitilia maanani walitumia mapesa chungu nzima, FFU, Polisi, vipigo na vitisho, helikopta mbili, wakamnunua na Mwendawzimu Mtikila ili awachafue viongozi wa juu wa CHADEMA. Sijui watamlaumu nani kwa kipigo walichokipata Tarime.

Mkuu BaK,

Kilichotokea Tarime sio kipigo kwa CCM, bali ni Demokrasia.

Kidumu Chama Cha Mapinduzi,

Kidumu Chama Tawala
 
Comandoo Es,

Maneno mazito sana haya,nilijua mkuu usingeweza kuingia mtini tangu jana kwa jinsi hata wana_CCM wenzako walivyotoweka.

Mkuu umeonyesha ukomavu wa hali ya juu.Siasa si ugomvi kama wengine walivyoonyesha kwa kutoweka hapa jamvini,kweli wewe kamanda.

Pokea heshima nzito kutoka kwangu mkuu!
 
Date::10/14/2008
Mashangingi ya CCM yatoweka Tarime usiku

*Ni baada ya ushindi wa kishindo wa Chadema

Na Waandishi wetu, Tarime
Mwananchi

VIONGOZI wa juu wa CCM pamoja na wafanyabiashara ambao magari yao ya kifahari (mashangingi) yalikuwa yakirandaranda wilayani Tarime wakati wote wa kampeni za uchaguzi wa ubunge na udiwani, juzi yalitoweka usiku wa manane baada ya kupata uhakika kuwa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimezoa viti vyote viwili.

Chadema ilifanikiwa kurejesha viti vyake viwili vilivyotangazwa kuwa wazi baada ya kifo cha Chacha Wangwe, aliyefariki kwa ajali ya gari zaidi ya miezi miwili iliyopita baada ya kupata ushindi mkubwa dhidi ya vyama vingine vitatu, kikiwemo chama tawala cha CCM.

Msimamizi wa uchaguzi wa jimbo la Tarime, Triasis Kagenzi alimtangaza mgombea ubunge kwa tiketi ya Chadema, Charles Mwera Nyanguru kuwa mshindi baada ya kuzoa kura 34,545 na hivyo kumwacha mbali mgombea wa CCM, Christopher Ryoba Kangayo, aliyepata kura 28,996.

Lakini wakati Kagenzi anatangaza matokeo hayo majira ya saa 5:13 mbele ya Mwera, Kangoye na wagombea wengine, viongozi wa juu wa CCM na makada wengine kadhaa walikuwa wameshatoweka Tarime usiku wa manane na haikuwa ajabu kwa Katibu Mkuu wa CCM, Yusuf Makamba, kuibukia Mwanza majira ya saa 6:00 na kuzungumza na waandishi.

Kutoka Tarime hadi Mwanza ni mwendo wa saa nane kwa gari la mwendo wa kawaida.

Ushindi wa Chadema ulianza kuonekana mapema baada ya matokeo kuanza kubandikwa jioni katika kata mbalimbali na hadi saa 6:00 usiku ilishadhihirika kuwa Mwera na mgombea wa udiwani kwa tiketi ya Chadema, John Heche walishanyakua viti hivyo; na hivyo kuwapa muda makada hao wa CCM kupanga mikakati ya kuondoka mapema iwezekanavyo.

Wakati Mwananchi ilipowasiliana na msemaji mkuu wa Katibu Mkuu wa CCM, Gabriel Athuman juzi usiku, alijibu akisema: "Tunajiandaa kuondoka. Wengine wanaenda Musoma na wengine Mwanza... tumeshashindwa vibaya, hatuwezi kusubiri hadi kesho (jana)."

Viongozi ambao wanasemekana kutimka usiku ni Makamba, aliyeelekea Mwanza, mwenyekiti wa CCM, Mkoa wa Mara, Makongoro Nyerere aliyerejea Musoma, mbunge wa Simanjiro, Christopher Ole Sendeka, aliyekuwa mkuu wa mkoa wa Mwanza na baadaye Morogoro, Stephen Mashishanga ambaye pia ni mjumbe wa NEC pamoja, na mkurugenzi wa propaganda wa chama hicho, Tambwe Hiza.

Hilo lilidhihirika saa chache baada ya Kagenzi kutangaza matokeo mjini Tarime wakati Makamba alipoongea na waandishi mjini Mwanza kuzungumzia matokeo ya uchaguzi huo mdogo.

"Nimekuja kukubali matokeo," alisema Makamba, ambaye aliweka kambi mjini Tarime tangu kuanza kwa kampeni hizo. "Mnajua kuwa asiyekubali kushindwa si mshindani. Sisi kama chama tumekubali matokeo katika uchaguzi huo kuwa tumeshindwa."

"Nawapongeza wananchi wa Tarime kwa kuonyesha demokrasia ya kweli kwa kuchagua viongozi wanaowataka. CCM itaendelea kutekeleza ilani yake kwa kupeleka maendeleo jimboni humo."


Lakini alipoulizwa zaidi kama wana mpango wa kukata rufaa kupinga matokeo hayo kama mgombea wao Kangoye alivyoeleza awali kuwa hakubaliani na matokeo ya kura hizo, Makamba aliuruka msimamo wa mgombea huyo wa chama chake akisema:

"Sisi kama chama tumekiri kushindwa na iwapo kama yeye mgombea ameamua kukataa matokeo hayo na anataka kwenda mahakamani hiyo ni haki yake.

"Msimamo wa chama kuhusu matokeo hayo, nimeshaueleza kuwa tumekubali kushindwa. Lakini mgombea naye ana sababu zake binafsi na yuko huru kugomea matokeo hayo na hata kwenda mahakamani."


Katika mkutano huo na waandishi wa habari, ambao ulifanyika kwenye hoteli ya New Mwanza inayomilikiwa na mjumbe wa Halmashauri Kuu wa taifa MNEC, Christopher Gachuma, Makamba alisindikizwa na mbunge wa Magu, Dk Festus Limbu, mbunge wa Maswa, John Shibuda pamoja na Katibu wa CCM, Mkoa wa Mwanza, Mwangwi Kundya Rajabu.

Kangoye alifika kwenye chumba cha kutangazia matokeo akiwa amechelewa na aliongozana na Katibu wa CCM wa Wilaya ya Tarime, Luteni Iddi Istambuli.

"Siyatambui matokeo haya kwa sababu ya kuwepo kasoro ndogo ambazo inabidi zifanyiwe marekebisho kwa ajili ya kutoa mbunge wa haki na halali," alisema Kangoye alipofuatwa na waandishi na ambaye awali alisema hakusaini kuridhia matokeo hayo kabla ya msimamizi wa uchaguzi, Kagenzi kusema kuwa wagombea wote wamekubali matokeo na kusaini fomu za kuridhia.

"Kasoro hizo ni nyingi, lakini pia siyakubali kwa vile yametangazwa wakati sisi tukiwa tunaendelea kukusanya kura zetu katika vituo."

Tangu juzi usiku, wafuasi wa Chadema walikuwa wakishangilia ushindi licha ya Tume ya Uchaguzi kusema kuwa, ingetangaza rasmi matokeo jana asubuhi; na shangwe zao zilikumbana na nguvu za dola kutokana na polisi kupiga mabomu ya machozi kuwatawanya wafuasi hao.

Shangwe hizo ziliendelea jana asubuhi baada ya wafuasi wa Chadema kukusanyika kwenye ofisi za chama chao majira ya 9:25 usiku. Wafuasi hao walikuwa wakipewa matokeo ya karibu vituo vyote 406 kwa njia ya ujumbe mfupi wa maandishi kutoka kwa mawakala wao.

"Chama cha wahuni kimechukua.. chama cha wahuni kimechukua," waliimba wafuasi hao wa Chadema kukejeli maneno ya Makamba ambaye kila aliposimama kwenye kampeni alisema, wengi waliokuwa wakijitokeza kukishabikia chama hicho cha upinzani ni wahuni na si wapigakura.

Licha ya kuimba, vijana hao walikuwa na mabango yaliyoandikwa: "Makamba wahuni wa Tarime so... Mwisho wa CCM umefika, Watanzania tunataka mabadiliko ya kweli sio kanga na kofia."

Furaha yao ilikamilika wakati mkurugenzi wa uchaguzi, Kagenzi alipotangaza matokeo kuthibitisha kuwa Chadema imerejesha mikononi mwake viti vyote viwili vya ubunge na udiwani.

"Nashukuru kuwa nimeshinda kama wananchi wa Tarime walivyotaka," alisema mshindi huyo wa kiti cha ubunge kwa tiketi ya Chadema, Charles Mwera mara baada ya kutangazwa kuwa mshindi na kuonyesha ishara ya vidole viwili kwenye mikono yote.

"Ushindi huu ni kwa ajili ya wananchi wa Tarime. Nitawatumikia bila ya kujali tofauti za kiitikadi na kisiasa."

Nje ya jengo ambalo matokeo ya uchaguzi yalitangazwa, wafuasi wa Chadema walikuwa wakihangaishana na polisi ambao walikuwa wakiwazuia kufika kwenye ofisi ya msimamizi wa uchaguzi. Wakati fulani polisi hao walizidiwa nguvu na kuamua kupiga mabomu ya machozi.

Hata hivyo, wananchi hao waliendelea kusonga mbele na ndipo ilipobidi Kamanda wa Operesheni Maalumu, Venance Tossi kuongeza askari na kuamuru watumie risasi za moto.

Matokeo ya nguvu ya Jeshi la Polisi kuwatawanya wananchi hao yalikuwa ni kujibiwa kwa mawe na askari mmoja alijeruhiwa vibaya kwenye jicho lake la kulia baada ya kutupiwa jiwe.

Shambulio hilo lilisababisha nguvu zaidi kutumika na wafuasi kadhaa walikamatwa katika purukushani hizo. Kutokana na polisi kutokuwa na gari kubwa, walilizuia lori la Shirika la Umeme (Tanesco), lenye namba za usajili SU 36270 lililokuwa likipeleka mafundi kazini na kuamuru libebe wananchi 15 waliokamatwa kuwapeleka polisi, huku wengine tisa wakichukuliwa na gari la halmashauri lenye namba SM 4249.

Hata hivyo, polisi walionekana kuzidiwa nguvu na hivyo kumwomba mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe kutoka ndani ya ukumbi wa kuhesabu kura za ubunge kwenda na maofisa wa polisi kuwatuliza wanachama wake.

Ujumbe wa jeshi la polisi kuomba Zitto kwenda kuwatuliza wafuasi wa Chadema uliongozwa na afisa upelelezi wa Mkoa wa Mara (RCO), Deus Katto, ambaye naye alimsihi kukubali kutoka na kupanda gari namba T 305 ASC kwenda kuzungumza nao.

"Tafadhali nawaomba sasa mtulie... matokeo yetu hayataibiwa. Tumewabana na kila kitu ni safi na ushindi wetu uko pale pale, sasa tunamalizia kujumuisha kura na baada ya muda mtatangaziwa matokeo yenu na Mwera ndiye mbunge wenu," alisema Zitto.

"Sasa nawasihi kuanza kuondoa mawe na vizuizi vyote barabarani ambavyo mlikuwa mmeweka na kuacha wananchi waendelee kupita…sawa?"

Baada ya Zitto kuwatuliza vijana hao walipunguza hasira na kuanza kutulia kusubiri matokeo ambapo baada ya matokeo kutangazwa, vijana hao walilipuka kwa furaha na kuanza kushangilia ushindi huo huku wakizungukazunguka mjini Tarime.

Story na Frederick Katulanda, Musa Juma na Mpoki Bukuku.
 
Wakuu,nawashukuru nyoote kwa kuchangia hii thread.Hatukulaal mpaka kikaeleweka.

Heshima mbele kwa wanaJF na heshima mbele kwa Tarime na CHADEMA.
 
kp_351.jpg
 
Mkuu MwK. Demokrasia sio kushindwa kwa CCM na Upinzani kushinda; Bali ni mwananchi kumchagua anayempenda bila kubughudhiwa.

Kidumu Chama Cha Mapinduzi

Kidumu Chama Tawala.

Mkuu Ladslaus,

Sidhani kama umeona sehemu yoyote ile nikisema kuwa demokrasia lazima ccm washindwe. Kinachoongelewa hapa ni nguvu kubwa sana na mapesa kibao ambayo serikali ya ccm na wapambe wake - Mtikila, Mbatia na Hiza walitaka kutumia Tarime ili kuendeleza status quo.

Watu wa Tarime wamechukua kofia, tisheti, vitenge, pesa, na pombe BUT mwisho wa siku wamekataa sera za ugomvi na uzushi ambazo serikali ya ccm na wapambe wake walitaka kuzileta Tarime. Wananchi wakifikia kiwango cha kwenda kupiga kura bila kujali vipigo na vitisho vya polisi - basi demokrasia ya nchi au eneo husika inahesabiwa kuwa inapanda.

Otherwise, mtizamo wako wa kutumia post zako zaidi ya ishirini zilizopita kutosema chochote but "kidumu cha mapinduzi" pia unaheshimika maana hii ni forum huru kinyume na mafisadi wengine wanavyodai kila siku kuwa JF sio huru
 
Mkuu PM,

Habari nilizonazo za ndani ni kwamba mkulu alipoambiwa kwamba wabunge wote wasiokumbatia ufisadi wamegoma kwenda Tarime, akaamua kuwa hataki anything to do na huko, lakini ninakubali hoja yako kama ulivyosema kua hakutakiwa kusubiri kuitwa, alitakiwa kuwa wa kwanza kufika huko

Tena nyeti zaidi nasikia Makamba na wenzake walivizia jana usiku wa saba, ndio wakaondoka kimya kimya huko Tarime, kurudi Dar. Halafu nasikia nyeti zaidi ni kwamba hawa viongoziw a mafisadi wanashukuru sana majimbo mawili yaliyobaki Biharamulo na Mwibara, hayatagombewa mapaka next uchaguzi kwa sababu CCM walipitisha mswaada unaokataza uchaguzi wa majimbo madogo in two years kabla ya uchaguzi mkuu, sasa vipi kina Zitto wakishinikizwa kuuulilia huo mswaada ubatilishwe ili na hayo majimbo yafanyiwe uchaguzi sasa? Tujue ukweli ulipo au?


Mkuu ES,

Unataka rais wa nchi awe anaenda kwenye kampeni za chaguzi ndogo za wabunge?

Binafsi naona itakuwa kupoteza muda. Kuna akina Makamba na Msekwa labda na mawaziri lakini sio rais wa nchi.

Nafikiri kama sikosei rais wa mwisho kwenda kwenye chaguzi ndogo alikuwa Mkapa hiyo 1998 kule Temeke kwa Mrema na bado walishindwa.

Binafsi sishangai CCM kushindwa Tarime. Kwa siasa za TZ ili kushinda jimbo inatakiwa uwe na watu on the ground. CCM inatumia madiwani na watendaji kujipatia ushindi. Kwa Tarime CHADEMA wanaongoza halmashauri na hivyo walikuwa na watu muhimu on the ground ambao ndio huwa wanaleta ushindi.

CCM wanashindwa kule Pemba kwasababu hizo hizo. Ukisikia kura zinaibiwa, wanaopanga wizi ni hao madiwani na watendaji, sasa kama hawapo, sio rahisi kabisa kwa CCM kufanya ujanja wowote.

Ni muhimu sana kuwa na watu kule chini kama vyama vya upinzani vinataka kuishinda CCM.
 
I mean CCM tumeshindwa this one na it hurts badly, kwa sababu hakuna reasonable excuse hapa, zaidi ya kukosa dira na muelekeo kisiasa na kiuongozi, sasa ni wakati wa viongozi wasiokuwa na uwezo kuwajibika au wawajibishwe, ninasema hivi kwa wanachama wote wa CCM, tusijidanganye hapa kua eti hili ni jimbo moja tu, hapana haba na haba hujaza kibaba period! Huu ni mwanzo tu kama CCM hatujiangalii kwenye kioo, hata 2010 itakuwa aibu kubwa zaidi ya hii,

Na tusidanganyane hapa hii aibu inakwenda straight kwako mwenyekiti, rais wa jamhuri kabla ya mtu yoyote mwingine, ni kwamba tuna viongozi wabovu wasiokuwa na uwezo kabisaa, sasa waondolewe kabla ya aibu zaidi

Pole sana. I can feel your pain, bro! Ndio maana mimi baada ya uchaguzi wa 1995, niliamua kubakia Independet.
 
Hakuna silaha mbaya kama determination. Wananchi wa Tarime wameshinda kwa sababu washaamua kuwa kwa njia yeyote ile Chama Cha Majizi lazima kisipewe nafasi. Determination inasababisha watu kuwa na uvumilivu,mbinu na absolute focus kwenye kile wanachohitaji.

Mwisho nakupongeza FMES kwa ujumbe mzito, na kuonyesha ukomavu katika siasa.

Mpaka kitaeleweka tu. Hakuna cha mabomu, marungu, pilipili wala Mtikila.
 
Kwa wakuu wote JF, kwanza heshima mbele sana, na pia kama mwanachama hai na mkereketwa wa CCM, nitoe heshima zangu nzito kwa kuutambua ushindi wa chama chetu cha taifa cha wananchi yaani Chadema, kwa ushindi mkubwa sana huko jimbo la ubunge la Tarime, infact jana nilikuwa sehemu ambapo pia alikuwepo Mama Migiro, ambaye at one point aliniuliza "...vipi huko JF, Tarime tupo wapi?..." nikamjibu kuwa hatujawahi kuwa popote huko zaidi ya chini, I mean:-

1. CCM tumeshindwa Tarime, vibaya sana tena sana na ni aibu tena kubwa sana, ukijumlisha maovu yote yaliyofanywa huko na baadhi ya viongozi wa CCM ambao nusu yao nimeongea nao leo, kwa kweli ni aibu kubwa sana, and I hope kwamba huu uchaguzi sio min-refferendum ya 2010, maana nina wasi wasi sana kwamba it is a refferendum tena kwa 100% ya uchaguzi wa 2010.

2. Huu ushindi ni ujumbe tosha kwetu CCM, kwamba get rid of rogue leaders kama Makamba, na Msekwa get them out tena now, maana hawa ni kundi la mafisadi, I mean wachawi wako within us kwa sababu hawana uwezo wa kuongoza taifa kwenye level ya chama kinachotawala, sasa nashangaa Rais Kikwete akiwachekea hawa fukuza now!

3. Mwenyekiti Rais Kikwete, sasa baada ya huu ujumbe kusiwe na kuchekeana tena, otherwise tunakwenda down tena kwa kasi kali sana kwa sababu this is a true picture ya what to come mbele ya safari, Republicans waliposhindwa viti vichache tu ndani ya Congress pamoja na kwamba walikua bado ni majority, walimtoa mbio Spika Gingrich, sasa CCM tuache kuechekeana kwa sababu hakuna excuse hapo, CCM nzima ilikuwepo huko Tarime, sasa iliyoshindwa hapa ni CCM sio anybody else!

4. CCM tunapaswa kuwaomba radhi wananchi wa Tarime, kwa sababu nina uhakika kwa 100% kwamba niliyoyasikia kutoka huko yaani maovu yetu ni kweli yamefanyika, lakini simply politics ni kwamba wananchi wamekataa ujinga na uongo period!

5. CCM this time tuna viongozi wabovu sana, tena sana wakumbatiaji wa rushwa na mafisadi, wasiokuwa na uwezo wa kuongoza, wasiokuwa na uwezo wa kuona mbali, I mean Mheshimiwa rais wakati mwingine sijui unapewa ushauri na nani kwamba Msekwa, aliyekuwa spika kwa karibu miaka 15 kiongozi wa chama na serikali kwa miaka karibu 40, halafu siku moja anapigwa chini kisiasa na kukosa kila kitu na kuwa jobless, leo unamuona huyu anafaa kua makamu wako wa kuongoza chama tawala taifa?

- Eti ni mwanasiasa gani wa kweli asiyeweza ku-navigate political fate yake mwenyewe? Sasaa leo unampaje ku-navigate CCM taifa kama sio kufilisika kwa hao washauri wako wa siasa?

- Waziri ameacha jiji halina umeme, anakimbilia kupiga kampeni za uchaguzi hivi hawa wananchi wa Tarime, wanatakiwa kuwa wajinga kiasi gani jamani?

- Tizama akili ya siasa ya Mkamba, hivi kweli unaweza kumtumia Mtikila kushinda uchaguzi wa jimbo la wananchi wenye akili timamu kama Tarime?

6. Hawa ni viongozi gani wa chama ambao hawana hata heshima ndani ya chama chao kutoka kwa viongozi wengine wenzao kwa sababu ninaambiwa kuwa ilifika mahali wakagundua kua hawana uwezo wa kuongoza CCM kushinda huko Tarime, wakaanza kujaribu kuwashawishi baadhi ya viongozi wengine kwenda huko Tarime, lakini hata kusaini hizo barua za kuwaomba wameshindwa badala yake wakajaribu kusingizia kuwa zimeandikwa na kikao cha sekretarieti chini ya mwenyekiti wa CCM, ambaye kila mwananchi anajua kuwa hakuwepo wakati zikiandikwa licha ya hao viongozi waliotumiwa, what kind of leadership is this kama sio a joke?

I mean CCM tumeshindwa this one na it hurts badly, kwa sababu hakuna reasonable excuse hapa, zaidi ya kukosa dira na muelekeo kisiasa na kiuongozi, sasa ni wakati wa viongozi wasiokuwa na uwezo kuwajibika au wawajibishwe, ninasema hivi kwa wanachama wote wa CCM, tusijidanganye hapa kua eti hili ni jimbo moja tu, hapana haba na haba hujaza kibaba period! Huu ni mwanzo tu kama CCM hatujiangalii kwenye kioo, hata 2010 itakuwa aibu kubwa zaidi ya hii,

Na tusidanganyane hapa hii aibu inakwenda straight kwako mwenyekiti, rais wa jamhuri kabla ya mtu yoyote mwingine, ni kwamba tuna viongozi wabovu wasiokuwa na uwezo kabisaa, sasa waondolewe kabla ya aibu zaidi,

Halafu as a nation imefika wakati wa kuliangalia tena suala la ruzuku in general, mimi ninafikiri umefika wakati wa ku- do away na ruzuku kwa sababu zinasaidia one thing only, nacho ni ku-off balance ushindani wa kweli wa kisiasa kwa taifa letu, na kudhoofisha kabisa upinzani wa kweli wa kisiasa nchini iondolewe au itafutwe njia nyingine ya kuleta balance haiwezekani chama kimoja kipate shillingi millioni 99, na vingine millioni 10, mpaka 30 halafu ukategemea kuwepo na ushindani ambao ni balanced na politically heathy kwa taifa.

Kwa kumaliza ninapenda kutoa heshima zangu kwa Chadema, kwa huu ushindi mzito sana, kutoka jimbo la mkoa aliozaliwa Baba wa Taifa letu, mhasisi wa CCM, hiyo ni aibu kubwa sana kwa viongozi wetu wote wa CCM, mlioshirki huko Tarime, shame on you, yaani kwa mara ya kwanza kuona uchaguzi mdogo ambao mmeshindwa hata kumshawishi mwenyekiti wa CCM kushirki, sasa kama mwenyekiti mwenyewe amewashitukia itakuwaje wananchi wa huko? Kwa nini mwenyekiti hakuenda huko? Maana yake ni moja tu kua hawaamini hawa wasaidizi wake, sasa mheshimiwa rais unangoja nini kuwaondoa mara moja?

Again heshima kwa Chadema kwa ushindi wenu mzito, ambao kwa jinsi nilivyoambiwa na waliokuwepo kwa maneno ya kizungu, ilikuwa ni no contest na mimi ninaamini kwa 100% kuwa ni kweli!

Mungu Aibariki Tanzania.
Mkuu FMES,
Umetoa analysis ya nguvu na bila chembe ya unafiki.Mimi si msomaji sana wa vitabu,lakinii kuna jamaa yangu ni msomaji mzuri wa vitabu kama alivyo Mwanakijiji na Mkumbo.Huyo jama alinisimulia alisoma kitabu cha mwandishi mmoja(alitaja jina),alisema kuwa ukitaka kumfahamu mtu tabia yake angalia watu wanaomzunguka.
Hivyo Mwenyekiti wa chama chenu anajichora kuzungukwa na watu wenye upeo mdogo,anajivunjia heshima.Hata kule Rungwe alipoamua kuwazodoa Mwakipesile na Mulla namweleza ya kuwa amepoza munkari kwa mda tu.Jambo la msingi ni kuwang'oa wanafiki wale ambao wako chini ya mamlaka ya uteuzi wake.Akizidi kuchelewa yatamkuta ya dictator Mugabe.Tarime ndio indicator yake.
 
Last edited:
Field Marshall umenena!

Inabidi sasa sie akina CCM tujichunguze kwa makini kabisa na kufanya marekebisho ya makusudi vinginevyo aibu hii tutaendelea kuipata. Haijawahi kutokea CCM kuanguka kama ilivyoanguka Tarime. Pamoja na vigogo wote hao mpaka UWT kujiingiza kwenye kampeni bado wana Tarime wakasema 'No!' Huenda kusingelikuwepo ulazima wa kuwepo polisi wengi kiasi kile kura za Chadema zingelikuwa nyingi zaidi ya hizo walizopata. Ni dhahiri wapo walioogopa kwenda kupiga kura kwa kuhofia usalama wao.

Tatizo lililopo ni kwamba huenda viongozi wa CCM hawataki kuamini na kukubali kwamba sasa CCM kimeanza kupoteza popularity hata miongoni mwa wana CCM wenyewe! Yapasa wale wanaodhani kwamba CCM bado ni chama kinachopendwa, wajiulize mara mbili kama hiyo dhana ndio ukweli wenyewe.

Siku zote tumekuwa tukishuhudia kwamba watu wa mijini ndio 'vizabizabina' ama 'malipyoto' ambao huonyesha wazi hisia zao dhidi ya CCM ama Serikali. Kwa maana hiyo, mara zote ushindi wa kishindo wa CCM umekuwa ukitokana na kura za watu wa vijijini ambao kwao wao chama walichokuwa wakikijua ni CCM. Halikadhalika, hata baada ya Mwalimu Nyerere kuachia madaraka na hata baada ya kifo chake, wapo wananchi wa vijijini waliokuwa wakidai kwamba wao wanataka kukipigia kura chama cha Nyerere. Sasa hivi mambo yamebadilika, haihitaji hata kufanya utafiti wa kina kujua kwamba watu wa vijijini nao wameishaanza kujua nini kinachoendelea ndani ya CCM na baadhi yao wamepoteza imani na Chama walichokuwa wakikiamini na kukipa kura 'automatic'.

Kama alivyosema Field Marshall, lazima viongozi wa juu wa CCM wabadilike. Viongozi wetu wafike mahali wasikilize, waelewe na wakubali kile kinachosemwa na wananchi. Wakubali kwamba kuna mahali pamekwenda kombo na kusababisha wananchi kuanza kukikataa CCM. Wakubali kurekebisha mambo kwa kukubali kwa dhati kwamba wamewakosea wana CCM wenzao na wananchi kwa ujumla. Wasipofanya hivyo na kuendelea na mtindo wa kuwafanya wananchi ni wajinga wasiojua kupambanua jema na baya, CCM kitaendelea kupoteza umaarufu wake na hatimaye kuanza kushindwa katika chaguzi zijazo.

Wana CCM tunasikitika kushindwa katika uchaguzi huu wa ubunge na udiwani Tarime, lakini wa kulaumiwa wapo!

Siku hizi, KiGumu Chama cha Mapinduzi!
 
Field Marshall umenena!

Inabidi sasa sie akina CCM tujichunguze kwa makini kabisa na kufanya marekebisho ya makusudi vinginevyo aibu hii itaendelea. Haijawahi kutokea CCM kuanguka kama ilivyoanguka Tarime. Pamoja na vigogo wote hao mpaka hata wa UWT Taifa kujiingiza kwenye kampeni bado wana Tarime wakasema 'No!' Huenda kusingelikuwa na utitiri wa polisi kura za Chadema zingelikuwa nyingi zaidi ya hizo walizopata kwa sababu wapo walioogopa kwenda kupiga kura kwa kuhofia usalama wao.

Tatizo lililopo ni kwamba huenda viongozi wetu hawataki kuamini kwamba sasa CCM imeanza kupoteza popularity hata miongoni mwa wana CCM wenyewe! Wale wanaodhani kwamba CCM bado ni chama kinachopendwa, wajiulize mara mbili kama dhana hiyo ndio ukweli wenyewe.

Katika chaguzi huko nyuma tumeshuhudia kwamba mara nyingi watu wa mijini ndio wanaokuwa 'vizabizabina' ama 'malipyoto' ambao huonyesha hisia zao dhidi ya CCM ama Serikali. Kwa maana hiyo, mara zote ushindi wa kishindo wa CCM umekuwa ukitokana na kura za watu wa vijijini ambao kwao wao chama walichokuwa wakikijua ni CCM. Sasa hivi, haihitaji hata kufanya utafiti wa kina kujua kwamba watu wa vijijini wamebadilika, wameishaanza kujua nini kinachoendelea na wamepoteza imani na Chama walichokuwa wakikiamini na kukipa kura 'automatic'.

Kama alivyosema Field Marshall, lazima viongozi wa juu wa CCM wabadilike. Viongozi wetu wafike mahali wakubali kile kinachosemwa na wananchi. Wakubali kwamba kuna mahali pamekwenda kombo na kusababisha wananchi kuanza kukikataa CCM. Wakubali kurekebisha mambo kwa kukubali kwa dhati kwamba wamewakosea wana CCM wenzao na wananchi kwa ujumla. Wasipofanya hivyo na kuendelea na mtindo wa kuwafanya wananchi ni wajinga wasiojua kupambanua jema na baya, CCM kitaendelea kupoteza umaarufu wake na hatimaye kuanza kushindwa katika chaguzi zijazo.

Wana CCM tunasikitika kushindwa katika uchanguzi huu wa ubunge na udiwani Tarime. Lakini, wa kulaumiwa wapo!

Siku hizi; KiGumu Chama cha Mapinduzi!
 
Mkuu Ladslaus,

Sidhani kama umeona sehemu yoyote ile nikisema kuwa demokrasia lazima ccm washindwe. Kinachoongelewa hapa ni nguvu kubwa sana na mapesa kibao ambayo serikali ya ccm na wapambe wake - Mtikila, Mbatia na Hiza walitaka kutumia Tarime ili kuendeleza status quo.

Watu wa Tarime wamechukua kofia, tisheti, vitenge, pesa, na pombe BUT mwisho wa siku wamekataa sera za ugomvi na uzushi ambazo serikali ya ccm na wapambe wake walitaka kuzileta Tarime. Wananchi wakifikia kiwango cha kwenda kupiga kura bila kujali vipigo na vitisho vya polisi - basi demokrasia ya nchi au eneo husika inahesabiwa kuwa inapanda.

Otherwise, mtizamo wako wa kutumia post zako zaidi ya ishirini zilizopita kutosema chochote but "kidumu cha mapinduzi" pia unaheshimika maana hii ni forum huru kinyume na mafisadi wengine wanavyodai kila siku kuwa JF sio huru

Mkuu Mwafrika wa Kike,
Nimekupata, lakini una ushahidi wowote kuwa Mtikila na Mbatia walitumiwa na CCM huko Tarime?
Umesema nimetuma post zaidi ya ishirini bila kusema chochote zaidi ya "Kidumu Chama Cha Mapinduzi", Je umesema kweli au umeandika ili kuwafurahisha wale mlio kwenye 'mrengo' unaofanana?
Hivi ndugu yangu, kila mwana CCM ni fisadi? maana umesema "... pia unaheshimika maana hii ni forum huru kinyume na mafisadi wengine wanavyodai kila siku kuwa JF sio huru". Kwa mujibu wa hii kauli yako kila mwana CCM ni fisadi. (hata mie umeniita fisadi).

Kumbuka kuwa Biblia inasema hivi: Eliya aliukimbia mkono wa Yezebeli.... akakimbia hadi jangwani, na tazama neno la Mungu likamjia, naye akamwambia, "Unafanya nini hapa, Eliya?" Eliya akajibu 'Nimeona wivu mwingi kwa ajili ya Bwana Mungu wa majeshi; kwa kuwa wana wa Israeli wameyaacha maagano yako, na kuzivunja madhabahu zako, na kuwaua manabii wako kwa upanga; NAMI NIMESALIA PEKE YANGU ... .... Neno la Mungu akamwambia: ..... .... "Nitajisazia katika Israeli watu elfu saba, kila goti lisilomwinamia Baali, na kila kinywa kisicho mbusu" (1Falme 19).

Baada ya kukuandikia hayo ningependa kukuarifu kuwa: - Mafisadi wako vyama vyote vya kisiasa.
Hata kama kuna mafisadi ndani ya CCM, sio Kila Mwana CCM ni fisadi.

Asante kwa mchango wako ambao haukuwa 'bias'.

 
Mkuu Mwafrika wa Kike,
Nimekupata, lakini una ushahidi wowote kuwa Mtikila na Mbatia walitumiwa na CCM huko Tarime?
Umesema nimetuma post zaidi ya ishirini bila kusema chochote zaidi ya "Kidumu Chama Cha Mapinduzi", Je umesema kweli au umeandika ili kuwafurahisha wale mlio kwenye 'mrengo' unaofanana?
Hivi ndugu yangu, kila mwana CCM ni fisadi? maana umesema "... pia unaheshimika maana hii ni forum huru kinyume na mafisadi wengine wanavyodai kila siku kuwa JF sio huru". Kwa mujibu wa hii kauli yako kila mwana CCM ni fisadi. (hata mie umeniita fisadi).

Kumbuka kuwa Biblia inasema hivi: Eliya aliukimbia mkono wa Yezebeli.... akakimbia hadi jangwani, na tazama neno la Mungu likamjia, naye akamwambia, "Unafanya nini hapa, Eliya?" Eliya akajibu 'Nimeona wivu mwingi kwa ajili ya Bwana Mungu wa majeshi; kwa kuwa wana wa Israeli wameyaacha maagano yako, na kuzivunja madhabahu zako, na kuwaua manabii wako kwa upanga; NAMI NIMESALIA PEKE YANGU ... .... Neno la Mungu akamwambia: ..... .... "Nitajisazia katika Israeli watu elfu saba, kila goti lisilomwinamia Baali, na kila kinywa kisicho mbusu" (1Falme 19).

Baada ya kukuandikia hayo ningependa kukuarifu kuwa: - Mafisadi wako vyama vyote vya kisiasa.
Hata kama kuna mafisadi ndani ya CCM, sio Kila Mwana CCM ni fisadi.

Asante kwa mchango wako ambao haukuwa 'bias'.


Ladslaus,

Nimepotea kabisa, sielewi unachosema hapa! Nimeshindwa kuona uhusiano kati ya unachomjibu Mwafrika wa Kike na hiyo nukuu uliyoweka hapa! Ingawa inawezekana ni kweli kuwa mafisadi wako katika vyama vyote vya siasa, mafisadi wanaotusumbua sasa na wanaotuumiza ni wale wanaoendelea kututawala kifisadi, walioko kwenye chama tawala kinachotoa sera, taratibu, mielekeo, na usimamizi wa rasilimali zetu, ambavyo vyote sasa pamoja na sisi wananchi tunaathirika na ufisadi huo. Hao mafisadi wa vyama vingine unaosema (kama wapo) ni "pilipili iliyoko shamba", haiwashi! Kwa hiyo hao walioko nje ya system hatuna shida nao, watashughulikiwa na wanachama wenzao huko. Sisi (kama taifa) tuna shida na wanaotuibia leo hii, kwa wizi wa kuaminiwa. Aliyeapa kutumikia nchi kwa uaminifu lakini sasa kageuka kiapo hicho, huyo ndiyo mbaya wetu. Ambaye hajachukua kiapo hicho, hatuna shida naye, lakini siku na yeye pia akipata nafasi hiyo kama atafanya ufisadi tutamshupalia pia kama tunavyofanya leo.
 
Ladslaus,

Nimepotea kabisa, sielewi unachosema hapa! Nimeshindwa kuona uhusiano kati ya unachomjibu Mwafrika wa Kike na hiyo nukuu uliyoweka hapa! Ingawa inawezekana ni kweli kuwa mafisadi wako katika vyama vyote vya siasa, mafisadi wanaotusumbua sasa na wanaotuumiza ni wale wanaoendelea kututawala kifisadi, walioko kwenye chama tawala kinachotoa sera, taratibu, mielekeo, na usimamizi wa rasilimali zetu, ambavyo vyote sasa pamoja na sisi wananchi tunaathirika na ufisadi huo. Hao mafisadi wa vyama vingine unaosema (kama wapo) ni "pilipili iliyoko shamba", haiwashi! Kwa hiyo hao walioko nje ya system hatuna shida nao, watashughulikiwa na wanachama wenzao huko. Sisi (kama taifa) tuna shida na wanaotuibia leo hii, kwa wizi wa kuaminiwa. Aliyeapa kutumikia nchi kwa uaminifu lakini sasa kageuka kiapo hicho, huyo ndiyo mbaya wetu. Ambaye hajachukua kiapo hicho, hatuna shida naye, lakini siku na yeye pia akipata nafasi hiyo kama atafanya ufisadi tutamshupalia pia kama tunavyofanya leo.

Mkuu Kithuku, "Eliya alifikiri kuwa amebaki mwenyewe mwema" lakini walikuwapo wengine.
Nimetaka kumwambia Mwafrika wa Kike kuwa Hata kama anaona/anajua kuwa kuna mafisadi ndani ya CCM, sio wote ni mafisadi, bali kuna wanachama wengine ambao sio mafisadi (Kama Mimi).

Mkuu Kithuku, kumbuka watani wetu "Kenya"; Wapinzani wakati huo wakiongozwa na Mwai Kibaki walikuwa wanamshtumu sana Moi na chama cha KANU katika mambo mengi; lakini walipoingia madarakani walionyesha wazi kuwa Ni afadhali ya Moi na KANU yake. Sikumbuki kama wakati wa Moi na KANU kuliwahi kutokea mauaji kama yaliyotokea baada ya uchaguzi wa Dec 27 2007 hapo Kenya.

Ninachoamini ni kuwa hata leo Chama chochote kikiingia madarakani kinaweza kuwa cha mafisadi mara mia ya CCM.


 
Mkuu Kithuku, "Eliya alifikiri kuwa amebaki mwenyewe mwema" lakini walikuwapo wengine.
Nimetaka kumwambia Mwafrika wa Kike kuwa Hata kama anaona/anajua kuwa kuna mafisadi ndani ya CCM, sio wote ni mafisadi, bali kuna wanachama wengine ambao sio mafisadi (Kama Mimi).
Mkuu Kithuku, kumbuka watani wetu "Kenya"; Wapinzani wakati huo wakiongozwa na Mwai Kibaki walikuwa wanamshtumu sana Moi na chama cha KANU katika mambo mengi; lakini walipoingia madarakani walionyesha wazi kuwa Ni afadhali ya Moi na KANU yake. Sikumbuki kama wakati wa Moi na KANU kuliwahi kutokea mauaji kama yaliyotokea baada ya uchaguzi wa Dec 27 2007 hapo Kenya.
Ninachoamini ni kuwa hata leo Chama chochote kikiingia madarakani kinaweza kuwa cha mafisadi mara mia ya CCM.


Ladslaus,

Pamoja na kwamba sikubaliani na mengi uliyosema hilo hitimisho maana yake ni kwamba tutakuwa tunacheza pata potea kwa kubadilisha uongozi. Sasa swali kwako ni hili, tubaki na huu uongozi ambao kwa hali zote umeoza ama tujaribishe bahati yetu kwa uongozi mpya. Tukiweza kujenga tabia ya kubadilisha uongozi kila ukiboronga, hao watakaokuja wapya watajitahidi wakijua wazi kabisa hatma yao wasipotimiza wajibu. Hii ni kawaida duniani kote kwa nchi makini na ndio njia pekee ya kupata utawala bora.

Kuna wanaCCM wanaoona huu ubovu na wangependa uongozi ndani ya chama ndio ubadilike kama navyosema FMES. Sawa lakini wanasahau kuwa wamekuwa wakibadilisha uongozi ndani ya chama kila baada ya miaka mitano, lakini kila mara uongozi unaofuatia umekuwa mbovu zaidi. Hii maana yake nini - ni kuwa the party is rotten to the core. Tumesema mara nyingi humu kuwa huwezi kuogelea kwenye tope ukatoka msafi, na mimi naongezea kuwa huwezi kuishi kwenye uvundo usinuke.

UFISADI kwenye CCM imekuwa way of life ikilindwa na dola. Hii ndiyo maana kuna sauti za wanaCCM wanaomtetea JK na kusema kwamba kazungukwa na viongozi wanaompotosha. Jambo hili haliingii akilini na ukweli ulio sahihi ni kuwa CCM haisafishiki tena - kansa yake imeenea mwili mzima. Ambao hawajaathirika hawawezi kuendelea kubaki humo kama alivyoonyesha mfano Kijana Waitara. Ladslaus, muunge mkono Waitara kwa kuipa mgongo CCM na kupaaza sauti ya bye, bye na tufungue ukurasa mpya.
 
Unataka rais wa nchi awe anaenda kwenye kampeni za chaguzi ndogo za wabunge?

Binafsi naona itakuwa kupoteza muda. Kuna akina Makamba na Msekwa labda na mawaziri lakini sio rais wa nchi.

Nafikiri kama sikosei rais wa mwisho kwenda kwenye chaguzi ndogo alikuwa Mkapa hiyo 1998 kule Temeke kwa Mrema na bado walishindwa.

Mkuu Mtanzania,

Heshima yako bro, angalia kumbu kumbu mkuu Rais wa jamhuri alienda Kiteto kwenye kampnei ambazo zilifanyika siku chache bada ya kutolewa kwa Lowassa, sasa kilichomshinda hapa kwenda Tarime ni nini hasa?

Katika kikao kimoja cha siri jana na kutathmini matokeo ya Tarime nasikia amekubali kwua it is aboput time sasa Makamba should go, maana yeye kama mwenyekiti hana uwezo wa kumtoa Makamu.

Chama kinapogombea, mwenyekiti wa kile chama ni lazima awepo hakuna excuse hapo!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom