Uchaguzi 2025 Watanzania tupige kura 5

Uchaguzi 2025 Watanzania tupige kura 5

Malata Junior

JF-Expert Member
Joined
Nov 29, 2011
Posts
3,104
Reaction score
2,550
Heshima kwenu wakuu!

Kama wengi tunavyojua watanzania tunatarajia kufanya uchaguzi wa serikali za mitaa mwaka 2024 na uchaguzi mkuu mwaka 2025.

Kwa kujifunza kutokana na uchaguzi mkuu uliomalizika nchini Kenya hivi karibuni ni wakati sasa kwa Tanzania kuendesha uchaguzi wa serikali za mitaa na uchaguzi mkuu kwa pamoja, yaani tuchague. Rais, mbunge, diwani, mwenyekiti wa mtaa/Kijiji na mwenyekiti wa kitongoji.

Ikiwezekana pia wabunge wa viti maalumu tuwachague sisi WANANCHI badala ya kuteuliwa na vyama.Kama Kenya wameweza kupiga kura 6 kumchagua Rais, Gavana, Seneta, mbunge na mwakilishi wa wanawake kwa nini sisi tushindwe?

Kwa kufanya hivyo tutakuwa tumepunguza gharama za uchaguzi kwa kiasi kikubwa na pia uchaguzi Tanzania utakuwa unasimamiwa na chombo kimoja ambayo ni tume ya Taifa ya uchaguzi badala ya uchaguzi wa serikali za mitaa kusimamiwa na serikali kupitia TAMISEMI.
 
Tanzania kuendesha uchaguzi wa serikali za mitaa na uchaguzi mkuu kwa pamoja,yaani tuchague Rais,mbunge,diwani,mwenyekiti wa mtaa/Kijiji na mwenyekiti wa kitongoji.Ikiwezekana pia wabunge wa viti maalumu tuwachague sisi WANANCHI badala ya kuteuliwa na vyama.Kama Kenya wameweza kupiga kura 6 kumchagua
Muundo na utaratibu wa Uchaguzi Tz unahitaji mabadiriko makubwa, ili kufanikisha kuwa na uchaguzi HURU na HAKI.
 
Umewaza vyema sana, lakini tujiulize kama mpaka sasa serikali imebaki na uchaguzi wa serikali za mitaa muda uliobaki utawatosha hao nec kuandaa uchaguzi wa serikali za mitaa ikiwa watapewa hilo jukumu?
Maana muda uliobaki ni mdogo ukilinganisha na maandalizi ya kazi yenyewe.
Marekebisho ya sheria na kanuni zake...
Mabiresho ya uendeshaji wa uchaguzi na mifumo yake nk.
 
Ikiwezekana pia wabunge wa viti maalumu tuwachague sisi WANANCHI badala ya kuteuliwa na vyama.Kama Kenya wameweza kupiga kura 6 kumchagua Rais, Gavana, Seneta, mbunge na mwakilishi wa wanawake kwa nini sisi tushindwe?
Uwachague viti maalum kwenda kumwakilisha nani?! Hopeless kabisa wewe.
 
Back
Top Bottom