Uchaguzi mkuu NCCR Mageuzi

Uchaguzi mkuu NCCR Mageuzi

Waridi

JF-Expert Member
Joined
Mar 30, 2008
Posts
1,025
Reaction score
172
WanaJF,
Hii ni kutaka kukuhabarisheni kwamba ndani ya chama cha NCCR-Mageuzi kinachondelea kwa sasa ni hatua za mwisho mwisho za kuhitimisha mchakato wa uchaguzi mkuu wa viongozi wa kitaifa wa chama.
Kama ilivyo ada, kila baada ya miaka mitano unafanyika uchaguzi wa namna hii.
Itakumbukwa kwamba hadi sasa NCCR imekwisha kuwa chini ya uongozi wa wenyeviti wanne tofauti kwa nyakati tofauti
  • alianza Mhe.Mabere Marando
  • akafuatia Mhe.Agustine Mrema
  • akaja Mhe.Aidari Maguto(marehemu)
  • na wa sasa Mhe.James Mbatia

Katika uchaguzi huu, habari za ndani zinatonya kwamba wanaowania Uenyekiti ni wawili (sijajua kama wote watapitishwa)

Vile vile yaelekea nafasi nyinginezo kv. makamu mwenyekiti,katibu mkuu,naibu katibu mkuu,mweka hazina zitakamatwa na sura mpya kabisa kwa sababu wengi wa waliogomea nafasi hizo na wenye mwelekeo wa kushinda si wale waliokuwa wakizishikiria.
Wachunguzi wa mambo wanasema, mwelekeo huo ni ishara kwamba chama hiki kimepania kujijenga upya kabisa, ya kale yatapita...

Tega sikio, soon nitakuhabarisheni nani kang'olewa, nani kashinda, nani kawaje.
Duru zinasema mtanange huu ni Jumapili ya juma hili.
 
Tunashukuru kwa taarifa mkuu Waridi,

Vipi hakuna nafasi ambazo wadau hapa wanaweza kurusha kete zao au "Too late to catch the train?"
 
Mkuu,
Pazia la kurejesha fomu litafungwa soon, any interested mdau aseme nimuunganishe kwa mkuu wa idara husika, kuna kitu kama 60 hours to go
 
Sina hakika kama wameishachelewa,
wamechelewa kufanya nini?
na kumbe nani kawahi, wapi?

Yamkini unazungumzia lengo la kila chama cha siasa... kuongoza dola?
 
Mbona mambo yao yamekuwa ni kimyakimya sana?

Kama waandishi wa habari wako hapa JF watusaidie kujibu hilo swali, maana nijuavyo mimi NCCR kilitangaza wazi mara kadhaa kupitia press release kwamba kiko katika mchakato wa uchaguzi mkuu, na hata wagombea kadhaa baada ya kuchukua fomu walijieleza mbele ya waandishi wa habari.
Vile vile ofisi ya katibu mkuu ilisambaza waraka nchi nzima kuwataarifu wanachama wajitokeze kugombea na wamejitokeza.
Nahofu watu wasianze kudhani iko namna ya usiri, hata kama ingekuwepo ni vema sasa nimekuleteeni taarifa hizi. Kama nilivyodokeza nitakuhabarisheni developments time after time.
 
Ndio maana ya uchaguzi. Huenda wakaja watu wenye speed kali na wenye mvuto.

Chaguzi zenyewe za kibongo mkuu?Watu wanapanga safu kabla hata ya uchaguzi mwenyekiti mpaka wajumbe wanajulikana.
Subiri hao nccr wataje matokeo utaona sura ni zilezile tu Mbatia,Mvungi...
 
Vipi MBATIA anatetea kiki chake?
 
The question ni kuwa kitakuwa chama kweli cha siasa, au kitaendelea kuwa kile kile kinachotumiwa na kina Marando ku-weaken na ku-destabilize opposition, au kufuga majasusi wanaokiyumbisha kila kukicha? Kama wameamua kufanya mambo kimya kimya ili kukisafisha na kutowapa nafasi wanaokiharibu well and good, tusubiri nini kitaendelea.
 
Wakuu,
Kutoka jikoni NCCR naambiwa jua la kurejesha fomu limekuchwa na wafuatao ndio fomu zao ziko mezani kuwania nafasi kuu saba za uongozi wa chama.

Mwenyekiti
  1. John Bula Dodo
  2. James Francis Mbatia

Makamu Mwenyekiti- Bara
  1. Mama Rakia Abubakari Hassan
  2. Hashim Rungwe
Makamu Mwenyekiti - Zanzibar
  1. Haji Hambari Khamis

Katibu Mkuu
  1. Sam Ruhuza

Naibu Katibu Mkuu- Bara
  1. Raurent Tara
  2. Joseph Serasini

Naibu Katibu Mkuu- Zanzibar
  1. Musa Kombo Musa
  2. Ali Juma Omari

Mweka hazina
  1. Mama Mariam Mwakingwe
  2. Sebastian Thomas
Majina haya yatahakikiwa kesho katika kikao cha halmashauri kuu ya taifa kabla ya kupelekwa mkutano mkuu, a day later
 
The question ni kuwa kitakuwa chama kweli cha siasa, au kitaendelea kuwa kile kile kinachotumiwa na kina Marando ku-weaken na ku-destabilize opposition, au kufuga majasusi wanaokiyumbisha kila kukicha? Kama wameamua kufanya mambo kimya kimya ili kukisafisha na kutowapa nafasi wanaokiharibu well and good, tusubiri nini kitaendelea.

Angalia list ya wagombea, no Marando, no Mvungi, No Mwaiseje... katika safu ya juu ya uongozi unaomaliza muda wake, ni wawili tu wamegombea tena... sawa na 28.5%, obviously safu itakuwa na upya.
 
Wakuu,
Kutoka jikoni NCCR naambiwa jua la kurejesha fomu limekuchwa na wafuatao ndio fomu zao ziko mezani kuwania nafasi kuu saba za uongozi wa chama.

Mwenyekiti
  1. John Bula Dodo
  2. James Francis Mbatia

Makamu Mwenyekiti- Bara
  1. Mama Rakia Abubakari Hassan
  2. Hashim Rungwe
Makamu Mwenyekiti - Zanzibar
  1. Haji Hambari Khamis

Katibu Mkuu
  1. Sam Ruhuza

Naibu Katibu Mkuu- Bara
  1. Raurent Tara
  2. Joseph Serasini

Naibu Katibu Mkuu- Zanzibar
  1. Musa Kombo Musa
  2. Ali Juma Omari

Mweka hazina
  1. Mama Mariam Mwakingwe
  2. Sebastian Thomas
Majina haya yatahakikiwa kesho katika kikao cha halmashauri kuu ya taifa kabla ya kupelekwa mkutano mkuu, a day later

Katika hii miaka mitano inayoishia, Mbatia ameshindwa kuinusuru NCCR.
Chama kimeendelea kudorora kila siku, sasa huyo John Bula mbona mgeni masikioni mwangu katika duru za kisiasa, ataweza kweli kuinusuru NCCR?
NCCR inatakiwa kurudi kwenye chati kama zamani ili kuongeza ushindani na kutanua wigo wa demokrasia.Kwahiyo basi kama Mbatia atashinda tena anwajibika kubadilisha mikakati ya kukiongoza chama chake ili kiweze kushindana badala ya kusindikiza ama kutumiwa na mahasidi kuivuruga demokrasia.
Mi naamini kabisa kuwa mwenyekiti ndiye anayetoa taswira ya chama husika.
Au Bula amewekwa kumsindikiza Mbatia?Kwangu mimi bado sioni kama Bula atatoa ushindani wa kutosha kwa Mbatia.Labda kama mimi ndiye simfahamu vizuri bw.Bula naomba kufahamishwa.

BTW mbona mgombea urais mwanasheria Edmund Sengondo Mvungi hajawania nafasi yeyote?au yeye ni maalum na uraisi tuuu!!!????
 
Katika hii miaka mitano inayoishia, Mbatia ameshindwa kuinusuru NCCR.
Chama kimeendelea kudorora kila siku, sasa huyo John Bula mbona mgeni masikioni mwangu katika duru za kisiasa, ataweza kweli kuinusuru NCCR?
NCCR inatakiwa kurudi kwenye chati kama zamani ili kuongeza ushindani na kutanua wigo wa demokrasia.Kwahiyo basi kama Mbatia atashinda tena anwajibika kubadilisha mikakati ya kukiongoza chama chake ili kiweze kushindana badala ya kusindikiza ama kutumiwa na mahasidi kuivuruga demokrasia.
Mi naamini kabisa kuwa mwenyekiti ndiye anayetoa taswira ya chama husika.
Au Bula amewekwa kumsindikiza Mbatia?Kwangu mimi bado sioni kama Bula atatoa ushindani wa kutosha kwa Mbatia.Labda kama mimi ndiye simfahamu vizuri bw.Bula naomba kufahamishwa.

BTW mbona mgombea urais mwanasheria Edmund Sengondo Mvungi hajawania nafasi yeyote?au yeye ni maalum na uraisi tuuu!!!????

Mkuu Mwita,
Sidhani kutofahamika kwa Bula kunaweza kuwa sababu pekee ya kumwangusha, itategemea competence yake. Aidha kama unavyosema, endapo ni kweli Mbatia hakufanya vizuri basi Bula anaweza kutumia upenyo huo kushinda.
Kuhusu Mvungi, sidhani kama ana umaalum wa kugombea urais, usishangae akijitokeza mtu/watu wapya kabisa kuwania urais kwa tiketi ya NCCR come 2010
 
sasa huyo John Bula mbona mgeni masikioni mwangu katika duru za kisiasa, ataweza kweli kuinusuru NCCR?
Ni kweli huyu jamaa ni mgeni hata kwangu mimi katyika siasa za upinzani. Au amewekwa kama kanyabwoya kuonyesha kuwa Mbatia alikuwa na mshindani?
 
Ni kweli huyu jamaa ni mgeni hata kwangu mimi katyika siasa za upinzani. Au amewekwa kama kanyabwoya kuonyesha kuwa Mbatia alikuwa na mshindani?

Mimi sioni tatizo katika upya wa Bula, badala yake naona ishara njema kwani mtu mpya kajitokeza na kwa mantiki hiyo huenda ana jipya.
Kwa taarifa nilizo nazo Bula ni candidate anayetokea upcountry, ni changamoto hasa kwa Mbatia ambaye 'katokea' Uholanzi kuja kutetea kiti chake.
Nani kamuweka nani hapo sijui na sidhani. kila mmoja wao kajaza fomu kwa wakati wake.
 
Mimi sioni tatizo katika upya wa Bula, badala yake naona ishara njema kwani mtu mpya kajitokeza na kwa mantiki hiyo huenda ana jipya.
Kwa taarifa nilizo nazo Bula ni candidate anayetokea upcountry, ni changamoto hasa kwa Mbatia ambaye 'katokea' Uholanzi kuja kutetea kiti chake.
Nani kamuweka nani hapo sijui na sidhani. kila mmoja wao kajaza fomu kwa wakati wake.

Si tatizo wiapo siasa zetu zisingekwua na mizengwe. katika mfumo wa siasa safi, jambo kama hili ni zuri tu. lakini katika mfumo huu tulioujenga wa mizengwe, inakuwa vigumu sana kuamini kuwa mwenyekiti wa chama wa wilaya anaweza kumshinda mwenyekiti wa taifa anayetetea kiti chake.
 
Mkuu Mwita,
Sidhani kutofahamika kwa Bula kunaweza kuwa sababu pekee ya kumwangusha, itategemea competence yake. Aidha kama unavyosema, endapo ni kweli Mbatia hakufanya vizuri basi Bula anaweza kutumia upenyo huo kushinda.
Kuhusu Mvungi, sidhani kama ana umaalum wa kugombea urais, usishangae akijitokeza mtu/watu wapya kabisa kuwania urais kwa tiketi ya NCCR come 2010

Waridi,
tunazungumzia nafasi ya mwenyekiti wa taifa wa chama cha siasa cha NCCR, nafasi ambayo ni kubwa na nyeti.Itawezekana vipi mtu asiyefahamika kabisa katika ulingo wa siasa, tena siasa zenyewe hizi za bongo aweze kumwangusha mwenyekiti anayetetea nafasi yake?manake usisahau kuwa wapiga kura ni watanzania hawa tunaowajua.Kama kweli ni wengi hatumjui huyo bura hata hao wapiga kura wa NCCR hapana shaka watakuwa hawamjui, sasa watawezaje kumpa uenyekiti mtu wasiyemfahamu?Je alishawahi kuwa kiongozi wa kisiasa kwenye ngazi yoyote,kama una ufahamu wowote juu ya hili nisaidie.
Hiyo competence unayoizungumzia inawezaje kuthibitishwa?nani atakayeithibitisha?
au unazungumzia competence kwa upande wa kitaaluma au mi sijakuelewa?hebu nisaidie kuifahamu hiyo competence unayoizungumzia.
 
wanajf,
hii ni kutaka kukuhabarisheni kwamba ndani ya chama cha nccr-mageuzi kinachondelea kwa sasa ni hatua za mwisho mwisho za kuhitimisha mchakato wa uchaguzi mkuu wa viongozi wa kitaifa wa chama.
Kama ilivyo ada, kila baada ya miaka mitano unafanyika uchaguzi wa namna hii.
Itakumbukwa kwamba hadi sasa nccr imekwisha kuwa chini ya uongozi wa wenyeviti wanne tofauti kwa nyakati tofauti
  • alianza mhe.mabere marando
  • akafuatia mhe.agustine mrema
  • akaja mhe.aidari maguto(marehemu)
  • na wa sasa mhe.james mbatia

katika uchaguzi huu, habari za ndani zinatonya kwamba wanaowania uenyekiti ni wawili (sijajua kama wote watapitishwa)

vile vile yaelekea nafasi nyinginezo kv. Makamu mwenyekiti,katibu mkuu,naibu katibu mkuu,mweka hazina zitakamatwa na sura mpya kabisa kwa sababu wengi wa waliogomea nafasi hizo na wenye mwelekeo wa kushinda si wale waliokuwa wakizishikiria.
Wachunguzi wa mambo wanasema, mwelekeo huo ni ishara kwamba chama hiki kimepania kujijenga upya kabisa, ya kale yatapita...

Tega sikio, soon nitakuhabarisheni nani kang'olewa, nani kashinda, nani kawaje.
Duru zinasema mtanange huu ni jumapili ya juma hili.


mambo ya ngoswe!............................................
 
Back
Top Bottom