Uchaguzi serikali za mitaa: Ambao hatujajiandikisha na hatuna mpango wa kujiandikisha tukutane hapa

Uchaguzi serikali za mitaa: Ambao hatujajiandikisha na hatuna mpango wa kujiandikisha tukutane hapa

Unajua nn..hamna serikali iloharibu maana kamili ya upigaji kura kama hii ya sasa.

Watu wamechoka, ma walichoshwa na tabia zilizotokea za chaguzi ndogondogo zilizopita hapo nyuma.

Watu hawaoni maana tena, maana wapige wasipige, ..hamna mtu atakayetangaza matokeo yasomfurahisha mkuu wa wilaya,wamkoa, Rais.

Nifanyeje sasa?????
Wacha tule buyu tu
 
Yaani napata wapi ujasiri na ndevu zangu kwenda kuandika jina langu eti nikapige kura??? Nikaangalie pambano ambalo mmoja kafungwa kamba mikoni na mmoja anapiga tu eti tunalazimishwa kumshangilia huyu mshindi wa kupangwa.
Kwenye hili Rais ajue yeye ndio chanzo na hatutajitokeza hata watangaze mpaka usku wa manane sisi hatutaenda na hata watufungulie mashtaka hatutaenda.
Haha mkuu huendi hata kwa fimbo
 
Mkuu kwa watu wenye akili timamu na wanao penda justice and democracy kwa siasa zilivyo sasa huwezi kwenda kupiga kura.
Na hata kwaka ujao ni wachache sana watapiga kura.

Hii iwe fundisho kwa watawala kuwa na justice pia waheshimu mawazo ya wananchi . Haiwezekani uwaambie wananchi waombe msamaha kwa kuchagua upinzani au mtu mwingine usie mtaka wewe kiongoz pia uminywaji wa democracy unaoendelea ni vema tu ili kusiwe na vita vya kuchukiana kuumizana tuamue kurudisha utawala wa chama kimoja maana nadhani hii ya vyama vingi ukweli imetushinda.

Mkuu mbaga jr, siasa sio uhasama ila nikupata platform ya wananchi kuelezea hisia zao kwanini wamemchagua huyu na wamemwacha huyu ili itusaidie ku learn theough mistakes lakini inapogeuka kuwa vita na kuumizana na kutoana uhai hapo tunadhani ni vema waungwana kutothubutu hata kusogea kujiandikisha.
Asipokuelewa basi tena
 
Naona uvivu hata nikijiandikisha sidhani kama kura yangu itasaidia maana matokeo yameshapangwa. kwanza kura zitapigwa siku moja kabla ya wengine wote hapo ndio kuna ukakasi siwezi piga kura
Aisee hadi wewe
 
Mimi sitajisumbua tena maana nina Passport na NaID
Na mvua hizi uache kulala zako ukapange foleni ya kupiga kura ambayo kwa vyovyote tu itapuuzwa
 
Yaani umeleta uzi jioni hii nagongewa odd. Naulizwa kama nimejiandikisha. Nikawajibu ndio. Wakasepa.
Aisee ndio wanapita nyumba kwa nyumba. Mimi wakiniuliza nawaambia sijajiandikisha na sitaki, nione watafanyaje
 
Mimi hata wazo tu sina.
Nipoteze muda kujiandikisha na kwenda kupiga kura ilhal matokeo yameshapangwa?
Bora nilale aiseh!
 
Wakajiandikishe tu maana Sjaona kipya ntakachogundua...
Maana mshindi tayari anajulikana na hata akichaguliwa tofauti baada ya miez sita anaunga mkono juhudi.
Wewe nilikuona jana kwenye kituo cha kuandikishia
 
mimi kilichonivunja moyo ni kauli ya rais aliposema haya wakat ana waapisha wakurugenz... NAKULIPA MSHAHARA NAKUPA GARI ZURI HALAFU UKATANGAZE WAPINZANI WAMESHINDA..... kauli hii umenifanya kuacha kujiandikisha tena napiga kampeni ya waziwazi kuhamasisha watu wasipige kura Kama yeye alivyowaambia Watanzania waziwazi kuwa wasitangaze wapinzani wameshinda
 
Huku tukielezana kwa nini hatujajiandikisha. Kwa upande wangu mimi naona uvivu....hivyo tu
Wale 'wazalendo' pia karibuni
Matokeo yanajulikana kwa hiyo kwenda kujiandikisha Ni kupoteza muda tu
 
Wote ambao hamtajiandikisha mpaka kufikia kesho mtachukuliwa hatua kali......Ice cream za ukwaju nyie.....
 
Back
Top Bottom