Uchaguzi wa 2020 ulivyoweka vibaraka wa Mwigulu Jimbo la Iramba

Uchaguzi wa 2020 ulivyoweka vibaraka wa Mwigulu Jimbo la Iramba

Lyambalyetu

JF-Expert Member
Joined
Apr 6, 2021
Posts
278
Reaction score
255
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba Innocent Msengi ni ndugu na rafiki wa karibu wa Dr. Mwigulu. Huyu bwana hujinasibu alimaliza kidato cha nne. Lakini ukweli ukweli hatakiwi kujisema hivyo kwa kuwa alikuwa darasani na kakangu mimi na aliambulia Daraja la Sifuri - kitu ambacho huwa hakisemi kabisa.
Dr. Mwigulu alimtumia huyu kuiba kura na wakajisahau hadi kura za JPM akaziiba nyingi kuliko hata idadi ya waliopiga kura. Ajabu sana! Huyu bwana hakutakiwa kuwa Mwenyekiti wa Halmashauri yetu kwa sababu kwanza huwa hawezi hata kuwasilisha hoja vizuri, hana weledi wa kusimamia vikao vya madiwani wetu na hata uwezo wa kujibu baadhi ya hoja hana kabisa. Walifanya vigisu na Mwigulu wake wakaengua wagombea wote wazuri ambao pengine wangetokea watu wazuri wa kuongoza Halmshauri yetu. Mwigulu kaweka Timu yake pale akifikiri kuwa 2025 atapenya kirahisi. Mwenyekiti wa CCM Wilaya ambaye pia anatokea nyumbani kwao Mwigulu tayari ameshachokwa - huyu bwana Samweli ndiyo alikuwa kinara wa wizi wa kura 2020. Alishiriki moja kwa moja kutengeneza kura za Mwendazake na kupanga timu ya madiwani wafuata upepo.
Madiwani wa Viti Maalumu karibia wote amewaweka yeye na Mwigulu kuanzia yule Dayana Masangya, Esther Yonah, nk.
Kwa kweli kwa hali ilivyo kwa sasa Iramba haina uongozi makini wa kisiasa kwa sababu ni uongozi uliowekwa na Dr. Mwigulu kwa ajili ya kuutumia kama daraja la kuvukia ili kutimiza ndoto zake. Hakuna uwezekano wowote kama Iramba itasonga mbele sasa.
Rai yangu ni kumsihi Dr. Mwigulu kutubu na kujutia wizi alioufanya wakati wa Uchaguzi wa Mwaka 2020 - amepata nafasi aitumie vizuri na kuwaletea maendelea WanaIramba na isiwe ubabaishaji kama ambavyo hawa madiwani wameanza kuonesha. Mwigulu anaenda kuongoza miaka 15 kama Mbunge lakini kwa jimbo letu hamna lolote la maana ambalo kalifanya ambalo linampa uhalali wa kuendelea kuongoza jimbo hili. Ameshachokwa na ndiyo maana mbinu imekuwa ni kuiba kura tu. Mwaka 2025 hatukubali ijirudie labda atumie uchawi!
 
Nikupe namba za mwigulu +255688008888, hizo mwambie moja kwamoja? Vile vile mbona hukusema mapema wakati na baada ya uchaguzi au unaleta umbea tu baada ya mwamba kupasuka.
 
Huu si umbea bali halisi,uchaguzi 2020 ulijaa wizi ambao haujawahi kutokea tangu kuanzishwa taifa la Tanzania.
Na historia haiongopi. Wanairamba tunajua jinsi viongozi hawa walivyong'ang'aniza kujipa nafasi ya kutuongoza. 2025 hata mapanga tutakatana tu!
 
+255688008888
Usifikiri kinachoandikwa ni uzushi mie kakangu mwenyewe kashiriki kwenye huo wizi wa kura kwa hiyo si uwongo. Mtu anayeiba uchaguzi ukimwambia waziwazi hata kukuua anaweza akafanya. We kula hela zake Mwigulu ulale!
 
mwacheni ale bata,uzuri sasa ndoto za urais hazipo tena.

mkitaka kumung'oa mwigulu,ombeni apokonywe uwaziri na mchakato wa kura za maoni uwe fair.

kinyume na hapo,we msubirie labda 2030!
 
Mm kila siku naandika kwamba 2020 kulikuwa na wizi wa kura
1. Wasimamizi wa Vituo walivifungua saa 9 alfajir na hapo alianza kumpigia kura mwendazake na madiwani na wabunge.
2. Pale ofisi ya ccm vijana waliitwa wale wasiojielewa hapo walipewa kura na kupiga ndiyo kwa magufuli na viongozi wengine wa ccm waliahidiwa 5000 hawajapewa mpaka leo.
ASANTE MUNGU KWA KUTUTENDEA MAAJABU YAKO. HATUNA CHA KUKULIPA ILA KUKUSHUKURU EE BWANA
 
mwacheni ale bata,uzuri sasa ndoto za urais hazipo tena.

mkitaka kumung'oa mwigulu,ombeni apokonywe uwaziri na mchakato wa kura za maoni uwe fair.

kinyume na hapo,we msubirie labda 2030!
Kwa 2025 kama hali itaendelea hivi jimboni basi nina uhakika anatolewa hata kama ni kwa mapanga! Kikubwa labda achukue hatua sasa afanye cha kumpa legacy kwa wananchi wa Iramba! Ninasikia sikia kuwa Jimbo hilo linaweza likagawanyishwa!
 
Mm kila siku naandika kwamba 2020 kulikuwa na wizi wa kura
1. Wasimamizi wa Vituo walivifungua saa 9 alfajir na hapo alianza kumpigia kura mwendazake na madiwani na wabunge.
2. Pale ofisi ya ccm vijana waliitwa wale wasiojielewa hapo walipewa kura na kupiga ndiyo kwa magufuli na viongozi wengine wa ccm waliahidiwa 5000 hawajapewa mpaka leo.
ASANTE MUNGU KWA KUTUTENDEA MAAJABU YAKO. HATUNA CHA KUKULIPA ILA KUKUSHUKURU EE BWANA
Mwenyezi Mungu atawageukia hata hawa akina Mwigulu kwa matendo yao ya 2020 pamoja na kupewa UWaziri - mpaka mitano hii ijayo atakuwa ameshawageukia hakika na tutaona utukufu wake!
 
Usifikiri kinachoandikwa ni uzushi mie kakangu mwenyewe kashiriki kwenye huo wizi wa kura kwa hiyo si uwongo. Mtu anayeiba uchaguzi ukimwambia waziwazi hata kukuua anaweza akafanya. We kula hela zake Mwigulu ulale!
Nipo mbarali nakula viazi vitamu na wali tu hata sijui Jimbo lenu linafananaje.
 
Mwigulu katajirika akiwa kwenye siasa,


2022 atapanga timu hatari itakayombeba 2025!


Yupo tayari kuwaandaloa m100 ili awapange mwakani.


Atawapoteza mkimletea shobo,
 
Mwigulu katajirika akiwa kwenye siasa,


2022 atapanga timu hatari itakayombeba 2025!


Yupo tayari kuwaandaloa m100 ili awapange mwakani.


Atawapoteza mkimletea shobo,
Mwenyezi Mungu yupo - Mwendazake aliliweka hadi Jeshi kwapani lakini wapi bhana!
 
Mm kila siku naandika kwamba 2020 kulikuwa na wizi wa kura
1. Wasimamizi wa Vituo walivifungua saa 9 alfajir na hapo alianza kumpigia kura mwendazake na madiwani na wabunge.
2. Pale ofisi ya ccm vijana waliitwa wale wasiojielewa hapo walipewa kura na kupiga ndiyo kwa magufuli na viongozi wengine wa ccm waliahidiwa 5000 hawajapewa mpaka leo.
ASANTE MUNGU KWA KUTUTENDEA MAAJABU YAKO. HATUNA CHA KUKULIPA ILA KUKUSHUKURU EE BWANA
Kama unaushahidi kura ziliibiwa mbona hujasema tangu mwanzo au mgombea aliyeshindwa mbona hajaenda Mahakamani kushitaki ili matokeo yatenguliwe?
 
Back
Top Bottom