Uchaguzi wa Kenya: Kilichokataliwa kilikuwa bora zaidi kuliko kilichotarajiwa kuwa bora

Uchaguzi wa Kenya: Kilichokataliwa kilikuwa bora zaidi kuliko kilichotarajiwa kuwa bora

eliakeem

JF-Expert Member
Joined
May 29, 2009
Posts
17,214
Reaction score
15,853
Ikumbukwe kuwa huu ni uchaguzi wa marudio baada ya ule wa kwanza kutupiliwa mbali na mahakama baada ya kuona ya kuwa uchaguzi huo ulikuwa na kasoro nyingi mno.

Baada ya kufuta ule uchaguzi wa kwanza, jambo lililotegemewa ni kuwa uchaguzi wa marudio ungekuwa na marekebisho makubwa sana kutokana makosa yaliyobainishwa kwenye ule uchaguzi wa kwanza. Lakini kilichoonekana wazi ni kwamba kasoro zilizojitokeza ni nyingi. Maswali ya kujiuliza kwenye uchaguzi wa marudio:
Kenya imeenda mbele au imerudi nyuma katika kutatua kasoro zilizojitokeza kwenye uchaguzi uliopita?
Kupitia uchaguzi huu wa marudio, demokrasia ya Kenya imesonga mbele au imerudi nyuma?
Je kuna nafasi kwa wale wanaohisi kuhujumiwa kwenye uchaguzi wa marudio kurudi mahakamani?
Kuna kila dalili ya kuwa rais Uhuru hatakubaliwa baadhi ya maeneo ya nchi, hilo litatatuliwa vipi?
Uhuru Kenyatta atafanya nini kudumisha umoja wa kitaifa?

Kenya yagawika ikielekea uchaguzi mpya wa Rais Okt 26 | Matukio ya Afrika | DW | 23.10.2017
 
Acha wakome wameyatengeneza weenyewe

Tuna shida sana na hizi demokrasia za kukopa (loan democracy) toka kwa wazungu.
Hiyo ni kama mitihani ya vyuo vya ulaya inayoitwa re-exams, ambayo kila mtu huruhusiwa kufanya, hata usipofeli, ili kuboresha alama ulizopata kwenye mtihani wa kwanza. Sasa nyakati nyingine mwanafunzi anaweza apate alama chache kuliko alizopata mtihani wa kwanza. lakini uzuri wake ukipata alama ndogo, basi zile nyingi za mtihani wa kwanza zinabaki.

Hicho ndicho kilichotokea Kenya, kwenye re-exam wamepata alama chache zaidi kuliko alama walizopata mtihani wa kwanza. Katika maana ya kwamba uchaguzi wa awali ulikidhidhi vigezo vingi vya uchaguzi kuliko uchaguzi wa marudio ambao umefanyika leo tarehe 26/Oktoba/2017.
 
Nimepatwa na 'deja vu' kwa wanaoelewa naona kama kuna siku masaa kama haya niliona uzi kama huu hapa hapa jf. Ni kama ndoto yaani hata hii comment ninayoandika naikumbuka. Dah.
 
Kuna kituo nimeona kina kuku tu.
Halafu kuna county nne za magharibi ambazo uchaguzi umesimamishwa kutokana na vurugu, hivyo pengine matokeo ya urais yanaweza yasitangazwe mpaka by election ya hizo county.
Very sad.
 
Nimepatwa na 'deja vu' kwa wanaoelewa naona kama kuna siku masaa kama haya niliona uzi kama huu hapa hapa jf. Ni kama ndoto yaani hata hii comment ninayoandika naikumbuka. Dah.

Usikurupuke bwana mdogo, organise your mind before you attemp to do anything in here.
 
52eb2f18964b233e0594dd5018db2f0a.jpg
 
Mleta uzi hebu tusaidieni pia kuorodhesha hizo kasoro ukiacha azimio la NASA kususia, changamoto ya mvua na vurugu maeneo ya NASA.
 
Hongera Rais Mteule Uhuru Muigai Kenyatta, PhD
 
Nimepatwa na 'deja vu' kwa wanaoelewa naona kama kuna siku masaa kama haya niliona uzi kama huu hapa hapa jf. Ni kama ndoto yaani hata hii comment ninayoandika naikumbuka. Dah.

Kwa hiyo wewe ni 'clairvoyant' eeh au ndo mpaka kwa wanaoelewa tu
 
Back
Top Bottom