Cute Wife
JF-Expert Member
- Nov 17, 2023
- 1,906
- 5,000
Wakuu,
UPDATE: Mwabukusi ashinda Urais TLS kwa kura 1274
Jumla ya kura: 2218
Kura zilizoharikika: 3
1. Boniface Mwabukusi - 1274
2. Sweetbert Nkuba - 807
3. Kapteni Ibrahim Bendera - 58
4. Paul Kaunda - 51
5. Emmanuel Muga - 18
6. Revocatus Kuuli - 7
=====
UPDATE saa nne usiku: Tundu Lissu atoa shukrani kwa mawakili wenzake kwa sapoti waliyompa kipindi chote alichokuwa kwenye matatizo (baada ya kushambuliwa na watu wasiyojulikana. Atoa hoja kuhusu wamasai wa Ngorongoro kupelekwa Tanga, ambako kutokana na sheria za ushaguzi mtu hatakiwi kupiga kura tofauti na kituo ambacho alijiandikisha. Je, hatma yao itakuaje pindi itakapofika wakati wa uchaguzi?
Pendekezo lake (Lissu) ni kwamba uongozi unaokuja uchukue suala hili na kuangalia namna ya kuingilia kati
UPDATE saa Saba Mchana: TLS waomba radhi kupitia ukurasa wao wa X baada ya kupost kuwa zoezi la upigaji kura limeisha wakati mawakili wakiwa wanasubiri karatasi za kupigia kura ziongezwe.
Kusoma zaidi kuhusu taarifa hii soma hapa: TLS waomba radhi kwa post yao waliyoweka mtandao wa X kuhusu zoezi la kupiga Uchaguzi wa Rais TLS kumalizika
======
UPDATE saa sita mchana: Ukurasa wa X wa TLS wamepost kuwa uchaguzi umeisha, lakini upande mwingine taarifa ni kuwa karatasi bado zinazubiriwa kuongezwa ili zoezi la kupiga kura liendelee kwa wale ambao bado hawajapiga kura.
Zaidi kuhusu taarifa hii soma hapa: Ukurasa wa TLS X umesema zoezi la kupiga kura limeisha, upande mwingine wanasema wanasubiri karatasi za kupiga kura ziongezwe, ukweli ni upi?
===
UPDATE majira ya saa tano asubuhi: Zoezi la kupiga kura limesimama baada ya karatasi kuisha, mawakili wanasubiri karatazi ziletwe ili zoezi liendelee.
Zaidi kuhusu hili soma hapa: Uchaguzi wa Rais TLS: Karatasi za kupigia kura zimeisha, mawakili wanasubiri karatasi nyingine ziletwe ili zoezi liendelee
====
Leo ndio leo, ni kivumbi na kijasho, hatma ya Urais TLS kugundulika leo.
Uchaguzi wa Rais wa TLS uliokuwa unasubiriwa kwa hamu, kufanyika leo Agosti 2, 2024. Je nani ataibuka mshindi kati ya wagombea hawa sita?
Kama ulikosa mdahalo wa wagombea hawa pita hapa Mdahalo wa Wagombea Urais Chama cha Mawakili Tanzania Bara (TLS) mwaka 2024
1. Capt. Ibrahim Mbiu Bendera
2. Paul Revocatus Kaunda
3. Sweetbert Mkuba
4. Boniface Mwabukusi
5. Emmanuel Agustino Muga
6. Revocutus Lubigili Kibwe
Kwa kufatilia kwangu naona upinzani mkubwa upo kati ya
Sweetbert Mkuba na Boniface Mwabukusi.
Je, unadhani mshindi atatoka kati ya hawa wawili au tutapata mshangao wa kufunga mwaka kwa asiyetarajiwa kabisa kuibuka mshindi?
Usikae mbali na uzi huu kupata updates zote za yanayoendelea kwenye uchaguzi huu.
UPDATE: Mwabukusi ashinda Urais TLS kwa kura 1274
Jumla ya kura: 2218
Kura zilizoharikika: 3
1. Boniface Mwabukusi - 1274
2. Sweetbert Nkuba - 807
3. Kapteni Ibrahim Bendera - 58
4. Paul Kaunda - 51
5. Emmanuel Muga - 18
6. Revocatus Kuuli - 7
UPDATE saa 4:40 usiku: Baadhi ya mawakili warekodiwa wakiimba wana imani na Mwabukusi, tukio lililofanya na wengine waliokuwa ukumbini watoke kwenda kuangalia kuna nini. Za ndaniiiii ni kuwa Mwabukusi kachukua kijiji. Tusubiri taarifa rasmi ya Kamati maana mpaka sasa hola!
UPDATE saa nne usiku: Tundu Lissu atoa shukrani kwa mawakili wenzake kwa sapoti waliyompa kipindi chote alichokuwa kwenye matatizo (baada ya kushambuliwa na watu wasiyojulikana. Atoa hoja kuhusu wamasai wa Ngorongoro kupelekwa Tanga, ambako kutokana na sheria za ushaguzi mtu hatakiwi kupiga kura tofauti na kituo ambacho alijiandikisha. Je, hatma yao itakuaje pindi itakapofika wakati wa uchaguzi?
Pendekezo lake (Lissu) ni kwamba uongozi unaokuja uchukue suala hili na kuangalia namna ya kuingilia kati
UPDATE saa Saba Mchana: TLS waomba radhi kupitia ukurasa wao wa X baada ya kupost kuwa zoezi la upigaji kura limeisha wakati mawakili wakiwa wanasubiri karatasi za kupigia kura ziongezwe.
Kusoma zaidi kuhusu taarifa hii soma hapa: TLS waomba radhi kwa post yao waliyoweka mtandao wa X kuhusu zoezi la kupiga Uchaguzi wa Rais TLS kumalizika
======
UPDATE saa sita mchana: Ukurasa wa X wa TLS wamepost kuwa uchaguzi umeisha, lakini upande mwingine taarifa ni kuwa karatasi bado zinazubiriwa kuongezwa ili zoezi la kupiga kura liendelee kwa wale ambao bado hawajapiga kura.
Zaidi kuhusu taarifa hii soma hapa: Ukurasa wa TLS X umesema zoezi la kupiga kura limeisha, upande mwingine wanasema wanasubiri karatasi za kupiga kura ziongezwe, ukweli ni upi?
===
UPDATE majira ya saa tano asubuhi: Zoezi la kupiga kura limesimama baada ya karatasi kuisha, mawakili wanasubiri karatazi ziletwe ili zoezi liendelee.
Zaidi kuhusu hili soma hapa: Uchaguzi wa Rais TLS: Karatasi za kupigia kura zimeisha, mawakili wanasubiri karatasi nyingine ziletwe ili zoezi liendelee
====
Leo ndio leo, ni kivumbi na kijasho, hatma ya Urais TLS kugundulika leo.
Uchaguzi wa Rais wa TLS uliokuwa unasubiriwa kwa hamu, kufanyika leo Agosti 2, 2024. Je nani ataibuka mshindi kati ya wagombea hawa sita?
Kama ulikosa mdahalo wa wagombea hawa pita hapa Mdahalo wa Wagombea Urais Chama cha Mawakili Tanzania Bara (TLS) mwaka 2024
1. Capt. Ibrahim Mbiu Bendera
2. Paul Revocatus Kaunda
3. Sweetbert Mkuba
4. Boniface Mwabukusi
5. Emmanuel Agustino Muga
6. Revocutus Lubigili Kibwe
Kwa kufatilia kwangu naona upinzani mkubwa upo kati ya
Sweetbert Mkuba na Boniface Mwabukusi.
Je, unadhani mshindi atatoka kati ya hawa wawili au tutapata mshangao wa kufunga mwaka kwa asiyetarajiwa kabisa kuibuka mshindi?
Usikae mbali na uzi huu kupata updates zote za yanayoendelea kwenye uchaguzi huu.