Elections 2010 Uchakachuaji HAUPO! - NYARAKA HIZI HAPA NI FAKE

Elections 2010 Uchakachuaji HAUPO! - NYARAKA HIZI HAPA NI FAKE

Status
Not open for further replies.
TISS wanajua mahakamani watatolewa nock out bse Slaa ana ushaidi ndo maana wameamua wajibu via waandishi wa habari.
Ata EPA WALISEMA walimwambia mropokaji.
Sijawai ona TISS wanajitetea kwa waandishi wa habari toka nizaliwe yaani nowdays imekuwa taasisi ya kawaida sana
Its common sense mtu akikuzushia sifa unaenda mahakamani kwa TISS imekuwa kinyume mahakama kwao ni waandishi wa habari very unprofessional and ridiculous
 
Wote tumesikia kuhusu shutuma ambazo Dr.slaa ameitupia agency yetu ya usalama...lakini kitu ambacho mimi sikielewi ni kuhusu ujibuji wa hizi tuhuma na mazoea ya watanzania kuamini bila kudai uchunguzi au kuuliza zaidi...
1.Dr.slaa amezusha tuhuma hizo na kama kweli kazusha tuhuma hizo...reaction ya kwanza ya usalama ingekuwa kum sue dr.slaa kwa kuwapaka matope,chombo pekee kinachoweza kuprove kwamba dr.slaa kazusha tuhuma hizo ni mahakama kwa hiyo tungetegemea kuwa usalama wangemfungulia dr.slaa mashitaka.

2.Ni kweli...hapa kuna fact mija kubwa kuwa,dr.slaa pamoja na uanasiasa wake ni mtu ambaye anasimama kwenye maneno yake,ndiyo maana baada ya usalama kuzikataa hizo tuhuma akawaambia kuwa waende mahakamani ambako kila upande utatakiwa kupeleka ushahidi wa kutetea upande wake na pia watanzaania tutajua ukweli kuhusu uhusikaji wa usalama wa taifa kwenye uchakachuaji wa matokeo...

Au niseme hivii...kwa historia hakuna mtu hata mmoja aliyejitokeza kwenda mahakani kutokana na shutuma ambazo zimelekezwa kwake na dr.slaa hivyo kutunyima watanzania kujua ukweli na badala yake tunapewa press conference kibaoo...
Ni kwamba haya maneno yaliyoenea kwenye jamii kwamba mpaka usalama umesema basi dr.slaa kakosea,haujengi taifa kwani sasa watu watakuwa wanaangalia cheo na jina la taasisi kwamba kama ni agency yoyote ya serikali bac wanasema ukweli...Ni natural path kukataa kitu pale unapohusishwa nacho uwe ni ukweli au uongo hasa kitu ambacho kina consequence nyingi kama hiki.....Raisi Clinton alipohusishwa na kashfa ya mapezi na sekretari wake si alikataa lakini wamarekani hawakutaka kuishia kwenye hotuba yake ya kujisafisha,walidai utafiti zaidi ili UKWELI ujulikane na baada ya uchunguzi ukweli ukajulikana...
hivyo ili wananchi wajue kwamba nchi yao inaendeshwa kidemokrasia na hakukuwa na uchakachuaji wowote wa kura uliyoihusisha usalama,uchunguzi huru ufanyike la sivyo hakuna ukweli wowote ambao wanachi wamesikia na itakua aibu kwa nchi yetu na usalama pia!!!!

Nimekusoma na nimekuelewa vizuri, hapo kwenye nyekundu labda tuiweke hivi, Usalama wa taifa kwa sasa ni chombo kilicho wazi na kinajulikana na kipo mwa mujibu wa sheria, lakini kazi zake ni za siri, Usalama wa taifa haimpeleki mtu mahakamani (Kumbuka kesi ya uhaini watu wa usalama walifanya kazi kubwa sana lakini kwenye kushtaki halikuwa suala lao), bali watafanya uchunguzi na mwisho issue inakuwa handled police, na wala Usalama sio taasisis ya kukurupuka kwenye vyombo vya habari na ndio maana hawana msemaji wa UWT, tatizo Slaa kawachoma mkuki wa ukweli na jamaa wamepoteza mwelekeo na kutokujua ni nini cha kufanya, kama Slaa alikuwa na hoja, hao jamaa wangemwita na kuchunguza madai yake kama ni kweli basi wangedili na waliohusika kwa sheria zao na kama Slaa ni muongo wangeipeleka kesi police na hatimae mahakamani
 
Usalama wa Taifa imeoza, haina maadili na ni aibu sana kwa Taifa letu. Sio chombo cha sisi Watanzania kujivunia tena. Hata wafanyakazi wake wakionekana mtaani wanatakiwa watembee vichwa chini na si kifua mbele kama zamani walipokuwa wanaheshimika na kutetemekewa na kuonekana kama akina James Bond. Sasahivi wakipita wanaonekana ni wachakachuaji tu!

Chombo hiki enzi za mwalimu kilikuwa na sifa sana na maadili kwa kulinda usalama wa wananchi, lakini sahivi kinalinda usalama wa JK na CCM.

Tatizo chombo hiki kiko chini ya ofisi ya rais, mnadhani wamtetea nani?

Ushauri wangu ni kama mkurugenzi wa usalama anaipenda nchi yake ingawa alishinikizwa na boss wake, nadhani ingekuwa busara akajiuzuli. Angalau nafsi yake itakuwa na amani kidogo kwa dhambi aliyolazimishwa kuutendea umma wa wa Watanzania kwa shinikizo la boss wake JK. Na pia hata Mungu atamwonea huruma.

Otherwise na wewe, na usalama wa CCM na kuchakachua mna tuhuma ya kujibu, pamoja na NEC, jeshi na TAKUKURU na vibaka wengine wote mlioshiriki kwa aina moja au nyingine kukandamiza haki za wananchi na kutotimiza wajibu wenu.
 
Usalama wa Taifa imeoza, haina maadili na ni aibu sana kwa Taifa letu. Sio chombo cha sisi Watanzania kujivunia tena. Hata wafanyakazi wake wakionekana mtaani wanatakiwa watembee vichwa chini na si kifua mbele kama zamani walipokuwa wanaheshimika na kutetemekewa na kuonekana kama akina James Bond. Sasahivi wakipita wanaonekana ni wachakachuaji tu!

Chombo hiki enzi za mwalimu kilikuwa na sifa sana na maadili kwa kulinda usalama wa wananchi, lakini sahivi kinalinda usalama wa JK na CCM.

Tatizo chombo hiki kiko chini ya ofisi ya rais, mnadhani wamtetea nani?

Ushauri wangu ni kama mkurugenzi wa usalama anaipenda nchi yake ingawa alishinikizwa na boss wake, nadhani ingekuwa busara akajiuzulu. Angalau nafsi yake itakuwa na amani kidogo kwa dhambi aliyolazimishwa kuutendea umma wa wa Watanzania kwa shinikizo la boss wake JK. Na pia hata Mungu atamwonea huruma.

Otherwise na wewe, na usalama wa CCM mna tuhuma ya kujibu, pamoja na NEC, jeshi na TAKUKURU na vibaka wengine wote mlioshiriki kwa aina moja au nyingine kukandamiza haki za wananchi na kutotimiza wajibu wenu.
 
Kama baadhi ya wachangiaji walivyosema ni ngumu kwa mahakama zetu kutoa haki, na waTZ wameshapigwa mkwala kuwa upinzani unataka kumwaga damu, kwa hiyo hata Dr. Slaa akizungumza vipi bado kunawatanzania watasema huyu anataka kuleta fujo(uelewa wa watz ni mdogo sana hata wale wa mijini, akina malaria sugu ni wengi). Ninachoona mimi ili swala nikulipeleka kwa wafadhili tu.
 
Ya Ngoswe huwa namuachia Ngoswe, lakini mengine huwa nayajibu kama ningelikuwa mimi:

Nisingelimshtaki Dr. Slaa kwa sababu ningempa umaarufu, (na ndicho alichotafuta hapo) Namheshimu sana lakini wanaomzunguka wamempotosha sana, wamemdanganya sana, sababu ni kusema kwake tu Bungeni. hata sijui ilikuwaje mzee wetu wakamshawishi apoteze ubunge wake, naamini na nadhani ndio ukweli KUNA AGENDA YA SIRI DHIDI YA DK. SLAA NDANI YA CHADEMA. bado tunatazama :tape: hakika nawaambieni.. nimeanza kuona mbali sasa.. kwa maana kikao cha kumteua kuwa mgombea Urais kilifanyika Nairobi, hakuwa amejiandaa kwa hilo, ndio maana AKAMTAKA JUMA DUNI kuwa mgombea mwenza wake... Ingekuwaje hapo? Hao wanaosema CCM na CUF wameungana walilisahau hilo? pana ka-moshimoshi kanafuka hebu tusubirie.

AMANI TANZANIA
Lala kijana lala naona usingizi unakuuma!!!!!!!!!
 
Umenena sahihi kabisa, kukataa kupitia kwenye vyombo vya habari si kwamba umesema ukweli!! Dr. Slaa alipowatuhumu akina lowasa, karamagi na wenzake walikanusha vikali jambo hilo kupitia vyombo vya habari, but at the end of the day ukweli ukajulikana kwamba Dr. Slaa alisema ukweli!! My suggestion sasa Silaa aanze mwenyewe kwenda mahakamani

Sidhani kama unaelewa taratibu za kisheria.

Mtu akinituhumu kwamba mimi ni mwizi, kisha mimi nikakataa, bado kisheria sijajisafisha. Natakiwa kufungua kesi ya kusafisha jina langu mahakamani. Vinginevyo mtu huyo aende katika vyombo vya habari na kukanusha usemi wake.
Sisi wananchi wa Tanzania tunatakiwa, kwa hali na mali, kuwashindikiza UWT NEC na CCM kwenda Mahakamani kumshtaki Dr Slaa, Vinginevyo WANAKUBALI KWAMBA TUHUMA NI ZA KWELI NI MAHARAMIA, WAMEIBA KURA.

Dr Slaa aende Mahakamani kufanya nini??
 
Jamani niwaambie tu ni kweli usalama wa taifa, umeusika kuiba kura. Kuna rafiki yangu mmoja tulisoma naye miaka ya nyuma, anafanya kazi usalama wa taifa, nilipomuuliza vipi uchaguzi, aliniambia hivi" uchaguzi ni mgumu sana mwaka huu ila kikwete atashinda kwa sababu kuna maafisa usalama 400 wamesambazwa katika vituo mbalimbali nchi nzima, akaendelea kuniambia kuwa kitu kinachowachanganya zaidi ni kuwa kuna vituo vingi sana, nikamuuliza tatizo liko wapi kuwa na vituo vingi, alisema hivi hao wanausalama 400 wanatakiwa wachakachue kura ili zisiwe na tofauti kubwa sana kituo na kituo yaani kuwe na uwiano fulani"

Mheshimiwa Masauni,

Inaleta maana hebu unganisha na hii kuanzia Pretoria, Tunduma, Karatu, hadi vyombo vya habari...na kutishiana mahakamani!!!

https://www.jamiiforums.com/results-m...ka-huko-2.html
 
Usalama wa Taifa imeoza, haina maadili na ni aibu sana kwa Taifa letu. Sio chombo cha sisi Watanzania kujivunia tena. Hata wafanyakazi wake wakionekana mtaani wanatakiwa watembee vichwa chini na si kifua mbele kama zamani walipokuwa wanaheshimika na kutetemekewa na kuonekana kama akina James Bond. Sasahivi wakipita wanaonekana ni wachakachuaji tu!

Chombo hiki enzi za mwalimu kilikuwa na sifa sana na maadili kwa kulinda usalama wa wananchi, lakini sahivi kinalinda usalama wa JK na CCM.

Tatizo chombo hiki kiko chini ya ofisi ya rais, mnadhani wamtetea nani?

Ushauri wangu ni kama mkurugenzi wa usalama anaipenda nchi yake ingawa alishinikizwa na boss wake, nadhani ingekuwa busara akajiuzulu. Angalau nafsi yake itakuwa na amani kidogo kwa dhambi aliyolazimishwa kuutendea umma wa wa Watanzania kwa shinikizo la boss wake JK. Na pia hata Mungu atamwonea huruma.

Otherwise na wewe, na usalama wa CCM mna tuhuma ya kujibu, pamoja na NEC, jeshi na TAKUKURU na vibaka wengine wote mlioshiriki kwa aina moja au nyingine kukandamiza haki za wananchi na kutotimiza wajibu wenu.

Mkuu umenena nazito!

Umeseama yote yanayotakiwa kusemwa!!
 
Wachangiaji wote naungana nao...NEC ndo wakulaumiwa kwani hadi sasa wanaulizwa iweje wapiga kura halali waliojiandikisha ni 20millions lakini waliopiga kura ni 8millions tu......!hawana majibu....that means data zao ni inconsistence kabisa...kama hivyo ndivyo even matokeo walotoa sio ya kweli hata kidogo na hakuna haja ya kuwa na daftari la kupiga kura...data zao zote zipo kirushwa rushwa...mimi ni mtaalamu wa mambo ya computer na mawasiliano ya simu...utumiaji wa TEKNOHAMA ktk uchaguzi ni mzuri lakini kwa nchi kama ya Tanzania,ambayo kwanza ndo inaamkia katika TEKNOHAMA,mda wa reserch lazima upewe kipaumbele kwanza....na pia ni rahisi sana KUCHAKACHUA MATOKEO kupitia TEKNOHAMA kuliko wengi wanavyofikiri...
 
Umenena sahihi kabisa, kukataa kupitia kwenye vyombo vya habari si kwamba umesema ukweli!! Dr. Slaa alipowatuhumu akina lowasa, karamagi na wenzake walikanusha vikali jambo hilo kupitia vyombo vya habari, but at the end of the day ukweli ukajulikana kwamba Dr. Slaa alisema ukweli!! My suggestion sasa Silaa aanze mwenyewe kwenda mahakamani

Alichofanya Dr slaa ni kuwashitakia kwa wananchi kupitia media kwamba usalama wa taifa ndo waliofanikisha wizi wa kura ili wananchi watoe hukumu. kwa maana nyingine wananchi ndo mahakama.
 
Kama baadhi ya wachangiaji walivyosema ni ngumu kwa mahakama zetu kutoa haki, na waTZ wameshapigwa mkwala kuwa upinzani unataka kumwaga damu, kwa hiyo hata Dr. Slaa akizungumza vipi bado kunawatanzania watasema huyu anataka kuleta fujo(uelewa wa watz ni mdogo sana hata wale wa mijini, akina malaria sugu ni wengi). Ninachoona mimi ili swala nikulipeleka kwa wafadhili tu.

Uelewa wa WaTanzania si mdogo hata kidogo kama ulivodaid.uelewa wa waTanzania ni mkubwa lakini ndani yake kuna udhaifu wa UNYONGE na KUKOSA MATUMAINI. Watanzania wanaelewa kila kitu, wana uwezo wa kudadisi ili kupata undani pia ni watu wasiotaka kuburutwa.

Ttatizo kubwa linalotukabili Tanzania ni uhalalishwaji wa mtandao mkubwa wa Uharamia unaojumuisha Vyombo vyote vya dola, idara zote za serikali na mashirika ya umma pamoja na ofisi zetu zote za balozi.

Mtandao huu mkubwa wenye baraka zote kutoka Ikulu kwa MH Rais umekuwa ukitoa Baraka kwa mitandao midogo ya uharamia inayohusika moja kwa moja kuwabugudhi wananchi na kuwagandamiza kupitia serikali za mitaa, mahakama za mwanzo pia ofisi za CCM matawini na vitongojini na hata baadhi ya Mashirika ya kidini na NGO huko vijijini. KMfano mwananchi wakawaida ni nadra kutofautisha Ofisi ya CCM na Kituo cha Polisi,Si kwa kutoelewa bali kwa kushindwa kutofautisha utekelezaji na namna wote walivyo na mamraka ya Kipolisi. Mwnanchi wa Kawaida hawezi tofautisha Mamraka ya kisheria waliyo nayo Polisi na Watendaji wa CCM.
Mindao yote ya kiserikali iko funded na Wizi wa fedha za uendeshaji wa shughuli za kiserikali na kuwaibia wananchi moja kwa moja kutoka
mifukoni mwao.


CCM pamoja na kupata ruzuku ya mabilioni kila mwezi chanzo kikubwa cha mapato yao ni KUIBA kutoka hazina kuu ya serikali.

CCM hawawezi kuiba Bila kutumia watumishi wa serikali, watumishi wa serikali hawawezi kushiriki kuiba bila au kutiwa shinikizo na kibano aukuahidiwa kunufaika kwa namna moja au nyingine na wizi huo.

Mkubwa akisha iba mdogo naye anaiba kwa njia ileile hapo ndipo kigugumizi cha kila kiungo mwilini huanza kutokana na idadi ya wenye uwezo wa kumfunga paka kengere ianzapo kutoweka.

Siku zote Wanashitakiwa na kufungwa wezi wa kuku mbuzi na Mafenesi katika mashamba ya Wezi wakubwa wa fedha ya Umma na wezi wale walio nje ya mtandao.
Ukiona mtu anafikishwa mahakamani kutoka serikalini au ndani ya chama kwa wizi mtu huyo anafanywa Kondoo wa kafara tu au ameiba nje ya mtandao wa kiharamia.

Hii ni Domino Effect, Wizi ni jambo lililokusudiwa tangu awali lakini matokeo mengi tunyaonayo si jambo lililokusudiwa mwanzo ni jambo ambalo limewaponyoka. Hawawezi na pia hawajui namna ya kuzuia Domino effect hii kwa sababu ya uchafu mwingi nafsini na akilini mwao unawanyimao uwezo hamu nia na kasi ya kuvunja Domino Effect.
Zaidi wanaelewa kwamba wale wenye uwezo wa kukomesha Uharamia huu wana uwezo pia wa kuangamiza himaya zao za udharimu.Himaya zao za uhalifu zikiangamizwa nafasi zao uwepo wao na heshima walizo jijengea kwa Kiburi cha uharamia vyote vitatoweka.

Dawa pekee ya Kulinda himaya hii ya KIIBILISI ni kukumbatia aina zote za uovu, uoza na uharamia kwa gharama ya kodi atozwayo Mtanzania na uhai wake.

Watanzania kadhaa less than 5% wamefaidika moja kwa moja na wizi wa kimtandao kiasi cha kuamini kwamba huo ndo utaratibu wa kujikimu katika maisha. Pamoja na uelewa mkubwa wa Maharamia hawa wanajaribu kulinda mfumo uwapao mapato bila kutoa jasho wala kubughudhiwa. Hili kundi la 5% linajumuisha Watumishi wengi wa serikali na mashirika ya umma na wafanya biashara ambao mara nyingi hawana choice.

Kwa ushawishi mkubwa wa kundi hili la 5% kila mtu wengi wa Watanzania hupiga njozi na kuamini siku moja wao pia watafaidika na mtandao wa wizi. Labda ni jambo lenye manufaa kulinda mtandfao wa uhalifu.

Kauri za Dr Slaa za kubomoa Mtandao na kuunda utaratibu mpya ni tishio kwa hili kundi la 5% ndiyo maana kundi hili halioni taabu na halisiti kutawanya hofu iliyo ndani ya nafsi zao kwa Watanzania wote. Watu wa mtandao wa uovu wanajua fika kwamba Dr Slaa akishinda wao kama Maharamia wa kitaifa watanyolewa kavu na himaya yao itavunjika vipande. Wanajua kabisa kwamba asilimia 95% ya watanzania watafaidika na kuvunjika kwa himaya zao, kwa nini wasiwageuzie kibao wananchi na kuwaambukiza hofu waliyonayo kwa hasara yao wananchi wenyewe??

Huu ugumu wa serikali kuchukua hatua ndilo jambo tupaswalo kulichambua kisayansi na kuweka bayana na kinaga ubaga na kutoa shinikizo la nguvu kwa watendaji wa serikali kutoa majibu ya mswali yetu au kuachia ngazi.

Mashushsu wa MOSAD wameweza kulinda nchi yao Israel dhidi ya njama zote za mahasimu wao kwa kuimarisha utaalamu wa KuTrail Fedha inayoingia na kutoka kwa kila mtuhumiwa, kitaifa na kimataifa.
Ukitaka kukamata wahalifu wote ndani na nje ya serikali Tanzania fuata mtiririko wa fedha kabla na baada ya kitendo cha uovu.


Rais Kikwete anatabasamu na kusema" Ongezeko kubwa la Magari Dar ni dalili za maendeleo" Ujumbe wa moja kwa moja kwa waliofaidika na mtandao wa kiharamia "kumbukeni kwamba mtandao wa kiovu ndo ulowapa uwezo wakununua sehemu kubwa ya magari haya mnaweza kuuwa chanzo cha magidai yenu??
 
Wote tumesikia kuhusu shutuma ambazo Dr.slaa ameitupia agency yetu ya usalama...lakini kitu ambacho mimi sikielewi ni kuhusu ujibuji wa hizi tuhuma na mazoea ya watanzania kuamini bila kudai uchunguzi au kuuliza zaidi...
1.Dr.slaa amezusha tuhuma hizo na kama kweli kazusha tuhuma hizo...reaction ya kwanza ya usalama ingekuwa kum sue dr.slaa kwa kuwapaka matope,chombo pekee kinachoweza kuprove kwamba dr.slaa kazusha tuhuma hizo ni mahakama kwa hiyo tungetegemea kuwa usalama wangemfungulia dr.slaa mashitaka.

2.Ni kweli...hapa kuna fact mija kubwa kuwa,dr.slaa pamoja na uanasiasa wake ni mtu ambaye anasimama kwenye maneno yake,ndiyo maana baada ya usalama kuzikataa hizo tuhuma akawaambia kuwa waende mahakamani ambako kila upande utatakiwa kupeleka ushahidi wa kutetea upande wake na pia watanzaania tutajua ukweli kuhusu uhusikaji wa usalama wa taifa kwenye uchakachuaji wa matokeo...

Au niseme hivii...kwa historia hakuna mtu hata mmoja aliyejitokeza kwenda mahakani kutokana na shutuma ambazo zimelekezwa kwake na dr.slaa hivyo kutunyima watanzania kujua ukweli na badala yake tunapewa press conference kibaoo...
Ni kwamba haya maneno yaliyoenea kwenye jamii kwamba mpaka usalama umesema basi dr.slaa kakosea,haujengi taifa kwani sasa watu watakuwa wanaangalia cheo na jina la taasisi kwamba kama ni agency yoyote ya serikali bac wanasema ukweli...Ni natural path kukataa kitu pale unapohusishwa nacho uwe ni ukweli au uongo hasa kitu ambacho kina consequence nyingi kama hiki.....Raisi Clinton alipohusishwa na kashfa ya mapezi na sekretari wake si alikataa lakini wamarekani hawakutaka kuishia kwenye hotuba yake ya kujisafisha,walidai utafiti zaidi ili UKWELI ujulikane na baada ya uchunguzi ukweli ukajulikana...
hivyo ili wananchi wajue kwamba nchi yao inaendeshwa kidemokrasia na hakukuwa na uchakachuaji wowote wa kura uliyoihusisha usalama,uchunguzi huru ufanyike la sivyo hakuna ukweli wowote ambao wanachi wamesikia na itakua aibu kwa nchi yetu na usalama pia!!!!

Ndugu yangu umenena sahihi kabisaaaa!
Mimi ninaishi Arusha! Nilikuwepo kwenye mchakato woooote wa uchaguzi wa jimbo la Arusha mjini. Siku ya kutangaza matokeo, Batilda Buriani alikataa kusainin matokeo akidai hawezi kusaini hadi Lowassa aje. Ni kweli baada ya saa kadhaa kupita, Lowassa alifika hapa mjini ktk ukumbi wa manispaa/halmasahuri na kuingia hadi pale ndani tulipokuwepo. Punde kabla hajaingia ndani, wananchi waliokuwepo pale nje walimzomea sana. Kule ndani, alijaribu saaaaanaaa kumshawishi Lema Godbless achukue kiasi fulani cha pesa ili akubali na atangaze kuwa yeye (Lema) ameshindwa ubunge, Lowassa alifika hadi 900M. Lema akamwambia toka hapo nje waambie hao wananchi waliokusanyika kuwa unanipa hizi pesa wakikubali then njoo ndani tusaini. Lema akapiga simu kwa Ndessamburo na Mbowe nao wakaja. Punde matokeo yakatangazwa. Lakini ktk magazeti ya leo Lowassa anakanusha kuwa hakuhusika na jaribio la uchakachuaji wa matokeao ya Arusha. Hivyo basi naungana na wewe ndugu yangu kuwa hawa jamaa in how hata ukiwakuta Red-handed, watakaaaa tu. (watasema It wasn't me!).
Kuna Afisa Usalama mmoja (jina ninalihifadhi) aliporwa bastola na vibaka maeneo ya Shevers (eneo maarufu kwa vyangudoa) hapa Arusha.
haya yoote naweza kuyathibisha in the court of law.
 
Ya Ngoswe huwa namuachia Ngoswe, lakini mengine huwa nayajibu kama ningelikuwa mimi:

Nisingelimshtaki Dr. Slaa kwa sababu ningempa umaarufu, (na ndicho alichotafuta hapo) Namheshimu sana lakini wanaomzunguka wamempotosha sana, wamemdanganya sana, sababu ni kusema kwake tu Bungeni. hata sijui ilikuwaje mzee wetu wakamshawishi apoteze ubunge wake, naamini na nadhani ndio ukweli KUNA AGENDA YA SIRI DHIDI YA DK. SLAA NDANI YA CHADEMA. bado tunatazama :tape: hakika nawaambieni.. nimeanza kuona mbali sasa.. kwa maana kikao cha kumteua kuwa mgombea Urais kilifanyika Nairobi, hakuwa amejiandaa kwa hilo, ndio maana AKAMTAKA JUMA DUNI kuwa mgombea mwenza wake... Ingekuwaje hapo? Hao wanaosema CCM na CUF wameungana walilisahau hilo? pana ka-moshimoshi kanafuka hebu tusubirie.

AMANI TANZANIA
Wanausalama wa Taifa (TISS) kwa kujua kujenga hoja juu ya propaganda nina wa-adore kweli kweli.
naamini wewe umetumwa kama wenzio. kwa taarifa yako, hapa jukwaani siyo watu wepesi unavyofikiria. kila nukta tunaisoma na kuielewa zaidi ya text.
Najua mnalipwa pesa nyingi sana ndo maana hamuoni machungu na machozi ya watanzania wavija jasho mnaowakandamiza.

 
Ndugu yangu umenena sahihi kabisaaaa!
Mimi ninaishi Arusha! Nilikuwepo kwenye mchakato woooote wa uchaguzi wa jimbo la Arusha mjini. Siku ya kutangaza matokeo, Batilda Buriani alikataa kusainin matokeo akidai hawezi kusaini hadi Lowassa aje. Ni kweli baada ya saa kadhaa kupita, Lowassa alifika hapa mjini ktk ukumbi wa manispaa/halmasahuri na kuingia hadi pale ndani tulipokuwepo. Punde kabla hajaingia ndani, wananchi waliokuwepo pale nje walimzomea sana. Kule ndani, alijaribu saaaaanaaa kumshawishi Lema Godbless achukue kiasi fulani cha pesa ili akubali na atangaze kuwa yeye (Lema) ameshindwa ubunge, Lowassa alifika hadi 900M. Lema akamwambia toka hapo nje waambie hao wananchi waliokusanyika kuwa unanipa hizi pesa wakikubali then njoo ndani tusaini. Lema akapiga simu kwa Ndessamburo na Mbowe nao wakaja. Punde matokeo yakatangazwa. Lakini ktk magazeti ya leo Lowassa anakanusha kuwa hakuhusika na jaribio la uchakachuaji wa matokeao ya Arusha. Hivyo basi naungana na wewe ndugu yangu kuwa hawa jamaa in how hata ukiwakuta Red-handed, watakaaaa tu. (watasema It wasn't me!).
Kuna Afisa Usalama mmoja (jina ninalihifadhi) aliporwa bastola na vibaka maeneo ya Shevers (eneo maarufu kwa vyangudoa) hapa Arusha.
haya yoote naweza kuyathibisha in the court of law.
Aisee, hawa jamaa inabidi sasa watembee na bodyguard maana maisha yao yapo hatarini ktk kuilinda nchi na ccm
 
asnthe sana ndugu...tunapata shida sana kupigania ukweli na haki zetu za kikatiba kutoka kundi la watu wapenda madaraka kama kina lowassa....kuhusu hawa afisa usalama wetu ni wanatia aibu!!!!!ona huyo kaporwa na bunduki yake tena akiwa shivers!!!
 
Dr slaa atafute umaarufu kwanani ? Hivi ninani asiye mfaham slaa mpaka aangaike kutafuta umaarufu? Nahic umelogwa na bibi yako!!

heheeeeee e=heeeeee we slaaaa damu, umaarufu kwisha....... kama si umaarufu anaytafuta jemedari asiekubali shindwa jemedari gani CCM daima
 
Hapa tunatakiwa kuwa makini sana, siamini kitu kama hiki wanaweza kukiweka kwenye maandishi sio wapumbavu. ninachoofia ni kuwa kuna watu wanajiandaa kutaka kuifungia JF wanatafuta sababu unless Mkuu Invisible una uhakika na source but this is craps.

Tuwe makini tusipewe barua kama za mwananchi maana serikali na taasisi zake zote kama TBC wanakampenia CCM wazi wazi bila kuficha.
I think I was wrong, walotajwa kwenye hii kitu wangeangalia hii FAKE thing mapema wangepata majibu ya kumjibu Slaa alipotoka na barua hii... Wengine waliniuliza SOURCE! Niliamua ili watu wapate muda wa kupiga kura bila kukata tamaa basi iondoke (japo ujumbe ulishafika).

Nadhani kwa maandishi yako mkuu hapo unamaanisha nilikuwa nampigia kampeni Slaa waziwazi; ni jambo la kawaida kudaiwa UNATUMIWA au USHALIPWA etc... I normally take it
 
I think I was wrong, walotajwa kwenye hii kitu wangeangalia hii FAKE thing mapema wangepata majibu ya kumjibu Slaa alipotoka na barua hii... Wengine waliniuliza SOURCE! Niliamua ili watu wapate muda wa kupiga kura bila kukata tamaa basi iondoke (japo ujumbe ulishafika).

Nadhani kwa maandishi yako mkuu hapo unamaanisha nilikuwa nampigia kampeni Slaa waziwazi; ni jambo la kawaida kudaiwa UNATUMIWA au USHALIPWA etc... I normally take it
Haya uchaguzi umeisha, mwaga ukweli sasa :lol:
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom