Elections 2010 Uchakachuaji HAUPO! - NYARAKA HIZI HAPA NI FAKE

Elections 2010 Uchakachuaji HAUPO! - NYARAKA HIZI HAPA NI FAKE

Status
Not open for further replies.
Nyaraka hiyo ilikuwa ikitoa maelekezo ya Mpango huu ufanyike soma hapa chini na linganisha sasa:

Ili JK aweze kushinda kwa 80% kikao hicho kiliandaa njia hii!

CCM tayari wameshajihakikishia ushindi kwa vile tayari wameshakamilisha kazi yao. Katika uchaguzi wamekuwa wakitimiza ratiba tu lakini matokeo ya uchaguzi yanatambulika na mpango kamili wa kukamilisha matokeo hayo ni huu.

A). Upangaji wa vituo
NEC imekuwa ikiendesha zoezi la upangaji wa vituo chini ya uangalizi maalum wa watalaam wa IT (kama ambavyo imekwsiha kuelezwa na baadhi ya wadau hapa JF, ambao ni wa 16 na MBWA MKALI katika Post zilizopita).

i).Utaratibu wa awali ulikuwa ni kuandaa vituo halali ambavyo viliandaliwa na kukamilika.
ii). Utaratibu wa pili ulikuwa ni kuandaa vituo hewa ambavyo viliandaliwa baada ya vituo vya kwanza kukamilika (Hii ni kwa lengo la kutambua vituo awali na kutofautisha vile vya kuchahachulia).

Vituo Hewa:
Jambo hili limekuwa likiwatatiza wengi sana na wengine kushindwa kuamini iwapo jambo hili linawezekana. Ukweli linawezekana na hapa natoa mmoja ya kituo hewa.
· Hapa kwa mujibu wa tume vituo vimepangiliwa kwa majina/namba.
· Kituo ambacho nawatolea mfano hai ni Na. 00020941. Ama kwa jina kinaitwa Kituo cha Shule ya Msingi Kapangaja. Kipo katika Kata ya Bugongwa wilaya ya Ilemela na jimbo la Ilemela.
-Eneo hili la shule ya msingi limegawanywa na kuzaa jumla ya vituo 5.
-Tatizo lipo katika vituo viwili ambavyo ni kituo namba 4 na namba 5.
· Kituo Na. 4: Orodha ya majina ya wapiga kura imebandikwa ikiwa na kurasa 21. Kurasa hii inajumla ya wapiga kura 490. Kwa mujibu wa rekodi za Computer kituo hiki (kwa maana ya orodha yake) kilichapishwa Septemba 16, 2010.
-Ukiangalia kwa makini utakuna majina yake ambayo yamebainishwa kuwa ndiyo ya wapiga kura katika kituo hicho yanajirudia katika kituo namba 5.
-Tofauti iliyopo ni kuwa katika orodha hiyo ya namba 5 majina huku yamepunguzwa toka 490 na kuwa 402 hivyo kuwa na kurasa za majina 17 toffauti na 21 za kituo namba 4.
-Lakini orodha ya majina ya wapiga kura hiyo inaonyesha kuwa imechapishwa katika Computer Oktoba 16, 2010. (Maana yake ni kuwa hiki kimezalishwa baada ya kuwa vituo vyote vine vimekamilika hiyo Septemba 16, 2010). Hivyo ni kipya.

B). Upigaji Kura.
Kwa vile zoezi la upangaji kura limekamilika, kazi imebaki katika kupiga. Ukweli tukubali kura kwa sasa haziibiwi kwa kupiga, ingawa njia hii pia imeandaliwa kama njia ya dharula, lakini ni kwamba kura zitapigwa hivi.
· Kwa vile orodha ya majina iliyoonekana katika kituo namba 4, ndiyo yaliyojirudia kituo namba 5, basi watu hao (ambao ni wana CCM damu ama Polisi au JWT kama watakavyokuwa wameandaliwa) watajihimu kupiga kura na kukamilisha taratibu zote kituo namba 4.
· Kwa vile kila unapopiga kura kidole huwekwa wino maalum kama alama ya kumtambua aliyekwisha piga, basi wakitoka hapo watakwenda kufuta wino huo na kasha kubadili nguo zao na muda wa kurudi kituoni tena kwa ajili ya kupiga kura nyingine. Kura hii itakuwa kura ya pili kwa mtu mmoja kwa idadi ya watu 402 kituo namba 5 kati ya watu 490 wa idadi ya kituo namba 4.
· Watu hao watakuwa wakitumia shahada zao zile zile na kwa kuwa majina yao yamo katika daftari la kudumu la wapiga kura, na wino katika vidole vyao umefutwa kitaalam, basi watapiga kura bila ya wakala kulipwa hela kumshinikiza akubali au kumzuia kwa vile anachoangalia yeye ni shahada na kama imo katika daftari vitu ambavyo ni kweli vipo.
· Kwa vile wakali aliyewaona wakipiga kura katika kituo namba 4 hatotoka kuingia katika kituo namba 5, basi mamluki hao hawatabainika na hivyo watakuwa wamepiga bao la kisigino.
C). Kujumuisha matokeo.
Uchaguzi ukiisha kazi ya kujumuisha matokeo itakuwa imekwisha kwani wakifanikiwa hapo hawatakuwa na haja ya kuongeza kura nyingine juu yake kwani jambo hili litaleta utata na kuwafanya wabainike kama ambavyo ilitokea Kenya kwa kula kuzidi kutokana na ujumuishaji wake.
Hivyo Kikwete atashinda kwa 80% na CCM wataingia mtaani kushangilia wakati Chadema wakilia na kusaga meno na hapo uchaguzi utakuwa umeisha.

NJIA NYINGINE ZA WIZI ZINAZOTANGAZWA:
Kwa hakika mpaka sasa njia zote hizo zinatangazwa sitaki kuzipuuza kwa vile zote zinaweza kutumika lakini nyingi ambazo zimejulikana sasa zimetangazwa kwa makusudi kwa ajili ya kuwazubaisha wakazanie kuangalia huko huku wakitoa akili zao katika katika njii hii ambayo ilikomboa Jimbo la Busanda na Biharamulo.

mkuu,
hii analysis yako ndio haswaa watakachofanya.
Please nakuomba sana - hili bandiko lako lianzishie thread ya peke yake.
Kuliacha Ktk hii thread litazikwa na kusahaulika, watu wengi hawataliona na utakuwa hujaifanyia justice post yako na members.
Please just do it. It's extremely important.
Asante.
 
hilo ni kwa mwanza

kila kituo kina majina 100 hewa, na jumla ya vituo ni 53,000 nchi zima zidisha hapo uone ccm wana kura ngapi ambzo ni hewa!!

msiwe wabishi na kuanza kupayuka ovyo, hii barua ni ya kweli mimi nawambia

Wa 16 nakubali kwamba inaweza kuwepo vituo vyenye watu 100 au zaidi waliozidi ila usitumie maneno "kila kituo" Kijijini watu wanjuana familia zote na idadi ya watoto ulionao. Kwa hiyo kuna mbinu mbadala kwa ajili ya kuiba kijijini. Ni pamoja na kuonga mawakala na total ya kura isiyokweli.
 
Ni kweli kunaweza kuwa na mashaka juu ya authenticity ya hiyo barua hasa kwa sababu hatujui aliyeiweka hapa ameipataje. Bado najiuliza wamepata wapi guts za kuweka 'dhuluma' kama hii kwenye maandishi? Binafsi mashaka yangu hayatokani na makosa ya uandishi wa barua yenyewe (huwa wanafanya makosa ya kiuandishi makubwa kuliko haya!) bali jambo lenyewe. Hayo makosa pengne yamefanywa makusudi ili kuifanya isiaminike! Suala la whereabouts za JK katika tarehe zilizotajwa sio ishu sana.....sio kweli kwamba tunaweza kujua kwa uhakika JK yupo wapi kila siku na kwa masaa 24 (kumbuka wanatumia ndege pia kusafiri!).

Pamoja na hayo. Mimi naaza kutia shaka na hizo nyaraka. Umejiuliza kwa nini barua ya Chadema ya Kulalamikia vituo feki imeondolewa hapa jamvini? Mimi naona Ushabiki kwa CHADEMA ambao sio makini unaweza kuwaharibia siku hizi za mwisho. Kumbuka tumeambiwa hapa jamvini kuwa Lori la Bakhressa lilikamatwa Tunduma na kura Feki. Dr. Slaa akaitoa hadharani. Ona tamko la The National Electrol Commission of Tanzania - Homepage

Tuwe makini na tusipoteze dira dakika za majeruhi. Tusikunbali kudanganywa au kutiwa hofu kuhusu kura zetu. Mpigie yule unayeamini kuwa atakuongoza na anafaa kuingia IKULU. Usibadili msimamo wako kwa vitisho kama hivi sana sana kiwe kichocheo cha ku - diqualify mgombea wanaempigia debe. Mimi naona sasa washabiki wa CHADEMA wanapanick. Watuache tuchague bila kutishwa. Atakaye kumpa Dr. Slaa kura yake afanye hivyo kwa kuamini kuwa ni mtu bora na si kutishiwa na nyaraka au hadithi zisizo na ukweli ili tuamini kuwa Dr. Slaa ndio Mkombozi. kwa hila hizi watanifanya nianze kuamini tofauti na nilivyokuwa ninamuona Dr. Slaa. Ebu watu hawa wawe makini katika mikakati yao vinginevyo watampunguzia Mgombea huyo kura zake.
 
Hata kule Bukombe alipoona watu hawamtaki aliwaambia "kampigieni kura yeyote mnayemtaka ila CCM itashinda kwa kishindo". Huyu rais ni mropokaji na sasa mbinu zimefichuliwa. Mambo ya REDET na Synnovate yote yanadhihirisha hayo.
Wakuu hii isitukatishe tamaa. Twendeni tukapige kura na kura zetu zilindwe. Kuna haja ya kuongeza nguvu za ulinzi wa kura kwenye majimbo husika.

Leo Bana na Mdada wa Synovate walikuwa Raio One kile kipindi cha BBC eti walimalizia kwa kusema yale matokeo ya mwanzo yanaweza kubadilika kabisa yakawa sio yale eti katika uwanja wa siasa dakika kumi tuu zinatosha kubadilisha mwelekeo nikajiuliza sana na hitimisho lao lile mpaka sasa natafakari kitu gani kimewafanya wawe na change of mind
 
Wanachadema mna hasira kweli!!!!!!!!!! Sasa hapo una maana gani kutumia Phrase "hoja za kijinga". Nafikiri utabigwa butwaa sana tarehe 31. Kapige kura then subiri uone kama wewe tu ndiyo hauna hoja za kijinga!

Kuna swala hapa ngoja niliweke bayana, Ni kuwa tuondoe itikadi zetu za Udini/Ukabila kwa jambo muhimu kama hili la kuijenga nchi yetu sote sie ni watanzania ni wajibu wetu kuweka maslahi ya NCHI kwanza "COUNTRY FIRST" kwahiyo Mtu atoapo hija na kama unaiona imekaa kimtizamo kama hauelekei basi msahihishe na mpe mtazamo unaoufahamu ni Positive kwa nchi yetu kuliko kuambia oooh wewe ni CCM,CUF,CHADEMA haititusaidi kwani at last iwe ni CHADEMA AU CUF AU CCM atake ongoza bado ni mtanzania mwenzetu na tutamkosoa atakapo kosea na kumsahihisha kama tufanyavyo hapa.

Kama Msemavyo hili Janvi ni la POSITIVE THINKERS basi lets post positive ideals for the sake of our Country.

 
Tuwe makini na tusipoteze dira dakika za majeruhi. Tusikunbali kudanganywa au kutiwa hofu kuhusu kura zetu. Mpigie yule unayeamini kuwa atakuongoza na anafaa kuingia IKULU. Usibadili msimamo wako kwa vitisho kama hivi sana sana kiwe kichocheo cha ku - diqualify mgombea wanaempigia debe. Mimi naona sasa washabiki wa CHADEMA wanapanick. Watuache tuchague bila kutishwa. Atakaye kumpa Dr. Slaa kura yake afanye hivyo kwa kuamini kuwa ni mtu bora na si kutishiwa na nyaraka au hadithi zisizo na ukweli ili tuamini kuwa Dr. Slaa ndio Mkombozi. kwa hila hizi watanifanya nianze kuamini tofauti na nilivyokuwa ninamuona Dr. Slaa. Ebu watu hawa wawe makini katika mikakati yao vinginevyo watampunguzia Mgombea huyo kura zake.

LeopoldByongje,
Kwani kwenye barua hii Dr Slaa, CHADEMA na washabiki wao wanaingiaje/wanahusikaje? Kwa nini sio CCM, CUF, NCCR-Mageuzi au TLP?
 
narudia kusema, ccm inaipeleka nchi kubaya kwa tamaa zao zakutaka kutawala milele, wanataka uongozi wa nchi kwa mabavu, wameshindwa hoja, wameshindwa ushawishi, wanajiaandaa kwa madeni za kihuni, nawaonya Tena, Vijana wa Mwanza nawajua mimi, nawajua walivyo na morali, siku kama 3 hivi Mwanza, lakini nitapiga kura mwanza, nawaonya tena kuacha upuuzi wao, wataibomoa mwanza mapandemapande, Je Taifa liko Tayari kutengeneza wakimbizi baada ya wale wa Pemba ?
 
Wa 16 nakubali kwamba inaweza kuwepo vituo vyenye watu 100 au zaidi waliozidi ila usitumie maneno "kila kituo" Kijijini watu wanjuana familia zote na idadi ya watoto ulionao. Kwa hiyo kuna mbinu mbadala kwa ajili ya kuiba kijijini. Ni pamoja na kuonga mawakala na total ya kura isiyokweli.

niliyepost hapo najua nini kinaendelea. ingia ndani ya website ya nec ID 19272313 haina mwenye ID 19272312 ina mwenyewe
hebu ingia kwenye website ya nec uingize hizo namba then uniambie. nakusubiri nina dk 15 kuwa hapa janvini

ndo maana mnaambiwa mrinde kura mkiondoa tu.........
 
Nilikua na mawazo kama hayo hapo Chini.
Ila kuna vitu vingi sana vya kusaidia ushahidi
1.Confirmation ya mkutano Lakairo-Hii tumeipata
2.Kuna Signature, huyu mtu yupo na profile yake ipo kuanzia shule alizosoma-we can get the signature
3.Barua ina muhuri wa Halmashaur, Kama huu mhuri is that much Easy Accesible basi kuna Tatizo.
4.Invisible namuamini sana kwa umekini, na ndo maana JF ipo hapa ilipo.
need I say more?

Mkuu Invisible,

Kweli una uhakika hiyo barua imeandikwa na huyo anayesemekana ameandika?

Kama ni kweli, pelekeni kwenye vyombo vyote ili ukweli ujulikane. Hatuko hapa kutetea maovu kama ni kweli lazima kitendo hicho kilaaniwe na wahusika kuchukuliwa hatua. Ila my first instinct ni kwamba hiyo barua ni forgery; mtu anapanga mipango kama hiyo na ataweka kwenye maandishi

Kwa Tanzania lolote linawezekana na wacha tusubiri ukweli.

Kwanza niseme kwamba kama barua hii ni ya kweli basi uchaguzi hauna maana ni vyema usiwepo maana JK ni mtu wa hatari. Baada ya kusema hivyo niseme nina wasiwasi kidogo na barua hii. Kwanza je ni nani Wasimamizi wasaidizi wa Uchaguzi. Kama ni wale wanaosimamia uchaguzi ngazi ya wilaya then hii barua inaweza kuwa sahihi. Lakini kwa nini sensitve issue kama hii iwe official? Nafikiri haiwezakani?. Nikiangalia kwa makini hii barua haijaibiwa kutoka kwenye file na wala haina mhuri wa kupokelewa na ofisi yoyote...kwa hiyo ikoje hii?. Unaweza kusema ina sahihi...lakini sahihi ni scanned na rahisi mtu kuiba sahihi kama hiyo

Muhimu: Kila Chama kufuatilia vizuri vituo vya ziada na idadi ya watu ambao kwa makusudi imezidishwa. Hili linaonekana kuwa tatizo la kitaifa lililopangiliwa vyema na watakuwa wanajua idadi ya watu wanaozidi kila sehemu.

Conclusion: Hii barua nafikiri si ya kweli lakini sasa kuna uhakika kabisa wa moja ya mbinu itakayotumika kuiba kura

totally agree with you. Siamini hiyo barua kama imetoka halmashauri ni ya kweli

Selous,

Tarehe 16 Oktoba, JK na msafara wake walikuwa mkoa wa Pwani.

Mimi ninaamini hii barua ni hoax! Invisible ondoa hii thread
 
Kumbe kuna watu wana mtizamo binafsi usiofuata mkumbo wa majority.

I call you GREAT INDEPENDENT THINKERS.

Asanteni sana kwa kutokuendekeza siasa za kishabiki.
 
Dah! Nimechoka Kabisa! Halafu Mwisho wa Siku watasema Uchaguzi Ulikuwa Huru na wa Haki

Nashauri CHADEMA waitoke copy nyingi na Igawiwe kwa Nguvu ya Umma ili iweze Kuhukumu

Gadem Shit
Mimi nimeshasambaza copy za hiyo barua kwa watu wote waliopo kwenye e mail list yangu. Nimezigeuza kuwa pdf.
 


Kuna swala hapa ngoja niliweke bayana, Ni kuwa tuondoe itikadi zetu za Udini/Ukabila kwa jambo muhimu kama hili la kuijenga nchi yetu sote sie ni watanzania ni wajibu wetu kuweka maslahi ya NCHI kwanza "COUNTRY FIRST" kwahiyo Mtu atoapo hija na kama unaiona imekaa kimtizamo kama hauelekei basi msahihishe na mpe mtazamo unaoufahamu ni Positive kwa nchi yetu kuliko kuambia oooh wewe ni CCM,CUF,CHADEMA haititusaidi kwani at last iwe ni CHADEMA AU CUF AU CCM atake ongoza bado ni mtanzania mwenzetu na tutamkosoa atakapo kosea na kumsahihisha kama tufanyavyo hapa.

Kama Msemavyo hili Janvi ni la POSITIVE THINKERS basi lets post positive ideals for the sake of our Country.


You are right. watu humu wanashindwa kuelewa CCM ina mbinu nyingi za kudiscourage watu. Issue hapa ni kuscare vijana na wasomi waachane na mambo ya kura! Kupata headletter ya ofisi yoyote Tanzania ni rahisi na pia signature inaweza kuwa scanned. Bora hapa watu wangeongelea vipi mawakala wawezeshwe ili iwe ngumu kuwaonga. Na endapo SLaa ataingia kichwakichwa katika ili we definitely shall lose
 
Jamani hii ni vita, raha ya vita ni kujua mbinu za mpinzani wako na kuzitafutia Dawa, sasa tushajua cha msingi ni kuhakikisha kuwa hizo mbinu chafu hazifanikiwi kwa namna yoyote
 
@Buckreef... ulishaponza watu wakala ban na waliua wanasema ukweli kuhusu wewe... uko hapa kuwakilisha watu, umesoma lakini huna weledi ati unasema oindoa thread... kwasababu inakugusa eh???
 
dah hii hali ni mbaya sana kutaka urais kwa kumwaga damu, eti green guard wafanye kazi yao, sasa leo anaenda kuongea TBC1 ili iweje kama wamekubaliana kuwe na vituo hewa kila kata na majina ya vijana yasibandikwe. This is bullshit....Mkwere anatia aibu jamani.
 
Mimi nimeshasambaza copy za hiyo barua kwa watu wote waliopo kwenye e mail list yangu. Nimezigeuza kuwa pdf.

With all due respect, huna uhakika na origin ya document na authenticity yake. Unatuma email kwa chain ya receivers wewe ukiwa kama chanzo cha habari. Huko ni kukurupuka na kunaweza kuwa sawa na uchochezi.
 
Bahati mbaya tumekumbana na barua hizi ikabidi tuwashirikishe!

chakachua_halmashauri_mwanza1.jpg

chakachua_halmashauri_mwanza2.jpg
Copy za barua in pdf:
 

Attachments

Nachotaka kuuliza ni kimoja tu.. Kwa nini watu wanasema matumizi ya IT wakati wananchi watapiga kura zao kwa kutumia kalamu na dole gumba kisha kura zao zitahesabiwa kwa mkono moja baada ya nyingine pasipo kutumia machine au PC..

Katika kujihadhari na jambo hili, matumizi ya wajuzi wa IT yatahitajika wakati gani?..
Watahitajika wakati NEC inayapokea jimbo linatuma kura 200 PC ya NEC ina-rekodi kura 300 ni kazi ndogo tu hiyo.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom