Misterdennis
JF-Expert Member
- Jun 4, 2007
- 1,741
- 481
Nyaraka hiyo ilikuwa ikitoa maelekezo ya Mpango huu ufanyike soma hapa chini na linganisha sasa:
Ili JK aweze kushinda kwa 80% kikao hicho kiliandaa njia hii!
CCM tayari wameshajihakikishia ushindi kwa vile tayari wameshakamilisha kazi yao. Katika uchaguzi wamekuwa wakitimiza ratiba tu lakini matokeo ya uchaguzi yanatambulika na mpango kamili wa kukamilisha matokeo hayo ni huu.
A). Upangaji wa vituo
NEC imekuwa ikiendesha zoezi la upangaji wa vituo chini ya uangalizi maalum wa watalaam wa IT (kama ambavyo imekwsiha kuelezwa na baadhi ya wadau hapa JF, ambao ni wa 16 na MBWA MKALI katika Post zilizopita).
i).Utaratibu wa awali ulikuwa ni kuandaa vituo halali ambavyo viliandaliwa na kukamilika.
ii). Utaratibu wa pili ulikuwa ni kuandaa vituo hewa ambavyo viliandaliwa baada ya vituo vya kwanza kukamilika (Hii ni kwa lengo la kutambua vituo awali na kutofautisha vile vya kuchahachulia).
Vituo Hewa:
Jambo hili limekuwa likiwatatiza wengi sana na wengine kushindwa kuamini iwapo jambo hili linawezekana. Ukweli linawezekana na hapa natoa mmoja ya kituo hewa.
· Hapa kwa mujibu wa tume vituo vimepangiliwa kwa majina/namba.
· Kituo ambacho nawatolea mfano hai ni Na. 00020941. Ama kwa jina kinaitwa Kituo cha Shule ya Msingi Kapangaja. Kipo katika Kata ya Bugongwa wilaya ya Ilemela na jimbo la Ilemela.
-Eneo hili la shule ya msingi limegawanywa na kuzaa jumla ya vituo 5.
-Tatizo lipo katika vituo viwili ambavyo ni kituo namba 4 na namba 5.
· Kituo Na. 4: Orodha ya majina ya wapiga kura imebandikwa ikiwa na kurasa 21. Kurasa hii inajumla ya wapiga kura 490. Kwa mujibu wa rekodi za Computer kituo hiki (kwa maana ya orodha yake) kilichapishwa Septemba 16, 2010.
-Ukiangalia kwa makini utakuna majina yake ambayo yamebainishwa kuwa ndiyo ya wapiga kura katika kituo hicho yanajirudia katika kituo namba 5.
-Tofauti iliyopo ni kuwa katika orodha hiyo ya namba 5 majina huku yamepunguzwa toka 490 na kuwa 402 hivyo kuwa na kurasa za majina 17 toffauti na 21 za kituo namba 4.
-Lakini orodha ya majina ya wapiga kura hiyo inaonyesha kuwa imechapishwa katika Computer Oktoba 16, 2010. (Maana yake ni kuwa hiki kimezalishwa baada ya kuwa vituo vyote vine vimekamilika hiyo Septemba 16, 2010). Hivyo ni kipya.
B). Upigaji Kura.
Kwa vile zoezi la upangaji kura limekamilika, kazi imebaki katika kupiga. Ukweli tukubali kura kwa sasa haziibiwi kwa kupiga, ingawa njia hii pia imeandaliwa kama njia ya dharula, lakini ni kwamba kura zitapigwa hivi.
· Kwa vile orodha ya majina iliyoonekana katika kituo namba 4, ndiyo yaliyojirudia kituo namba 5, basi watu hao (ambao ni wana CCM damu ama Polisi au JWT kama watakavyokuwa wameandaliwa) watajihimu kupiga kura na kukamilisha taratibu zote kituo namba 4.
· Kwa vile kila unapopiga kura kidole huwekwa wino maalum kama alama ya kumtambua aliyekwisha piga, basi wakitoka hapo watakwenda kufuta wino huo na kasha kubadili nguo zao na muda wa kurudi kituoni tena kwa ajili ya kupiga kura nyingine. Kura hii itakuwa kura ya pili kwa mtu mmoja kwa idadi ya watu 402 kituo namba 5 kati ya watu 490 wa idadi ya kituo namba 4.
· Watu hao watakuwa wakitumia shahada zao zile zile na kwa kuwa majina yao yamo katika daftari la kudumu la wapiga kura, na wino katika vidole vyao umefutwa kitaalam, basi watapiga kura bila ya wakala kulipwa hela kumshinikiza akubali au kumzuia kwa vile anachoangalia yeye ni shahada na kama imo katika daftari vitu ambavyo ni kweli vipo.
· Kwa vile wakali aliyewaona wakipiga kura katika kituo namba 4 hatotoka kuingia katika kituo namba 5, basi mamluki hao hawatabainika na hivyo watakuwa wamepiga bao la kisigino.
C). Kujumuisha matokeo.
Uchaguzi ukiisha kazi ya kujumuisha matokeo itakuwa imekwisha kwani wakifanikiwa hapo hawatakuwa na haja ya kuongeza kura nyingine juu yake kwani jambo hili litaleta utata na kuwafanya wabainike kama ambavyo ilitokea Kenya kwa kula kuzidi kutokana na ujumuishaji wake.
Hivyo Kikwete atashinda kwa 80% na CCM wataingia mtaani kushangilia wakati Chadema wakilia na kusaga meno na hapo uchaguzi utakuwa umeisha.
NJIA NYINGINE ZA WIZI ZINAZOTANGAZWA:
Kwa hakika mpaka sasa njia zote hizo zinatangazwa sitaki kuzipuuza kwa vile zote zinaweza kutumika lakini nyingi ambazo zimejulikana sasa zimetangazwa kwa makusudi kwa ajili ya kuwazubaisha wakazanie kuangalia huko huku wakitoa akili zao katika katika njii hii ambayo ilikomboa Jimbo la Busanda na Biharamulo.
mkuu,
hii analysis yako ndio haswaa watakachofanya.
Please nakuomba sana - hili bandiko lako lianzishie thread ya peke yake.
Kuliacha Ktk hii thread litazikwa na kusahaulika, watu wengi hawataliona na utakuwa hujaifanyia justice post yako na members.
Please just do it. It's extremely important.
Asante.