Uchambuzi: Hali ya Usalama Duniani chini ya Rais Donald Trump. Ukraine imeambiwa ili kuwe na Amani isahau Crimea na je Dunia imejiandaa vipi

Uchambuzi: Hali ya Usalama Duniani chini ya Rais Donald Trump. Ukraine imeambiwa ili kuwe na Amani isahau Crimea na je Dunia imejiandaa vipi

Mnatuchosha xx ,
Kwani huyo Trump ndio rais wa dunia au wamerekani
Rafiki, usichoke hii ndiyo JF ukiingia hapa IF jivinjari.

Trump ndie raisi wa Dunia kwa sasa na kila mtu awe tayari kwa mshikemshike.
 
Urusi wanairudisha nyuma Dunia enzi za Goliati na Daudi,yaani mwenye nguvu anaweza kuongeza enao la nchi yake anavyo taka,Hali hiyo haiheshimu mipaka ya nchi Dunia ikenda huko basi vita zitakuwa nyingi sana ni heri Dunia ikaungana kupinga Hilo Putuni hafai
Mkuu, hiyo ndo hegemony (nguvu ya kisiasa, kiuchumi na kijeshi) na geopolitics (nguvu ya kisiasa kimataifa inounganishwa na eneo la kijiografia).

Unalinda rasilimali zako na zingine ukiona zamendewa au kumezewa mate ndo waziwahi kuzilinda.

Gaza ndio mradi wa Marekani lakini asiwe na tamaa, pana gesi ya kutosha pale.

Dunia yasonga mbele sasa mwenye nguvu mpishe.

Afrika ina uamuzi iende China na Russia au iende magharibi na Marekani.
 
Ukraine aliiacha Crimea kitambo ila Urusi alitaka eneo zaid ndo shida ilianzia hapo
Kama aliiacha asingeendelea kuishambulia kwa mabomu anopewa na NATO.

Na hapo ndipo mazee Lanza awaambia Ukraine wasahau Crimea.

Angesahau hilo lakini ni NATO/Marekani ndo walo nyuma ya Ukraine.
 
Mkuu, hata Marekani wenyewe wametoa taswira mbaya sanakwa kuwaachia Israeli waue watu wanavyopenda huko Gaza na sasa Lebanon.

Ni wazi kabisa kinofanyika ni uhalifu wa kivita lakini hata UN mikono imefungwa.
FAFO ya October 07 hiyo.
 
Waarabu WA buza bwana,Yani Rais wao kauawa,hanniya kauawa Teheran etii Leo Irani ana nguvu,hakuna nchi mashariki ya kati anaweza pigana na israeli
Mkuu, sasa hivi anaewindwa ni Ayatollah Khamenei na alindwa masaa yote kiwa chini ya uangalizi maalum.

Usije kushangaa yakatokea kama yale ya jenerali Suleiman.

Yasemwa Iran imegundua mfumo mzima wa ujasusi umeingiliwa na Mossad.

Hivyo sasa hivi watumia chekeche kuchuja mchele na makapi.

Kinoshangaza ni kwamba Iran ni moja ya nchi chache duniani ambazo zina wizara kamili ya ujasusi iitwayo Ministry of intelligence and Security (MOIS) na pia wana jeshi la mapinduzi la IRGC lakini badala ya kushughulika na masuala mazito ya kiusalama kwa makini wao wahangaika na wapinzani wa utawala wa Tehran pamoja na wale wa-Iran wanoipinga serikali.

Hivyo waweza kuona jinsi kazi ilivyo rahisi kwa vyombo kama Mossad kufanya uingiliaji (infiltration) kwenye viunga vya ujasusi ndani ya Iran yenyewe.
 
Kuingia kwa Trump inamaanw mwenye negotiations power kubwa hapo ni mrusi, subiri uone kama mrusi ataachia maeneo hayo
Kama unadhani Putin atakuwa na free lunch kutoka kwa trump pitia hii article, Nina hakika utarudi hapa kunishukur 🙏 🙏 🙏

 
Mkuu, hiyo ndo hegemony (nguvu ya kisiasa, kiuchumi na kijeshi) na geopolitics (nguvu ya kisiasa kimataifa inounganishwa na eneo la kijiografia).

Unalinda rasilimali zako na zingine ukiona zamendewa au kumezewa mate ndo waziwahi kuzilinda.

Gaza ndio mradi wa Marekani lakini asiwe na tamaa, pana gesi ya kutosha pale.

Dunia yasonga mbele sasa mwenye nguvu mpishe.

Afrika ina uamuzi iende China na Russia au iende magharibi na Marekani.
Fikra za namna hii zikipaliliwa Dunia haita kalika itakuwa vita Kila siku kwani hao wanyonge hawapo tayari kutawaliwa na wenye nguvu,chukulia nchi yako inatwaliwa na wageni na Mali zako wanasambaratisha,unalazishwa kuwatumikia ni wapuuzi watakaoikubali hali hiyo lkn wanaume kama Ukraine watakuwa tayari kufa
 
Urusi wanairudisha nyuma Dunia enzi za Goliati na Daudi,yaani mwenye nguvu anaweza kuongeza enao la nchi yake anavyo taka,Hali hiyo haiheshimu mipaka ya nchi Dunia ikenda huko basi vita zitakuwa nyingi sana ni heri Dunia ikaungana kupinga Hilo Putuni hafai
Mkiwa hamujui mambo msipende kujidhihirisha kama muna upumbavu mwingi kiasi hiki jipya lipi alolifanya Russia ambalo marekani ufaransa Uingereza mnawaona wamestaarabika hawajalifanya kama mipaka marekani kabeba Guam kabeba guantanamo bay kabeba sehemu tele mkiwa hamuna akili musitake kila mtu ajue kama hamna akili
 
Kama ni hivyo Urusi itakuwa imetoa taswira mbaya sana Duniani, sasa Nchi yoyote yenye nguvu inaweza kumvamia jirani yake na kuteka eneo lolote ilitakalo na kusema kuwa ni lake.
Kama ilivyo toa taswira mbaya marekani kuteka maeneo ya watu ama sijakuelewa
 
Fikra za namna hii zikipaliliwa Dunia haita kalika itakuwa vita Kila siku kwani hao wanyonge hawapo tayari kutawaliwa na wenye nguvu,chukulia nchi yako inatwaliwa na wageni na Mali zako wanasambaratisha,unalazishwa kuwatumikia ni wapuuzi watakaoikubali hali hiyo lkn wanaume kama Ukraine watakuwa tayari kufa
Wanyonge wengine mbona hamkuwasemea au hamuwasemei au wao hawafai kusemewa
 
Mkiwa hamujui mambo msipende kujidhihirisha kama muna upumbavu mwingi kiasi hiki jipya lipi alolifanya Russia ambalo marekani ufaransa Uingereza mnawaona wamestaarabika hawajalifanya kama mipaka marekani kabeba Guam kabeba guantanamo bay kabeba sehemu tele mkiwa hamuna akili musitake kila mtu ajue kama hamna akili
Kwani marekani akitenda uharifu ndo uharifu kuendelea we mbona lugha yako si ya kistaarabu?
 
Kwani marekani akitenda uharifu ndo uharifu kuendelea we mbona lugha yako si ya kistaarabu?
Kama nimekukwaza kwa lugha zangu naomba uniwie radhi sana mkuu nisamehe ila kama uhalifu hautakiwi uendelee kwanza lazima haki za watu zilizochukuliwa huko kwengine na wengine zirejeshwe marekani mtoaji msaada mkubwa kwa ukraine ili arejeshe maeneo yake wakati huo huo yeye anakalia maeneo ya watu unapata uhalali gani wakuikandia Russia kwanza kabla ya kuanzia na marekani anaijaza silaha Ukraine
 
Kama nimekukwaza kwa lugha zangu naomba uniwie radhi sana mkuu nisamehe ila kama uhalifu hautakiwi uendelee kwanza lazima haki za watu zilizochukuliwa huko kwengine na wengine zirejeshwe marekani mtoaji msaada mkubwa kwa ukraine ili arejeshe maeneo yake wakati huo huo yeye anakalia maeneo ya watu unapata uhalali gani wakuikandia Russia kwanza kabla ya kuanzia na marekani anaijaza silaha Ukraine
Hakuna muharifu anayepaswa kutetewa awe Rasia,Iran,Israeli au USA
 
Back
Top Bottom