Oya Tusepe
JF-Expert Member
- Aug 3, 2016
- 265
- 870
Salam,
Kuna baadhi ya watu wamekuwa wakishindwa kuelewa kwamba katika jamii yoyote kupata umaarufu na heshima kuna gharama yake, tena gharama kubwa!.
Twende sambamba katika uchambuzi huu ili uweze kuelewa kinagaubaga, ya kwamba ni kwanini ni vigumu kumpoteza kijana Naseeb Abdul na kuizima kabisa nyota yake?
Kwa wanaofuatilia game ya mziki wetu wa Bongo wanaelewa kwamba Diamond si msanii wa kwanza wa kizazi kipya kupendwa sana na mashabiki zake, wapo watu waliowahi kuhusudiwa ndani na nje ya mipaka ya Tanzania na kupata mafanikio makubwa mfano tunae bwana Nice Mkenda, Mr Nice na wengine wengi.
Baada ya Diamond Platnumz kupokelewa rasmi na wa Tz wenzake kwenye game ya mziki, upepo wa sanaa nzima ya uimbaji wa Bongo ulibadilika kabisa jambo liliongeza speed ya kazi nzuri zaidi kutoka kwa wasanii wengine..
Pius unajaribu kusema nini?!!..
Anhaa.. Ninachojaribu kusema ni kwamba, unakumbuka video za wanamuziki wa Tanzania kabla ya ujio wa mtoto wa Tandale? Uvaaji je? Uzingativu wa mambo ya Muonekano kuanzia sura mpaka mwili mzima ikiwa ni pamoja na "fitness".. Mbinu mbalimbali za scandel za kibiashara? Attention ya media?.. Mambo haya yalifanya watanzania bila kujali lika kuanza kuwa makini na kufatilia burudani na vitimbwi vya ndani ya nchi yao katika upande wa sanaa ya uimbaji kwa kasi kubwa.
Pius mbona kama sijakupata vizuri?..
Ok ngoja niseme hivi: Hivi unajua kwamba hata mitindo ya uvaaji wa vijana wa kibongo imekuwa influenced pakubwa na kijana Diamond Platnumz? (Kubali au kataa ni juu yako).
Diamond Platnumz amejitengenezea ufalme katika akili za vijana wengi sana wa Tanzaia, wanamsikiliza na wanafanya anachofanya au anachotaka yeye.
Vijana wapya kwenye game wanashindwa kuelewa jambo moja ambalo ni kubwa sana kibiashara, kutengeneza Ngome.
Unapoanza biashara yoyote ile jambo la kwanza unalopaswa kulizingatia sana ni Aina gani ya wateja unaoenda kudeal nao.
Watanzania ni watu wanaowaheshimu sana wale vinara wanaoanzisha mambo makubwa au kuleta mabadiliko.
Fikiria jambo moja.. Hivi ulishawahi kujiuliza ni nini kitatokea endapo atashindanishwa Diamond Platnumz na Juma Nature " kiroboto" nini kitatokea? Amini usiamini Nature ataibuka mshindi.. Kwanini? Kwa sababu watanzania wanawaheshimu waanzilishi.
Kulingana na mambo ambayo Diamond Platnumz ameifanyia nchi ya Tanzania daima mchango wake hautafutika abadan.. Ni mbunifu na ni moja kati ya wasanii wachache unayeweza kusikilza playlist ya nyimbo zake zote bila kuchoka kuanzia asubuhi mpaka usiku, anafanya kazi nzuri.
Fikiria jambo jingine.. Yupo wapi Fundi Rich mavoko? Ommy Dimpoz, Ali Kiba, Asley na wengine wengi wenye sauti za kuvutia? Mbona hawana ushawishi mkubwa kama bwana Nasseb? Kuna makosa.
Diamond Platnumz ni kama Clouds Fm tu.. Ili kuviondoa hivi vitu mchezoni inahitaji muda na kizazi kingine.. Mtu mmoja anayeitwa Warren Buffet àliwahi kusema kila kampuni itaweza kudumu kwenye soko na kuwa stable katika ubunifu wa kawaida kwa muda wa miaka 30 na kama ubunifu hautaongezeka hata zaidi basi kampuni hiyo itafutika na kusahaulika kabisa.. Warren anazungumzia swala la generation.
Nitoe rai kwa vijana wanaojaribu kumchalenji bwana Nasseeb tena kwa kugeza mbinu zake za kibiashara kwamba WAKAE CHONJO na kwa tahadhari kubwa.
Mwisho napenda kutoa ushauri kwa kijana Konde boy kwamba afanye kazi na atafute ubunifu mpya na sio kuiga iga mambo.. Na wala usitafute kuonewa huruma na yeyote. Apambane kutengeneza Ngome yake mpya kwakuwa ni suala na muda mrefu.
Kuna baadhi ya watu wamekuwa wakishindwa kuelewa kwamba katika jamii yoyote kupata umaarufu na heshima kuna gharama yake, tena gharama kubwa!.
Twende sambamba katika uchambuzi huu ili uweze kuelewa kinagaubaga, ya kwamba ni kwanini ni vigumu kumpoteza kijana Naseeb Abdul na kuizima kabisa nyota yake?
Kwa wanaofuatilia game ya mziki wetu wa Bongo wanaelewa kwamba Diamond si msanii wa kwanza wa kizazi kipya kupendwa sana na mashabiki zake, wapo watu waliowahi kuhusudiwa ndani na nje ya mipaka ya Tanzania na kupata mafanikio makubwa mfano tunae bwana Nice Mkenda, Mr Nice na wengine wengi.
Baada ya Diamond Platnumz kupokelewa rasmi na wa Tz wenzake kwenye game ya mziki, upepo wa sanaa nzima ya uimbaji wa Bongo ulibadilika kabisa jambo liliongeza speed ya kazi nzuri zaidi kutoka kwa wasanii wengine..
Pius unajaribu kusema nini?!!..
Anhaa.. Ninachojaribu kusema ni kwamba, unakumbuka video za wanamuziki wa Tanzania kabla ya ujio wa mtoto wa Tandale? Uvaaji je? Uzingativu wa mambo ya Muonekano kuanzia sura mpaka mwili mzima ikiwa ni pamoja na "fitness".. Mbinu mbalimbali za scandel za kibiashara? Attention ya media?.. Mambo haya yalifanya watanzania bila kujali lika kuanza kuwa makini na kufatilia burudani na vitimbwi vya ndani ya nchi yao katika upande wa sanaa ya uimbaji kwa kasi kubwa.
Pius mbona kama sijakupata vizuri?..
Ok ngoja niseme hivi: Hivi unajua kwamba hata mitindo ya uvaaji wa vijana wa kibongo imekuwa influenced pakubwa na kijana Diamond Platnumz? (Kubali au kataa ni juu yako).
Diamond Platnumz amejitengenezea ufalme katika akili za vijana wengi sana wa Tanzaia, wanamsikiliza na wanafanya anachofanya au anachotaka yeye.
Vijana wapya kwenye game wanashindwa kuelewa jambo moja ambalo ni kubwa sana kibiashara, kutengeneza Ngome.
Unapoanza biashara yoyote ile jambo la kwanza unalopaswa kulizingatia sana ni Aina gani ya wateja unaoenda kudeal nao.
Watanzania ni watu wanaowaheshimu sana wale vinara wanaoanzisha mambo makubwa au kuleta mabadiliko.
Fikiria jambo moja.. Hivi ulishawahi kujiuliza ni nini kitatokea endapo atashindanishwa Diamond Platnumz na Juma Nature " kiroboto" nini kitatokea? Amini usiamini Nature ataibuka mshindi.. Kwanini? Kwa sababu watanzania wanawaheshimu waanzilishi.
Kulingana na mambo ambayo Diamond Platnumz ameifanyia nchi ya Tanzania daima mchango wake hautafutika abadan.. Ni mbunifu na ni moja kati ya wasanii wachache unayeweza kusikilza playlist ya nyimbo zake zote bila kuchoka kuanzia asubuhi mpaka usiku, anafanya kazi nzuri.
Fikiria jambo jingine.. Yupo wapi Fundi Rich mavoko? Ommy Dimpoz, Ali Kiba, Asley na wengine wengi wenye sauti za kuvutia? Mbona hawana ushawishi mkubwa kama bwana Nasseb? Kuna makosa.
Diamond Platnumz ni kama Clouds Fm tu.. Ili kuviondoa hivi vitu mchezoni inahitaji muda na kizazi kingine.. Mtu mmoja anayeitwa Warren Buffet àliwahi kusema kila kampuni itaweza kudumu kwenye soko na kuwa stable katika ubunifu wa kawaida kwa muda wa miaka 30 na kama ubunifu hautaongezeka hata zaidi basi kampuni hiyo itafutika na kusahaulika kabisa.. Warren anazungumzia swala la generation.
Nitoe rai kwa vijana wanaojaribu kumchalenji bwana Nasseeb tena kwa kugeza mbinu zake za kibiashara kwamba WAKAE CHONJO na kwa tahadhari kubwa.
Mwisho napenda kutoa ushauri kwa kijana Konde boy kwamba afanye kazi na atafute ubunifu mpya na sio kuiga iga mambo.. Na wala usitafute kuonewa huruma na yeyote. Apambane kutengeneza Ngome yake mpya kwakuwa ni suala na muda mrefu.