Nanyaro Ephata
JF-Expert Member
- Jan 22, 2011
- 1,234
- 1,815
- Thread starter
- #61
Kitabu.Mossad
Mwandishi.Michael Bar Zohar & Nissim Mishal
Mchambuzi.Nanyaro EJ
Chapter 10
“I WANT A MIG-21!”
Mwandishi anasema kuwa Mfalme Hasan wa pili wa Moroco alikuwa anapenda maisha ya anasa,na alikuwa anaendekeza umagharibi sana.Hii ilimfanya atengwe nan chi nyingine za Kiarabu,nay eye Mfalme kuhofia kuuwawa na Misri.Kwa Mossad ilikuwa ni fursa ya kupata mshirika katika Ulimwengu wa Kiarabu,hivo haraka sana walijipenyeza ndani ya Serikali ya Moroco ambako walitoa usaidizi wa ulinzi na mafunzo kwa kikosi maalum cha kumlinda Mfalme!
Mwaka 1965 waziri wa mambo ya ndani wa Moroco ambaye alikuwa mtu katili na jeuri sana,mtu aliyeuwawa kila mpinzani wa Mfalme,na mfalme alimwamini sana.Huyu waziri aliwasiliana na Meir Amit ambaye alikuwa mkurugenzi wa Mossad kumwomba amsaidie kumtafuta mpinzani mkuu wa Mfalme Bwana Mehdi Ben-Barka,ambaye sio kuwa mpinzani tu alikuwa adui namba moja wa Ufalme,huyu jamaa alihukumiwa kifo akiwa hayupo,na haikujulikana amejificha wapi,jitihada za Moroco kumpata ziligonga mwamba na sasa waliomba msaada wa Mossad.Mossad ambao wametapakaa duniani kote waliweza kugundua kuwa huyu bwana alikuwa amejificha nchini Uswisi,ambako walimfuatilia kwa muda mrefu na siku moja alienda Paris ambako alitekwa na kisha kupotea kabisa.Kupotea kwake kulikuja kuwa skendo kubwa hasa baada ya serikali ya ufaransa kugundua kuwa Israel ilihusika……..hali hii ilileta sintofahamu kubwa maana ilikuwa kinyume kabisa na utaratibu wa Mossad ikabidi Waziri mkuu aunde tume kuchunguza sakata hili(Wakati huo Amit alikuwa hakubaliki kabisa ndani ya Mossad)
Mkurugenzi wa Mossad alikuwa mtu mwenye akili,aliamua kufanya operesheni Diamond ambayo ilikuja kumpa heshima kubwa sana.Hii ni operesheni iliyotorosha ndege ya kivita aina ya MiG 21,ndege hii ilitengenezwa huko Urusi,ilikuwa na teknolojia kubwa sana,hata magharibi hawakuwa na ndege hii.Kwa Wazayuni ilikuwa jambo gumu lakini ilikuwa lazima walifanye.Wakati huo Urusi ilikuwa imegawa ndege hizi kwa baadhi ya nchi za kijamaa ikiwepo Iraq.Mossad walifanya upelelezi wao wakagundua kuwa wanaweza kutumia mgogoro wa Wakurdi na serikali kujipenyeza ndani ya Iraki,hivo walianza kutoa msaada wa silaha kwa wapiganaji wa Kikurdi ambao walikuwa wanapigana dhidi ya Serikali ya Bagdad!
Mossad walikuja kumgundua Pilot mmoja ambaye hakupendezwa na amri za kuwaua watoto na wanawake wa kikurdi,huyu Pilot aliitwa Redfa,na kwa miaka mingi hakupanda cheo hivo akawa amejaa uchungu mkali.Wataalam wa Mossad wakaanza kumtongoza na kumwahidi fedha nyingi sana pamoja maisha yeye na familia yake.Baada ya muda mrefu wa mazungumzo Piloti akaingia kingi na operesheni ikaandaliwa
Pilot Redfa alichukuliwa na Mossad ambako alifanyiwa mafunzo mbalimbali kwa siri,na wakakubaliana siku ambayo yeye Redfa angerusha ndege MiG 21 kama vile anaenda kwenye majukumu ya kawaida ya kijeshi,akiwa angani alipaswa kuielekeza Israel ambako angetua kwenye moja ya viwanja vya kijeshi.Kabla hajaondoka familia yake yote ilipelekwa Uingereza kisha USA na baadae wangekuja kukutana Israel ambako wangeishi maisha yao yote.Pilot alikubali na siku ikapangwa ambayo nchini Israel ni watu wanne tu walijua kuhusu hili na Redfa alichukua ndege na kuitoroshea nchini Israel……hii ilikuwa na mwaka mmoja tangu mazungumzo yaanze,na miezi kumi kabla ya vita ya siku sita kuanza..Kwa Israel ilikuwa faraja kubwa
Pilot Redfa na familia yake waliishi Israel ila dhambi ya usaliti ilimwandamana ikabidi aombe kuhamia Ulaya angalau asahau.hata huko Ulaya hali iliendelea kuwa mbaya na mwaka 1988 miaka 22 baadae alifariki kwa ugonjwa wa mstuko wa moyo.Mazishi yake yalifanywa na serikali ya Israel
Mwandishi.Michael Bar Zohar & Nissim Mishal
Mchambuzi.Nanyaro EJ
Chapter 10
“I WANT A MIG-21!”
Mwandishi anasema kuwa Mfalme Hasan wa pili wa Moroco alikuwa anapenda maisha ya anasa,na alikuwa anaendekeza umagharibi sana.Hii ilimfanya atengwe nan chi nyingine za Kiarabu,nay eye Mfalme kuhofia kuuwawa na Misri.Kwa Mossad ilikuwa ni fursa ya kupata mshirika katika Ulimwengu wa Kiarabu,hivo haraka sana walijipenyeza ndani ya Serikali ya Moroco ambako walitoa usaidizi wa ulinzi na mafunzo kwa kikosi maalum cha kumlinda Mfalme!
Mwaka 1965 waziri wa mambo ya ndani wa Moroco ambaye alikuwa mtu katili na jeuri sana,mtu aliyeuwawa kila mpinzani wa Mfalme,na mfalme alimwamini sana.Huyu waziri aliwasiliana na Meir Amit ambaye alikuwa mkurugenzi wa Mossad kumwomba amsaidie kumtafuta mpinzani mkuu wa Mfalme Bwana Mehdi Ben-Barka,ambaye sio kuwa mpinzani tu alikuwa adui namba moja wa Ufalme,huyu jamaa alihukumiwa kifo akiwa hayupo,na haikujulikana amejificha wapi,jitihada za Moroco kumpata ziligonga mwamba na sasa waliomba msaada wa Mossad.Mossad ambao wametapakaa duniani kote waliweza kugundua kuwa huyu bwana alikuwa amejificha nchini Uswisi,ambako walimfuatilia kwa muda mrefu na siku moja alienda Paris ambako alitekwa na kisha kupotea kabisa.Kupotea kwake kulikuja kuwa skendo kubwa hasa baada ya serikali ya ufaransa kugundua kuwa Israel ilihusika……..hali hii ilileta sintofahamu kubwa maana ilikuwa kinyume kabisa na utaratibu wa Mossad ikabidi Waziri mkuu aunde tume kuchunguza sakata hili(Wakati huo Amit alikuwa hakubaliki kabisa ndani ya Mossad)
Mkurugenzi wa Mossad alikuwa mtu mwenye akili,aliamua kufanya operesheni Diamond ambayo ilikuja kumpa heshima kubwa sana.Hii ni operesheni iliyotorosha ndege ya kivita aina ya MiG 21,ndege hii ilitengenezwa huko Urusi,ilikuwa na teknolojia kubwa sana,hata magharibi hawakuwa na ndege hii.Kwa Wazayuni ilikuwa jambo gumu lakini ilikuwa lazima walifanye.Wakati huo Urusi ilikuwa imegawa ndege hizi kwa baadhi ya nchi za kijamaa ikiwepo Iraq.Mossad walifanya upelelezi wao wakagundua kuwa wanaweza kutumia mgogoro wa Wakurdi na serikali kujipenyeza ndani ya Iraki,hivo walianza kutoa msaada wa silaha kwa wapiganaji wa Kikurdi ambao walikuwa wanapigana dhidi ya Serikali ya Bagdad!
Mossad walikuja kumgundua Pilot mmoja ambaye hakupendezwa na amri za kuwaua watoto na wanawake wa kikurdi,huyu Pilot aliitwa Redfa,na kwa miaka mingi hakupanda cheo hivo akawa amejaa uchungu mkali.Wataalam wa Mossad wakaanza kumtongoza na kumwahidi fedha nyingi sana pamoja maisha yeye na familia yake.Baada ya muda mrefu wa mazungumzo Piloti akaingia kingi na operesheni ikaandaliwa
Pilot Redfa alichukuliwa na Mossad ambako alifanyiwa mafunzo mbalimbali kwa siri,na wakakubaliana siku ambayo yeye Redfa angerusha ndege MiG 21 kama vile anaenda kwenye majukumu ya kawaida ya kijeshi,akiwa angani alipaswa kuielekeza Israel ambako angetua kwenye moja ya viwanja vya kijeshi.Kabla hajaondoka familia yake yote ilipelekwa Uingereza kisha USA na baadae wangekuja kukutana Israel ambako wangeishi maisha yao yote.Pilot alikubali na siku ikapangwa ambayo nchini Israel ni watu wanne tu walijua kuhusu hili na Redfa alichukua ndege na kuitoroshea nchini Israel……hii ilikuwa na mwaka mmoja tangu mazungumzo yaanze,na miezi kumi kabla ya vita ya siku sita kuanza..Kwa Israel ilikuwa faraja kubwa
Pilot Redfa na familia yake waliishi Israel ila dhambi ya usaliti ilimwandamana ikabidi aombe kuhamia Ulaya angalau asahau.hata huko Ulaya hali iliendelea kuwa mbaya na mwaka 1988 miaka 22 baadae alifariki kwa ugonjwa wa mstuko wa moyo.Mazishi yake yalifanywa na serikali ya Israel