Kenge wa dondo
JF-Expert Member
- Nov 2, 2016
- 263
- 169
Safi sana mkuu!
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Atarudi tu jamaa hana mizungushoMazeee vp, mbona umeenda mazima?
Kuna jamaa anaitwa The Bold huyo jamaa ni noma, story inaanza January hadi Desemba.Atarudi tu jamaa hana mizungusho
Yule jamaa yupo hivyo tangu zamaniKuna jamaa anaitwa The Bold huyo jamaa ni noma, story inaanza January hadi Desemba.
hahahahaKuna jamaa anaitwa The Bold huyo jamaa ni noma, story inaanza January hadi Desemba.
Hahaha nyingine hadi miaka miwili kama the other halfKuna jamaa anaitwa The Bold huyo jamaa ni noma, story inaanza January hadi Desemba.
Hii Kuna mpka Movie wametengeneza...Kitabu.Mossad
Mwandishi.Michael Bar Zohar & Nissim Mishal
Mchambuzi.Nanyaro EJ
Chapter 21
FROM THE LAND OF THE QUEEN OF SHEBA
Mwandishi anasema kuwa haya yalikuwa mashairi ya mshairi maarufu Haim Idissis,maneno ya mashairi haya yaliongeza ladha kwenye safari,sawa na zile nyimbo wakati wa kutwanga mahindi!
The moon is watching from above On my back is a small bag of food
The desert beneath us has no end ahead And my mother promises my little brothers:
“A little more, a little more, Lift up your legs, a last push Toward Jerusalem.” Kama tuliviona huko nyuma jamii ya Wazayuni ilitapakaa hadi Ethiopia,mwandishi anasema kuwa hii ni moja ya jamii ambayo iliteseka sana katika mpango wao wa kurejea kwenye nchi ya ahadi,huko nchini Ethiopia waliishi kwenye milima na mabonde na kwa miaka mingi waliishi Bibilia
Hawa WaIsrael, wa Ethiopia waliitwa jina maarufu FALASHA,neno Falasha lililenga kuwashusha hadhi yao,yaani Wa Israel kutoka pembe nyingine za dunia waliwaona hawa wa Ethiopia kama watu washamba,ambao wapo chini ya kiwango,kwa kawaida hata kabla ya kuundwa kwa Taifa la Israel,huwa na utamaduni wa kwenda kuhiji Yerusalem,lakini hawa Falasha waliishi miaka mingi pasipo kwenda
Mwaka 1977 ndio Serikali ya Israel chini ya waziri mkuu Menachem Begin alipoitaka Mossad wafanye kila waliwezalo wawarejeshe Falasha katika nchi ya ahadi,itakumbukwa kuwa uanzishwaji wa Taifa la Israel ulienda sambamba na kuwarejesha Waisrael katika ardhi waliyopora kutoka kwa Wapalestina
Wakati mpango huu unaanza Ethiopia ilikuwa kwenye vita vya wenyewe kwa wenyewe,hivo Israel ikaingia dili na serikali ya Mengistu kuwa wao Israel itaisadia Ethiopia vifaa vya kivita,lakini ndege hiyo itakayokuja na silaha ndio itaondoka ikiwa imejaa waisrael kuwarejesha kwao,hivo ndege kubwa ikawa inatua na mzigo wa silaha inaondoka na abria ikiwa imejaa,mpango huu ulidumu kwa miezi sita tu na kuja kuvunjika baada ya ulimi wa Waziri wa mambo ya nje ya Israel bwana Moshe Dayan,kuteleza wakati anahojiwa na gazeti moja la uswisi,ambako alikiri kuwa ni kweli Israel wanatoa msaada wa silaha za kivita kwa utawala wa Ethiopia,hii habari ilimkasirisha Bwana Mengistu hivo akatupilia mbali makubaliano na Mossad hapo hapo
Baada ya haya makubaliano kuvunjika ilibidi Waisrael watoroshwe kwa siri kupitia Sudan,wakati huo Sudan ilikuwa hasimu wa Israel ,hivo ikalazimu utoroshaji ufanyike kupitia makambi ya wakimbizi,Wazayuni walilazimika kusafiri kwa miguu umbali mrefu porini,huku wakigongwa na nyoka na nge,na wengine kufa njaa au kiu,wengne walivamiwa na watu wabaya na kunyanganywa kila walichokuwa nacho,ilikuwa safari ngumu hasa kwa wanawake na watoto,lakini tumaini lao ilikuwa kufikia nchi ya ahadi(Safari hii ni kama ile ya waisrael kutoka utumwani misri)
Wakati huo Baba mmoja alipoteza wa.toto wanne kwa mpigo,Kila asubuhi wasafiri walihesabu maiti za ndugu jamaa na marafiki waliokufa,angalau kila familia kulikuwa na msiba
Hadi mwaka 1981 angalau wazayuni 4000(elfu nne) walipoteza maisha katika harakati za kurudi nchini kwao,nchi ya ahadi…hii ni idadi ya Waisrael kutoka kushi tu
Baada ya hali kuwa mbaya yaani kushindwa kuwachukua wenzao kutoka Addis na kushindwa kupitia Sudan Mossad walianzisha kampuni ya Utalii na usafiri iliyosajiliwa Ulaya.Hii kampuni ambayo ilikuwa ni cover ilitafuta beach huko Sudan na kuinunua kwa lengo la kuweka hapo hotel ya Kitalii na kufanya mambo mbalimbali ya kitalii,hii kampuni ya Mossad iliingia mkataba na Serikali ya Sudan na ikawa inalipwa kodi na tozo mbalimbali.Mossad wakafungua Hotel iliyoitwa Arous Resort.Hapo walijenga vyumba vichache na mahema(Majengo ambayo sio ya kudumu).Wale maofisa wa Mossad ambao walikuwa wamepeana nafasi mbalimbali za menejimenti hapo Hotelini walikuwa na kazi moja tu usiku kwenda kwenye kambi za wakimbizi,na maeneo ambayo waliishi Waisrael na kujitambulisha kwao,moja ya utambulisho muhimu ilikuwa SALA(Waisrael wana aina yao ya SALA ambayo ni Uniform duniani kote)popote ambako utata ulitokea SALA ndio iliyoondoa utata huo! Wakishafikishwa hotelini walisafirishwa usiku kupitia bahari nyekundu kuelekea Israel,zoezi hili lilifanyika kwa usiri mkubwa sana kuepuka kushtukiwa na mamlaka za Sudan na Ethiopia
Mwandishi anasema kuwa kulikuwa na Waisrael weusi kabisa ambao hawakuamini kuwa kua Waisrael weupe(Kuna Waisrael weusi kabisa na Waisrael weupe,na wale wa kati kama Waarabu)..sasa hawa weusi wa Ethiopia waliishi milimani,maisha duni ya upweke na hawakujua kuwa kuna wenzao weupe,ila walijua kuwa kuna nchi ya ahadi…hawa SALA ndio iliwaunganisha!Pale hotelini wafanyakazi wazawa walihisi kuna kitu kisicho cha kawaida ila hawakujali sana kwa kuwa waliona hayawahusu alimradi wanalipwa mshahara wao!
Waliendelea na utaratibu huu kwa muda lakini ilikuwa inawachukua muda mrefu,maana watu walikuwa ni wengi.Siku moja watalii na wateja waliamka asubuhi na kukuta menejimenti nzima haipo,wale waajiriwa wachache wenyeji walikuta barua kutoka kwa menejimenti kuwa wameshindwa kuendelea na biashara hivo kila anayedai atalipwa kwa njia benki ndani ya wiki mbili,na wateja waliokuwa wamefanya booking watarejeshewa fedha zao.Hapo ukawa mwisho wa Arous Resort!
Mossad wakaamua kuja na mpango mwingine mwaka 1982,mpango hatari lakini wenye ufanisi mkubwa..Mossad waliamua kutuma vijana wao Sudan ambao walitafuta eneo fulani kisha wakalitengeneza kama uwanja wa ndege,hapo Mossad walipanga kurusha ndege ambayo ingetua kwenye uwanja huo ili kuwatorosha wenzao.Mpango huu ulifanikiwa ambako ndege ya abiria ilichukua watu 213,kazi hii iliendelea kwa wiki kadhaa ila baadae Serikali ya Sudan ilishtuka,Mossad wakatelekeza ule uwanja wa kwanza kisha wakaenda mbali kuweka uwanja mwingine,safari hii walikuwa wanaleta ndege saba zenye uwezo wa kubeba abria 200 kila mmoja
Kati ya 1982 hadi 1984 zaidi ya Waisrael wenye asili ya Ethiopia(Waethiopia wenye asili ya Israel) laki moja na nusu walisafirishwa kurejeshwa kwao na Mossad
Mwanzoni mwa 1985 hali ya uchumi ya Sudan ilidorora na usalama ukawa shakani,Serikali ya Sudan ikaomba msaada wa chakula na silaha kutoka Washington,mara moja Mossad wakajua na wakaomba USA iwaachie hiyo kazi ambayo Israel ingetoa silaha na chakula cha msaada,kwa masharti ya Serikali ya Sudan kuruhusu ndege za Israel kutua na kuchukua raia wake(Mwenye njaa hana tabia) Sudani ilikubali sharti hili na mara moja Mossad wakatekeleza hii iliitwa operesheni Musa………………katika kipindi cha siku arobaini Zaidi ya wazayuni 8000 walirejeshwa nchi yao ya ahadi
Mwaka 1991 Israel ilianzisha operesheni Solomon kwenye moja ya matukio muhimu Ndege ilibeba abiria 1087 ila wakati wa kushuka ikawa na abiria 1088,mama mmoja alikuwa amejifungua ndani ya ndege! Hadi mwaka huo operesheni zote,Musa,Solomoni,Queen Sheba zilifanikiwa kurejesha Waisrael laki tano(nusu milioni) katika nchi yao.
Mwandishi anasema kuwa bado jitihada zinaendelea hadi leo kuhakikisha kuwa inawarejesha wenzao(makabila kadhaa)yaliyopo nchini Ethiopia,ila kumekuwa na ugumu mno wa kukamilisha kazi hii….inasemekana bado kuna kazi ya siri inaendelea kufanyika,ila siku ya mwisho wote watarejea kwao!
…………………………………Mwisho……………………………
Mpenzi msomaji ni matarajio yangu kuwa uchambuzi huu umekuwa wa kuburudisha,kuelimisha na kukupa hari ya kusoma kitabu,ambao ndio msingi wake
Nanyaro EJ