Uchambuzi: Shirika la ujasusi la Uisraeli Mossad

Uchambuzi: Shirika la ujasusi la Uisraeli Mossad

Kitabu.Mossad
Mwandishi.Michael Bar Zohar & Nissim Mishal
Mchambuzi.Nanyaro EJ
Chapter 20

THE CAMERAS WERE ROLLING

Mwandishi anasema kuwa January 18,2010 maofisa kadhaa wa Mossad waliingia Dubai,wakitokea miji mbalimbali ya Ulaya.Maofisa hawa walifikia katika hotel mbalimbali wakiwa na pasi za kusafiria za mataifa mbalimbali.Mossad walikuwa na operesheni kabambe ya kumwua kiongozi wa Hamas ambaye alikuwa ameshiriki kwenye matukio kadhaa dhidi ya Wazayuni
Ilikuwa miaka michace tangu wamwue Imad na daima Mossad wameamini katika kumpiga mchungaji ili kondoo watawanyike
Mahmoud Al-Mabhouh au “AbuAbed,”alizaliwa mwaka 1960 huko gaza,alijiunga na Hamas na kushiriki kwenye matendo ya mauaji dhidi ya Wazayuni,siku moja huko gaza alimpa lift askari wa Israel alipoingia tu kwenye gari akampiga risasi za kutosha,kisha akajipiga picha na marehemu na baadae kumzika!kwa muda mrefu Israel ilitafuta huyu askari wake alizikwa wapi bila mafanikio.Hivo wakaanzisha operesheni ya kumwua bwana Mahmoub.
Mwandishi anasema haijulikani kwa nini Mossad waliamua kuendesha hii operesheni Dubai wakati wanajua kabisa kuwa mji wote umejaa camera kuanzia uwanja wa ndege hadi hotelini.
Kwa kutambua hizi camera wale maofisa wa Mossad walikuwa wanajibadilisha mara kwa mara,mfano angeingia hotel akiwa na mustachi na kutoka akiwa hana ni kiparangoto kabisa.Bwana Mahmoub alifika Dubai na kufikia hotel ya nyota tano ya Al Bustan Rotana,alifikia chumba namba 230 ni chumba ambacho hakikuwa na balcony na alifanya makusudi kabisa kutaka chumba cha juu ghorofa ya pili na kikiwa hakina balcony kwa sababu za kiusalama.Bwana Mahmoub aliingia chumbani bila kujua kuwa kuna watu wa Mossad waliokuwa wanamfuatilia,na ambao walimlia timing wakati anaingia kwenye lift na wao wakaingia bila kubonyeeza kitufe,ni kama na wao walikuwa wanenda floor namba mbili,wote wakashuka kwenye ngazi,hawa vijana wa mossad walikuwa wamevalia kama wanamichezo,wakiwa na taulo za kujifutia jasho wanazotumia wanamichezo…Bwana Mahmoub aliingia chumbani kwake na wale vijana wakajifanya kukosea floor kisha wakarudi na kutokomea kabisa paspojulikana.Hii timu ilitoa taarifa kwa wenzao na kisha ofisa mmoja ambaye alikuwa hapo hapo (ni moja ya timu nzima ya watu 21)alienda eneo la shoping mall ambako alitumia simu ya public(kwenye kibanda)akapiga simu pale pale Al Bustan Rotana na kubook chumba namba 237 hiki ni chumba kinachoangaliana na kile alicholala Bwana Mahmoub yaani vipo kwenye floor moja vinatenganishwa na korido tu.Yule Jamaa aliefanya booking anafika hotelini kisha kujiandikisha akiwa anapanda lift kuelekea chumbani,anakutana kwenye lift na mwenzake kisha kumpa ule ufunguo wa chumba nay eye kushuka tena ngazi bila hata kufika chumbani,na siku hiyo hiyo alipanda ndege kuelekea Italia(Kwamba hata baadae ikija kutafutwa nani alifanya booking ya chumba 237 itakutwa alishaondoka,na aliyelala sie aliyefika mapokezi)
Mossad walikusudia kutumia chumba hiki 237 kama ngome yao ya mauaji ya bwana Mahmoub.
Bwana Mahmoub aliondoka hotelini hapo kwenda kufanya manunuzi ilikuwa ni jioni ya saa kumi na nusu,wakati alipotoka tu vijana wa mossad ambao walikuwa chumba namba 237 walitumia muda huo kuchakachua mfumo wa kielectronic wa mlango wa chumba cha Mahmoub na ndani ya muda mchache walikuwa na uwezo wa kuingia chumbani kwa kadi bandia waliyotengeneza.Kule mjini alikoenda Bwana Mahboub alikuwa anafuatiliwa kwa karibu sana na Mossad bila yeye kujua
Bwana Mahboub alirejea hotelini majira ya saa mbili na nusu usiku ,alipoingia tu chumbani kwake wale vijana wa Mossad walifungua mlango na kisha kumwua hapo hapo na kumlaza kitandani,walitoka na kwenye mlango wa chumba wakabandika kibao cha DON’T DISTURB hiki ni kibao huwekwa na mteja ikiwa hutaki usumbufu,baada ya kufanikiwa kufanya mauaji Mossad walipanda ndege kila mmoja akalelekea mwelekeo tofauti na mwingine,.Saa nne usiku mke wa Mahboum alipiga simu na kutuma ujumbe bila kujibiwa aliingiwa na wasiwasi akalazimika kuwajulisha Hamas ambao nao walimtuma mtu wao aende hapo hotelini,alipofika na kujaribu kupiga chumbani simu ya hotelini pia haikupokelewa,hotel wakalazimika kuingia chumbani walikokutana na mwili ukiwa umeachana na roho…..Dr wa hapo hotelini alipouchunguza mwili alisema amekufa kwa shinikizo la moyo,familia iligoma na kutaka uchunguzi ufanyike kwa kuwa waliamini Mossad watakuwa wamehusika.Hamas walitoa taarifa kuwa mossad ndio wanahusika na kifo cha Mahboum na walisema mwanzoni walimpiga shoti ya umeme na kisha kumwua kwa kutumia mto
Ilikuja kugundulika kuwa Mahboub alichommwa sindano kisha mtu ukawekwa juu yake ili ionekane alijiua,kufuatia kusumbuliwa na tatizo la moyo.Hata hivo wachunguzi wa maswala ya mauaji walisema modi operandi inafanana kabisa na ile ya Mossad au ya idara za kijasusi za Magharibi
Mataifa mengi hasa UK,ujerumani ambao pasipot zao zilitumika zililaani kitendo hicho,na kwenye baadh ya nchi maofisa wa Mossad walifukuzwa
 
Kitabu.Mossad

Mwandishi.Michael Bar Zohar & Nissim Mishal

Mchambuzi.Nanyaro EJ



Chapter 21



FROM THE LAND OF THE QUEEN OF SHEBA



Mwandishi anasema kuwa haya yalikuwa mashairi ya mshairi maarufu Haim Idissis,maneno ya mashairi haya yaliongeza ladha kwenye safari,sawa na zile nyimbo wakati wa kutwanga mahindi!

The moon is watching from above On my back is a small bag of food

The desert beneath us has no end ahead And my mother promises my little brothers:

“A little more, a little more, Lift up your legs, a last push Toward Jerusalem.” Kama tuliviona huko nyuma jamii ya Wazayuni ilitapakaa hadi Ethiopia,mwandishi anasema kuwa hii ni moja ya jamii ambayo iliteseka sana katika mpango wao wa kurejea kwenye nchi ya ahadi,huko nchini Ethiopia waliishi kwenye milima na mabonde na kwa miaka mingi waliishi Bibilia

Hawa WaIsrael, wa Ethiopia waliitwa jina maarufu FALASHA,neno Falasha lililenga kuwashusha hadhi yao,yaani Wa Israel kutoka pembe nyingine za dunia waliwaona hawa wa Ethiopia kama watu washamba,ambao wapo chini ya kiwango,kwa kawaida hata kabla ya kuundwa kwa Taifa la Israel,huwa na utamaduni wa kwenda kuhiji Yerusalem,lakini hawa Falasha waliishi miaka mingi pasipo kwenda

Mwaka 1977 ndio Serikali ya Israel chini ya waziri mkuu Menachem Begin alipoitaka Mossad wafanye kila waliwezalo wawarejeshe Falasha katika nchi ya ahadi,itakumbukwa kuwa uanzishwaji wa Taifa la Israel ulienda sambamba na kuwarejesha Waisrael katika ardhi waliyopora kutoka kwa Wapalestina

Wakati mpango huu unaanza Ethiopia ilikuwa kwenye vita vya wenyewe kwa wenyewe,hivo Israel ikaingia dili na serikali ya Mengistu kuwa wao Israel itaisadia Ethiopia vifaa vya kivita,lakini ndege hiyo itakayokuja na silaha ndio itaondoka ikiwa imejaa waisrael kuwarejesha kwao,hivo ndege kubwa ikawa inatua na mzigo wa silaha inaondoka na abria ikiwa imejaa,mpango huu ulidumu kwa miezi sita tu na kuja kuvunjika baada ya ulimi wa Waziri wa mambo ya nje ya Israel bwana Moshe Dayan,kuteleza wakati anahojiwa na gazeti moja la uswisi,ambako alikiri kuwa ni kweli Israel wanatoa msaada wa silaha za kivita kwa utawala wa Ethiopia,hii habari ilimkasirisha Bwana Mengistu hivo akatupilia mbali makubaliano na Mossad hapo hapo

Baada ya haya makubaliano kuvunjika ilibidi Waisrael watoroshwe kwa siri kupitia Sudan,wakati huo Sudan ilikuwa hasimu wa Israel ,hivo ikalazimu utoroshaji ufanyike kupitia makambi ya wakimbizi,Wazayuni walilazimika kusafiri kwa miguu umbali mrefu porini,huku wakigongwa na nyoka na nge,na wengine kufa njaa au kiu,wengne walivamiwa na watu wabaya na kunyanganywa kila walichokuwa nacho,ilikuwa safari ngumu hasa kwa wanawake na watoto,lakini tumaini lao ilikuwa kufikia nchi ya ahadi(Safari hii ni kama ile ya waisrael kutoka utumwani misri)

Wakati huo Baba mmoja alipoteza wa.toto wanne kwa mpigo,Kila asubuhi wasafiri walihesabu maiti za ndugu jamaa na marafiki waliokufa,angalau kila familia kulikuwa na msiba

Hadi mwaka 1981 angalau wazayuni 4000(elfu nne) walipoteza maisha katika harakati za kurudi nchini kwao,nchi ya ahadi…hii ni idadi ya Waisrael kutoka kushi tu

Baada ya hali kuwa mbaya yaani kushindwa kuwachukua wenzao kutoka Addis na kushindwa kupitia Sudan Mossad walianzisha kampuni ya Utalii na usafiri iliyosajiliwa Ulaya.Hii kampuni ambayo ilikuwa ni cover ilitafuta beach huko Sudan na kuinunua kwa lengo la kuweka hapo hotel ya Kitalii na kufanya mambo mbalimbali ya kitalii,hii kampuni ya Mossad iliingia mkataba na Serikali ya Sudan na ikawa inalipwa kodi na tozo mbalimbali.Mossad wakafungua Hotel iliyoitwa Arous Resort.Hapo walijenga vyumba vichache na mahema(Majengo ambayo sio ya kudumu).Wale maofisa wa Mossad ambao walikuwa wamepeana nafasi mbalimbali za menejimenti hapo Hotelini walikuwa na kazi moja tu usiku kwenda kwenye kambi za wakimbizi,na maeneo ambayo waliishi Waisrael na kujitambulisha kwao,moja ya utambulisho muhimu ilikuwa SALA(Waisrael wana aina yao ya SALA ambayo ni Uniform duniani kote)popote ambako utata ulitokea SALA ndio iliyoondoa utata huo! Wakishafikishwa hotelini walisafirishwa usiku kupitia bahari nyekundu kuelekea Israel,zoezi hili lilifanyika kwa usiri mkubwa sana kuepuka kushtukiwa na mamlaka za Sudan na Ethiopia



Mwandishi anasema kuwa kulikuwa na Waisrael weusi kabisa ambao hawakuamini kuwa kua Waisrael weupe(Kuna Waisrael weusi kabisa na Waisrael weupe,na wale wa kati kama Waarabu)..sasa hawa weusi wa Ethiopia waliishi milimani,maisha duni ya upweke na hawakujua kuwa kuna wenzao weupe,ila walijua kuwa kuna nchi ya ahadi…hawa SALA ndio iliwaunganisha!Pale hotelini wafanyakazi wazawa walihisi kuna kitu kisicho cha kawaida ila hawakujali sana kwa kuwa waliona hayawahusu alimradi wanalipwa mshahara wao!



Waliendelea na utaratibu huu kwa muda lakini ilikuwa inawachukua muda mrefu,maana watu walikuwa ni wengi.Siku moja watalii na wateja waliamka asubuhi na kukuta menejimenti nzima haipo,wale waajiriwa wachache wenyeji walikuta barua kutoka kwa menejimenti kuwa wameshindwa kuendelea na biashara hivo kila anayedai atalipwa kwa njia benki ndani ya wiki mbili,na wateja waliokuwa wamefanya booking watarejeshewa fedha zao.Hapo ukawa mwisho wa Arous Resort!

Mossad wakaamua kuja na mpango mwingine mwaka 1982,mpango hatari lakini wenye ufanisi mkubwa..Mossad waliamua kutuma vijana wao Sudan ambao walitafuta eneo fulani kisha wakalitengeneza kama uwanja wa ndege,hapo Mossad walipanga kurusha ndege ambayo ingetua kwenye uwanja huo ili kuwatorosha wenzao.Mpango huu ulifanikiwa ambako ndege ya abiria ilichukua watu 213,kazi hii iliendelea kwa wiki kadhaa ila baadae Serikali ya Sudan ilishtuka,Mossad wakatelekeza ule uwanja wa kwanza kisha wakaenda mbali kuweka uwanja mwingine,safari hii walikuwa wanaleta ndege saba zenye uwezo wa kubeba abria 200 kila mmoja

Kati ya 1982 hadi 1984 zaidi ya Waisrael wenye asili ya Ethiopia(Waethiopia wenye asili ya Israel) laki moja na nusu walisafirishwa kurejeshwa kwao na Mossad

Mwanzoni mwa 1985 hali ya uchumi ya Sudan ilidorora na usalama ukawa shakani,Serikali ya Sudan ikaomba msaada wa chakula na silaha kutoka Washington,mara moja Mossad wakajua na wakaomba USA iwaachie hiyo kazi ambayo Israel ingetoa silaha na chakula cha msaada,kwa masharti ya Serikali ya Sudan kuruhusu ndege za Israel kutua na kuchukua raia wake(Mwenye njaa hana tabia) Sudani ilikubali sharti hili na mara moja Mossad wakatekeleza hii iliitwa operesheni Musa………………katika kipindi cha siku arobaini Zaidi ya wazayuni 8000 walirejeshwa nchi yao ya ahadi

Mwaka 1991 Israel ilianzisha operesheni Solomon kwenye moja ya matukio muhimu Ndege ilibeba abiria 1087 ila wakati wa kushuka ikawa na abiria 1088,mama mmoja alikuwa amejifungua ndani ya ndege! Hadi mwaka huo operesheni zote,Musa,Solomoni,Queen Sheba zilifanikiwa kurejesha Waisrael laki tano(nusu milioni) katika nchi yao.

Mwandishi anasema kuwa bado jitihada zinaendelea hadi leo kuhakikisha kuwa inawarejesha wenzao(makabila kadhaa)yaliyopo nchini Ethiopia,ila kumekuwa na ugumu mno wa kukamilisha kazi hii….inasemekana bado kuna kazi ya siri inaendelea kufanyika,ila siku ya mwisho wote watarejea kwao!

…………………………………Mwisho……………………………

Mpenzi msomaji ni matarajio yangu kuwa uchambuzi huu umekuwa wa kuburudisha,kuelimisha na kukupa hari ya kusoma kitabu,ambao ndio msingi wake

Nanyaro EJ
 
Kitabu.Mossad

Mwandishi.Michael Bar Zohar & Nissim Mishal

Mchambuzi.Nanyaro EJ



Chapter 21



FROM THE LAND OF THE QUEEN OF SHEBA



Mwandishi anasema kuwa haya yalikuwa mashairi ya mshairi maarufu Haim Idissis,maneno ya mashairi haya yaliongeza ladha kwenye safari,sawa na zile nyimbo wakati wa kutwanga mahindi!

The moon is watching from above On my back is a small bag of food

The desert beneath us has no end ahead And my mother promises my little brothers:

“A little more, a little more, Lift up your legs, a last push Toward Jerusalem.” Kama tuliviona huko nyuma jamii ya Wazayuni ilitapakaa hadi Ethiopia,mwandishi anasema kuwa hii ni moja ya jamii ambayo iliteseka sana katika mpango wao wa kurejea kwenye nchi ya ahadi,huko nchini Ethiopia waliishi kwenye milima na mabonde na kwa miaka mingi waliishi Bibilia

Hawa WaIsrael, wa Ethiopia waliitwa jina maarufu FALASHA,neno Falasha lililenga kuwashusha hadhi yao,yaani Wa Israel kutoka pembe nyingine za dunia waliwaona hawa wa Ethiopia kama watu washamba,ambao wapo chini ya kiwango,kwa kawaida hata kabla ya kuundwa kwa Taifa la Israel,huwa na utamaduni wa kwenda kuhiji Yerusalem,lakini hawa Falasha waliishi miaka mingi pasipo kwenda

Mwaka 1977 ndio Serikali ya Israel chini ya waziri mkuu Menachem Begin alipoitaka Mossad wafanye kila waliwezalo wawarejeshe Falasha katika nchi ya ahadi,itakumbukwa kuwa uanzishwaji wa Taifa la Israel ulienda sambamba na kuwarejesha Waisrael katika ardhi waliyopora kutoka kwa Wapalestina

Wakati mpango huu unaanza Ethiopia ilikuwa kwenye vita vya wenyewe kwa wenyewe,hivo Israel ikaingia dili na serikali ya Mengistu kuwa wao Israel itaisadia Ethiopia vifaa vya kivita,lakini ndege hiyo itakayokuja na silaha ndio itaondoka ikiwa imejaa waisrael kuwarejesha kwao,hivo ndege kubwa ikawa inatua na mzigo wa silaha inaondoka na abria ikiwa imejaa,mpango huu ulidumu kwa miezi sita tu na kuja kuvunjika baada ya ulimi wa Waziri wa mambo ya nje ya Israel bwana Moshe Dayan,kuteleza wakati anahojiwa na gazeti moja la uswisi,ambako alikiri kuwa ni kweli Israel wanatoa msaada wa silaha za kivita kwa utawala wa Ethiopia,hii habari ilimkasirisha Bwana Mengistu hivo akatupilia mbali makubaliano na Mossad hapo hapo

Baada ya haya makubaliano kuvunjika ilibidi Waisrael watoroshwe kwa siri kupitia Sudan,wakati huo Sudan ilikuwa hasimu wa Israel ,hivo ikalazimu utoroshaji ufanyike kupitia makambi ya wakimbizi,Wazayuni walilazimika kusafiri kwa miguu umbali mrefu porini,huku wakigongwa na nyoka na nge,na wengine kufa njaa au kiu,wengne walivamiwa na watu wabaya na kunyanganywa kila walichokuwa nacho,ilikuwa safari ngumu hasa kwa wanawake na watoto,lakini tumaini lao ilikuwa kufikia nchi ya ahadi(Safari hii ni kama ile ya waisrael kutoka utumwani misri)

Wakati huo Baba mmoja alipoteza wa.toto wanne kwa mpigo,Kila asubuhi wasafiri walihesabu maiti za ndugu jamaa na marafiki waliokufa,angalau kila familia kulikuwa na msiba

Hadi mwaka 1981 angalau wazayuni 4000(elfu nne) walipoteza maisha katika harakati za kurudi nchini kwao,nchi ya ahadi…hii ni idadi ya Waisrael kutoka kushi tu

Baada ya hali kuwa mbaya yaani kushindwa kuwachukua wenzao kutoka Addis na kushindwa kupitia Sudan Mossad walianzisha kampuni ya Utalii na usafiri iliyosajiliwa Ulaya.Hii kampuni ambayo ilikuwa ni cover ilitafuta beach huko Sudan na kuinunua kwa lengo la kuweka hapo hotel ya Kitalii na kufanya mambo mbalimbali ya kitalii,hii kampuni ya Mossad iliingia mkataba na Serikali ya Sudan na ikawa inalipwa kodi na tozo mbalimbali.Mossad wakafungua Hotel iliyoitwa Arous Resort.Hapo walijenga vyumba vichache na mahema(Majengo ambayo sio ya kudumu).Wale maofisa wa Mossad ambao walikuwa wamepeana nafasi mbalimbali za menejimenti hapo Hotelini walikuwa na kazi moja tu usiku kwenda kwenye kambi za wakimbizi,na maeneo ambayo waliishi Waisrael na kujitambulisha kwao,moja ya utambulisho muhimu ilikuwa SALA(Waisrael wana aina yao ya SALA ambayo ni Uniform duniani kote)popote ambako utata ulitokea SALA ndio iliyoondoa utata huo! Wakishafikishwa hotelini walisafirishwa usiku kupitia bahari nyekundu kuelekea Israel,zoezi hili lilifanyika kwa usiri mkubwa sana kuepuka kushtukiwa na mamlaka za Sudan na Ethiopia



Mwandishi anasema kuwa kulikuwa na Waisrael weusi kabisa ambao hawakuamini kuwa kua Waisrael weupe(Kuna Waisrael weusi kabisa na Waisrael weupe,na wale wa kati kama Waarabu)..sasa hawa weusi wa Ethiopia waliishi milimani,maisha duni ya upweke na hawakujua kuwa kuna wenzao weupe,ila walijua kuwa kuna nchi ya ahadi…hawa SALA ndio iliwaunganisha!Pale hotelini wafanyakazi wazawa walihisi kuna kitu kisicho cha kawaida ila hawakujali sana kwa kuwa waliona hayawahusu alimradi wanalipwa mshahara wao!



Waliendelea na utaratibu huu kwa muda lakini ilikuwa inawachukua muda mrefu,maana watu walikuwa ni wengi.Siku moja watalii na wateja waliamka asubuhi na kukuta menejimenti nzima haipo,wale waajiriwa wachache wenyeji walikuta barua kutoka kwa menejimenti kuwa wameshindwa kuendelea na biashara hivo kila anayedai atalipwa kwa njia benki ndani ya wiki mbili,na wateja waliokuwa wamefanya booking watarejeshewa fedha zao.Hapo ukawa mwisho wa Arous Resort!

Mossad wakaamua kuja na mpango mwingine mwaka 1982,mpango hatari lakini wenye ufanisi mkubwa..Mossad waliamua kutuma vijana wao Sudan ambao walitafuta eneo fulani kisha wakalitengeneza kama uwanja wa ndege,hapo Mossad walipanga kurusha ndege ambayo ingetua kwenye uwanja huo ili kuwatorosha wenzao.Mpango huu ulifanikiwa ambako ndege ya abiria ilichukua watu 213,kazi hii iliendelea kwa wiki kadhaa ila baadae Serikali ya Sudan ilishtuka,Mossad wakatelekeza ule uwanja wa kwanza kisha wakaenda mbali kuweka uwanja mwingine,safari hii walikuwa wanaleta ndege saba zenye uwezo wa kubeba abria 200 kila mmoja

Kati ya 1982 hadi 1984 zaidi ya Waisrael wenye asili ya Ethiopia(Waethiopia wenye asili ya Israel) laki moja na nusu walisafirishwa kurejeshwa kwao na Mossad

Mwanzoni mwa 1985 hali ya uchumi ya Sudan ilidorora na usalama ukawa shakani,Serikali ya Sudan ikaomba msaada wa chakula na silaha kutoka Washington,mara moja Mossad wakajua na wakaomba USA iwaachie hiyo kazi ambayo Israel ingetoa silaha na chakula cha msaada,kwa masharti ya Serikali ya Sudan kuruhusu ndege za Israel kutua na kuchukua raia wake(Mwenye njaa hana tabia) Sudani ilikubali sharti hili na mara moja Mossad wakatekeleza hii iliitwa operesheni Musa………………katika kipindi cha siku arobaini Zaidi ya wazayuni 8000 walirejeshwa nchi yao ya ahadi

Mwaka 1991 Israel ilianzisha operesheni Solomon kwenye moja ya matukio muhimu Ndege ilibeba abiria 1087 ila wakati wa kushuka ikawa na abiria 1088,mama mmoja alikuwa amejifungua ndani ya ndege! Hadi mwaka huo operesheni zote,Musa,Solomoni,Queen Sheba zilifanikiwa kurejesha Waisrael laki tano(nusu milioni) katika nchi yao.

Mwandishi anasema kuwa bado jitihada zinaendelea hadi leo kuhakikisha kuwa inawarejesha wenzao(makabila kadhaa)yaliyopo nchini Ethiopia,ila kumekuwa na ugumu mno wa kukamilisha kazi hii….inasemekana bado kuna kazi ya siri inaendelea kufanyika,ila siku ya mwisho wote watarejea kwao!

…………………………………Mwisho……………………………

Mpenzi msomaji ni matarajio yangu kuwa uchambuzi huu umekuwa wa kuburudisha,kuelimisha na kukupa hari ya kusoma kitabu,ambao ndio msingi wake

Nanyaro EJ
Hii Kuna mpka Movie wametengeneza...
 
Back
Top Bottom