Uchambuzi wa Mkataba wa kuendesha bandari ya Dar es Salaam kati ya Tanzania na Dubai

Uchambuzi wa Mkataba wa kuendesha bandari ya Dar es Salaam kati ya Tanzania na Dubai

huyu Musukuma ana nini ndani yake? Ina maana ana ushawishi mkubwa humo ndani kiasi aonekane ukimpata yeye umewapata wote, mi naona kama the guy is overrated, sijui lakini maana siasa za bongo uchwarauchwara mwingi ndiyo una count a lot.
 
Huu mkataba unaiingiza rasmi Tanzania kwenye biashara za Kimataifa.

Wenye uelewa wa biashara za Kimataifa watalielewa hilo.

Mambumbumbu wa biashara mtabaki bandari imeuzwa, imeuzwa.

Imeuzwa kupelekwa wapi?
Mzanzibari katika ubora wake.
 
Mkataba ujadiliwe kama una tija, ila DPWorld wako makini sana
Sawa lakini wapewe miaka 20 tu jumla na 5 kati yake ya probation. Pia wawe na mkakati wa kuwajengea Watanzania uwezo baada ya hiyo miaka 20 Watanzania wenyewe ndio waendeshe bandari yao.
 
Inawezekana kila awamu iliyopita walikuwa wanauza kilicho karibu,na wenda vimeisha,awamu hii wamefikiriii,wakaona bandari inafaa.
 
Inawezekana kila awamu iliyopita walikuwa wanauza kilicho karibu,na wenda vimeisha,awamu hii wamefikiriii,wakaona bandari inafaa.
Unaweza kutoa mfano wa kilichouzwa awamu iliyopita?
 
Kwanza kwanini umejitokeza leo kutetea ili Hali kesho Bunge litakaa kwa shughuli hiyo?

Kujitikeza kwako kutetea huu mkataba as an individual ndiyo kuna leta maswali. Mbona nguvu ni kubwa hivi?

Mbona kama kuna kiwewe?

Nisingeliandika kama ungekuwa unahojiwa na chombo cha habari lakini kuitisha press kutetea ndiyo wengi tunona nyie lomolomo ndiyo mnatangulizwa kuweka mamb Sawa. Ungelitulia ukasubiri kesho nafasi unayo Bungeni.

Mimi siwezi kukubali kusikia porojo zako kwenye press ili Hali mkataba huo umeandaliwa na wasomi wakubwa wanaojua namna ya kula kwa wasiojitambua.

Kweli nisikilize porojo ili Hali wewe hujui hata kutamka neno" contractual term" kwa usahihi.

Hivi mh. Msukuma ule mkataba ukiusoma wewe utaulewa unamaanisha Nini kweli?

Ndugu tulia kwanza jambo lichakatwe hizi porojo ni kwasababu tumeruhusu kuingia mjengoni Sifa moja wapo ni "anayejua kusoma na kuandika kiswahili"

Wewe siyo mtaalamu wa SHERIA

Tukienda kwa pupa, kesho akiingia Rais mzalendo akaona kuna madudu kwenye mkataba akataka kuvunja ndiyo utaona wanakamata mali zetu ZILIZOPO nje ya nchi.

Msukuma tulia kaka, Wacha bunge lipitie kesho na Bunge la wananchi nalo halipo nyuma tunafuatilia. Hatutaki yajirudie Yale ya migodi namna tulivyopigwa. Kila tukijaribu Jamaa wanakimbilia MIGA.

Msukuma Mimi Nina nusu ya umri wako, napenda nami watoto wangu wakute nchi ikiwa vizuri.

Acha tujue, je ni lifetime au ni miaka 100 au la!

Mungu ibariki Tanzania 🇹🇿
Wewe uliyeunganisha Uzi wangu hufai
 
Kama ni hakika jambo hili lipo, huyu mama SSH atakuwa ameliingiza taifa kwenye historia mbaya. Marais wote wamepita lakini hajatokea hata mmoja aliyechezea Bandari namna hii! Mama huyu anaishia kubaya
Yeye hajui kinachoendelea zaidi ya kusifiwa wanaume wanapiga pesa tu
 
Mnamlaumu na kudhihaki sana Chief Mangungo lakini mjuwe yeye na mkalimani wake hawakusoma wala kujua Kijerumani, tofauti na watawala wa Sasa wenye ma PhD ya ukweli na uongo.
 
Back
Top Bottom