Uchawi ulivyotamalaki milima ya Same Upareni

Uchawi ulivyotamalaki milima ya Same Upareni

Kuna ajali ilitokea nikiwa kule.. Ilitokea pale Makanya karibu na stand fuso iligongana na gari dogo.. Fuso iliumia sana.. Lakini siku 2 kabla kuna mzee alikuwa keshatoa onyo (alitapeliwa na dereva asiyemfahamu) Akasema huyo dereva hatakatiza hapa makanya na nataka asife bali avunjike mikono na miguu tu.. Na niishuhudie hiyo ajali
Wakati ajali husika inatokea mzee alikuwa pale stand na dereva alivunjika mikono na miguu yote

Sema Wazee Wakongwe kadiri wanavyofariki naona Hali itakuwa shwari.
 
Halafu tena gari yenyewe ni Toyota Stout ya mwaka 1986, ambazo zimebaki Kilimanjaro tu. Miaka ya nyuma niliitafuta sana mpaka nikatoa Tangazo hapa bila mafanikio yoyote.
Mkuu hii ni Land Cruiser Pick Up hao NEWL ndio wanazotumia kusambaza mafuta kwenye minara, siku hizi wanatumia na Nissan Hardbody pia.

Hizo Toyota Stout nyanda za juu kusini zipo kibao nipe deal hata leo inapatikana Kuna wazee wamepaki nyumbani.
 
Tukirudi kwenye ajali husika tujihoji haya
Kwanini mmiliki kaamua kuitelekeza gari yake ya mamilioni pale?

Sidhani kama mzee Lema anaweza itelekeza gari yake, maana ndiye mmliki wa Northern Engineering a.k.a NEWL

Na hizo gari zao huwa zinafungwa GPS

Je dereva wake kakimbilia wapi?
Je wafanyakazi wa kampuni kuna mahali waliharibu?

Kwa kawaida kwenye hizi kampuni za kuhudumia minara, watu wanaitwa Field Technicians au Supervisors ndio husambaza wese kwa kutumia hizo gari za kampuni...

Bahati mbaya sana, hizo gari huwa ni mbovu mbovu na kawaida sana kuona gari zao zimepata breakdowns...

Chance kubwa ni hilo gari lazima lilikuwa na kasoro ya kiufundi, na ukichukulia jiografia ya huko mlimani lazima lingetii effect ya gravity...

Pia si ajabu technician aliyepewa hiyo gari kafanya tu hujuma, pengine madai au maslahi yake hayajasikilizwa au fanyiwa kazi...
 
Nimezaliwa Makanya
Nimekulia na Kusomea Makanya kuanzia chekechea, shule ya msingi mpaka Kidato cha nne,
Niliondoka Makanya nilipofaulu Kidato cha nne.

Makanya ndio kwetu, Makanya ndio watu wangu, nami ni mtoto wao.

Hayo unayosema yapo Kwa kiasi,

Makanya Ushirikina na Uchawi upo na unaathari labda Kwa wageni wasio wazawa.

Makanya inamchanganyiko wa Makabila kutokana na kilimo cha zao la Mkonge.

Wenyeji wengi ni Wapare,
Lakini pia kuna
Wamasai, wasambaa, Wachaga kidogo, Warundi, Wanyambo, Wasukuma, NK.

Pia wapo wanyiramba.

Uchawi Kwa kiasi kikubwa unapatikana Milimani ambapo ipo Mashariki mwa kamji Ka Makanya.

Wasambaa na watu wa Tanga wameongeza nafasi ya UCHAWI katika mji huo wenye ukame.

Makanya ndio Makao makuu ya Biashara ya Mirungi Afrika Mashariki.

Mirungi hiyo itokayo Milimani hasa Tae, Suji, Parane na Chime ina ladha inayopendwa na watumiaji ukilinganisha na Mirungi ya Kenya na Somalia.

Uchawi pia unaisaidia Biashara hiyo ya Mirungi kuendelea kuexist mbali na Rushwa.

Polisi Wanoko wasiotaka Rushwa hukipata cha mtema kuni wakifuatilia Wauza Mirungi huko Milimani.
Hivyo hujikuta wanapata madhara na kuamua kuacha au huamishwa kabisa kituo cha kazi.

Kipindi nakua, baadhi ya ajali za barabarani zilihusishwa na Uchawi na Ushirikina.

Makanya na Hedaru ni moja ya miji Maarufu wilayani Same na pia inaongoza Kwa ujanja ujanja.

Sisi Wana Makanya tunapendana mno,
Nilipoona tu reply yako mtafiti nikajua utashusha data za kutosha sana.
 
Huwa nacheka sana baadhi ya watu wakipinga kwa nguvu zote kuwa hakuna uchawi! Hawa hawajatembea wakajionea kwa macho yao na kushuhudia live kabisa, SIO KUSIMULIWA
Last week kuna picha ilitrend mitandaoni ikionesha gari la Landcruiser pickup likiwa limekita pua juu ya paa la nyumba ya udongo na kudumbukia ndani..Achana na ubora na uimara wa nyumba ambayo pamoja na kuathirika kwenye paa lake lakini kuta zimebaki salama licha ya kuangukiwa na gari lenye uzito wa tani hivi

Baada ya picha ile kuzagaa mitandaoni kuna wanahabari walichukua muda kwenda kupata ukweli na uhalisia wa tukio zima na wakatuletea na video.! Katika video husika mashuhuda wakalihusisha tukio zima na imani za kishirikina! Mwenye gari kampuni ya minara ya Arusha kaingia mitini na kulitelekeza gari lake ambalo liliserereka lenyewe likapata support ya waya za umeme na kwenda kuishia kujikita kwenye nyumba husika.. Hakukuwa na vifo wala majeruhi licha ya kwamba wakati wa tukio kuna mtoto alikuwa kalala ndani

Mimi nilikuwa mitaa ya huko mwanzoni mwa mwaka huu.. Nilienda kwenye mishe zangu personal
Nilienda Milima ya kati ya Hedaru na Same eneo linaitwa makanya Kijiji cha TAE..Kwa hakika kule niliukuta ushirikina katika uhalisia wake
Kule mahakama ya haki ni ushirikina!!! hakuna dhuluma, hakuna wizi, hakuna kugeukana hakuna kusalitiana..!!! Ukizingua kwenye hayo moto utakuwakia...Kule ni heshima, adabu, ukweli na uaminifu
Wizi wa bodabida ni tatizo kubwa Tanzania lakini sio Makanya wala Tae...Wakati naelekea Tae tukapita mahali porini kuna bodaboda imeegeshwa kwenye mti nikaambiwa ina wiki mbili hapo na mwenyewe alitoa tu taarifa kwa ndugu zake kuwa ilimuishia mafuta..Akaiacha hapo akauchapa mpaka Makanya akaenda zake aendako
Safari yangu ya Tae ilinikutanisha na mambo ya ajabu lakini mengine ya kutisha..Kwa kifupi Tae kunaogopeka kati ya vijiji vyote vya kule
Tae mpaka leo hakuna usafiri wa Jumuiya kwenda na kurudi Makanya licha ya kwamba kuna umbali wa kama Kilometers 20 hivi...huko ni boda au kuuchapa na ni kupanda ama kushuka milima na vilima..!
Magari yaendayo Tae ni kwa ajili ya waendao kwa waganga wa kienyeji, misiba , shughuli za kiserikali na miradi
Tae kuna vilinge maarufu vya kuua, kuharibu, kutengenezwa mambo yako.. Na wakuu wake hawaingiliani bali wanashirikiana
Nikiwa kule nilishuhudia nyumba zilizoachwa na wahanga wa usaliti kwenye siasa
Wahanga wa usaliti kwenye biashara (mirungi, bhangi na gongo)
Wahanga wa wizi mbalimbali
Wajuaji nknk
Nilikaa Tae siku tatu tuu lakini niliyoyaona kule yanafaa kuandikiwa kitabu kizima!

Tukirudi kwenye ajali husika tujihoji haya
Kwanini mmiliki kaamua kuitelekeza gari yake ya mamilioni pale?
Je dereva wake kakimbilia wapi?
Je wafanyakazi wa kampuni kuna mahali waliharibu?
Bado natafuta wasaa nifike eneo la tukio..Na nikienda huko nitawaletea mrejeshoView attachment 1828122
Na maelezo yake haya hapa
 
Nenda Kasulu Nyamnyusi Utajiridhisha
Hayo Mambo Ni Magumu Ila Yapo Sana

Hapa Dsm kwangu nyumbani nina store Ndogo nimehifadhi mapipa makubwa ya maji, Wife amekua analalamika kwamba huwa anayajaza maji lakini asbuhi anakuta yamepungua.

iliniwia vigumu sana kuamini siku moja nikamwambia jaza maji lakini usiyaguse kabisa hayo mapipa kwasababu nilihisi huwa anayatumia halafu anasahau, kweli kajaza nime monitor siku mbili hakuna lilitokea.

siku ya tatu nikamwambia aweke ile pipe anayotumia kujazia maji ibaki ndani ya pipa, Sikuamini nilichokiona kesho yake mapipa yalikua nusu.

kwasababu siamini haya mambo ya kuroga na kurogana napata shida sana ya kungamua nini kilitokea
 
Back
Top Bottom