Baba Ndubwi
JF-Expert Member
- Sep 27, 2013
- 1,223
- 1,992
Wakuu naimani kwa pamoja tunaendelea kujikinga sisi na familia zetu dhidi ya COVID-19.Ni jukumu letu sote kujikinga,kuwakinga na kuwaelimisha wengine jinsi ya kujikinga.
Moja kati ya visa vingi ambavyo nimewahi kukumbana navyo katika maisha ya kuteswa na kutaabishwa na wachawi kwa miaka zaidi ya 20 ktk tasnia hii ya wazee wa nguvu za giza/wachawi/wanga au wazee wa kuloga/kuruka usiku ni hili;
Yakupasa kufahamu ya kwamba;Mchawi akitaka kukuua/kukuharibia maisha muda mwingine hutengeneza mbinu za kupoteza ushahidi(haswa wachawi ndugu,kama wanatoka kwenye ukoo au familia) kiasi kwamba hata watu au wanandugu hawawezi kuhisi kama umethulumiwa haki yako ya kuishi au mafanikio.
Yatatengenezwa mazingira na mwisho wa siku itaonekana ulikuwa ni uzembe wako ama bahati mbaya wewe kuharibikiwa maisha ama kupoteza maisha.
Mwaka 2018 nilikwenda Morogoro kijiji kinaitwa kisama,kama unakwenda magogoni yaani njia ya kwenda ngerengere.
Ni pale ukifika ubena kama unatokea dar basi unakula kona kushoto.
Huko nilikwenda kwa ajili ya biashara ya mbao baada ya kualikwa na jamaa yangu tena kiroho safi kabisaa.
Usafiri wa kwenda huko kijiji cha Chanyumbu kata ya Kisama ni wa shida balaa,gari ni coaster au daladala za dar zinazozamiaga ruti na ni moja tuu kwa siku, na kipindi cha masika hakuna usafiri tena wa gari zaidi ya pikipiki na sio nyingi maana wengi hufungia ndani toyo zao.
Nilifika kijijini Kisama;Kazi ilianza,ni mwendo wa masaa 3 kwa mguu kwenda chaka,msituni yaani huko ni mwendo wa kupiga kambi chaka,full mijoka na mifisi kufukuzia ng'ombe za wamang'ati,mjengo ni kusimamisha miti kisha kuweka turubai tuu juu basi pembeni no ukuta na mvua ikianza hapo ni mtafutanoo,ni mwendo wa kulala wima kama mchongoma,mkeshaa(nadhani wavunaji wa mbao,wazee wa chain saw watakuwa wananielewa hapo).
Kiukweli walipanga kunimaliza kabisa hawa wachawi;Porini mimi nilikuwa msimamizi wa ile chain sawa jamaangu yeye akaondoka akaniachia kwa makubaliano fulani.
Kila mara watu niliokuwa nao porini walikuwa wakinieleza vile nimekuwa nikiota usiku,napiga makelele na kutamka maneno yanayooashiria niko kwenye mapigano.."Niachenii,msinifungee". Moja kati ya maneno niliyowahi kuyatamka.(nilielezwa asubuhi baada ya kuamka) na ilikuwa kawaida mimi kuota ndoto hatari,za hovyo,chafu za kishetani.
Mwezi mmoja baadae sijui hata ilikuwaje tuu,siku hiyo tumetoka chaka jioni nikakuta ujumbe pale kijijini kwa mwenyeji wetu eti jamaangu anadai mashine nikabidhi,nisisimamie tena.
Nikasema sawa ila lipa kwanza madai yangu ya usimamizi duuh hapo ndipo balaa lilipoanzia,jamaa bila aibu akagoma kulipa,akadai nilizoiba zinanitosha.
Aise sijui tuu ilikuwaje mtu aloambiwa aichukue chain saw kaanza kuniropokea,ghaflaa nikabeba panga lah ni Mungu tuu lakini dhumuni ilikuwa nimkate halafu afe/adhurike me nipotezwe jela.Hata mwenyeji wetu alishangaa sanaa kuniona nimepagawa na kuleta balaa kubwa,watu kibaoo.
Mgogoro ule uliisha baada ya kulipwa nusu ya pesa tu na iliyobakia mpaka leo sijalipwa.
Baada ya wiki nikaamua siondoki, naendelea kupambana chaka.Nikazungumza na jamaa mwengine alikuwa na chain saw,nikanunua mafuta na chakula tukazama chaka(nikawa boss na mimi)akanichania mbao,zikasombwa kuletwa kijijini ili wanunuzi toka Chalinze/Magindu waje kuzinunua.Sasa hapo ndipo nilipoiona dunia chungu.
Kila aliyekuaja alikuwa akiangalia anasema mbao super kweli nitakuja,lakini cha kushangaza kwesho yake haji mtu utasikia tuu alishapita na mzigo kachukulia kwingine.
Nilikaa wiki 3 mzigo hauuziki,Tumboni kuna dude lilikuwaga linafanya kama linafinya,maumivu makalii na hali hii ilikuwa inajitokeza haswa nikiwa nafanya inshu za kusaka pesa.
Na lilikuwa likishika hili dude hapo hakuna kitu kitafanikiwa,yaani yatatokea mazingira flani tuu inshu itavurugika tena kwa ugomvi au mimi kuondoka tuu.
Wiki ya tatu baadae nilikata tamaa,sijauza mbao hata moja.Jamaangu kutoka jiji fulani akanambia niende tuu kwanza nikapumzike ili nijipange upya(namshukuru sanaa sana huyu jamaa).
Alinitumia nauli,saa moja usiku niliondoka kwa mguu kuelekea chalinze.Usiku kucha nilichanja mbuga umbali wa zaidi ya kilometa 75, nikipitia njia ya seregeti A na B.Nilifika chalinze mishale ya saa tano asubuhi.
Nikadaka ndinga mpaka jijini.
Cha ajabu nlivyofika jijini kesho yake mtu niliyemuachia mzigo wa mbao kule kijijini akawa hapatikani kwenye simu,kaja kupatikana siku 3 baadae.Ananambia siku nimeondoka tuu kesho yake mzigo ukaunuliwa woote ila simu ndo ilimuharibikia.
Pia akadai mtoto wake usiku huo alishikwa na homa kali hivyo akalazimika kumega pesa ya mauzo ya mbao ili kumnusuru mtoto so atanirejeshea,nikamwambia shaka hakuna.
Daah,kumwambia anitume kilichobakia sikuamini, ni robo ya pesa nlokuwa nimewekeza kwenye ile biashara. Na hapo ndio ukawa mwisho wangu wa biashara ya mbao.
Visa vingine nitaandika kadiri nitakavyokuwa ninapata muda.
Moja kati ya visa vingi ambavyo nimewahi kukumbana navyo katika maisha ya kuteswa na kutaabishwa na wachawi kwa miaka zaidi ya 20 ktk tasnia hii ya wazee wa nguvu za giza/wachawi/wanga au wazee wa kuloga/kuruka usiku ni hili;
Yakupasa kufahamu ya kwamba;Mchawi akitaka kukuua/kukuharibia maisha muda mwingine hutengeneza mbinu za kupoteza ushahidi(haswa wachawi ndugu,kama wanatoka kwenye ukoo au familia) kiasi kwamba hata watu au wanandugu hawawezi kuhisi kama umethulumiwa haki yako ya kuishi au mafanikio.
Yatatengenezwa mazingira na mwisho wa siku itaonekana ulikuwa ni uzembe wako ama bahati mbaya wewe kuharibikiwa maisha ama kupoteza maisha.
Mwaka 2018 nilikwenda Morogoro kijiji kinaitwa kisama,kama unakwenda magogoni yaani njia ya kwenda ngerengere.
Ni pale ukifika ubena kama unatokea dar basi unakula kona kushoto.
Huko nilikwenda kwa ajili ya biashara ya mbao baada ya kualikwa na jamaa yangu tena kiroho safi kabisaa.
Usafiri wa kwenda huko kijiji cha Chanyumbu kata ya Kisama ni wa shida balaa,gari ni coaster au daladala za dar zinazozamiaga ruti na ni moja tuu kwa siku, na kipindi cha masika hakuna usafiri tena wa gari zaidi ya pikipiki na sio nyingi maana wengi hufungia ndani toyo zao.
Nilifika kijijini Kisama;Kazi ilianza,ni mwendo wa masaa 3 kwa mguu kwenda chaka,msituni yaani huko ni mwendo wa kupiga kambi chaka,full mijoka na mifisi kufukuzia ng'ombe za wamang'ati,mjengo ni kusimamisha miti kisha kuweka turubai tuu juu basi pembeni no ukuta na mvua ikianza hapo ni mtafutanoo,ni mwendo wa kulala wima kama mchongoma,mkeshaa(nadhani wavunaji wa mbao,wazee wa chain saw watakuwa wananielewa hapo).
Kiukweli walipanga kunimaliza kabisa hawa wachawi;Porini mimi nilikuwa msimamizi wa ile chain sawa jamaangu yeye akaondoka akaniachia kwa makubaliano fulani.
Kila mara watu niliokuwa nao porini walikuwa wakinieleza vile nimekuwa nikiota usiku,napiga makelele na kutamka maneno yanayooashiria niko kwenye mapigano.."Niachenii,msinifungee". Moja kati ya maneno niliyowahi kuyatamka.(nilielezwa asubuhi baada ya kuamka) na ilikuwa kawaida mimi kuota ndoto hatari,za hovyo,chafu za kishetani.
Mwezi mmoja baadae sijui hata ilikuwaje tuu,siku hiyo tumetoka chaka jioni nikakuta ujumbe pale kijijini kwa mwenyeji wetu eti jamaangu anadai mashine nikabidhi,nisisimamie tena.
Nikasema sawa ila lipa kwanza madai yangu ya usimamizi duuh hapo ndipo balaa lilipoanzia,jamaa bila aibu akagoma kulipa,akadai nilizoiba zinanitosha.
Aise sijui tuu ilikuwaje mtu aloambiwa aichukue chain saw kaanza kuniropokea,ghaflaa nikabeba panga lah ni Mungu tuu lakini dhumuni ilikuwa nimkate halafu afe/adhurike me nipotezwe jela.Hata mwenyeji wetu alishangaa sanaa kuniona nimepagawa na kuleta balaa kubwa,watu kibaoo.
Mgogoro ule uliisha baada ya kulipwa nusu ya pesa tu na iliyobakia mpaka leo sijalipwa.
Baada ya wiki nikaamua siondoki, naendelea kupambana chaka.Nikazungumza na jamaa mwengine alikuwa na chain saw,nikanunua mafuta na chakula tukazama chaka(nikawa boss na mimi)akanichania mbao,zikasombwa kuletwa kijijini ili wanunuzi toka Chalinze/Magindu waje kuzinunua.Sasa hapo ndipo nilipoiona dunia chungu.
Kila aliyekuaja alikuwa akiangalia anasema mbao super kweli nitakuja,lakini cha kushangaza kwesho yake haji mtu utasikia tuu alishapita na mzigo kachukulia kwingine.
Nilikaa wiki 3 mzigo hauuziki,Tumboni kuna dude lilikuwaga linafanya kama linafinya,maumivu makalii na hali hii ilikuwa inajitokeza haswa nikiwa nafanya inshu za kusaka pesa.
Na lilikuwa likishika hili dude hapo hakuna kitu kitafanikiwa,yaani yatatokea mazingira flani tuu inshu itavurugika tena kwa ugomvi au mimi kuondoka tuu.
Wiki ya tatu baadae nilikata tamaa,sijauza mbao hata moja.Jamaangu kutoka jiji fulani akanambia niende tuu kwanza nikapumzike ili nijipange upya(namshukuru sanaa sana huyu jamaa).
Alinitumia nauli,saa moja usiku niliondoka kwa mguu kuelekea chalinze.Usiku kucha nilichanja mbuga umbali wa zaidi ya kilometa 75, nikipitia njia ya seregeti A na B.Nilifika chalinze mishale ya saa tano asubuhi.
Nikadaka ndinga mpaka jijini.
Cha ajabu nlivyofika jijini kesho yake mtu niliyemuachia mzigo wa mbao kule kijijini akawa hapatikani kwenye simu,kaja kupatikana siku 3 baadae.Ananambia siku nimeondoka tuu kesho yake mzigo ukaunuliwa woote ila simu ndo ilimuharibikia.
Pia akadai mtoto wake usiku huo alishikwa na homa kali hivyo akalazimika kumega pesa ya mauzo ya mbao ili kumnusuru mtoto so atanirejeshea,nikamwambia shaka hakuna.
Daah,kumwambia anitume kilichobakia sikuamini, ni robo ya pesa nlokuwa nimewekeza kwenye ile biashara. Na hapo ndio ukawa mwisho wangu wa biashara ya mbao.
Visa vingine nitaandika kadiri nitakavyokuwa ninapata muda.