Uchimbaji Madini katika Mbuga zetu Ufikiriwe mara mbili kabla ya hatua kuchukuliwa

Mtasema na na kububujikwa na machozi ila MAMA SAMIA TUNAKUOMBEA UWE MALIKIA WA NCHI
 
Utalii sio wa wanyama peke yake. Morocco, Egypt na Dubai wana wanyama? Tatizo ni kama hayo madini yatachimbwa huku mnufaika akiwa mchimbaji na sio nchi. Kama sheria ya madini iko vizuri yachimbwe tu.
 
Moja ya uamuzi wa hovyo kabisa kutoka kwa kiongozi mkuu, sijui washauri wake ni akina nani?!.
Sio kila sehemu unawaza uwekezaji...athari zake ni kubwa tena endelevu kuliko faida utakayoipata.
Migodi inaenda sambamba na hekaheka nyingi ambazo hazifai kabisa katika hifadhi ya wanyama pori.
Hivi Sa100 anadhani marais walimtangulia hawakujua kwamba baadhi ya hifadhi kuna madini lakini hawakuthubutu kufanya anachotaka kukifanya??
Jamani washauri wa huyu mama ni akina nani hao wasio na uchungu na nchi yao???
Blasting za migodi anazijua kweli huyu?!.

Hata hivyo Serengeti iko ktk orodha ya urithi wa Dunia chini ya UNESCO hivyo hawawezi kukubali upuuzi huo wa kuanzisha mgodi wa dhahabu ndani ya Serengeti.
Kauli mbiu ya Serengeti ni Serengeti shall never die!!.
 
Hivi mkianza kulipua Baruti kwenye hìzo Mbuga za Wanyama kuna mnyama atabàkia?!
 
Nje ya mada, ktk nchi nyingi za Kiafrika ikiwamo Tz ni muhimu sana sana nchi ikapata Rais intelligent.
Nasema hivyo kwasabb washauri wa marais huwa wanaangalia boss anataka nn so watashauri kulingana na uelekeo boss anaotaka kuuchukua hata kama uamuzi huo utaigharimu nchi kwa ujumla wenyewe wataitikia tu NDIO boss.
Na hii ni hatari zaidi kwa nchi zenye katiba mbovu kama yetu inayomfanya Rais ni sawa na Mungu kwamba hakosei!!.
 
UCHIMBAJI MADINI KWENYE MAPORI YETU NDIYO ADUI NAMBA MOJA WA MAZINGIRA YETU, TUTAFAKARI KWA KINA!
/Makandarasi wa Tanzania waunga juhudi za rais wetu /

°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°
°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°

Umoja wa Wakandarasi na Wahandisi wa Tanzania wamemchangia Rais Samia Suluhu helikopta yenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 10 kwa ajili ya shughuli za kampeni mwaka 2025.
 
Hata yakichimbwa bado nchi itapata faida kidogo sana. Mara ya mwisho nilisikia serikali inapata 4% ya mrabaha. Kuliko kuziua mbuga kwa madini yanayoisha na yasiyokuwa na faida bora tuendelee kuzilinda mbuga ambazo zina faida za moja kwa moja kwa mwananchi. Ninadhani mama hii 2025 inamletea mapichapicha.. ashauriwe.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…