KERO Uchimbaji Mchanga unavyoharibu barabara ya Goba - Mpakani kwenda Madale (Dar)

KERO Uchimbaji Mchanga unavyoharibu barabara ya Goba - Mpakani kwenda Madale (Dar)

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
A

Anonymous

Guest
Tusaidiane kufikisha hili kwa mamlaka husika.

UCHIMBAJI MCHANGA UNAVYOHARIBU BARABARA YA GOBA - MPAKANI KWENDA MADALE.

Kutokea Goba - Mpakani , eneo maarufu kama "kwa ajali" ukiwa unaenda Madale kabla hujakutana na barabara ya mbopo, Kuna mto una tenganisha haya maeneo.

Changamoto ni kwamba;
1. Hakuna Daraja kabisa la kupitia hapo, licha ya kwamba barabara hiyo inatumika kwa shida sana.

2. Kuna watu wanaokuja na kuchimba mchanga katika mto huo, jambo ambalo linaharibu barabara na Lina hatarisha maisha ya wakazi walioko jirani.

3. Inaonekana jambo hili ni haramu lakini inawezakana Kuna Uongozi umepokea rushwa kuficha uovu huo. Kwasababu kuna Wakati Polisi akija wachimba mchanga hukimbia.

Naomba Mamlaka husika (serikali), ishughulikie jambo hili. Na tufahamu kama ni halali wao kuchimba mchanga hapo ? (Wana kibali?) Na kama Wana kibali , Je, serikali haioni uharibifu mkubwa wa miundombinu unao fanyika?

PXL_20240518_104818361.PORTRAIT.ORIGINAL.jpg

PXL_20240518_105011456.PORTRAIT.ORIGINAL.jpg

PXL_20240511_143511833.PORTRAIT.jpg

PXL_20240511_143452546.PORTRAIT.jpg
 
Mkuu mchanga usipoondolewa hapo, kina cha maji sikita pungua.. Mto utajaa kwa haraka?
 
Back
Top Bottom