Uchina itaiomba Tanzania (kama bado haijafanya hivyo) iwapatie kituo cha kijeshi (military base)

Uchina itaiomba Tanzania (kama bado haijafanya hivyo) iwapatie kituo cha kijeshi (military base)

Soma vizuri uzi wangu, usifananishe na uvamizi. Makubaliano ya kujenga base yanahusisha kukodisha ardhi kwa malipo, muda wa kukaa, nini kiingizwe n.k.
Acha ujinga wewe mtumwa wa fikra. Kwa nini usishauri Tz ikaombe military base pale China??[emoji57][emoji57]

Sent from my SM-A205F using JamiiForums mobile app
 
Nchi zinazoendelea zipo kwenye nafasi nzuri ya kuiga teknolojia na kufanya mambo makubwa kwa kipindi kifupi kuliko zile zilizoendelea.

Mawazo ya kipumbavu kama haya ya kitumwa ya kuwategemea wengine hayatakiwi tena nyakati hizi. Tunatatakiwa kujijenga wenyewe kwa kuwatumia walioendelea kiuchumi na kiteknolojia.

Tunawahitaji wageni tuwasome na kuwamalizia mbali. Tunaweza na wanasiasa na watawala wajue hilo. Tatizo kubwa ni watawala kujipendekeza kwa wageni.

Watawala wanatakiwa kuwatumia raia wao kuwashughulikia na kuwadhibiti wageni kama wachina, wahindi na wazungu.
 
Inategemea mikataba. Guantanamo ilitolewa na Dikteta wa Cuba Batista kwa muda usiojulikana. Mimi ninachoongea ni mikataba mizuri. Pili usisikie tu. Cuba yenyewe haitaki Wamarekani waondoke Guantanamo maana wanapata kodi, watu wao wanapata kazi.....
Huu si mfano mzuri wa kutoa.
Ukiwa na base na kusiwepo vita unaweza pata faida za kiuchumi ila ikitokea vita utajua hujui. Mfano Russia iingie vitani na NATO alafu zile missile sites zilizoko Poland iziache hilo ni sawa na haiwezekani. China ikipigana na Marekani leo hii itataka ilete meli zake kublock pale Red Sea, hapo itatumia base ya Djibouti kwa ajili ya service na replenishment ya meli. Hapo tiyari ushakaribisha mashambulizi ya Marekani.

Kuna sababu kwa nini US ina base pale kisiwa cha Hawaii ambapo kuna population ndogo sana na base kubwa kabisa pale Guam ambako ni mbali na mainland US na ni watu wachache mno. Hawa hawatapigania homeland, ikifika hatua hiyo watasaini kuacha vita. Japan alipopigwa akaondolewa Asia nzima angetaka kusaini vita iishe angekubaliwa
 
Germany, France, Italy,United Kingdom, USA, China na Saudi Arabia wote hao wana military bases Djibouti
Yaani kanchi kadogo ila kamezungukwa na Wanajeshi wa kila aina

Na wote wamekaa karibu karibu sana
Hivi nyie military bases mnazichukuliaje. Nikajua mnamaanisha zile bases haswa zenye wanajeshi angalau 10,000 kumbe mnasema hivi vituo vya mazoezi ambapo unakuta contingency ya wanajeshi 500 wanaokaa miezi miwili na kuondoka.

Djibouti najua ana base ya China na ya Marekani tu. Hizo nyingine ni tuvituo twa kupumzikia kina HMS Queen Elizabeth zikipita na clue imechoka ije ipumzike.
 
Hivi nyie military bases mnazichukuliaje. Nikajua mnamaanisha zile bases haswa zenye wanajeshi angalau 10,000 kumbe mnasema hivi vituo vya mazoezi ambapo unakuta contingency ya wanajeshi 500 wanaokaa miezi miwili na kuondoka.

Djibouti najua ana base ya China na ya Marekani tu. Hizo nyingine ni tuvituo twa kupumzikia kina HMS Queen Elizabeth zikipita na clue imechoka ije ipumzike.

Hahaha mkuu mbona hivyo tena
Hata wakiwa 20
Hapo nchi zote wameweka meli zao na personnel pia

Mimi nilikuwa napinga kuwa Ukimkaribisha mchina, Mmarekani atakasirika hilo tu ndio maana nikaandika nchi nyingi zipo djibouti na wako sawa tu

Don’t get me wrong buddy
 
Mentality za weak azz people wanaofikiria mchina atawatoa kwenye njaa zao, hakuna short cut ni kazi kwa bidii tuu na kuacha ufisadi wa aina yeyote ule
 
Mentality za weak azz people wanaofikiria mchina atawatoa kwenye njaa zao, hakuna short cut ni kazi kwa bidii tuu na kuacha ufisadi wa aina yeyote ule
Methinks your Medulla Oblongata is on a long holiday. You do not know that military bases renting is a business just like other businesses. You get paid just as you get paid for selling other services. Now, jump on your Bodaboda, somebody is waiting for you to give him a ride home. Leave this thread. You will NEVER understand it!
 
Hatutaki military base ya kigeni kwenye ardhi yetu.
 
Kwa nini hawa 'illiterates' na 'functional fools' hawatoi mawazo yao tu hadi watukane? It beats me! Ni inferiority complex yao ndiyo inayowafanya hivyo? Sitaweza kujua.
Kama nitafika mbinguni kwenye Ufalme wa Mungu, ombi langu ni moja tu: aniletee mbele mtu kama huyu, anifungulie fuvu la kichwa chake nipate kuona exactly ameweka nini ndani yake? Hayumkini mtu unaandika hoja, halafu mtu aje akutukane, tu!
Acha ujinga wewe mtumwa wa fikra. Kwa nini usishauri Tz ikaombe military base pale China??[emoji57][emoji57]

Sent from my SM-A205F using JamiiForums mobile app
Kwa nini hawa 'illiterates' na 'functional fools' hawatoi mawazo yao tu hadi watukane? It beats me! Ni inferiority complex yao ndiyo inayowafanya hivyo? Sitaweza kujua.
Kama nitafika mbinguni kwenye Ufalme wa Mungu, ombi langu ni moja tu: aniletee mbele mtu kama huyu, anifungulie fuvu la kichwa chake nipate kuona exactly ameweka nini ndani yake? Hayumkini mtu unaandika hoja, halafu mtu aje akutukane, tu!
Kwa nini huleti hoja ya kuwa Tanzania iombe military base China, halafu uwa convince watu kuwa hiyo ndiyo option bora? It is so simple!
 
wapi UAE imekubali acha uongo. UAE ina military base ya ufaransa na waamerica hakuna wachina porojo hizo
 
Habari zinazotembea hivi sasa ni kuwa punde hivi Uchina itaiomba Tanzania (kama bado haijafanya hivyo) iwapatie kituo cha kijeshi (military base). Kama ilivyoomba nchi kadhaa ikiwemo UAE, Pakistan, Tajikistan (UAE imekwishawapa).

Najua ombi hilo likifika Tanzania kuna wale watakaosema 'lakini siasa ya Tanzania ni kutofungamana na kokote!' Au, 'wajua sisi Tanzania ni nchi ya amani' au 'mbona hiyo itatuletea matatizo'na mambo mengi yanayoonesha ugandaji wa fikra za karne ya 20.

Zama zimeendelea mbele na hivi sasa kuna uhalisia mpya. Ukitazama jinsi mataifa yanavyofukuzana kushindana katika kutengeneza na kulimbikiza silaha, utajua kuwa it is a matter of time, kabla ya vita kuu ya dunia 3 kutinga. Katika vita kama hiyo hakuna atakayejali kuwa Tanzania ni 'nchi isiyofungamana na dola lolote'.

Linalotakikana sasa ni kuwa 'pragmatic' na kukubali ombi la nchi hii ambayo tayari ni namba 1 katika mambo mengi isipokuwa machache tu ambayo Marekani bado inaongoza (utengezaji wa ndege za abiria/kivita, nano technology, AI...).

Ni vizuri kuwa juu ya mgongo wa ndovu wakati chui anashambulia kuliko kuwa unatembea kwa miguu.

Kuna saikolojia inayomfanya mwingine aone anaweza kukuamini pindi unapokuwa tayari kumsaidia wakati wa dhiki, kuliko wakati tayari amepata ofa nyingine.

Faida za kuwepo military base Tanzania zitakuwa nyingi ikiwemo kupata ujuzi wa vyombo vya kisasa na pengine kuanzisha viwanda vya kutengeneza silaha za kisasa. Ili mradi tu mkataba utakaoingiwa uwe unatazama maslahi mapana ya Tanzania.
Cacophony trivial writings

Sent from my SM-G9350 using JamiiForums mobile app
 
UAE gani imekubali kuwa na military base ya Mchina? UAE ni US ally na kuna airbase ya kurusha drones kuzurula Middle East.

UAE haiwezi kubali kinjaanjaa kama Djibouti ilivyofanya. UAE anaomba kila siku US imuuzie F-35 alafu iruhusu base ya China si itakuwa kama kesi ya Turkey na S400 za Urusi. Alafu UAE haamini tena silaha za Mchina, US ilipokataa kumuuzia drones akaenda kwa China akauziwa drones zinadondoka ovyo. Kwa vile hana njaa akazigawa zile drones.

Ukiruhusu China iwe na base kwako usitarajie US akuuzie silaha. Hakuna anayetaka uwe unaoperate silaha zake wakati huo mifumo ya adui wake inakusoma vizuri kwa uwazi. US inaringa kuuza silaha na UAE inazitaka sana hizo made in US.

Sisi Tanzania njaa kali hata tukipewa silaha za Mchina zinazidi mahitaji yetu. Tuko situated sehemu nzuri hapa Afrika, ukitokea Tanzania unafika Kusini, Kaskazini, katikati kirahisi. Alafu tuko stable kiusalama na hatuna dalili za fujo. Ila tulikubali base ya yeyote lazima kuna vitu tutakosa au kupata. Sioni faida kubwa sana naona ni bora tuwe neutral
Wachina kwa sasa hawana deal tena.

Xi nchi imemshinda.

Sioni faida yeyote ya kumkumbatia mchina, bora US ambaye hata analeta quality investments kuliko hao machinga wa kichina waliojazana kkoo.
 
Wakikubaliwa na Tanzania ( Serikali ) pamoja na JWTZ Wenyewe naiona ile Safari ya Tanzania kuanza 'Kuchukiwa' na Marekani itaanza kwani inasemekana kuwa nchini Kenya Marekani ama wameshaweka hiyo 'base' yao au ndiyo wanajiandaa kuiweka sasa, hivyo uwepo wa China karibu yao kutakuwa ni tatizo na hata tishio Kwao.

Katika hili Umakini unahitajika sana tu.
Marekani wakati wa utawala wa Bush hadi utawala wa Obama walikuwa wanataka kuweka makao makuu ya kamandi ya Afrika hapa Tanzania kwa sababu kadhaa; sasa hivi makao makuu ya kamandi ya Afrika nadhani bado yako Ujerumani. Sababu kubwa ya marais Bush na Obama kuja Tanzania na kusaka kiwanja cha kujenga makao makuu hayo, lakini maombi yao yalikataliwa, nadhani kwa msukumo fulani kutoka AU. Nakumbuka kipindi hicho watu wakisema nchi inatambulika sna hadi maraisi wa marekani wanashindana kuja Tanzania, lakini ukweli walikuwa wanakuja kutafuta maslahi yao.
 
Ukishawapa naval base ,utaweza kuwadhibiti wewe!? Zaidi ya wao kuudhibiti ukanda wote wa bahari kwa maslahi yao. Tamaa mbele mauti nyuma. Tafuteni vya kwenu. Ukorofi wa mchina kawaulize majirani zake huko baharini.
Nashangaa sana watu wanawasifu wachina. Wanawapiga mkiwa kwenu tena wakiwa kama raia wageni, je mkiwapa hiyo military base itakuwaje?

China ya akina Mao sio China ya Xi jinping
 
Wachina kwa sasa hawana deal tena.

Xi nchi imemshinda.

Sioni faida yeyote ya kumkumbatia mchina, bora US ambaye hata analeta quality investments kuliko hao machinga wa kichina waliojazana kkoo.
Mchina sio mstaaabu kama mzungu ila wote sioni kwa nini tumpe ardhi aweke majeshi yake hapa. Hata kama ni pesa ndio tutapata ila si ni sawa na kuwauzia uhuru wetu. Ni hela ndio ila za moto
 
Back
Top Bottom