Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 21,967
- 32,074
Ya kwako mwenyewe haya. Ya kuokoteza kwenye vijiwe vya gahawa na mitaani. "Rumours" hapa Bongo ndio penyewe. Ukiambiwa ulete ushahidi wa hiyo memo ya CCT kwenda kwa Mrema hautaweza. Mzee Mohamed, matatizo ya Waislam hapa Tanzania na kwingineko duniani yako kwa Waislam wenyewe. Ukiyaelekeza matatizo haya kwingine unazidi tu kuyalea na kuyakuza matatizo haya. Tabia moja mbaya ya matatizo ni kuitana.
WC,
Mimi sina ugomvi na fikra zako.
Nachofanya hapa si kuwa wewe ukubali haya ninayosema.
La hasha.
Nataka dunia nayo isikie upande wetu Waislam tunasemaje
katika matatizo haya yanayokabili nchi yetu.
Ndiyo maana umeona nimeandika Kizungu.
Iko siku Insha Allah dunia ndiyo watakujakuwa wapatanishi
wetu.
Hawawezi kupatanisha ikiwa hawajui chanzo cha ugomvi.
Kwa hakika uansema kweli akija mtu akanambia lete ushahidi
wa kimahakama nitashindwa tena vibaya sana.
Lakini ukweli utabaki pale pale kuwa nchi imo katika matatizo
makubwa.
Mwisho.
Ndugu yangu basi huna cha kunijibu cha kweri kwa yote niliyo
kuandikia kwa adabu na taadhima ila ijaza yangu ni kunikejeli?
Hiyo ''kijiwe'' na ''gahawa ya mitaani'' inaingiaje hapa?
Mimi si mtu wa ''kijiwe'' wala wa ''mitaani.''
Kunywa kahawa sawa ni katika mila zetu wa pwani kama nyie
mnvayokunywa ulevi.
Umepata kusoma humu mie hata siku moja nikakuita mlevi wa tembo nk.
Fanya staha tuwe na mnakasha wa kistaarabu.
Basi unashindwa hata kuniheshimu kwa utu uzima wangu?
Mimi sijawa adui yenu.
Kiwango hiko lau kama tunakijongelea bado hatujafika na Insha Allah
Mungu hatotufikisha huko.
Ukweli utadhihiri na tutarekebisha pale tulipojikwaa.