...Hii tabia ya watu kujifanya watetezi wa jamii fulani sasa imekuwa kama mtaji wa kutokea. Baada ya 'Mwembechai Killings', prof. Njozi sasa ni VC wa Muslim University Morogoro(MUM)-ameula, ukilinganisha na nafasi aliyokuwa nayo UDSM. Kwa sasa yupo kimya-hakuna 'maajabu' yoyote aliyoyafanya MUM yanayoendana na kariba yake, badala yake tunaona vyuo vingine vidogo kama SJUT vikikua na kufungua campus sehemu mbali mbali nchini. Njozi yeye bado yuko Moro na MUM yake!
Njozi ameshatoka, sasa ni zamu ya Mohamed Said. Huyu anafaidika kwa namna mbali mbali, mojawapo kubwa ni kuuza kutangaza na kuuza kitabu chake-ndiyo maana hachelewi kukushawishi ukisome kitabu chake. Pia anafagilia namna kinavyotumika Ulaya. MS anajua kwamba kama itatokea nafasi ya serikali kujadiliana na waislamu, basi naye atakuwemo na hivyo kufaidi binafsi kama ilivyokuwa kwa Njozi.
Kadiri maisha yanavyozidi kuwa magumu, tutaendelea kuona harakati za aina mbalimbali. Harakati za MS na wengineo, hazina tofauti na za Mungiki-you create terror, you create wealth! Leo tunaona harakat za kidini,kesho zinakuja harakati zitakazowaunganisha watu maskini,n.k. Suala la Mtwara ni mfano mzuri, na Mtwara kwa sasa haina kiongozi. Umejiuliza hali itakuwaje akijitokeza 'kiongozi' wa wana kusini? Patachimbika!
Mwisho, wakati tunalia wakristo 'kuwadhulumu' na 'kuwahujumu' waislam, hakuna hujuma na dhuluma kubwa kupita ya ukoloni na ukoloni mamboleo. Humsikii MS akiwalaumu waarabu wala wazungu maana wanampa chakula-wanamkaribisha kwenye mihadhara na kumpatia fedha. Sio kwamba wazungu wanampenda MS au wanaamini kazi aliyoifanya-they believe in keeping their friends close and their enemies closer! Mtu anayechukia ukristo kwa kiwango cha MS hawezi kuwa rafiki wa wazungu. Wazungu hawapendi extremism kwenye dini-they have learnt the hard way!
Kama kweli si ni wazalendo, tuhoji tunafaidika vip na maliasili yetu kama wanavyofanya wanamtwara. Nani anayesaini mikataba ya Mangungo gizani? Kwanini hatujulishwi tutafaidika nini na vip na uwekezaji? Tukihoji maliasili yetu inavyotumika tunaweza hata kuondoa 'imbalances' ktk jamii kama zipo, sio kwa kulilia yaliyopita, tena kwa upotoshaji!