Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

Unaona kama umepata pakupumulia, wapi? ulijidai kuruka kwenda Iringa huko ukakutana na ma uppercut ya uhakika, ukaanza oooh, wewe hujui historia ya machifu, lakini ukaufyata hukuendelea, unakumbuka ulipojidai unamjuwa chifu wa huko ukaulizwa "Abdu Mkwawa?" ukabana kimya kama hukuona.

Nakuonea huruma sana kujitosa kwenye maji yaliyokuzidi kimo na kuogelea hujui. Naona wenzako wamekutupia tyubu ujivutevute, ukisha pata pumzi njoo na jingine.

Tunasubiri, ulisema ukimaliza la Mkwawa utakuja na la Abushiri, vipi? maji marefu? Naona la Mkwawa umeomba ukatafute data kama ulivyoomba kuleta klip ukaingia mitini wala huiongelei, nna uhakika na la Mkwawa limekuwa ni knockout ya ki Tyson (zile za raundi ya kwanza) kwako. Pole sana, lakini usikate tamaa, jitahidi ndio ukubwa huo.

Zomba,

Chunguza kitu kimoja.

Kuna post naziweka hapa zina habari ambazo ningetegemea
ningeulizwa habari zaidi lakini naona kimya hawazigusi kitu
kama vile wanaziogopa.

Kwengine nikieleza habari hizo huwa kunakuja maswali mengi
ya kutaka kujua zaidi.

Humu ninachokiona ni maswali ya mtego kutaka kuumbua.

Nimegusia jinsi Lawi Sijaona alivyoitwa Lindi kutoka Newala
na Suleiman Masudi Mnonji.

Hii ilikuwa 1953.
Kisha nikaeleza jinsi Mnonji alivyounda TANU na wenzake.

Mwisho nikaeleza Nyerere alivyomfunga Mnonji baada ya
uhuru.

Mwisho nikaeleza barua ya masikitiko Mnonji aliyomwandikia
Nyerere kumwambia kuwa ikiwa yeye Nyerere ana ushahidi
wa yeye Mnonji kutaka kupindua serikali yake ampeleke
mahakamani akajibu mashtaka la hana basi amwache huru
arejee nyumbani kwake.

Mwisho wa barua Mnonji akamkumbusha Nyerere khisani
iliyokuwapo hapo nyuma kati yake na yeye.

Barua hii ilikuwa ''dictation'' Mnonji akimwambia Sijaona
jela na Sijaona akiandika.

Ile ilikuwa barua ya mkono ambayo Mnonji alimuomba
Sijaona ampe Nyerere.

Sijapata swali lolote katika mikasa kama hii na mfano wa
huu.
 
Mag3 katika bandiko lako 2868 nayaangalia yafutayo na yatokanayo na kitabu, majibu na hoja za Mohamed Said.

1. Alichokiandika Mohamed ni kitu alichokuwa na majibu yake na utafiti ulilenga katika kukamilisha kile alichofikiri na si kile alichotafiti.

a) Ameonyesha bias ya uandishi kwa kuelekeza watu kuamini kile alichokusudia na si kile alichokitafiti
b) Aliandika katika mtazamo wa kushambulia ''attack'' kundi fulani la jamii na watu fulani si kutokana na hukumu ya historia bali kile alichodhani kuwa ima yeye au wazazi au ndugu zake hawakutendewa wema au walionewa.
c) Ameshindwa kuthibitisha maandiko yake kwa hoja za kitafiti,kukwepa maswali au hoja zinazoonekana kukinzana na a, b hapo juu.

Hoja: Endapo Mohamed alifanya utafiti asingeweza kuzama katika historia ya uhuru wa Tanganyika kwa kuzama katika TANU na kukwepa historia iliyoanzia karne nyingi. Mathalani, Mohamed hakueleza undani wa AA au TAA kwa kutambua kuwa hilo litaharibu historia nzima anayoidai, wala kulezea harakati nyingine nje ya Dar, mfano Mbiru na Wapare, vyama vya wafanyakazi n.k.

Mfano, angeandika kwa undani kuhusu AA na TAA ni dhahiri asingekuwa na hoja ya Nyerere kufundishwa siasa mwaka 1952 ili hali twajua kuwa alianza siasa miaka 6 kabla ya hapo tena katika uwakilishi wa jimbo kama Tabora.
Hilo peke yake lingetosha kupunguza nguvu za ziada anazompatia Abdul Sykes.

Ni kwasbabu ya kuonyesha bias, Mohamed amejikuta anaficha ukweli wa historia ya kweli.
Kwa vile lengo ni kushambulia kundi fulani, bwana Said ameacha makusudi mchango wa shirika la Maryknoll huku akiufahamu vema.

Kibaya zaidi ameenda mbali na kuudharau kwa kusema ni 'ticket' moja. Wakati akiudharau mchango huo Mohamed ameutukuza sana mchango wa ticket moja uliofanywa na wazee wake. Hapa ukweli upo wapi katika double standard kama hii.

Ili kukamilisha lengo alilokusudia,Mohamed amewaandika washiriki wa uhuru wasio katika kundi lake kwa dhalili ya hali ya juu. Amewataja kwa imani zao kama viambatanisho vya majina yao na kuacha mchango wao katika mapambano.

Katika hilo la bias, Mohamed ameandika kurusa za kutosha kuhusu Mwapachu kuliko alivyomwandika Mtamila aliyekuwepo kabla ya Mwapachu. Mo amemuelezea Mshume Kiyate kiasi kwamba Rais wa TAA Dr Vedastus Kyaruzi mchango wake hauonekani.

Kila mmoja alikuwa na mchango na si sahihi kuufanya mchango fulani bora kuliko mwingine hasa kwa kuangalia majina na viambatanisho vya imani zao. Hilo linaondoa hata hoja dhaifu iliyokuwepo.

Mohamed ameshindwa kuthibitisha madai yaliyomo ndani ya kitabu chake. Hata pale alipojaribu, MO alikwenda nje ya taratibu za utafiti na kanuni za asili za ''kisheria'' natural justice.

Mathalani, amelituhumu Kanisa kuhusika na mambo mengi maovu na mengi yaliyozuia harakati.
Ameshindwa kuthibitisha ushiriki wa kanisa, kinyume chake kunukuu habari za mtu mwingine ambaye kimsingi angekuwa chanzo cha utafiti wa ushahidi na si yeye kuwa ushahidi(sivalon).

Kwa vile uandishi wake ni katika misingi ya ''attack'' na siyo academic, Mohamed ameshindwa kutetea hoja zake kimantiki.
Mfano, hajaeleza kwanini ilipangwa njama ya kuondoa Nyerere katika uongozi wa TANU mara mbili wakati huo akiwa hana uongozi wa nchi au vyombo vya dola na akiwa chini ya baraza la wazee wa TANU waliokuwa wazee wake.

Moh ameshindwa kutetea hoja ni kwanini ukristo wake ulionekana kikwazo hata kabla ya kuingia madarakani na kwanini majaribio hayo yalipangwa. Pengine hapa alitaka kuficha hisia za udini ambazo ni sehemu ya malalamiko yake ya leo.

Mo ameshindwa kututhibitishia mkakati wa Nyerere kuumaliza Uislam na kuingiza ukristo ulianza lini na kwa mbinu gani.
Kinyume chake ametumia kifo cha EAMWS kumtupia lawama kama sehemu ya ukristo na kanisa.
Ameshindwa kututhibitishia ushiriki wa kanisa kwa ushahidi hivyo kubaki kuamini ndivyo ilikuwa.

Lakini pia ameshindwa kutetea hoja za EAMWS kwanini ilikufa huko kwingine na ni nani alihusika kuiua.
Kwa vile hoja yake haisimami yenyewe, Mo amewashirikisha baadhi ya waislam kama sehemu ya njama.

Iwe iwavyo mtu aliyekuwa na mtazamo tofauti na malengo ya MO huyo alikuwa kibaraka. Alikuwa kibaraka kama Amir Kweyamba aliyekuwa kachero wa serikali, lakini wale waliokula njama dhidi ya serikali walibaki kuwa waislam safi.

Mo ameupotosha umma mara nyingi katika hali ya kujenga hoja na pengine kuficha ukweli.
mfano, si kweli kuwa Nyerere alikuja Dar mwaka 1952, si kweli kuwa alionana kwa mara ya kwanza na Sykes mwaka 1952, si kweli kuwa viongozi wa TAA hawakumjua, si kweli kuwa alianza siasa mwaka 1952, si kweli aliandikiwa hotuba bila kujua alikwenda UNO kusema nini akiwa msomi mkubwa ndani ya TANU.

Ni katika upotoshaji huo, Mohamed ameacha kwa maksudi mchango uliotolewa na wazawa wengine wasio na imani kama yake. Amejikuta akikweza watu kwa majina ili kuficha majina yasiyompendeza.
Mfano, tunauthamini mchango wa Yusuf Ngozi lakini je, Yusuf alikuwa katika nafasi aliyokuwa nayo Dr Vedastus Kyaruz, Clement Mtamila, Stephen Mhando, Cecil Matola, Dunstan Omar na wengine ?

Mifano na hoja ni nyingi sana lakini kwa ufupi nimalizie kwa kusema, alichoandika Mohamed ni kutumia majina, nyakati na matukio ili kupata nafasi ya kushambulia sehemu ya jamii yetu kwa kudhalilisha na kudharau michango yao.
Hili limefanyika kwa kutumia majina kama Nyerere au kwa shambulizi la dini.

Amefanya hivyo kwa kuhadaa kuhusu utafiti kwasababu alijua kile alichokusudia kabla ya kuanza utafiti.
Mohamed amefanya hivyo ili kujenga uhalali wa kundi fulani juu ya umiliki wa nchi na kupitia hilo apenyeze madai yake ambayo mengi hayana uthibitisho kama kilivyo kitabu chake.

Sehemu kubwa ya maandiko yake yanatokana na ''third party'' na wengi aliowahoji ima walikuwa na duku duku au walieleza ukweli ambao Mo hapendi uwekwe hadharani. Ameshindwa kutuwekea shajara alizosoma na akitaka tuamini kile kilichomo ndani ya shajara. Kanuni za uandishi hasa wa kitafiti hazikubaliani na hilo.

Ili kuhakikisha kuwa jamii aliyokusudia kuieleza ina amini na haipati nafasi za kuhoji hoja zake, Mohamed ametumia sehemu kubwa ya utafiti wake na maandishi kujenga chuki, kuleta farki na uhasama.

Ametumia dhana kuhusu kile marehemu walichokifikiri hata kama hakuwahi kuwahoji na ameshindwa kuwahoji walio hai ili kupata upande wa pili.

Mo anafahamu kuwa sehemu rahisi sana ya kufikia malengo yake ni kutumia dini. Hili analifanya kwa njia ya ''sisi dhidi yao''

Ushahidi kuwa ameshindwa kutetea hoja zake,amepotosha, ameficha baadhi ya ukweli na ameshindwa kujibu hoja au maswali na pale alipojaribu alifanya hivyo kwa udhaifu, unatueleza kilichomo ndani ya mistari aliyoandika.
Na hapa ndipo taifa linapopaswa kutupia jicho.

Asante sana Kaka Nguruvi3, na ndio maana mimi sikupenda sana mada kama ya Mkwawa na wengine ziingie humu kwani bado kuna viporo vingi havijajibiwa kwenye histohisia ya Mzee Mohamed ya 1950's

Nadhani Kaka Mohamedi hakulitendea haki kundi kubwa "lililosahahuliwa" kama kweli alikuwa na nia ya kulitetea kundi hilo kwa mujibu wa mabandiko yake,
Pilika za kugombea uhuru kwa upande wa Mzizima hazikuwa za Waislamu wala za Wazulu na Wamamnyema pekeyao, Waislamu, Wakristo, Wapagani na Waabudu Mizimu walishiriki kama Watanganyika bila kuangalia itikadi ya Imani zao wala makabila yao, tofauti na Mzee Mohamed anavyotaka kutuweka kwenye itikadi ya Kiimani na Kikabila

Baada ya Nyerere kusomewa Dua na Waislam pale kwa Tambaza, Kundi lingine lisilokuwa la Kiislamu lilimuita Nyerere na Kumfanyia Tambiko ambalo halikuwa la Kiislam(Hotuba ya Nyerere ya Kuaga 1985), Tambiko lilifanywa mbele ya hao Waislam (Tambaza at el) na wala (Waislam) hawakupinga kufanyika tambiko lililo kinyume na Uislam, kwa wale Waislam waliona kila iman inaplay part yake kwenye pilikpilka za kutafuta uhuru,

kwa Mohamedi kitendo cha kusomewa Dua ya Kiislamu ndio kinapewa kipaumbele lakini hilo la tambiko halimuhusu kwa sababu waliofanya hilo tambiko si wazee wake, yeye wazee wake ni wale Waislam wa Kizulu na Kimanyema. na hapo ndio unaweza kuona Mzee Mohamed ana Nia na Malengo gani kwenye hii Histohisia aliyoiandika na anayosimamia
 
Yericko,Mkwawa alikuwa Muislam.Waislam hatubatizwi tunazaliwa tayari ni Waislam.
Thanks 4 the info. mimi nilifikili Waislaam wanabatizwa kama sisi Wakristo, nilipo soma maelezo ya Mr.Zomba ndio nilielewa kiundani tofauti za ki-imani kati ya dini zetu mbili specifically mambo ya UBATIZO..
 
Yericko,

Mkwawa alikuwa Muislam.
Waislam hatubatizwi tunazaliwa tayari ni Waislam.
Hebu oneni hichi kituko!...jamani ni kweli Mungu yupo, ila hizi dini tumeletewa na wajanja wachache tu.

Wazungu walituletea ukristo

Waarabu walituletea uislaam....kabla ya waAfrica tulikuwa hatuna dini isipokuwa matambiko ya kimizimu tu.

Kweli wafia dini kazi mnayo.
 
Inaaminika na Mwalimu Nyerere amelithibitisha katika hotuba yake kuwa nyakati zingine walikwenda kutambika,

Swali la kujiuliza kwa wadau wote ni, Je walitambika Kikristu, Kiislamu ama kipagani/kijadi?

Tukipata jibu sasa tujenge hoja kwa dhana ya hoja ya udini ya Mohamed Said na waambata wao!
 
Mmeathiriwa na Mohamed Said,

Nilishasema juu ya mambo ya kichifu Mohamed Said hataniweza, anahitaji msaada wa haraka, na nikaongeza kuwa hata kama muumba amuongezee miaka 60 mingine mbele katika uhai wake, basi kwamambo yahusuyo uchifu na himaya zake afrika atabaki kuwa msikilizaji wangu tu!

Nasema tena upya kuwa historia ya Mkwavinyika Mwamuyinga haijui,

Hajui kwanini alijua kusoma na kuandika Kiarabu, eti anasema alizaliwa akiwa Muislamu????

Hivi pale Rungemba alipolala Mnyigumba baba yake mzazi wa Mkwavinyika Mnyigumba paliwahi kuwa na chembe la uislamu?

Mohamed Said nakujuza tu kuwa jina la Abdala kwa chifu Mkwawa alilipata akiwa tayari ni chifu na alilipata baada ya mahusiano mazuri na waarabu waliokuwa wakimuuzia nguo na vitu vingine, ndipo akajua kusoma na kuandika na akaiga kuswali kiarabu!

Walipokuja Wajerumani nao pia walimfundisha tamaduni zao za kusali na kusoma na kuandika,

Nenda pale Kalenga kuna maandishi mengi sana ya kijerumani,

Kumbuka Mkwawa Mnyigumba kwa dini alikuwa muamini wa DINI za ASILI/Jadi

Na maandishi ya Mkwawa yote ni mawasiliono ya barua kati yake na wajerumani

Na zaidi kuna mahali maalumu alipokuwa akisali kwa KIKRISTU (kijerumani)

Nakusihi na kukuonya Mohamed Said usijifungie kiudini tu, utasinyaa kwa kila jambo!

Yericko,

Mbona wewe kutwa ni vitisho tu?
Mnakasha hausafiri kwa vitisho.

Mnakasha unastawishwa kwa hoja.

Fika Makumbusho ya Mkwawa Kalenga kuna barua Mkwawa kawaandikia
Wajerumani mwaka 1896.

Barua hii Mkwawa kaanza kwa kusema, ''Bismillah Rahman Rahim.''
Huu ni ufunguo wa Muislam.

Mpagani haanzi mambo yake kwa maneno hayo.

Hayo mengine wala sina haja ya kujibu.
 
Mmeathiriwa na Mohamed Said,

Nilishasema juu ya mambo ya kichifu Mohamed Said hataniweza, anahitaji msaada wa haraka, na nikaongeza kuwa hata kama muumba amuongezee miaka 60 mingine mbele katika uhai wake, basi kwambo yahusuyo uchifu na himaya zake afrika atabaki kuwa msikilizaji wangu tu!

Nasema tena upya kuwa historia ya Mkwavinyika Mwamuyinga haijui,

Hajui kwanini alijua kusoma na kuandika Kiarabu, eti anasema alizaliwa akiwa Muislamu????

Hivi pale Rungemba alipolala Mnyigumba baba yake mzazi wa Mkwavinyika Mnyigumba paliwaji kuwa na chembe la uislamu?

Mohamed Said nakujuza tu kuwa jina la Abdala kwa chifu Mkwawa alilipata akiwa tayari ni chifu na alilipata baada ya mahusiano mazuri na waarabu waliokuwa wakimuuzia nguo na vitu vingine, ndipo akajua kusoma na kuandika na akaiga kuswali kiarabu!

Walipokuja Wajerumani nao pia walimfundisha tamaduni zao za kusali na kusoma na kuandika,

Nenda pale Kalenga kuna maandishi mengi sana ya kijerumani,

Na yote ni mawasiliono ya barua kati yake na wajerumani

Na zaidi kuna mahali maalumu alipokuwa akisali kwa KIKRISTU (kijerumani)

Nakusihi na kukuonya Mohamed Said usijifungie kiudini tu, utasinyaa kwa kila jambo!

Tatizo siyo kukuweza tatizo kila unapotia mguu watu wameishapita huko ulichokiandika hapa kimedhirisha ulivyokuwa mtupu kwenye historia.
 
Inaaminika na Mwalimu Nyerere amelithibitisha katika hotuba yake kuwa nyakati zingine walikwenda kutambika,

Swali la kujiuliza kwa wadau wote ni, Je walitambika Kikristu, Kiislamu ama kipagani/kijadi?

Tukipata jibu sasa tujenge hoja kwa dhana ya hoja ya udini ya Mohamed Said na waambata wao!

Nadhani tumejichokea.
Tunahitaji mapumziko.

Mnasemaje wana ukumbi?

Mnaona tija yoyote katika
mnakasha wa namni hii?

Hapa inatakiwa subra ya
Nabii Ayub.
 
Yericko,

Mbona wewe kutwa ni vitisho tu?
Mnakasha hausafiri kwa vitisho.

Mnakasha unastawishwa kwa hoja.

Fika Makumbusho ya Mkwawa Kalenga kuna barua Mkwawa kawaandikia
Wajerumani mwaka 1896.

Barua hii Mkwawa kaanza kwa kusema, ''Bismillah Rahman Rahim.''
Huu ni ufunguo wa Muislam.

Mpagani haanzi mambo yake kwa maneno hayo.

Hayo mengine wala sina haja ya kujibu.

Sasa naamini wazi kuwa historia huijui ndugu yangu, umebobea kidini zaidi!

Nakupa swali kisha jibu lake ndio ufunguo wako!

Mjerumani na Muarabu nani alitangulia kufika Tanganyika?
 
Inaaminika na Mwalimu Nyerere amelithibitisha katika hotuba yake kuwa nyakati zingine walikwenda kutambika,

Swali la kujiuliza kwa wadau wote ni, Je walitambika Kikristu, Kiislamu ama kipagani/kijadi?

Tukipata jibu sasa tujenge hoja kwa dhana ya hoja ya udini ya Mohamed Said na waambata wao!

Yericko,
Bado una hamu.

Wewe kweli bado una uso wa kuzungumzia hotuba?
 
Nadhani tumejichokea.
Tunahitaji mapumziko.

Mnasemaje wana ukumbi?

Mnaona tija yoyote katika
mnakasha wa namni hii?

Hapa inatakiwa subra ya
Nabii Ayub.

Tatizo lako lilelile la asili la kukwepa hoja muhimu na kushangiilia kusifiwa na wasiojua historia
 
Asante sana Kaka Nguruvi3, na ndio maana mimi sikupenda sana mada kama ya Mkwawa na wengine ziingie humu kwani bado kuna viporo vingi havijajibiwa kwenye histohisia ya Mzee Mohamed ya 1950's

Nadhani Kaka Mohamedi hakulitendea haki kundi kubwa "lililosahahuliwa" kama kweli alikuwa na nia ya kulitetea kundi hilo kwa mujibu wa mabandiko yake,
Pilika za kugombea uhuru kwa upande wa Mzizima hazikuwa za Waislamu wala za Wazulu na Wamamnyema pekeyao, Waislamu, Wakristo, Wapagani na Waabudu Mizimu walishiriki kama Watanganyika bila kuangalia itikadi ya Imani zao wala makabila yao, tofauti na Mzee Mohamed anavyotaka kutuweka kwenye itikadi ya Kiimani na Kikabila

Baada ya Nyerere kusomewa Dua na Waislam pale kwa Tambaza, Kundi lingine lisilokuwa la Kiislamu lilimuita Nyerere na Kumfanyia Tambiko ambalo halikuwa la Kiislam(Hotuba ya Nyerere ya Kuaga 1985), Tambiko lilifanywa mbele ya hao Waislam (Tambaza at el) na wala (Waislam) hawakupinga kufanyika tambiko lililo kinyume na Uislam, kwa wale Waislam waliona kila iman inaplay part yake kwenye pilikpilka za kutafuta uhuru,

kwa Mohamedi kitendo cha kusomewa Dua ya Kiislamu ndio kinapewa kipaumbele lakini hilo la tambiko halimuhusu kwa sababu waliofanya hilo tambiko si wazee wake, yeye wazee wake ni wale Waislam wa Kizulu na Kimanyema. na hapo ndio unaweza kuona Mzee Mohamed ana Nia na Malengo gani kwenye hii Histohisia aliyoiandika na anayosimamia

Kituko,

Alichofanya Mohamed Said ni kuandika.

"Historia iliyofichwa Kuhusu Harakati za Waislam Dhidi ya Ukoloni wa Waingereza katika Tanganyika."

Pitia vizuri hiyo hotuba ya Nyerere anakuambia mwenyewe baada ya kumsomea dua wanamfanyia matambiko hao hao Wazee wa Dar es Salaam.

Matambiko ni mila za makabila wala siyo kitu kigeni.
 
Last edited by a moderator:
Asante sana Kaka Nguruvi3, na ndio maana mimi sikupenda sana mada kama ya Mkwawa na wengine ziingie humu kwani bado kuna viporo vingi havijajibiwa kwenye histohisia ya Mzee Mohamed ya 1950's

Nadhani Kaka Mohamedi hakulitendea haki kundi kubwa "lililosahahuliwa" kama kweli alikuwa na nia ya kulitetea kundi hilo kwa mujibu wa mabandiko yake,
Pilika za kugombea uhuru kwa upande wa Mzizima hazikuwa za Waislamu wala za Wazulu na Wamamnyema pekeyao, Waislamu, Wakristo, Wapagani na Waabudu Mizimu walishiriki kama Watanganyika bila kuangalia itikadi ya Imani zao wala makabila yao, tofauti na Mzee Mohamed anavyotaka kutuweka kwenye itikadi ya Kiimani na Kikabila

Baada ya Nyerere kusomewa Dua na Waislam pale kwa Tambaza, Kundi lingine lisilokuwa la Kiislamu lilimuita Nyerere na Kumfanyia Tambiko ambalo halikuwa la Kiislam(Hotuba ya Nyerere ya Kuaga 1985), Tambiko lilifanywa mbele ya hao Waislam (Tambaza at el) na wala (Waislam) hawakupinga kufanyika tambiko lililo kinyume na Uislam, kwa wale Waislam waliona kila iman inaplay part yake kwenye pilikpilka za kutafuta uhuru,

kwa Mohamedi kitendo cha kusomewa Dua ya Kiislamu ndio kinapewa kipaumbele lakini hilo la tambiko halimuhusu kwa sababu waliofanya hilo tambiko si wazee wake, yeye wazee wake ni wale Waislam wa Kizulu na Kimanyema. na hapo ndio unaweza kuona Mzee Mohamed ana Nia na Malengo gani kwenye hii Histohisia aliyoiandika na anayosimamia

Wewe kinakushinda nini kuandika hayo ya waze wako wa kipagani aliyoyawacha Mohamed Said? mbona hukuuliza kwanini kitabu cha kivukoni kiliwaacha wote? mwenzako aliona wazee wake wapigania Uhuru hawakutajwa na kitabu cha kivukoni akaanza kuandika chake, wewe jee? hebu tueleze mzee wako yupi wakipagani alimweka nyerere nyumbani kwake? mzee wako yupi wa kipagani alimpelekea resheni nyerere nyumbani kwake? mzee wako yupi wa kipagani alikuwa akimpa lifti nyerere kumpeleka pugu? mzee wako yupi wa kipagani alikwenda kuchukuwa michango tanga ya kuchangia safari ya nyerere? mzee wako yupi wa kipagani alikuwa kwenye AA, TAA, TANU ambae kivukoni walimtaja na Mohamed Said hakumtaja?

Au hilo kundi la wazee wako walikuwa wakitambika tu?
 
Kuwarudisha maanayake ni kuuwaunganisha na waliopo si kuwatenga tena!

Alichokifanya Mohamed Said hakina tofauti na anachokilalamikia!

Ulichokifanya wewe ni kipi? vipi kuhusu Abushiri? maana zile za uso za knockout za Mkwawa nimeziona nikawa nashangilia, nangoja.
 
Lingekuwa jambo jema sana kama tutafanya hivyo,

Nitaajitahidi kuiweka vema na kila msomaji aone kwa macho yake ya nyama!
Hii ndiyo nafasi yako humu jamvini...ukitumwa u-fail hiki au kile ...usjiingize katika usiyoyajua!

*Wewe ni mtoto wa ngapi kwa julius nyerere?..hawa TBC hawa! wana "urasimu" kwelikweli.
 
Inaaminika na Mwalimu Nyerere amelithibitisha katika hotuba yake kuwa nyakati zingine walikwenda kutambika,

Swali la kujiuliza kwa wadau wote ni, Je walitambika Kikristu, Kiislamu ama kipagani/kijadi?

Tukipata jibu sasa tujenge hoja kwa dhana ya hoja ya udini ya Mohamed Said na waambata wao!

Soma hotuba ya Nyerere hapo juu anakuambia Wazee wamemchukuwa wamemfanyia dua hao hao wazee wakamfanyia matambiko ya jadi. Kama unapingana na maneno ya mzee wako basi wewe ni NUNDA...Mzee wako anakiri Wazee wa Dar es Salaam kwanza wengine baadaye wewe bado utaki tu.
 
Umechoka kulizungumzia hili jambo ambalo wewe umelipotosha?

Mpaka sasa hujaonesha wapi limepotoshwa, hebu tupe nukuu japo ya sentensi moja tu ili uwe katika ukweli? ukishindwa ina maana wewe ndio umejaribu kupotosha lakini umeshindwa, ukakimbilia Iringa nako zikakunyeeshea, haafu leo una ubavu kweli hata wa kuandika? haya tunangoja.
 
Sasa naamini wazi kuwa historia huijui ndugu yangu, umebobea kidini zaidi!

Nakupa swali kisha jibu lake ndio ufunguo wako!

Mjerumani na Muarabu nani alitangulia kufika Tanganyika?

Naomba nikuulize, Wa"iraq"w unawajuwa? kama huwajui muulize Slaa katibu Mkuu wa chadema atakueleza ni watu gani hao. Ukipata jibu njoo utuhadithie.

Iraqw man
 
Back
Top Bottom