Mag3 katika bandiko lako 2868 nayaangalia yafutayo na yatokanayo na kitabu, majibu na hoja za Mohamed Said.
1. Alichokiandika Mohamed ni kitu alichokuwa na majibu yake na utafiti ulilenga katika kukamilisha kile alichofikiri na si kile alichotafiti.
a) Ameonyesha bias ya uandishi kwa kuelekeza watu kuamini kile alichokusudia na si kile alichokitafiti
b) Aliandika katika mtazamo wa kushambulia ''attack'' kundi fulani la jamii na watu fulani si kutokana na hukumu ya historia bali kile alichodhani kuwa ima yeye au wazazi au ndugu zake hawakutendewa wema au walionewa.
c) Ameshindwa kuthibitisha maandiko yake kwa hoja za kitafiti,kukwepa maswali au hoja zinazoonekana kukinzana na a, b hapo juu.
Hoja: Endapo Mohamed alifanya utafiti asingeweza kuzama katika historia ya uhuru wa Tanganyika kwa kuzama katika TANU na kukwepa historia iliyoanzia karne nyingi. Mathalani, Mohamed hakueleza undani wa AA au TAA kwa kutambua kuwa hilo litaharibu historia nzima anayoidai, wala kulezea harakati nyingine nje ya Dar, mfano Mbiru na Wapare, vyama vya wafanyakazi n.k.
Mfano, angeandika kwa undani kuhusu AA na TAA ni dhahiri asingekuwa na hoja ya Nyerere kufundishwa siasa mwaka 1952 ili hali twajua kuwa alianza siasa miaka 6 kabla ya hapo tena katika uwakilishi wa jimbo kama Tabora.
Hilo peke yake lingetosha kupunguza nguvu za ziada anazompatia Abdul Sykes.
Ni kwasbabu ya kuonyesha bias, Mohamed amejikuta anaficha ukweli wa historia ya kweli.
Kwa vile lengo ni kushambulia kundi fulani, bwana Said ameacha makusudi mchango wa shirika la Maryknoll huku akiufahamu vema.
Kibaya zaidi ameenda mbali na kuudharau kwa kusema ni 'ticket' moja. Wakati akiudharau mchango huo Mohamed ameutukuza sana mchango wa ticket moja uliofanywa na wazee wake. Hapa ukweli upo wapi katika double standard kama hii.
Ili kukamilisha lengo alilokusudia,Mohamed amewaandika washiriki wa uhuru wasio katika kundi lake kwa dhalili ya hali ya juu. Amewataja kwa imani zao kama viambatanisho vya majina yao na kuacha mchango wao katika mapambano.
Katika hilo la bias, Mohamed ameandika kurusa za kutosha kuhusu Mwapachu kuliko alivyomwandika Mtamila aliyekuwepo kabla ya Mwapachu. Mo amemuelezea Mshume Kiyate kiasi kwamba Rais wa TAA Dr Vedastus Kyaruzi mchango wake hauonekani.
Kila mmoja alikuwa na mchango na si sahihi kuufanya mchango fulani bora kuliko mwingine hasa kwa kuangalia majina na viambatanisho vya imani zao. Hilo linaondoa hata hoja dhaifu iliyokuwepo.
Mohamed ameshindwa kuthibitisha madai yaliyomo ndani ya kitabu chake. Hata pale alipojaribu, MO alikwenda nje ya taratibu za utafiti na kanuni za asili za ''kisheria'' natural justice.
Mathalani, amelituhumu Kanisa kuhusika na mambo mengi maovu na mengi yaliyozuia harakati.
Ameshindwa kuthibitisha ushiriki wa kanisa, kinyume chake kunukuu habari za mtu mwingine ambaye kimsingi angekuwa chanzo cha utafiti wa ushahidi na si yeye kuwa ushahidi(sivalon).
Kwa vile uandishi wake ni katika misingi ya ''attack'' na siyo academic, Mohamed ameshindwa kutetea hoja zake kimantiki.
Mfano, hajaeleza kwanini ilipangwa njama ya kuondoa Nyerere katika uongozi wa TANU mara mbili wakati huo akiwa hana uongozi wa nchi au vyombo vya dola na akiwa chini ya baraza la wazee wa TANU waliokuwa wazee wake.
Moh ameshindwa kutetea hoja ni kwanini ukristo wake ulionekana kikwazo hata kabla ya kuingia madarakani na kwanini majaribio hayo yalipangwa. Pengine hapa alitaka kuficha hisia za udini ambazo ni sehemu ya malalamiko yake ya leo.
Mo ameshindwa kututhibitishia mkakati wa Nyerere kuumaliza Uislam na kuingiza ukristo ulianza lini na kwa mbinu gani.
Kinyume chake ametumia kifo cha EAMWS kumtupia lawama kama sehemu ya ukristo na kanisa.
Ameshindwa kututhibitishia ushiriki wa kanisa kwa ushahidi hivyo kubaki kuamini ndivyo ilikuwa.
Lakini pia ameshindwa kutetea hoja za EAMWS kwanini ilikufa huko kwingine na ni nani alihusika kuiua.
Kwa vile hoja yake haisimami yenyewe, Mo amewashirikisha baadhi ya waislam kama sehemu ya njama.
Iwe iwavyo mtu aliyekuwa na mtazamo tofauti na malengo ya MO huyo alikuwa kibaraka. Alikuwa kibaraka kama Amir Kweyamba aliyekuwa kachero wa serikali, lakini wale waliokula njama dhidi ya serikali walibaki kuwa waislam safi.
Mo ameupotosha umma mara nyingi katika hali ya kujenga hoja na pengine kuficha ukweli.
mfano, si kweli kuwa Nyerere alikuja Dar mwaka 1952, si kweli kuwa alionana kwa mara ya kwanza na Sykes mwaka 1952, si kweli kuwa viongozi wa TAA hawakumjua, si kweli kuwa alianza siasa mwaka 1952, si kweli aliandikiwa hotuba bila kujua alikwenda UNO kusema nini akiwa msomi mkubwa ndani ya TANU.
Ni katika upotoshaji huo, Mohamed ameacha kwa maksudi mchango uliotolewa na wazawa wengine wasio na imani kama yake. Amejikuta akikweza watu kwa majina ili kuficha majina yasiyompendeza.
Mfano, tunauthamini mchango wa Yusuf Ngozi lakini je, Yusuf alikuwa katika nafasi aliyokuwa nayo Dr Vedastus Kyaruz, Clement Mtamila, Stephen Mhando, Cecil Matola, Dunstan Omar na wengine ?
Mifano na hoja ni nyingi sana lakini kwa ufupi nimalizie kwa kusema, alichoandika Mohamed ni kutumia majina, nyakati na matukio ili kupata nafasi ya kushambulia sehemu ya jamii yetu kwa kudhalilisha na kudharau michango yao.
Hili limefanyika kwa kutumia majina kama Nyerere au kwa shambulizi la dini.
Amefanya hivyo kwa kuhadaa kuhusu utafiti kwasababu alijua kile alichokusudia kabla ya kuanza utafiti.
Mohamed amefanya hivyo ili kujenga uhalali wa kundi fulani juu ya umiliki wa nchi na kupitia hilo apenyeze madai yake ambayo mengi hayana uthibitisho kama kilivyo kitabu chake.
Sehemu kubwa ya maandiko yake yanatokana na ''third party'' na wengi aliowahoji ima walikuwa na duku duku au walieleza ukweli ambao Mo hapendi uwekwe hadharani. Ameshindwa kutuwekea shajara alizosoma na akitaka tuamini kile kilichomo ndani ya shajara. Kanuni za uandishi hasa wa kitafiti hazikubaliani na hilo.
Ili kuhakikisha kuwa jamii aliyokusudia kuieleza ina amini na haipati nafasi za kuhoji hoja zake, Mohamed ametumia sehemu kubwa ya utafiti wake na maandishi kujenga chuki, kuleta farki na uhasama.
Ametumia dhana kuhusu kile marehemu walichokifikiri hata kama hakuwahi kuwahoji na ameshindwa kuwahoji walio hai ili kupata upande wa pili.
Mo anafahamu kuwa sehemu rahisi sana ya kufikia malengo yake ni kutumia dini. Hili analifanya kwa njia ya ''sisi dhidi yao''
Ushahidi kuwa ameshindwa kutetea hoja zake,amepotosha, ameficha baadhi ya ukweli na ameshindwa kujibu hoja au maswali na pale alipojaribu alifanya hivyo kwa udhaifu, unatueleza kilichomo ndani ya mistari aliyoandika.
Na hapa ndipo taifa linapopaswa kutupia jicho.