Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

Kama Ritz kaja kusema ovyo kuhusu Madrasa upo sahihi. La kama si hivyo msome Confucius. Anasema "A fool despises good counsel, but a wise man takes it to heart."

kichwakigumu,

Tujikite kwenye munakasha tuyaache hayo mie binafsi Madrasa ni sehemu muhimu kwangu.
 
Last edited by a moderator:


ndugu mchambuzi heshima mbele,,
naomba clarifications hapa,,

"mkutano mkuu wa TAA 1954 uliozaa TANU as a political movement na sio chama cha kisiasa"

sio contradictions??
 
Mchambuzi,

Na maswali mawili kwako.

1) Unaweza kututajia hao viongozi 16 wa TAA majina yao ili tupate kujifunza.

2) Unaweza kututajia wanachama 20 wa TANU wa mwanzo.

Nadhani kuja kwako kwenye huu munakasa utaongeza tija kwa wasomaji.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu, umemwambia mambo ya msingi, lakini mtu mwenyewe yupo hapa kutetea uislam wa mzee Mohamed Saidi na heshima ya wala rushwa wa CCM kwa vile tu mwenyekiti ni muislam!hivyo hata kuelewa.
 

Mchambuzi,

Umeanza vizuri lakini ulivyoingiza kujisifia na kumwambia zomba, hajui chochete hawezi kupambana na wewe umekosea...unadhani zomba, atakaa kimya subiri majibu yake.
 
Last edited by a moderator:
ndugu mchambuzi heshima mbele,,
naomba clarilifications hapa,,

"mkutano mkuu wa taa 1954 uliozaa tanu as a political movement na sio chama cha kisiasa"

sio contradictions??

Kilichotokea 1954 kwenye TAA general conference was renaming TAA to TANU; TANU ikawa na mtazamo wa kisiasa zaidi tofauti na TAA ambayo haikuwa na orientation kubwa ya kisiasa; The Registrar of General of Societies (leo hii anaitwa msajili wa vyama vya siasa), hakukipatia TANU usajili kama chama cha Siasa 1954, suala hilo lilifuata baada baada ya mapambano makubwa baina ya TANU na serikali ya mkoloni;

Kwa kifupi, as soon as mkoloni alipojua kwamba TANU inaundwa to replace TAA, legislation governing the operation of societies was amended to create stumbling blocks for TANU;

Kwahiyo 1954 TANU ilizaliwa kama organization yenye mtazamo wa kisiasa katika muktadha wa kudai uhuru wa watanganyika, lakini hakikuwa chama cha siasa kwa mujibu wa sheria, hivyo kiliendelea kuwa a political movement kwa muda;
 
mkuu, umemwambia mambo ya msingi, lakini mtu mwenyewe yupo hapa kutetea uislam wa mzee mohamed saidi na heshima ya wala rushwa wa ccm kwa vile tu mwenyekiti ni muislam!hivyo hata kuelewa.

hebu toka basi uwaachie watu wenye akili zao wachambue mambo hapa..!
Kwani ni lazima uchangie??
Hapa watu timamu wanazungumza yenye utimam wewe unakuja kutafuta umaarufu??
Toa madudu yako hapa..
 


thanks..
Tuendelee..
 
Mkuu, umemwambia mambo ya msingi, lakini mtu mwenyewe yupo hapa kutetea uislam wa mzee Mohamed Saidi na heshima ya wala rushwa wa CCM kwa vile tu mwenyekiti ni muislam!hivyo hata kuelewa.

Asante kwa kunijulisha hilo Gwalihenzi; Sina muda wa kujadiliana na watu wanaorudisha taifa letu nyuma kimtazamo;
 
Ritz,
swali lako kuhusu majina ya waasisi wa TANU na pia wanachama 20 wa kwanza wa TANU per post number 2971, majibu yangu ni kama ifuatavyo:


  1. J.K Nyerere – territorial president
  2. Germano Pacha – kanda ya magharibi
  3. Kirilo Japhet – Kanda ya Kaskazini
  4. Joseph Kimalando – Kanda ya Kaskazini
  5. C. Milinga – Kanda ya mashariki
  6. A . Iranga – Kanda ya Ziwa
  7. L. Bagohe – Kanda ya Ziwa
  8. S. Kandoro – Kanda ya Ziwa
  9. Kisungutwa Gabara – Kanda ya Ziwa
  10. S. Kitwana – Kanda ya Ziwa
  11. Tewa Said Tewa – Kanda ya Mashariki
  12. D. Azizi – Kanda ya Mashariki
  13. A. W Sykes – Kanda ya Mashariki
  14. A. K. Sykes – Kanda ya mashariki
  15. G Kunambi – Kanda ya Mashariki
  16. J Kasessa – Kanda ya Mashariki
  17. John Rupia – Kanda ya Mashariki.

Hawa ndio walikuwa ni waasisi wa TANU kwa mujibu wa historia ya taifa letu, wajumbe wa mkutano mkuu wa TAA 1954 uliozaa TANU, na wanachama kumi na saba wa kwanza wa TANU; Wengine waliofuatia katika kundi hili ni pamoja na Paul Bomani na wengine ambao wengi wao waliunda baraza la kwanza la mawaziri la serikali ya TANU;

Wanachama wengine wengi walifuatia baadae lakini wa mwanzo walitokea Dar-es-salaam, Tabora, Tarime, Singida na Mara Kaskazini. Sina majina yao.
 
Mnakasha unaendelea vizuri sana tunazidi kufyonza historia ya nchi yetu Tanganyika.Wanajamvi wafuatao THE BIG SHOW zomba KichwaNgumu tafadhali sana kwa faida yetu wote nawaomba mpunguze mbwembwe na lugha yenye ukakasisi.Si lazima kuchangia kila kitu mambo mengine ni vyema ukakaa kimya na kuwapa nafasi wajuzi watuze bila choyo.

Mzee wangu Mohamed Said yapo maswali mengi nilitegemea ungeyajibu lakini mpaka sasa pg #149 unayakimbia na kibaya zaidi unategemea msaada wa mashabiki wako ambao kwa kiasi kikubwa wameshindwa kukusaidia,baya zaidi wanayumbisha mjadala sijui kwa maslahi ya nani !.
 
Last edited by a moderator:
Ndugu yangu Mchambuzi umeongea jambo muhimu sana ambalo niliwaeleza hawa ndugu zangu,

Niliwasihi tunapojadili masuala haya kwanza tuangalie FILOSOFIA ya AA, TAA na TANU

Kwakuanza tu unabaini kuwa AA na TAA havikuwa vyama vya siasa, hivyo filosofia yavyo haikuwa kwa ukombozi wa Tanganyika,

Kisha tukiangaza TAWA tunaona wazi kuwa kilikuwa na MALENGO chanya kwa Tanganyika ndiomaana hata baada ya kufutwa kiongozi wake mkuu Mwalimu Nyerere alihamishia filosofia yake TAA na ndipo mageuzi huru ya TAA yakawepo na kwenda kwenye mlengo wa ukombozi zaidi hadi kuzaliwa TANU!

Mohamed Said na wafuasi wake leo naamini toka moyoni kuwa hajui kwanini ilizaliwa TANU ilihali TAA ilikuwepo,

Kimsingi ukiwahoji watatumia dhana na filosofia za uwepo wa AA na kuzaliwa kwa TAA jambo ambalo ni kinyume!
 

Historia ya nchi yangu ilinifundisha kuwa Waarabu wanakuja kuchukuwa watumwa hapa, lakini leo naona kuwa Mohamed Said ameandika kuna meli ilikuwa ikipeleka watumwa huko Atlantic inaitwa "Jesus", hilo wewe ulifundishwa shuleni kwenu?

Wewe historia unayoijuwa ilikufundisha kuwa TANU ilibuniwa Burma? ilikufundisha kuwa mweka hazina wa kwanza wa TANU ndio huyohuyo alikuwa mweka hazina wa Jammiat'ul Islamiya?

Unaweza kuwa sawa unaposema historia ya nchi yangu siijui kwani ilifichwa na wale walio na fikra kama zako waliokutangulia, lakini nnakuhakikishia kuwa nipo katika kujifunza kila kukicha, tena nimepata Maalim mzuri sana Mohamed Said, ambae darsa lake naona hata wewe limekuvutia ukaja na yako ya kivukoni.

Pia nnakuhakikishia nnaijuwa ni nini maana ya "political movement" na nnaijuwa ni nini maana ya "chama cha siasa" vitu ambavyo wewe vimekushinda kuvielezea kwa lugha moja. Kung'ang'ania kuyaongelea hayo mawili kwa lugha tofauti kunaonesha ni jinsi usivyojuwa unachotaka kukisema, kipi cha ajabu hapo hata moja liwe kwa Kiswahili "chama cha siasa" na lingine liwe kwa Kiingereza "political movement"? hakuna ila ni upeo wako tu ulipoishia.

Hivi wewe unaweza unajiona kuwa unaweza haswa kujadiliana na kujitapa kuwa wewe ni una "kiwango" wakati hata kunyoosha sentesi kwa lugha moja huwezi? umenisahau? labda kweli kiwango chako ni cha chini sana mpaka unaona hutoweza kujadiliana na mimi.

Nakurudisha tena ukajaribu kuziondoa "contradictions" ulizojifunga nazo, kama kiwango chako kinakuruhusu kuziona, nna mashaka kama unaziona.

Hujaleta jipya katika maandiko yako zaidi ya kujichanganya, unataka kurudisha ya kivukoni? hapa utatulizana, usiwe na shaka.
 

Upo sahihi; Mwanzoni, walichokuwa wanadai watanganyika kupitia hizo taasisi ilikuwa sio kumwondoa mkoloni bali kutaka ashirikishe watu weusi, hasa katika suala zima la kuondoa social exclusion katika masuala kama elimu, na pia fairness katika kodi, na fursa nyingine mbalimbali;
 
Orodha hii ndio iliyoanza kuwasahau wazee wa Mohamed Said. Hataki HISTORIA ya TANU ianzie hapo.
 
Last edited by a moderator:
Tunaendelea vizuri Mkuu Mchambuzi katoa orodha ya wanachama 17.Nimepitia yote naona kanda ya mashariki ina wajumbe nane kati ya wajumbe kumi na saba labda wachambuzi wa historia wangetujuza kanda ya mashariki ilikuwa inajumuisha eneo lipi.Idadi ya wazee wa Mohamed Said ni watatu kati ya wajumbe kumi na saba.

 
Last edited by a moderator:

Jadili contradictions zangu kwa hoja kwa jinsi ulivyo highlight kwenye bandiko husika hoja moja baada ya nyingine - huku ukitoa mawazo yako mbadala, sijaona bado, sana sana unajichanganya tu;
 

Ni kweli, na binafsi sielewi kwanini ilitokea hivyo; Lakini kwa wale wenye upeo mdogo kama zomba, wanaweza kudai kwamba haya yalikuwa ni makosa ya Nyerere wakati TAA ilikuwa ni chombo ambacho Nyerere hakuwa na mahusiano nacho kabla ya 1954;
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…