Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar


Wild Card,

Wapi nimekiri makosa na upungufu wa kitabu changu?
Huu ndiyo ujanja wenu wa kumaliza mnakasha?

Haifai kabisa kutiliana maneno kinywani.
Ikiwa mnataka tumalize mnakasha na tumalize kiungwana.

Wala mimi sitakuulizeni kuhusu suala la ''uchochezi wangu.''
Nimekuwa hapa jamvini siku zote.

Wasikilizaji watatuhukumu.
 
Naomba nikuulize swali Mohamed Said, mnakasha huu umekuonyesha mapungufu ya kitabu chako au haujakusaidia kwa lolote?

Yericko,

Haujanionyesha upungu wowote katika kitabu changu.
Kunisaidia mnakasha umenisaidia sana tena sana.

Nimeelewa kwa nini hata Nyerere hakupenda historia
ya wazee wangu ijulikane.

Lakini kubwa limenidhihirishia lile nililokuwa nimefunzwa...
1 ni sawasawa na 20...

 
Kitabu chochote au kazi yeyote ya maandishi isipokuwa vitabu vya Mungu lazima viwe na mapungufu kwani mwanadamu sio mkamilifu.

Ustaadh wangu Mohamed umeweza kufikisha ujumbe na kwahakika ukiona watu wanakosoa ujuwe ujumbe umefika. Mungu akupe afya nzuri ili uendelee kufikisha mazuri uliyonayo kwetu. Mi nilipata kuhudhuria mada yako moja kule marekani mwaka juzi kwa kweli uliweza kuweka mambo mazuri sana. Mwenyezi Mungu akupe afya njema daima.
 

Ahsante sana ndugu yangu,
Hakika kazi yoyote ya binadamu ina makosa.

Amin Amin Amin.
 



ndugu moh said.,awali ya yote sisi tukushukuru sana kwa darsa hili,,
wengi tumenufaika,na wengi sana tulikuwa gizani,

ila naomba nikukumbushe kidogo kuhusu uwanja wa masumbwi mkuu wangu,

kama wewe ni kiongozi wa bench la ufundi wa bondia wako anaepigana ndoti na mpinzani machachari mithili ya muhamadi ally,na wewe pamoja na benchi lako ukaona wazi wazi ya kwamba bondia wako kachoka na haliwez tena pambano,unachofanya wewe na benchi lako la ufundi ni kurusha taulo kati kati ya uringo na mpambano huisha papo hapo,hiyo husaidia kumwokoa na kusave maisha yake..

Wanachokifanya ndugu hao ni kurusha taulo kati kati ya uringo ili wamwokoe ndugu yao yericko anaetapa tapa kwa hoja.
Hongera sana ndugu yetu moh said,mungu akubariki sana.
 
Daaah hakika huu mjadala ni mtamu sana! Pia nadiriki kusema ningependa mijadala yote hiwe namna hii!
 

Mohamed Said,

Hii inanikumbusha kisa cha Moshe Dayan na Yasser Arafat walipokuwa wanakutana Camp David kutafuta amani mashariki ya kati.

Moshe Dayan akifika Israel anaanza kupora ardhi ya Palestine akihojiwa anasema wameongea Camp David.

Sasa sijui Mohamed Said amekiri wapi na WildCard, sijui kayatoa wapi haya maneno.
 
Last edited by a moderator:

Nimefurahi kusikia kuwa umenufaika na mnakasha huu,

Lakini natilia shaka umakini wako katika kitabu chako ikiwa hakuna ulipobaini mapungufu kwenye kitabu chako kutokana na mnakasha huu!

Kwamjadala tuliouendesha hapa naamini hata kama kitabu chako ingekuwa kakiandika Bob Bequn bado angekubaliana nami kuwa amegundua mapungufu na katika matoleo yake yajayo angekihuisha!
 

Yaani hao ndio walikuja kueneza fitna eti Nyerere aliwatupa kwenye serikali yake. Ni nafasi gani angewapa yarabi! Walitaka uwaziri mkuu? Au u-Gavana wa BoT? Au ujaji? Ha ha ha ha! Lakini Mwalimu alikuwa muungwana sana; hakuna ambaye hakupata kanafasi fulani kuthamini mchango wake. Kama sio serikalini basi angalau kwenye Chama hata kaujumbe ka NEC angalau. Kule ng'ambo wenzao walikuwa wanapotea katika mazingira yasiyoeleweka.
 

Mnakasha huu tupo post 156 mpaka saizi kuna watu zaidi ya 30,000 wanaufutilia nakushauri ungeanza post ya kwanza kuusoma ungejifunza mengi sana.
 

Ritz,
Wakati Yasser Arafat anakutana na Yitzhak Rabin Camp David, Moshe Dayan alishafariki kitambo.
 

Kimsingi watanzania wengi bado wanamambo yaliyowekewa viulizo,

Wanahitaji kuyajua na sio kulabdia ama kupishanisha:

Mathalani:

Je Tanzania ina mfumo kristu?

Je nani maasisi wa TANU?

Je ni kweli wapo wanaukombozi waliofutwa katika historia kama anavyodai Mohamed Said?

Ni historia ya nyaraka zipi au kitabu gani anayodai ndugu Ndugu Mohamed Said kuwa imeacha wazazi wake?


Je ni ile ya kitabu kilichoandikwa na chuo cha kivuko tu ndio iliyomsukuma kuandika kitabu chake?
 
Last edited by a moderator:

Yericko,

Mnakasha unaendelea?

Kama unaendelea nikuulize imekuwaje
clip ya hotuba ya Baba wa Taifa?

Inakuja tusubiri?

 
Yericko,

Mnakasha unaendelea?

Kama unaendelea nikuulize imekuwaje
clip ya hotuba ya Baba wa Taifa?

Inakuja tusubiri?

Mkuu kunamambo muhimu mimi na wewe hatujawekana sawa naimani hata wasomaji wetu bado wanahitaji kujua hayo hapo juu.

Hotu sijaenda kuifata tena hii ni kutokana na majukumu yaliyonisonga kwa wiki hii lakini nitajitahidi.

Hilo lisiwe kikwazo kwakuwajuza waswahili wenzetu juu ya hayo ya uhuru wa tanganyika
 
Mchambuzi,

..Lakini inasemekana Mwalimu alipendekeza uhuru upatikane miaka ya 70.

..wananchi walipopata habari hizo walichukizwa sana na kumshinikiza kwamba hawataki uhuru ucheleweshwe.

..Gavana alikuwa anawaogopa TANU kwasababu walikuwa ni radicals, na walikuwa hawafanyi juhudi zozote zile kuandikisha wanachama wa kiasia, au kizungu.

..hicho ndicho kikasababisha gavana, Chifu Marealle, na ma-settler, kuanzisha chama cha UTP ambacho kiliruhusu wanachama wa rangi zote.

..TANU ilikuwa inawatishia machifu kwasababu ilikuwa ndiyo kimbilio la watu wengi waliokosa nafasi za uongozi ktk mfumo uliopo. kwa mfano waliokosa kuchaguliwa kutumikia ktk mabaraza ya machifu walikuwa wakikimbilia kujiunga na TANU. Kwa msingi huo, gavana na machifu, hawakuwa wamekosea kwamba TANU ilikuwa tishio kwa machifu. the fact kwamba Mwalimu alikuja ku-abolish Uchifu ni uthibitisho wa madai ya gavana.
 
Last edited by a moderator:

Asante kwa elimu juu ya hilo, nachofahamu ni kwamba Mwalimu had options kadhaa juu ya lini hasa uhuru wa nchi upatikane lakini sikuwa na ufahamu wa kina kulingana na maelezo yako hapo juu;
 
KUna mambo ambayo ni factual:

TANU imeanzishwa mwaka 1954 - period. hatuzungumzii mtu alikuja na wazo lini.. mtu akiwa na wazo la kuoa binti fulani na mwaka fulani hatuanzi kuhesabu ndoa siku alipopata wazo na hata jina la mwenza wake. Ndoa huanza inapofungwa. Wanaotaka kusema TANU ilianzia Burma ni kuchezea maneno tu.

TANU ilipoanza kiongozi wake alikuwa Mwalimu Nyerere - wapo wanaotaka awe Sykes au mtu mwingine yeyote. Haliwezekani historia imeshaandikwa. Kusema kuwa kiongozi wa kwanza wa TANU alikuwa Nyerere siyo dharau wala kejeli kwa wengine waliokuwepo it is just a fact. Kwa mfano, huwezi kumuondoa John Okello kwenye Mapinduzi ya Zanzibar hata kama humtaki.

Waasisi wa TANU siyo kila mtu aliyekuwa mwanachama wa kwanza wa TANU au aliyeunga mkono TANU toka mwanzo. Unapozungumzia waasisi unazungumzia watu wale waliokaa chini na kuanzisha TANU. Wale waliokubaliana kuua TAA na kuunda TANU ndio waasisi. Marekani kwa mfano unapozungumzia Foounding Fathers unazungumzia wale wajumbe wa mkutano uliotangaza Azimio la Uhuru 1776. Marekani inawataja wale waliotia sahihi Azimio la Uhuru na walioandika Katiba ya Marekani (Framers of the Constitution) kama kundi kuu la Waasisi wa Marekani. Lakini Saba kati yao ndio wanajulikana sana kama Founding Fathers - George Washington, John Adams, Alexander Hamilton, Benjamin Franklin, John Jay, Thomas Jeffferson, na James Madison.

Kwa Tanzania unaweza kabisa kuweka orodha ya watu ambao tunaweza kuwaita Waasisi wa TANU (siyo waasisi wa Tanganyika) - hili ni lile kundi la viongozi wa TAA kukaa chini na kuivunja ili kuunda TANU. Majina yao yamewekwa hapo.

Kutoka hapo kuna kundi la Wapigania Uhuru ambao kwa ujumla wao tunaweza kuwaita Waasisi wa Tanganyika - Sasa hawa siyo wote walikuwa wanachama wa TANU au kama walikuwa wanachama wameingia baadaye. Katika kundi hilo wamo wale wote ambao walishiriki katika harakati za Uhuru kwa kutoa mchango wa aina mbalimbali ikiwemo kushiriki katika nafasi mbalimbali za uongozi katika sehemu mbalimbali nchini. Hawa ndio unaweza kuwaita Mashujaa wa Uhuru.

Orodha hii ni tofauti na wale walioupinga Ukoloni - kabla ya Vita ya Majimaji kulikuwepo na juhudi za makabila mbalimblai kuupinga ukoloni sehemu mbalimbali nchini. Mashujaa wetu hawa ni wale wote waliopigana kumkataa Mjerumani na utawala wake sehemu zote na kwa namna zote ambapo anayejulikana kati yao zaidi ni Chief Mkwawa wa Wahehe na kina Nduna Songea wa Wangoni na wenzake walionyongwa pale Songea. Hawa wazee ndio waliotangulia wapigania uhuru ndio maana katika historia tuna kipindi kinaitwa "Anti-colonial movement " na Independence Struggle (harakati za uhuru).

Tatizo kubwa la maandishi ya Bw. Said kama nilivyoonesha katika ukosoaji wangu mara kwa mara ni kuwa amejaribu kupotosha historia akitumia lugha ya kuipotosha historia. Kwa mfano anaposema katika "kupigania uhuru tulipigana sisi" kwa makusudi anataka kuashiria (imply) kuwa ni wao peke yao walipigania uhuru - anajua akisema "na sisi tulipigania uhuru" atakuwa anazimua hoja yake.

Mimi matumaini yangu ni kuwa vijana wetu ambao wametusoma hapa katika mamia haya ya kurasa watakuwa wamejifunza siyo tu historia zaidi bali pia kufikiri kwa usahihi (critical thinking). Watakuwa wamejifunza kusikiliza hoja na kuzipima na hata kuzikataa bila kujali zinatolewa na nani au vipi. Ni matumaini yangu wale ambao walikuwa wanaamini tu kauli za Bw. Said sasa hivi wamejifunza kugungua mara moja anaposema vitu visivyo na msingi katika historia na pale ambapo anatupa simulizi zuri ambalo halina utata na pale ambapo anaweza hisia zake kwenye tukio na kulipa tafsiri kwa hisia zake siyo kwa historia ilivyo.

Nina uhakika mada hii imepunguza vya kutosha tu watu wanaoamini simulizi lake lisilo na msingi wa kanuni za historia.
 

Yericko,

Hili nalo vipi unasemaje?:



[TABLE="class: cms_table_MsoNormalTable"]
[TR]
[TD="colspan: 2"] On the formation of TANU, Iliffe has noted that: [/TD]
[TD][/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="colspan: 2"] ''...none of the published accounts, even those of politicians like S.A. Kandoro or E.B.M. Barongo, is particularly revealing. Available government records contain little of importance. President Nyerere has never analysed the process in public...The most difficult problem of all is to evaluate president Nyerere's own role in the process of transformation, specially the extent to which he was planning a mass movement or was led into it by provincial politicians already involved in mass action. [1][/TD]
[TD][/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="colspan: 2"]
Abdulwahid now 30 years old, had accomplished the ambition of his lifetime, an ambition which had originated from his late father, who 25 years before had predicted a continuous struggle between Africans of Tanganyika and the colonial state.

Kleist Sykes had foretold the role of the next generation. In a letter he wrote in 1933 to Mzee bin Sudi, then president of the African Association, Kleist at the tender age of 29 years had this to write:
[/TD]
[TD="width: 59"][/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="width: 59"][/TD]
[TD="width: 601, colspan: 2"][/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="width: 601, colspan: 2"] Kleist talked about ‘civilization,' which today would mean ‘self-determination', and about tribes which TANU transformed into a nation. In 1954, a quarter of a century later in the same building, 25 New Street, which he had helped to build through self-help, the new generation in Tanganyika was transforming the African Association which he had founded in 1929 into an open political party, the aim which was to prepare the people for independence. And among those leading the emerging mass movement were his three sons, Abdulwahid, Ally and Abbas. [/TD]
[TD="width: 59"][/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="width: 601, colspan: 2"] Ally Sykes designed the TANU membership card and chose the national colours and emblem.

The colours were black representing the African race and green for the land. The design of the card was similar to his Tanganyika Legion card. After finishing designing the card he approached the Tanganyika Standard Newspapers to have the card printed for him. Out of his own pocket he had the first 1000 cards printed and using TAGSA funds he printed another 2000 cards. Card No. 1 was issued by Ally Sykes to TANU Territorial President Julius Kambarage Nyerere and bears his signature.

It was proposed that the first few cards should be auctioned and the money collected should go to the Party treasury. Abdulwahid, Ally, Dossa Aziz, Rupia and others bid for the cards. Ally outbid his elder brother Abdulwahid and received TANU card No. 2; Abdulwahid was issued with card No. 3; Dossa Aziz card No. 4; Phombeah card No. 5; Dome Okochi, one of the Kenyan nationalists in TANU, got card No. 6 and Rupia card No. 7. Bibi Titi Mohamed got card No. 16; Idd Tosiri card No. 25.
[/TD]
[TD="width: 59"][/TD]
[/TR]
[TR]
[/TR]
[TR]
[TD="width: 601, colspan: 2"][/TD]
[TD="width: 59"][/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="width: 601, colspan: 2"][/TD]
[TD="width: 59"][/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="width: 59"][/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="width: 601, colspan: 2"][/TD]
[TD="width: 59"][/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="width: 601, colspan: 2"] Soon after the formation of TANU, the United Nations visiting mission came to Tanganyika in August, 1954. By then TANU was not yet registered by the government.

The Party received its registration on 30th of November, 1954 after it had overcome numerous frustrating formalities put forward to it by the government.

Bibi Zainab, Ally Sykes' wife remembers the day, a hot afternoon when Nyerere came to their house at Kipata Street (now Kleist Sykes Street) where Abdulwahid and Ally were waiting for him to give them information on the registration of the party. Nyerere looked tired and worried.

He sank in a sofa burying his face in his arms and was silent for a time. Abdulwahid and Ally were waiting for him to speak. Nyerere had bad news. The government had refused to register TANU.

Nyerere told them that the government had refused them registration on technicalities. In a dramatic show of organisation and tact, after learning that the government had turned down TANU's application on the grounds that TANU had not enough members, Abdulwahid asked Said Chamwenyewe to go to Rufiji, his home area, to register members for TANU. Rufiji is a predominantly Muslim area. TANU therefore had no problem in getting members. In fact the early members of the party were from Gerezani and Rufiji.

Iliffe has noted that:
[/TD]
[TD="width: 59"][/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="width: 601, colspan: 2"] ''The pattern of TANU's support in Dar es Salaam needs study, but financial returns for 1958 show the bulk of support in the old African quarters-Kariakoo, Ilala, Gerezani... by September, 1955 Dar es Salaam, with some 110,000 people, had taken some 25,000 of the 40,000 - 45,000 TANU membership cards issued throughout the country. It was the base from which TANU conquered Tanganyika.''[5][/TD]
[TD="width: 59"][/TD]
[/TR]
[/TABLE]



[1] Iliffe, 'The Role of African...' op. cit. p. 24.
[2] See Buruku, op. cit. p. 105.
[3] The present author has written a short article to clarify the
controversy. See New African (London) issues of March and May,
1985. The author's May article was in response to a March article
by Kasella Bantu.

[4] The TAA leadership did not draft a new constitution. The TANU
constitution was copied from Kwame Nkrumah's Convention Peoples'
Party (CPP), substituting TANU for CPP. Information from Tewa Said
Tewa.

[5] Iliffe, A Modern History... pp. 517-8.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…