zomba
JF-Expert Member
- Nov 27, 2007
- 17,240
- 3,930
Utafiti wa mohammed said haujawatendea haki wapigania uhuru wengine ambao hawakuwa waislamu lakini hawakunufaika chochote baada ya uhuru.
wapo ambao kupata uhuru tu ilikuwa ni mafanikio kwao na hawakuhitaji ziada.
wapo ambao kwa kiwango chao cha elimu wakati wa kuunda serikali mpya wasingeweza kumudu changamoto mpya.
badala ya kuangalia wapigania uhuru tuangalie ukweli kwamba baraza la kwanza la mwalimu lilikuwa na waislamu wasomi wa kutosha kulinda maslahi ya waislamu ndani ya serikali.
Unaonesha kuwa umefanya utafiti wa kutosha kurusha shutuma kwa Mohamed Said, kwanini wewe ungoje Mohamed Said na wewe usiwatendee haki kwa kuandika habari zao kama alivyofanya kwa wazee wake Mohamed Said baada ya kuona kuwa hawajatendewa haki kutokuelezewa na historia ya kivukoni.
Huoni kuwa itakuwa vyema na utatusaidia na sisi kutupa elimu kama alivyotupa elimu Mohamed Said.