Mohamed Said
Wewe na Harith Ghassany ni kama magazeti ya uhuru na mzalendo. Muelekeo mmoja tu. In fact ulimsaidia kumpa story zako za uongo alizoingiza kwenye kitabu chake. Wote mna chuki kwa Nyerere, ila yeye anamchukia zaidi kwa suala la muungano. Wewe unamchukia Nyerere kwa sababu babu yako aliwekwa ndani kwa u-radical wake. Ghassany ni mwarabu koko ambaye hakupenda utawala wa kisultani kupinduliwa, na anachukia waarabu kuhusishwa na biashara ya utumwa na yeye katika ujanja wake (kama wako) ametumia kuzifanya chuki zake ziwe pia chuki za waislam. Nyie wote wawili ni wajanja wajanja wa kutumia mambo ya ukweli mengi, na kupandikiza hisia zenu hasi ndani ya hayo mambo ili hisia hizo zionekane kama sehemu ya ukweli na wakati huo huo, lengo lenu la kuigawanya jamii likifanikiwa.
Kwa hiyo mtu hawezi kutafuta kitu cha kukupinga kutoka kwenye kitabu cha Ghassany, na hali kadhalika mtu hawezi kumpinga Harith Ghassany (kama gazeti la uhuru) kwa kutumia maandiko yako Moh Said (kama gazeti la mzalendo). Ni wale wale tu...
N,
Sawa sisi ni Uhuru na Mzalendo.
Kuna mtu alinambia kuwa nyie ni watu wa chama fulani.
Mimi si mtu wa kuambiwa neno nikaamini hapo hapo sasa dalili zinaanza kujitokeza.
Ala kumbe Uhuru na Mzalendo hawana maana.
Hivi wewe umejua lini hili?
Sasa fungua uzi mpya tujadili.
Ungelijua uungwana wa Harith na ukoo wake wa Waafrika pamoja na yeye mwenyewe
ungejuta kumtukana.
Nitakuonjesha kidogo.
Bibi yake Harith ni Mmanyema mweusi tiii Biti Tambwe na babu yake ni Muarabu wa Zanzibar
mwenye asili ya Kiomani.
Zanzibar walikuwapo wasichana wa Kiarabu lakini babu yake Harith alianguka kimapenzi na
msichana wa Kimanyema Mwafrika kama Waafrika wanavyokuja.
Posa zikenda na ndoa ikafungwa.
Ndiyo leo tuna huyu mjukuu Harith Ghassany.
Baba yake Mzee Ghassany alisoma Oxford pamoja na Mwinyibaraka.
Nikimjua Mzee Ghassany wala sikuuona huo Uarabu wake na kafanya kazi serikalini hadi alipostaafu.
Nikikutana na Harith huniimbia nyimbo za Kimanyema alizofunzwa na bibi yake.
Nyimbo hata mie sikupata bahati ya kuzijua.
Sasa mnapambana na kizazi hiki ambacho hakijaathiriwa na propaganda za Wamishonari na huku Bara
ngano zenu za Waarabu kutesa Waafrika.
Ndiyo hii Zanzibar ya leo inayodai uhuru wake.