zomba
JF-Expert Member
- Nov 27, 2007
- 17,240
- 3,930
Unataka tuendelee kwa matakwa yako?
Tuendelee kufuata ngano zako?
Nikusifu kwa moyo mmoja wa uandishi wa NGANO uliotukuka, kwakweli naamini Shigongo kwako haoni ndani!
Lakini kinyume chake ninakupuuza na kukulaani kwa kugeuza ngano zako za Gerezani kuwa historia ya Uhuru wa nchi hii takatifu!
Ninaamini nchi hii ngekuwa ya mfumo kristu kama unavyodai wewe, leo hii tungeshakusahau kwenye uso wa dunia!
Ungeshanyongwa siku nyingi sana hata matanga wangeshasahau nduguzo!
Lakini kwakuwa nchi hii ni tambarale iliyowekwa wima na kujengwa imara na Mtakatifu Julius Nyerere, wewe leo hii umesoma na unaendelea kulichonganisha taifa bila kufinywa wala kusonywa!
Wewe, ujinga huo ulikuwepo wakati wa dikteta Nyerere, sasa hakuna hiyo wala usijidanganye kutaka kujidai eti unamtisha mtu, hayo yalikwisha wakati alipong'atuliwa bila kupenda na kina Tiny.
Wanaochonganisha huwajui au unajidai tu? ni wale wanaosaini mikataba ya kuchota fedha serikalini na kuzipeleka makanisani.
Unafikiri tumesahau Nyerere alivyowadhulumu Masheikh na wazee wetu kwa kuwafunga, kuwafukuza na kuwapoteza pasi na hatia? Hilo hatutalisahau, sisi na vizazi vyetu, leo hii huna wa kumtisha kwa kauli zako finyu.
Umeshindwa kuonesha chochote kimoja katika maandiko ya Mohamed Said, watu wamekutupia ushahidi humu wa dhulma za nyerere na kanisa alilolitumikia, bado unajufanya huoni tu? sasa unaanza kuja na kauli za maudhi ili uwapandishe watu? tunakwambia sisi tunakupa za uso tu.
Haya ulisha kwenda kuzipata data kwa chifu Abdu Mkwawa? Jee umeshaupata upata mkanda wa hatuba ya nyerere? tumekupa offer ya kukulipia, hujaona? vipi kuhusu habari za Abushiri ulizojidai utazileta? yamekushinda?