Labda kuthibitisha chuki za muungwana bin Samtungo, ameulizwa swali na Mwankijiji kama walivyouliza wengine na hajaweza kulijibu. Swali ni kuwa wapi na kwa ushahidi gani wa Nyerere kuwatukana, kashifu Waislam hadharani au kwa siri.
Hakuna mahali popote ambapo Nyerere amekaririwa akiushaumbilia uislam na waislam ( labda kwa ''inasemekana'')
Hii maana yake ni kuwa dhana nzima ni ya kupanda na kuchomeka na haina mahali inaposimama yenyewe.
Mkuu wangu; swali hili liko at the core of the allegations za mzee wetu huyu. Hakuna kiongozi mwenye hisia za ubora wa dini, rangi, au nasaba yake ambaye hajawahi kuzisema hadharani na watu wakajua. Hitler alitukuza rangi yake -siyo sirini bali hadharani kabisa; Kina Milosevic walitukuza nasaba yao ya Kiserbia dhidi ya non-Serbs wa Serbia na Bosnia.. Idi Amin alitukuza Uafrika wake dhidi ya watu wengine wote hawa walifanya hadharani. Kaburu Botha na wabaguzi wa Deep South huko Marekani walitukuza rangi zao hadharani na haikuwa kificho.
Hakuna mtu yeyote kiongozi aliyeetukuza dini au rangi yake ambaye alifanya hivyo kwa kificho. Ahmedinajad na wenzie wote hawana siri. Hisia hii ya ubora haifikichiki kwa aliyonayo. Hata hapa unaweza kuona watu wanavyozungumza kwa ubora (superiority complex) inayotokana na dini.
Sasa, Nyerere kama kweli - NA TUMPE BENEFIT OF THE DOUBT Bw. Said...basi asingeweza kujificha kwa miaka zaidi ya 25 aliyokuwa akiongoza (miaka 31 tangu achukue uongozi wa TANU). Kungekuwepo angalau na barua, hotuba, mazungumzo ya sirini ambapo Nyerere ameusema vibaya Uislamu, au Waislamu.
Kama kuna mtu kasoma maandishi ya Bw. Said na mimi nimesoma maandishi yake mengi mno - HAKUNA MAHALI HATA PAMOJA - ambapo Bw. Said anamnukuu mzee wake YEYOTE (siyo Abdul, Rashad Ali, Dossa, Mshume Kiyate n.k) akisema amewahi kumsikia Nyerere akiutukana Uislamu, akiwakejeli Waislamu au akisema neno lolote baya kuhusu vyote viwili. HAKUNA.
Lakini jambo la pilli ambalo huwezi kuliona ni ushahidi wa aina yoyote wa agizo, amri, maelekezo yoyote ya Baba wa Taifa kwa mtu yeyote ambayo yalihusiana na kutowatendea haki Waislamu kwa misingi yoyote ile ya kidini.
Lakini la tatu ambalo kihistoria ni zito zaidi ni kuwa - HAKUNA jambo lolote ambalo Bw. Said anadai liliwatokea wazee wake wa Kiislamu ambalo halikuwatokea wazee wengine wasio Waislamu. Mfano mzuri ni uamuzi wa Nyerere kuvunja Baraza la Machifu ambao tunaweza kusema waliwakilisha watu wengi zaidi kuliko Waislamu na Wakristu. Watu wa jadi wangeweza (labda kwa haki) kudai kuwa Nyerere anawabagua katika uongozi na kuthibitisha hilo alivunja Baraza la Machifu.
Chief David Kidaha Makwaia kwa mfano alitupwa Tunduru. Kitu ambacho labda wengi hawakumbuki ni kuwa alizaliwa katika Uislamu na kukulia katika Uislamu. Alikuja kuingia ukatoliki baadaye ukubwani. Ukweli ni kuwa Waingereza walimfikiria Makwaia kama Rais wa kwanza wa Tanganyika kuliko Nyerere. Huyu amekufa juzi tu hapa (2007) lakini kwa vile hakuwa tena Muislamu basi hakumbukwi. Ana historia yake nchini lakini ni wachache sana wanajua baadhi ya mambo ambayo alifanikiwa kuyafanya.
Sasa Bw. Said ameamua kuimega historia na kutengeneza "sub-history' ambayo haifungi na matukio mengine ya historia. Anaangalia kwa jicho moja tu nalo ni la Uislamu. Sasa hili ni zuri kuvutia hisia lakini kwa mtu mwenye hekima ni lazima wahoji. Mifano miwili inatosha hapa:
Maasi ya Jeshi ya 1964 yalisababisha kamatakamata itokee; miongoni mwa watu waliokamatwa walikuwa ni mashehe na wengine wapinzani wa muda mrefu wa Mwalimu kuanzia 1958 na kabla. Sasa kama ingekuwa ni kamata kamata ya Waislamu tu basi hoja ni rahisi kujengwa lakini ni kweli walikamatwa Waislamu watupu? Kama walikamatwa na wasio Waislamu ni vipi basi kamata hiyo ionekane ni dhidi ya Uislamu unless kama wale wengine nao walishukiwa kushirikiana na Waislamu.
Tukio jingine ambalo huwa linatajwa sana ni kesi ya Uhaini ya 1969 ambapo mmojaa wa waliohusishwa ni Bi. Titi Mohammed. Kwa wengine hili lilikuwa ni dhidiya Waislamu. Ingekuwa kweli kama hawakukamatwa wengine. Lakini tuwakumbushe majina ya wale watu saba waliofikishwa mahakamani Juni 8, 1970 mbele ya Jaji Mkuu T. Georges
Bi. Titi Mohammed (Muislamu) (Muasisi wa TANU na mpigania Uhuru)
Michael Kamaliza (Waziri wa zamani wa Kazi - Mkristu)
William Chacha (Mwambata wa Kijeshi, Peking - Mkristu)
Grey Mattaka (mhariri gazeti la The Nationalist - Mkristu)
Oscar Kambona (mpigania Uhuru na Waziri wa zamani wa Ulinzi na Mambo ya Nje - Mkristu)*
John Chipaka (kiongozi wa chama cha ANC- Mkristu)
Eliya Chipaka (Kapteni wa JWTZ - Mkristu)
Alfred Mulinga (Luteni wa JWTZ - Mkristu)
* Kambona hakuhesabiwa kama miongoni mwa wale saba waliofikichwa mahakamani mwanzoni. Kambona alikuwa ameshatoroka kwenda Uingereza kabla ya kesi kuanza.
Sasa, kati ya wote hao saba ni mmoja tu Muislamu - Bi. Titi Mohammed. Lakini Bw. Said anaandika kana kwamba Nyerere alikuwa na baya dhidi ya Waislamu japo mtu angeweza kusema ilikuwa dhidi ya watu wa Kambona (wanne ya watuhumiwa walikuwa wanausiana na Kambona).
Sasa, vijana wanaosoma hapa natumaini wanapata mwanga kidogo wa kuelewa kwanini wengine tunachukulia hoja nyingi za Bw. Saiid ni za kutengeneza na zimeandikwa mahsusi kuvutia watu wasiotaka kutafuta ukweli.