Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

Hivi kwenye misikiti ya Bakwata huwa anasali peke yake tu au kuna waumini wengine pia?
Ndugu yangu, UISLAM ni zaidi ya mzee Mohamed. Ukiangalia mabaraza ya EID yanavyopendeza na misikiti hii yote inavyojaa waumini utajua tu hakuna mtu anaweza kuwaburuza Watanzania kwa jambo lolote. BAKWATA ni taasisi nzito sana kwa WAISLAM wa Tanzania kwa zaidi ya miaka 40 sasa.
 
Kugawana misikiti unayasema wewe Bakwata siyo chaguo la Waislam.
Chaguo la Waislam ni EAMWS? Kuna watu pia wanaamini Kikwete na CCM sio chaguo la WATANZANIA( zomba nipe like!).
 
Last edited by a moderator:
Leo tunawajuwa wazee wa Kiislaam walivyokuwa mstari wa mbele kupigania Uhuru, kupigania haki zao za msingi, walivyo asisi vyama vya kujiunganisha pamoja watetee maslahi yao iwe vya anasa au vya siasa tokea 1920s, lengo lake ndio muhimu.

Leo tunajuwa kuwa Nyerere alikaribishwa na hawa wazee, akala nao, akalala nao, majumbani mwao, ashaakum si matusi, wakamuenzi na hata kumfulia nguo zake kwa dhanna yao ya kuwa ni Mwaafrika mwenzao tena msomi hatokuwa na madhara kwao wala kwa dini yao, walifanya yote kwa nia safi kabisa kudhani kuwa watakuwa nae bega kwa bega.

Matokeo yake ni kusahau yote, hajui hata aliyemkaribisha kwake, pamoja na wazee wake na mke wake. Hivi Kariakoo ya miaka hiyo, ufunguwe duka la mafuta ya taa mtaa wa Mchikichi, hata Kiswahili vizuri hujui utakuwa huna msaada uliopewa na wenyeji? akafuliwa nguo zake na mama'ke Abdul Sykes, akila nae chakula chake, akamjulisha kwa wazee wake, akamuenzi kwa hali na mali, na wazee hawakurudi nyuma wakijuwa wamepata msomi mwenye muono, mwenye kujuwa kuongea, mwenye busara, oohh oohhh oooohh.

Matokeo yake tunayaona leo kwa macho yetu, tunayasoma yalivyoandikwa na Mohamed Said, tunahakikisha ni ya ukweli. Aaaah huyo ndie Nyerere.

Wanakuja humu na kejeli na viroja, leo hii hata wao wanawajuwa hao wazee waliompokea Nyerere, isingekuwa Mohamed Said wangewajuwa?? kwa historia ipi? Inashangza sana, badala ya wao kuona kuwa wameletewa upande wa historia waliokuwa hawaujuwi na watoe sifa kwa Mohamed Said wao wamekazania kulalama na hoja zisizo na msingi wala mshiko. Wanachotetea ni nini? hakijulikani.

Hakuna mpaka sasa, hata mmoja aliyekuja akasema Mshume ni wa kutunga, Said Tewa hakuwepo, EAMWS haikuwepo, Abdul Skes hakumkaribisha Nyerere. Mashado Plantan si kweli. Mama Maria hakuuza mafuta ya taa Mchikichi, Iddi Tosiri ni wa kubuni hakuwepo mtu namna hiyo. TAA haikuanzishwa na wazee wa Dar. AA haikuanzishwa na Kleist Sykes. Mweka hazina wa kwanza wa TANU hakuwa mweka hazina wa Jammiatul Islamiya fi Tanganyika nayo haikuanzishwa na Sykes

Jamani, hivi mnachobisha haswaa ni nini? tarehe fulani? siku fulani? kavaa nguo gani? hakulitumikia kanisa?

Rudini muisome hii historia kwa muono wenye manufaa, kwenu na kwa wenzenu. Itawafunguwa katika ubaguzi wa ujinga mliojifunga nao. Hakika mioyo yenu ina maradhi.
 
Kumbe na misikiti mmegawana! Ndio nafuu yetu hiyo tusiohangaika na DINI. Anavyoandika Mzee Mohamed humu ni kama vile anamiliki WAISLAM wote wa NCHI hii! Anasikilizwa na Waislam wote wa nchi hii!

Hizo i fikra zako,na hazipingwi,
Ni haki yako kikatiba kueleza kile kilicho ndan ya fikra zako,
Ila uhalisia hauko ivo..
 
mkuu zomba hapa ndo umepotoka kweli kweli..
..........Matokeo yake tunayaona leo kwa macho yetu, tunayasoma yalivyoandikwa na Mohamed Said, tunahakikisha ni ya ukweli. Aaaah huyo ndie Nyerere. ..........
yaani kwa vile tu yameandikwa na Mohamed Said ndo uyaamini na mpaka umeamua kuyapigania kwa nguvu zote yaonekane ni ya kweli? sasa hapa ukiambiwa una akili za kushikiwa utasema umetukanwa?
 
Last edited by a moderator:

Cha kuchekesha wale wale wanaokesha JF kuwadhihaki na kuwakejeli Waislam ndiyo wanaowasemea Waislam ni vituko vitupu.
 
Hizo i fikra zako,na hazipingwi,
Ni haki yako kikatiba kueleza kile kilicho ndan ya fikra zako,
Ila uhalisia hauko ivo..
uhalisia ukoje sasa? mbona nyinyi kila mkiulizwa swali mnajibu kiuwepesi wepesi tu bila kutoa ufafanuzi?
umeulizwa misikiti ya BAKWATA wanasali viongozi wa BAKWATA tu au?
 


Wanajitoa ufaham wao kwa makusudi,ila mioyoni mwao wanakiri uhalisia huu..!
Sisi hatuna muda wa kuwabembeleza,wakitaka waamini wasipotaka wachukue time zao..
 
Cha kuchekesha wale wale wanaokesha JF kuwadhihaki na kuwakejeli Waislam ndiyo wanaowasemea Waislam ni vituko vitupu.
sasa kama nyinyi kundi dogo mufilisi mnaudhalilisha Uislam na Dini ya Mnyezi Mungu, msiambiwe ukweli?
 
uhalisia ukoje sasa? mbona nyinyi kila mkiulizwa swali mnajibu kiuwepesi wepesi tu bila kutoa ufafanuzi?
umeulizwa misikiti ya BAKWATA wanasali viongozi wa BAKWATA tu au?

Ok,well,
What if kama nikikujibu wana swali viongozi wote,so what?ishu si misikiti ya kuswalia pekee,ishu ni misimamo ya wahusika wenyewe kulingana na mafundisho ya dini hii TUKUFU ya ALLAH s.w
 
Wanajitoa ufaham wao kwa makusudi,ila mioyoni mwao wanakiri uhalisia huu..!
Sisi hatuna muda wa kuwabembeleza,wakitaka waamini wasipotaka wachukue time zao..
uhalisia gani?
mnambembeleza nani? ili afanye nini?
mnabembeleza serikali ije kuwakamata kwa nguvu vijana wenu waende shule waachane na nyavu na makokoro baharini au?
 

Ahsante Zomba,
Wenzetu hawa hawajui utukufu wa ihsani.

Hebu tuwekee hapa "Jazaau ihsani..." huenda
wakawaidhika.

Muungwana haibi fadhila.
 
Ok,well,
What if kama nikikujibu wana swali viongozi wote,so what?ishu si misikiti ya kuswalia pekee,ishu ni misimamo ya wahusika wenyewe kulingana na mafundisho ya dini hii TUKUFU ya ALLAH s.w
kweli HOJA zikiisha kunabaki VILOJA.
 
uhalisia gani?
mnambembeleza nani? ili afanye nini?
mnabembeleza serikali ije kuwakamata kwa nguvu vijana wenu waende shule waachane na nyavu na makokoro baharini au?


Vip kijana unaejiita mzee,unakuja kasi kasi bila hata kujua mafuhum ya majibu yangu??
Nawaambia hamjalazimishwa kuamin haya,mkitaka mnaweza kuyapokea na kuyahifadhi mioyoni mwenu na msipotaka ni khiyari yenu kuyaacha na kuchukua time zenu..,ok?
 

WC,

Najua unapata tabu kuamini nisemayo kuhusu BAKWATA.

Ungependa iwe vinginevyo.

Mimi wajibu wangu ni kueleza ukweli na jinsi umma unavyojisikia
kuhusu BAKWATA na msimamo wa Waislam.

Ikiwa wewe unapenda kuamini kuwa BAKWATA ni kipenzi cha Waislam
mimi nina uwezo gani wa kukuzuia?

Atakae kuujua ukweli, ukweli uko wazi.
 

Usituondoe kwenye mada.....
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…