Mohamed,
Nina kaswali kamoja tu ka ziada kabla sijaaga mnakasha huu. Katika maandiko yako yoote sijaona mahali ambapo umechambua matokeo ya juhudi za Nyerere kutaifisha shule za misheni ili waislamu nao waweze kupata nafasi ya elimu.
Umekiri kuwa kulikuwepo imbalance ya elimu kati ya waislamu na wakristo na hili limezungumziwa sana na rafiki yangu Lawrence Mbogoni, ambaye kitabu chake The Cross versus the Crescent kinaanzia miaka ya 1880 hadi 1990. Ni kweli Waarabu/waislamu walikuja Tanganyika miaka 700 kabla ya hapo na wakakolonize maeneo kama vile Kilwa Mtwara na Bagamoyo, lakini hawa wamisheni wa kizungu walikuja miaka 600 baadaye na kuweza kufanikiwa katika muda mfupi tu, kujenga taasisi za maendeleo--hospitali na mashule--- kwa wafuasi wao. That being the case, and the fact that Julius Nyerere recognized the imbalance, do we give him any credit for taking steps, never taken before by colonialists, to rectify this imbalance? And taking Njozi's book, could not this be the reason Nyerere patted his regime for taking these steps , did these steps have positive results, or Nyerere was out of touch with reality? What is your comment?
Mkuu Jasusi, kila jambo linajulikana ukweli wake kinachofanywa na Swahib Mohamed ni kutafuta eneo ambalo litagusa sana hisia za watu ili achomeke hoja zake.
Hutamsikia akiongelea biashara kwasababu wafanyabiashara wengi tena waliofanikiwa watakinzana na hoja yake ya udini.
Hutasikia anaongelea kilimo kwasababu kilimo ni jambo lisiloamsha hisia.
Siku za karibuni anaongelea afya, kwabahati mbaya haongelei afya kama sekta inayoathiri maisha ya watu bali kama sehemu ya kushambulia Ukristo. Hapa ni ukristo kwasababu serikali ilikuwa ya Mwinyi. Hata kama itabidi basi itakuwa serikali na si Mwinyi.
Suala la elimu lipo wazi kabisa. Nina mfano wa eneo moja ambapo hadi 1933 Uislam ulikuwa haujaingia.
Kufikia 1950 hadi 1960 uwiano wa elimu ulikuwa 1:8 in favour of christian kwasababu walikuwa na shule zao.
Waislam wakachachamaa in a positive way. peleka watoto shule, jenga shule zao leo uwiano ni 1:1
Tafiti zinaonyesha(1980) mkoa ulioathirika kwa utapia mlo(malnutrition ) ni Kilimanjaro kwasababu wazazi hawakuwa na muda wa kuwalisha watoto kwa mpango mzuri( malnutrition siyo ukosefu wa chakula tu) mal=mbaya nutrition=feeding
in other words it's bad feeding. Kilimanjaro wazazi wanachakula lakini ulisha ni mbaya.
Hii ilitokana na jitihada za kuongeza kipato, mama peleka ndizi baba mwagia kahawa dawa, Kaka kalete mahindi, dada chambua kahawa. Mauzo ya KNCU pesa peleka sekondari. Hapo ndipo walipo kama ilivyo Mbeya na Bukoba.
Kama si hivyo wilaya moja ya Kilimanjaro isingekuwa na shule za sekondari nyingi kuliko mkoa mzima wa Lindi.
Shule zilijengwa kwasababu soko lipo, soko ni wakulima wanaopeleka watoto wao shule.
Wananchi wa Kilimanjaro walipoambiwa ukweli wa utapia mlo, hawakutafuta sababu au mchawi bali kufanyia kazi ushauri uliotolewa. Hapo ndipo thamani na hamasa ya watu vinapochangia maendeleo yao
Rufiji mtoto anaozwa miaka 16 kama ilivyo Bagamoyo, Mjasani, Kicheba na Mkanyageni pale Muheza.
Hamasa kuhusu elimu kwa baadhi ya maeneo ipo chini sana. Wala si pwani hata bara ingawa viwango vinapishana.
Ni kutokana na mgawanyo wa mambo kama dini, sehemu fulani inakuwa na wakazi wa imani fulani.
Kilimanjaro ni Christians na Tanga ni Moslems kwa mtazamo wa majina na dini hizi mbili ingawa si kweli kwani wapo wapagani n.k.
Mgawanyo huo unaambatana na tofauti kitaifa. Mathalani kama wilaya moja ya Kilimanjaroni ni zaidi ya mkoa wa Lindi katika mambo ya elimu basi usitegemee uwiano wa elimu kuanzia sekondari hadi chuo kikuu kulingana.
Mgawanyo utaakisi sana jiografi ya sehemu.
Jambo la muhimu ni kuliangalia tatizo kwa ukubwa wake kiinchi, kuangalia vyanzo vya tatizo na jinsi gani linaweza kutatuliwa kama nchi. Kuangalia mifano ya maeneo mengine ili kuona ni vipi wamefanikiwa.
Ni ujinga uliotukuka kudhani kuwa unaweza kuwa na mtaalamu kuanzia chuo kikuu tu. Kwamba amezaliwa akakimbia shule ikafungwa halafu akaibukia chuo kikuu.
Ni upotofu uliobobea kudhani kuwa tatizo ni mawaziri 10 na makatibu wakuu 10 na kufumbia macho malaki ya wanafunzi wanaoshinda chini ya uongozi wa kiranja mkuu.
Ni uzezeta kudhani kuwa NECTA ndio tatizo kwasababu leo anaweza kuwa mkuu wa NECTA ni mtu wa imani fulani na wala yeye asiweze kuleta mabadiliko kwasababu NECTA haifundishi inatahini, kama hakuna mtahiniwa NECTA itatahini maruhani?
Ni ututusa kufumbia macho tatizo la ndoa na utoro wa shule, uhuni uliokithiri na kudhani kuwa elimu inaingia vichwani kwa mavazi au kwa njia ya mnururisho kama si mpitisho.
Ni upumbavu kumtoa mtoto darasani aende kusikiliza kesi ya Ponda ukitegemea mtoto huyo kufaulu kwa njia ya kuwa na mkuu wa NECTA wa imani fulani.
Ukienda Peramiho, Magila, Ikizu, Haidom, Magila utakuta watu wasiojua kusoma au kuandika, ni vipi basi mfumo unaolalamikiwa usitoe ahueni kwao?
Ukitaka kumshinda mwanadamu kwanza muondolee kujiamini''confidence'' halafu mpumbaze, hapo utamsukuma na kuanguka. Literacy level yetu kama taifa imeanguka kutoka 80% hadi 60%.
Kwa maneno mengine kuanguka huku hakuchagui dini au kabila kama ilivyokuwa kwa mafanikio yake. T
uliwezaje kufika 80% kama kuna ubaguzi?
Ni lazima watu wakiri uwepo wa tatizo kuanzia katika familia kabla ya kutafuta kundi au mtu wa kumtwisha lawama.
Kwanini suluhu itafutwe kwa kuangalia dini fulani na si dhehebu fulani.
Kwanini watu wasijiulize Hindu Mandal, Agakhan, Ismailia wanafanikiwaje katika mfumo ule ule kandamizi.
Inasikitisha sana kuona watu wanaondoa jicho katika tatizo wanatafuta namna za kijinga, kipuuzi na kizembe kuficha au kulikimbia tatizo hilo.