Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

Katika Gazeti la Mwananchi la leo nimekutana na Historia ya KHADIJA BINTI KAMBA kwamba naye ni MWASISI wa TANU na pia amezungumzia kwamba nembo ya Taifa ni picha yake yeye na Mzee JUMA na asili yake amesema siku MWL NYERERE alipofanyiwa TAMBIKO baada ya kuteuliwa kuwa waziri Mkuu. Nauliza Je huyu alisahulika kwenye historia. Mzee Mohamed, Mwanakijiji, Ritz, Yericko na wengine mnaweza mkamuelezea kidogo huyo bibi.
 
kumbe Sykes hakumuachia Nyerere ila waligombea pamoja na Nyerere akashinda?
 
Kwani hao walikuwa na matatizo gani?

wote hao ni wa dini moja! katika nchi ambayo idadi ya waumini wa dini mbili kuu haitofautiani sana tunaona vitu kama hivi halafu mnasema tusiseme kuwa kuna udini!. lazima tutasema hata mkikasirika. hii imezidi tena. mfano wewe ungekuwa ndio muislamu ungeridhika na hili? ungekaa kimya?usijibu kwa ushabiki.
 
Hivi ni nani anayewachagua hawa viongozi wa NECTA?
 
Mimi nipo nimejikita zaidi kwenye hoja za msingi kupinga uchochezi wako mkuu,


Swahiba naomba nipe mtazamo wako kuwa ingetokea aliyeuawa pale Zanzibar kwa sababu za uchochezi wako na wawenzio ni Shehe, nini unadhani kingetokea?

ila mpaka sasa hujaweza ku prove huo uchochezi

labda nikusaidie, nukuu kwenye kitabu cha mzee Mohamed Said, na utoe citation na useme "hapa mzee Mohamed Said umechochea"

mwezi mzima and you could not figure that out.

kama anavosema Ritz, wewe ni mtupu hujui lolote

haya umekaribishwa Gahwa, unaanza kuuliza mambo ya "ingetokea, kingetokea"

yani hapa ndo umeonyesha udhaifu wako

Ninawasilisha
 
Last edited by a moderator:
Mimi nipo nimejikita zaidi kwenye hoja za msingi kupinga uchochezi wako mkuu,


Swahiba naomba nipe mtazamo wako kuwa ingetokea aliyeuawa pale Zanzibar kwa sababu za uchochezi wako na wawenzio ni Shehe, nini unadhani kingetokea?

Mzee Mwanakijiji angetoa tamko la kutaka Mufti wa Tanzania atoe tamko au ajiudhuru.
 
Ndiyo ushangae mtoto wa mjini anashindwa katika uchaguzi na wakuja asiyejua kuvaa wala kula chapati ha ha ha ha ha.
mtu anayeenda sokoni hana hata senti akitegemea fadhila ya matajiri wa mjini akina Sykes ila kwenye uchaguzi Nyerere kammwaga, hahahahahahahaahaha!
mbaya zaidi akiwa na miezi miwili tu ndani ya TAA, loh!
 

Zomba,

DVD Blue Ray ntaileta hapo hapo.
Haina chenga.

Ila nahofu ya jambo moja huyu sahib
wangu Yericko kwanza faluda anaijua?

Maana jamani lazima tuchukue tahadhari
asijepindukwa na tumbo ikawa tabu...
 
Mag3, Nguruvi3,

Tufahamisheni orodha ya Marais wa TANU waliopita tupeni majina yao.
......Julius Kambarage Nyerere, mwanasiasa mgeni katika TAA pale makao makuu akiwa amejiunga n uongozi wa chama miezi kumi na tano tu iliyopita, alichaguliwa rais wa kwanza wa TANU na John Rupia makamo wa rais. ........
hizi ni moja ya simulizi za mzee wako MS.
 
Ndiyo ushangae mtoto wa mjini anashindwa katika uchaguzi na wakuja asiyejua kuvaa wala kula chapati ha ha ha ha ha.

Ngongo,

Unatia kejeli.

Uchaguzi ule nimeueleza kwa kina humu ukumbini
na katika kitabu.

Nyerere mwenyewe hadi anaingia kaburini hili hakuligusa hata
kwa mbali.

Kama nisingeliandika hata nyie msingejua Nyerere kafikaje TANU.

Ikiwa wewe unaona kufanya mzaha katika hili unajisikia raha basi
mimi sitakuvurugia starehe yako.
 
binafsi sijaona bandiko lako kuhusu huo uchaguzi, ngoja nilitafute.
 
mtu anayeenda sokoni hana hata senti akitegemea fadhila ya matajiri wa mjini akina Sykes ila kwenye uchaguzi Nyerere kammwaga, hahahahahahahaahaha!
mbaya zaidi akiwa na miezi miwili tu ndani ya TAA, loh!

Z,

Mimi sikulaumu kwa hayo usemayo.

Hujui mapenzi walokuwanayo wana TANU
kwa viongozi wao.

Kipindi chote cha kudai uhuru Nyerere si Abdu
walikuwa wakihemea chakula majumbani mwao.

Kariakoo ofisi ya Market Master ikitoa kila kitu.

Mzee Abdallah alikuwa muhudumu ofisi ya Abdu
Sykes kanambia alikuwa akichinja kuku 20 kwa siku
akipeleka nyumbani kwa Abdu kwa ajili ya kitoweo.

Inakuchomeni kwa kuwa hamkujaliwa kupitia historia hii.

Lakini bezeni fanyeni kejeli ukweli utabaki ukweli hauwezi
kufutika.

Mshume Kiyate na Abdu Sykes walikuwapo pale Kariakoo Market
na hawa walikuwa mstari wa mbele kwenye TANU.
 
Wewe umejuaje kama ni wa dini moja?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…