Mzee hapa umeonesha uanaume wako na hapa sunna imefanyakazi hata mtume alisema yeye na uoga ni umbali kati ya mashariki na magharibi hakuna kumuogopa kiumbe aliyepita njia mbili za mkojo si maneno yangu ni maneno ya ulamaa HASSAN AL BASSARY hawa ni wanafunzi wa maswahaba wa mtume,KIUMBE ALIYEUMBWA KWA MANII UMUOGOPE HAIJI MZEE BIG UP KWA HILO KUMKAMATA ILUNGA SIO SULUHISHO LA DHULMA NCHI HII NA MFUMO KRISTO.
BH,
Imebidi niwaeleze maana nimeona wao wanadhani Waislam ni rahisi
kuwatia hofu.
Walianza na mie kutafutwa na vyombo vya usalama nchini.
Kisha wakaja na mie kusakwa na CIA na FBI.
Ilhali ikawa ni maneno ya vitisho.
Ndipo nikawapa historia yangu kuwaeleza kuwa mie sitafutwi kwa kuwa
nafahamika kiasi hata jiwe ukiliuliza kwangu litakuleta.
Nikawaeleza jinsi paper yangu kuhusu ugaidi niliyotoa Chuo Kikuu Cha
Ibadan, Nigeria ilivyowaghadhibisha Waamerika kiasi taarifa zangu zikatumwa
nyumbani na mwishowe nikatiwa mbaroni Uwanja wa Ndege.
Hao hao Waamerika baada ya miaka minne kupita wakanialika kwao kwenda
kuzungumza kwenye vyuo vyao na wakanikarimu sana.
Nikaamini kweli they dont have permanent friends nor parmanent enemies.
Wao kwao cha muhimu ni national intrests.
Nikumalizie hawakuniita bure there is no free lunch in Amerika.
Kuna mambo walikuwa wanatafuta yakini yake kutoka kwa "maadui" zao.
Hapa wakitakidi kuwa Waislam wa Tanzania ni maadui zao.
Waamerika hawajui kila kitu kuna mambo ni wajinga unaweza usiamini.
Haya tuyaache.
Niliwapa yakini ya kuwa Waislam wa Tanzania hawawachukii Waamerika.
Mjadala mkali.
Wakataka kujua mengine.
Nikawaeleza Waislam ndiyo wengi na ndiyo maana mapambano yote dhidi
ya dhulma za wakoloni Waislam ndiyo walikuwa mstari wa mbele.
Mshangao wa kishindo.
Nikawasihi wasijiongezee maadui kwa kuwanyanyasa Waislam wa Tanzania.
Nikawaeleza Waislam wana ugomvi na serikali kwa dhulma tunazofanyiwa lakini
hatuwachukii Wakristo.
Nikawaambia mmesoma kitabu changu na mmeona vipi Waislam walivyowatia
Wakristo katika harakati za kudai uhuru.
Walinipa shukurani nyingi na wakasema kuna mengi walikuwa hawayajui.
Tumeagana marafiki na wakawa wananiringishia na Kiswahili chao wakinambia
nisijidai ati lugha wamesoma kwetu.
Wananisimanga wananambia wao Kiswahili wamejifunza Amerika wamekuja Tanzania
kukipiga msasa.
Tunacheka.
Yapo mengi sana.