Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

Ushabiki na ujinga vinakutesa sana bwana mdogo, nani kakwambia habari ya Mbowe alikuwa anaifahamu Mohamedi Saidi peke yake? Mbona mnamsujudu huyo mzee wenu kama mtume vile!
 
mkuu umerudi toka Guantanamo?
pole kwa kifungo.
 
Nani alimpelekea na kwanini alimpelekea?

Je ulithibitisha kuwa kitabu hicho kilimfikia?
Hili suali Mohammed alimjibu Mzee kama hivi
MM,

Nishaeleza kuwa si lazima Nyerere awe hata kakisikia kitabu changu.
Sidhani kama baada ya kusema hivyo kuna haja tena ya kufatanafatana.
Mimi nimemfahamu vizuri.Nyerere siye aliyemtaka aandike bali alisababishe aandike historia ya Tanzania.Hivyo angepelekewa akakikalia kimya au asingepelekewa bado historia hiyo ya kweli inafanya kazi yake kufuta ile ya uongo.
Ukiacha hilo,hivi uthibitisho wa kitabu kumfikia Nyerere na kutokumfikia unadhani ndio itafuta ukweli wa yale aliyoyatenda katika utawala wake na ambayo yameshaandikwa.Halafu kwanini uwatukane watu wa usalama wa taifa wakati wa utawala wake?.Mkapa kwanini alipelekewa nakala ya The Mwembechai killings na watu na kazi yao wawache kumpelekea Nyerere nakala iliyomhusu mwenyewe.
Mbona walikuwa wakimpelekea mpaka umbea wa maisha ya raisi Mwinyi na mke wake bi Siti.Hivi unaamini watawacha kumpelekea kopi ya kitabu cha siri za maisha yake mwenyewe kilichotoka miaka kadhaa huku akiwa yu hai?.
Mohammed anasema kitabu alipelekewa mkononi na Mohammed naye ana vyanzo madhubuti vya kupatia habari kama ulivyoona katika maandishi yake kuliko shaka zako.Hivyo kaa na kujipa moyo kwako kuhusu kutokufika kitabu kwa Nyerere na Mohammed kaa kimya usimtaje aliyempelekea mkononi tuone kama itakuwa ndio utetezi wenu kwa ubaya wa Nyerere.
 

Tanzania Kwanza, taratibu, hizi mimi huziita "knock out punches".
 
Ushabiki na ujinga vinakutesa sana bwana mdogo, nani kakwambia habari ya Mbowe alikuwa anaifahamu Mohamedi Saidi peke yake? Mbona mnamsujudu huyo mzee wenu kama mtume vile!

Mod pamoja likes mungeweka na fimbo kuna watu huku hawaendi mpaka fimbo nani amekwambia mitume wanasujudiwa? use your common sense babu!
 
Fanya basi utafiti na wewe ;-)

Tafuta wazee wako walioifanyia mema taifa letuili tuwaweke kwenye historia kama kuiboresha.
 
Fanya basi utafiti na wewe ;-)

Tafuta wazee wako walioifanyia mema taifa letuili tuwaweke kwenye historia kama kuiboresha.

Mohamed Said hajaiboresha bali kaleta mpya kabisa na kuikana iliyokuwepo awali.
 

Kighoma Ali Malima aliwashtukia na kugundua uchakachuaji mitihani ya wanafunzi Waislamu! alipoanza kuleta mabadiliko unakumbuka Media na kanisa walianza propaganda ya kudai Malima kaigeuza Wizara Msikiti na kumshinikiza Mwinyi amsimamishe! baadae walimkolimba! sasa unataka JK nae akolimbwe?
 

Ami,

Prof. Haroub Othman yeye aliathirika sana na kitabu changu.
Alikwenda na akazungumza na Nyerere kuhusu yale niliyosema.

Habari hii sina haja ya kuirudia tena.
Nimeieleza hapa jamvini na ilileta ubishi mkubwa.

Prof. Haroub alimwomba Nyerere na yeye aeleze maisha yake
baada ya mimi kueleza uasisi wa TANU na matatizo yaliyotokea
baada ya uhuru kupatikana.

Alimweleza Nyerere kuwa endapo kama yeye hataeleza upande
wake wa historia ni wazi historia yake itaingia doa.

Prof. Haroub kanieleza maneno haya nje ya Msikiti wa Ibadh.
 

Ami,

Prof. Haroub Othman yeye aliathirika sana na kitabu changu.
Alikwenda na akazungumza na Nyerere kuhusu yale niliyosema.

Habari hii sina haja ya kuirudia tena.
Nimeieleza hapa jamvini na ilileta ubishi mkubwa.

Prof. Haroub alimwomba Nyerere na yeye aeleze maisha yake
baada ya mimi kueleza uasisi wa TANU na matatizo yaliyotokea
baada ya uhuru kupatikana.

Alimweleza Nyerere kuwa endapo kama yeye hataeleza upande
wake wa historia ni wazi historia yake itaingia doa.

Prof. Haroub kanieleza maneno haya nje ya Msikiti wa Ibadh.
 

Kubwajinga,
Nimekusoma.
 

Isalia,

Amin kwa sote.
 
Salaam,

Kwa mafundisho yako ndugu mohamed said, Nimepata kujua na kuamini kuwa historia yetu ina madoa mengi.

Nakuombea umri mrefu na mungu akulipe kwa kazi kubwa uliyoifanya.

Ukweli unaumiza siku zote.
 
Salaam,

Kwa mafundisho yako ndugu mohamed said, Nimepata kujua na kuamini kuwa historia yetu ina madoa mengi.

Nakuombea umri mrefu na mungu akulipe kwa kazi kubwa uliyoifanya.


Ukweli unaumiza siku zote.

Achahasira,
Amin kwa sote.
 
Aligundua uchakachuaji upi?
 
Salaam,

Kwa mafundisho yako ndugu mohamed said, Nimepata kujua na kuamini kuwa historia yetu ina madoa mengi.

Nakuombea umri mrefu na mungu akulipe kwa kazi kubwa uliyoifanya.

Ukweli unaumiza siku zote.
Hasa ukipindishwa
 
Mohamed Said hajaiboresha bali kaleta mpya kabisa na kuikana iliyokuwepo awali.
Kuwataja waliosahauliwa nikuleta historia mpya?
Bahati nzuri hao wote aliowataja wanaonekana sio kwa maandishi tu bali pia kwenye picha na Nyerere.

Sasa kilicholetwa kipya ni kipi?
Halafu ahadi ni deni!!
Ile audio uliyotuahidi imeishia wapi?
 

Attachments

  • image.jpg
    29.2 KB · Views: 35
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…