Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar


Mag3,
Sasa umehamia mipango miji?
JF ina majambo.

Siasa basi.
 
 
 
Katika kujadiliana fanya heshima.Usiwe unazungumzia mambo usiyo na elimu nayo.Tafsiri ya hiyo aya ni hivi
وَجَزَاءُ سَيِّئَةٍ سَيِّئَةٌ مِّثْلُهَا فَمَنْ عَفَا وَأَصْلَحَ فَأَجْرُهُ عَلَى اللَّهِ إِنَّهُ لا يُحِبُّ الظَّالِمِينَ
Na malipo ya uovu ni uovu mfano wa huo. Lakini mwenye kusamehe, na akasuluhisha, basi huyo malipo yake yapo kwa Mwenyezi Mungu. Hakika Yeye hawapendi wenye kudhulumu.
Hapo kilichoanzwa kulipa uovu kwa uovu.Halafu ndio ikafuatiwa na kusamehe.
Hivyo kulipa uovu kwa uovu ni bora zaidi ili kukomesha dhulma.Lakini ni kweli kuwa ukisamehe utalipwa na Mwenyezi Mungu.
Jukumu la kulipiza na kusamehe ni la mtu au watu binafsi.Ikiwa ni hivyo kwa tabia za kibinadamu kusamehe kunakuja kwa yule aliyekukosea kidogo na kwa bahati mbaya.
Wewe hufahamu lakini wengine waangalie kwamba uovu wa Nyerere kwa waliomkaribisha kwenye siasa na kwa waislamu ni mkubwa sana.Kwa vipi atasamehewa na kila mmoja wao.Wako waliomsamehe na watalipwa lakini kwa baadhi yetu na hatuna makosa. Hapana !.Sio yeye tu ambaye alifanya kwa kusukumwa na imani yake bali hata Kikwete anayefanya kwa kuwahofu nyinyi na kutii amri za mataifa ya nje naye hasameheki.
Unadhani kila tunachojenga nyinyi mkisaidiwa na Kikwete,Mkapa mnabomoa tutasamehe mara ngapi?.Katika hali ya kuacha dhulma iendelee na kuendelea kusamehe basi kuna ufafanuzi mwengine kuonesha kuwa hiyo ni dhambi pia.
Kuhusu aya ya 23:96 huo ulikuwa ni wito uliomuhusu zaidi Mtume S.A.W ambapo Allah alimuahidi ulinzi na kuahidi kuwashughulikia mwenyewe wabaya wa Mtume wake.Aya ya juu inatuhusu sisi sote ambao tuna jukumu la kujikurubisha kwa Allah S.W kwa kutekeleza kulingana na mafunzo yake.
 
 
Z,

Kwa darsa hiyo wenyewe mipango miji.
kama hilo linahusu mipango miji ni kwanini basi unapenda mipango miji ya gerezani tu ndo itambulike katika harakati za uhuru?
 
Al shabab ni extreme. Taliban ni extreme. Osama bin Laden alikuwa extreme. Rashid Kawawa alikuwa moderate.

Hapa naona tofauti ni majina ya watu wa nchi tofauti! Kawawa Mtanzania na Osama Msaudi na Taliban watawala wa zamani Afgani!
bado hamjajibu swali langu! tofauti ya Muslim moderate na extreme ni nini?
 
Nimeandika historia sikuandika mipango miji.
nafikiri tuishie hapo,
vinginevyo kilichoulizwa na Mag3 hakina uhusiano wowote na mipango miji,
kuulizwa ulipokuwa unaishi na nduguzo au wamanyema walipokuwa wanaishi havina uhusiano na mipango miji,
kuulizwa kwanini jina la mtaa liliitwa new street sio mipango miji, ni siasa na historia, mipango miji hawahusiani na kupanga majina ya mitaa.
 
SHIA na SUNNI wanachinjana IRAQ,PAKISTAN etc etc

Kabla Wazungu kuvamia Iraki na Pakistani ulisikia kuna vita vya kimadhehebu huko? yanayotokea Iraki na Pakistani ni uchochezi wa Wazungu! wanalipua na kuuwa watu huku wakidai ni vita kati ya Sunni na Shia! Zanzibar mapadri wanashambuliwa lakini mtuhumiwa ni magaidi! huku bara wanauliwa Mapadri, albino na kushambuliwa waandishi wa habari lakini wahusika ni Majambazi na wenye Imani za Kichawi!
Unaona Kizungumkuti hicho!
 

kwanini hujiulizi kwanini siku kuu ya IDD inasherekewa kiholela,mwaka jana nilifaidi IDD mara mbili nasafiri nakuta idd wakati nilipotoka ilikuwa jana yake
.

Mbona Urusi Krismasi haisherehekewi 25 december? Wakristo wa Dhehebu la Koptic pia hawali Krismas na Noeli tarehe hizo? Lakini unashangaa Waislamu kugawanyika kula Idi siku tofauti! na kuna ubaya gani hata wakila siku 3? mbona Nyinyi mnaanza Kula Krismasi tangu tarehe 20.december watu wanaanza Kusafiri na kurudi ni mpaka Januari 3! huku ni kufisadi nchi na kurudisha maendeleo ya nchi nyuma!
 
Kwa hiyo haya mauaji wapo sawa kutoa roho za watu.Vipi mauaji ya Joseph Koni Uganda?

Vita vya Wakatoliki wa Nodhern Ireland na WaLuteri wa England vilivyotoa roho za Watu hajui hilo? Vipi na Wakristo wa Kiserbia miaka ya 90 hawakuuwa Maelfu ya Waislamu wa Bosnia na vita baina yao na Wakristo wenzao wa Croesia amesahau mara hii? nadhani inatosha tusiharibu mnakasha wa Jericko Nyerere na Mohamed Saidi! wasitutoe ktk mstari!
 

Shekh MS,

Habari hii ya Profesa H.Othman kupata mshtuko hata na mimi nimeingiwa na wasiwasi kuhusu kifo chake! jee, alikufa kifo cha kawaida, ama aliugua muda mrefu au kilikuwa kifo cha kutatanisha?
 
Mkuu gazeti la kwanza liliandikwa kijerumani, kuna kipande cha picha yake nimekiweka hapa, 1911 linaitwa USAMBARA lilichapwa Lushoto, (nimeshangaa babu yangu aliishia darasa la 4 lakini anajua kijerumani balaa.
Wewe msambaa kweli akili zako ni zero.
Nilikua nafuatilia post zako kwa muda mwingi nikaona kwamba huprovide chochote bali ushabiki tu.

Wenzio wanaongelea gazeti la mtanganyika wewe unaongelea gazeti la mjerumani?
Tena wajerumani waliokua wanawatemea mate watoto wa kisambaa pale Dochi /Deutch ambapo ni chuo cha mahakama sasa.
Kawaulize mababu zako kuhusu wajerumani huko Usambara.
 

Ndio maana tunaona una matatizo.. kweli kabisa unaamini watu wenye kuvaa kanzu wanakamatwa!


Kosa langu ni hilo lakini sikuwa naandamana na maandamano yenyewe hayakuwapo.

Hhivi umewahi kukutana na mhalifu ambaye anakubali kuwa kafanya uhalifu? Au kwa vile hawa vijana ni wa "Kiislamu" basi unawapa benefit of the doubt?

Wajerumani Vita Vya Pili Vya Dunia wanawapiga na kuwatesa Wayahudi kisha wanawauliza
hivi mnajuakwa nini tunakupigeni?

Tunajisikia raha tukikupigeni.
Hapa ndipo tulipoifikisha Tanzania.

Angalia sasa! Yaani unathubutu hata kwa mbali kusema walichofanyiwa Wahayudi na Hitler ni sawa na unayoamini yanatokea Tanzania? Really? Kweli we mzee unapenda shari kweli!


Kuonekana na alama za Uislam unahatarisha maisha yako si njiani hata shule, vyuoni na makazini.
Katika hali kama hii nani wa kuonewa huruma?

Yaani kanzu sasa imekuwa "alama za Uislamu"? HIvi ni Waislamu wangapi wanavaa mavazi hayo na hawaulizwi lolote? Kama kweli unaamini hili mlalamikie Kikwete basi, Bilal, Othman na Mwema - wote hawa ni Waislamu na uwaambie kwanini wanawadhulumu Waislamu wenzao.

Mzee Said ulikofika kiakili huwezi kurudi; unaona dhulma kila mahali, unahisi uadui kila upitapo, na ukikutana na Mtu mwenye jina la Kiislamu katiwa pingu wazo lako la kwanza inaonekana ni kuhisi kafanyiwa vile kwa sababu ni Muislamu! Hatuna jinsi ya kukusaidia kwa kweli... Sikutana kukupyschoanalyze you lakini sasa nadhani itabidi nifanye hivyo...
 
Shekh MS,

Habari hii ya Profesa H.Othman kupata mshtuko hata na mimi nimeingiwa na wasiwasi kuhusu kifo chake! jee, alikufa kifo cha kawaida, ama aliugua muda mrefu au kilikuwa kifo cha kutatanisha?

TK,

Kifo kilikuwa cha ghafla.
Allah ndiye mjuzi.
 
Katika msiba wa Abdu Sykes watu wa protocal walimkalisha Nyerere jamvi
moja na Ahmed Rashad Ali na wakati wa kutoa sadaka ulipowadia Rashad
alikula pilau sinia moja na Nyerere mkono kwa mkono.

Kwanini walimkalisha na Dhwaalim? au hawakujua Nyerere ndiye alikuwa adui mkubwa wa Waislamu?
 

MM,

Waulize Wayahudi walokuwa Poland na wale walopita na kupona
Autshwitz.

Wewe una luxury ya kukaa huko uliko nyuma ya lap top ukafanya
hiyo psychoanalyis yako.

Sisi ni ndugu zetu ndiyo yanawakuta haya.
Tunakijua tunachosema.

Mimi si mjinga ukaja na hicho kibri chako.
Luambano alisema uongo Yesu katukanwa Mtambani.

Serikali ikaua Waislam Mwembechai.
Serikali ilipojua imedanganywa ishachelewa.

Maalim Matar kawekwa kizuizini kwa tuhuma za kupindua serikali.
Walomjua Maalim Matar walipigwa na butwaa kwani Matar hakuwa
anaishi dunia hii.

Kiasi ukimuuliza leo tarehe ngapi atakupa kalenda ya Kiislam.
Hakuwa nasi kabisa.

Fanya tahadhar unapozungumza na mimi kwa hisani yako.
Wewe wa kunisaidia mie.

Kuwa na adabu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…