Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar


Kumbukumbu nzuri masiku yamepita mengi hebu tutajie majina ya hao viongozi wa TANU.
 
Naona ujanja wako ni kum frustrate mtu unapojibu hoja zake ili asikuulize tena. Jaribu kukaa chini basi ujibu kiutu uzima kama ulivyomuamba aandike maswali yake. Nimesikia uzee ukishika kasi saa nyingine akili zinakuwa kama za kitotokitoto hivi.

Kaka! Ulichoandika ni tusi hata kwa wazee wako.
 

Ukweli ni kitu kizuri sana hasa katika historia,

Mohamed Said ameukwepa ukweli katika kitabu chake,

Nimejaribu kueleza kwakifupi tu pale juu kuwa kundi la wale vijana wakariakoo lilikabiliwa na changamoto kadhaa, Elimu na Woga.

Dr Kyaruzi aliisimamia TAA kwa weledi sana, lakini baada ya kuondoka iliyumba yaani waliokuwepo hawakuwa na uwezo wakuongoza mpaka mpigania ukombozi mwingine Julius Nyerere alipokuja kushika hatamu
 

Unachanganya habari.
Unaandika na hamaki.

Hapo ndipo zinaingia kejeli za kahawa nk. nk.
Huu ni mjadala tu kama nimekosea mahali unasema tu kiungwana.

Kleist alikuwa na kipaji cha hali ya juu katika uongozi.

Licha ya kuwa katibu muasisi wa AA mkwaka 1933 alikuwa katibu muasisi
wa Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika (Umoja wa Waislam wa Tanganyika)
Mzee bin Sudi akiwa rais.

Matola alikuwa rais kweli lakini mambo yote akifanya Kleist kwa kuwa Kleist
alikuwa kijana tajiri.

Hii ilimwezesha kufanya mambo mengi sana kwa urahisi.

Cecil Matola alikuwa kiongozi wa African Association na alipoondoka akaingia
Mzee bin Sudi kama rais.

African Association ilizorota mwaka 1933 baada ya kutokea ugomvi kati ya Erika Fiah
na Kleist.

Kleist alijitoa katika uongozi.

Ipo barua aliyoandika Mzee bin Sudi aliyoanza kwa Bismillah Rahman Rahim.

Barua hii Mzee bin Sudi alimwandikia Kleist kumbembeleza arudi AA wakiongoze
chama.

Habari hizi zipo katika mswada wa maisha ya Kleist.

Habari hii inaweza halikadhalika kupatika katika Illife (Modern Tanzanians)
''The Townsman Kleist'' Sykes kama alivyoandika mjukuu wake.

Dr. Kyaruzi aliingia TAA na Abdu Sykes 1950 na hakumaliza hata mwaka
Waingereza wakampa uhamisho Kingolwira Prison kisha Nzega.

Sababu ya uhamisho wa Dr. Kyaruzi ni ile TAA Political Sub Commttee waliyounda
wajumbe wakiwa Sheikh Hassan bin Amir, Abdu Sykes, Dr Kyaruzi, Said Chaurembo,
John Rupia, Hamza Mwapachu na Steven Mhando.

Kamati hii ilimchukua mwanasheria wa Kibyamuda Earle Seaton kama mshauri.
Seaton alikuwa rafiki yake Abdu Sykes.

Habari ni nyingi nisimame hapa kwa sasa.
Kwa ufupi TAA ikawa inafanya kazi kama chama cha siasa halisi.

Huo ndiyo ukawa ndiyo mwisho wake wa uongozi wake kama rais wa TAA.
kuanzia 1951 Abdu Sykes akawa Acting President na Secretary na 1952
Abdu akawa rais wa TAA.

Kuhusu Martin Kayamba nakusihi tufanye subra tutamzungumza.
Kwanza hebu linganisha haya niliyoandika hapa na hayo uliyoandika wewe.

Tukimaliza Insha Allah tutakuja kwa Martin Kayamba Mdumi.

Tuendelee Insha Allah na mjadala.
 
Naona ujanja wako ni kum frustrate mtu unapojibu hoja zake ili asikuulize tena. Jaribu kukaa chini basi ujibu kiutu uzima kama ulivyomuamba aandike maswali yake. Nimesikia uzee ukishika kasi saa nyingine akili zinakuwa kama za kitotokitoto hivi.

Hapana mkuu, punguza jazba twende taratibu.

Tujadiliane kwakuheshimiana sisi sote ni watanzania jamani.
 

Hapana TAA baada ya 1950 haikupata kusinzia.
Nakuwekea kitu hapa kutoka kitabu changu ''The Life and Times of Abdulwahid Sykes...'':

[TABLE="class: MsoNormalTable"]
[TR]
[TD] TAA Political Subcommittee, 1950
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD] No records exist which show that the African Association had a clear official policy or programme on the country's political situation.

To understand the direction of African politics as they appeared at that time one need to observe the behaviour of the leadership and its reaction to different African problems.

Abdulwahid's first move was to form what was known as TAA Political Subcommittee [1] comprising himself as secretary; Sheikh Hassan bin Amir as the Mufti of Tanganyika; Dr Kyaruzi; Mwapachu; Said Chaurembo who was the liwali at Kariakoo local court; John Rupia and Stephen Mhando. The task given to this committee was to deal with political issues in the country.

The creation of this committee was a turning point in the history of organised politics in colonial Tanganyika.

Throughout the entire twenty-five years of its existence, the African Association had functioned under a non-political constitution. For the first time, in 1950, TAA under new leadership gave itself political status, not by changing the existing constitution, but by forming a political committee within the Association.
[/TD]
[/TR]
[/TABLE]


[1] Annual Report of the Secretary of Tanganyika African Association, 7 January, 1951. Sykes' Papers.

Hayo unayosema ya kuwabeza wazee wangu ni historia hiyo ya Kivukoni iliyoanza na kumalizikia na Nyerere na wakija wengine kuandika ukweli magazeti yanakusanywa na kuchomwa moto. Haya ninayosema mimi ndivyo mambo yalivyokuwa lakini simlazimishi mtu aniamini. Wanaukumbi nawaachia wasome na waamue nani mkweli. Hapo juu nimeandika kwa mukhtasari tu yaliyofanywa na TAA katika uongozi wa Abdu Sykes.
 
Naona ujanja wako ni kum frustrate mtu unapojibu hoja zake ili asikuulize tena. Jaribu kukaa chini basi ujibu kiutu uzima kama ulivyomuamba aandike maswali yake. Nimesikia uzee ukishika kasi saa nyingine akili zinakuwa kama za kitotokitoto hivi.
Sweke 34, wala usiwe na wasi wasi ndugu yangu.
Baada ya kuondoa vikwazo vyote hiyo ndiyo silaha aliyo nayo katika majadiliano.
Tunafahamu weakness yake ni kudai heshima bila yeye kuwa tayari kutoa.
Tutamvumilia ili taifa lisijetumbukia kule anakotaka lielekee. Tutasimama kidete kuonyesha umma wapi script ilipotofautina na ngano kamili.
Mohamed anafaham kuwa kuna hoja nzito zitakazo mwacha wazi katika maswali.

Kwa faida ya wanajamvi na wale wanaodhani anaonewa, nitarejea swali moja baada ya jingine kwa kutumia kitabu chake na maoni yake hapa ili kila mtu achague ''nafaka'' aitakayo.
 
Hapana mkuu, punguza jazba twende taratibu.

Tujadiliane kwakuheshimiana sisi sote ni watanzania jamani.

Haya maneno ikiwa umenikusudia mimi unanionea.

Hakika mimi ni mzee lakini sijaonyesha athari zozote za umri.

Mnaoandika matusi na kejeli ni nyie vijana.

Nimo katika jamvi Bwana Nyerere nisome umjue mzee wetu Mwalimu Julius Kambarage
Nyerere.
 

Unanionea kusema unanivumilia.
Mie sijatukana mtu.

Labda kama umekusudia unanivumilia kwa haya
ninayoandika.

Huenda yanachoma kwa kuwa takriban mengi hamkuwa
mnayajua.
 

Maneno hayo nilikuwa namwambia mdau mmoja hapo aliyekuwa amekujbu kwa lugha kali zaidi!
 

Kumjua baba yangu mzazi mzee Julius Nyerere kupitia wewe bila shaka huko aliko anaweza kunipa laani ya milele!

Nitakuwa simtendei haki kabisa tena ni dhihaka,

Yeye anizae mimi kisha nije nimjulie kwa Mohamed Said?? Hahaa hebu nitake radhi ya kikombe cha gahawa mzee Said.

Nilikuuliza maswali juu ya siasa za Mwalimu akiwa Makerere University na akiwa Misheni Pungu nilikuwa na maana kubwa sana, hasa nikizingatia maelezo yako ya awali kuwa Abdulwakil Sykes ndie aliyemwingiza katika siasa jambo ambalo sio kweli!
 

Kwa hapa Dar es Salaam baba yako wengi wamemjua kupita kwa Abdu Sykes.
Usikatae hilo nakusihi sana.

Bibi yako Bi Muyuga (sijui kama napatia sawa jina) alikuwa akishinda nyumbani
kwa Bi Mluguru biti Mussa mama yake Abdu.

Umepata kusikia ile "scare" iliyotokea nyumbani kwa Abdu Sykes Nyerere alipougua
ghafla baada ya kula chakula kwa Abdu?

Ikadhaniwa Nyerere kalishwa sumu?

Muulize mama kizaazaa cha siku hiyo.
Bibi yako hakamatiki analia mikono kichwani anazunguka nyumba
nzima.

Hii ilikuwa pale Aggrey Street.
Wazee wetu wana hisani kubwa baina yao.

Ninaposema kumjua ni kule kumjua katika wakati ule
wa kupigania uhuru.

Huko Ikulu na Msasani wazee wetu hawakuwapo.
Walibakia kule kule Kariakoo.
 

Heheehee umenikumbusha jambo muhimu sana,

Kisa hicho cha kuugua ghafla kwa Mzee Nyerere baada ya kula chakula kwa Abdu, kilidakwa na wapinzani wake kisiasa na kugeuza kuwa propagana ya eti mama alirubuniwa na wakoloni amlishe sumu Mwalimu Nyerere, kwakweli watanzania uongo haukuanza leo au jana, ni wa karne na karne!
 
Hapana Mohamed Said, hapa unachombeza tu katika jitihada za kutaka kuwakweza wazee wako...mwaka 1950 Raisi na kiongozi Mkuu wa TAA alikuwa Dr. Kyaruzi, sasa inaingia vipi akilini unapodai hivi;
Yaani juhudi zote za Dr. Kyaruzi ambazo ndizo zilisababisha hadi akapewa uhamisho huzitaji na badala yake sifa zote unazielekeza kwa katibu wake, Abdul. Hilo moja lakini la kushangaza zaidi ni pale unapotoa dai la huyo huyo katibu kumteua Raisi wake kwenye kamati, duh!


Tuendelee...
 
Kumjua baba yangu mzazi mzee Julius Nyerere kupitia wewe bila shaka huko aliko anaweza kunipa laani ya milele!

Nitakuwa simtendei haki kabisa tena ni dhihaka,

Yeye anizae mimi kisha nije nimjulie kwa Mohamed Said?
Mkuu Yericko, nimekuwa nikilisoma tuu hili jina humu jf, nikijua ni ni jina tuu la Nyerere kama mwanaukoo tuu, sikuwahi kumsikia mtoto yoyote wa Kambarage kwa jina hili, kama hutajali, na sio kwa kuingilia your "right to privacy", unaweza kutuliza kiu yangu?.
Pasco.
 
Mzee Mohamed Said, jee huyu Bi Mluguru biti Mussa mama yake Abdu, ndiye huyu aliyekuwa akiiishi pale Upanga, opposite Califonia Dreamer?.

Naomba utuhadithie hicho kisa cha Nyerere "kulishwa sumu!".
Pasco.
 

Hili ndilo tatizo la maandishi yako mzee mwenzangu; unatutaka tuamini maneno yako kwa vile umeyasema hata kama hakuna ushahidi wowote. Kwamba tukitaka ushahidi hasa wa kihistoria utasema "amini kama hutaki basi". Sasa hiyo siyo historia. Unapoandika historia you only write on that which you have evidence of.

Kwa kweli ni bahati mbaya sana Nyerere hakupata kueleza vipi aliingia TAA Dar es
Salaam na ndiyo maana nyie wenzangu msiojua historia ya TANU mnababaika na
mengi ambayo hamkupata kuyasikia wala kuyasoma kabla.

Lakini hili si kweli; katika kitabu cha aliyekuwa mke wa Du Bois (ambaye alimhoji Nyerere mwanzoni mwa miaka ya sitini pale Dar) aliandika hili. Na katika kitabu cha We Must Run While They Walk cha William Edget Smith Nyerere ameeleza kwa kirefu sana jinsi alivyoingia kwenye TAA.


Hebu soma hapa chini kisha tuendelee na mjadala:

Nilishasoma haya kwenye kitabu chako; unachotoa hapa kama ushahidi ni maandishi yako wewe na madai (assertions) zako wewe. Unataka tukubali kwa vile umezisema hata kama ulichoandika hakina ushahidi.

Sawa
Maisha ya Nyerere katika siasa yalianza hapo.

Lakini hili si kweli. Nyerere alianza siasa akiwa Makerere siyo Dar. Hata kusema 'uongozi wa kisiasa" Nyerere hakuanzia Dar.


Nyerere alikuwa mgeni na alikuwa hana historia ya kuongoza mapambano ya umma dhidi ya serikali ya kikoloni.

Hili pia si la kweli kwani alishaanza harakati hizi tangu akiwa shuleni (Tabora) mwanafunzi.

Ukoo wa Sykes ulikuwa unatambulikana katika siasa za Dar es Salaam kwa takriban robo karne.

Ndio lakini walikuwa wanafahamika kwa sababu kwanza walikuwa ni mamluki wa Ujerumani ambao walikuja kkupigana na watu weusi ili kumtetea Mjerumani na hawakuwa very fond na Waingereza. Na katika maandishi yako unaonesha kuwa kina Sykes walikuwa na resentment kukbwa sana kwa Waingereza hasa kwa vile Uingereza haikufanya kile kilichotarajiwa kwa ex German Soldiers.

Wengine (kama mimi) wanaweza kusema kuwa Abdule Sykes alimpinga Muingereza sana si kwa sababu ya maslahi ya Watu weusi wengine au Tanganyika bali zaidi wa sababu ya walivyomfanyia baba yake. Unaweza kulielewa hili katika maandishi yako kumhusu Sykes.



Tukubali kwa sekunde kuwa ni kweli waliongoza harakati dhidi ya ukoloni. Je ni ushahidi gani ulio nao ambapo kina Sykes waliongoza harakati dhidi ya Mjerumani? Au Mjerumani hakuwa Mkoloni?


Uongozi wa ndani wa TAA wa Abdulwahid, Ally, Dossa Aziz na Rupia ulikuwa tayari
umekwishaamua kumpa Nyerere urais wa chama.''

Once again ni madai yako haya (assertion) lakini nikiuliza kuna ushahidi gani kukwa kina Abdulwahid na wenzie walikuwa tayari wameshaamua kumpa Nyerere urais? utasema ni maneno uliyosimuliwa. Maana kama walikuwa tayari wamekubali kumpa kwanini Sykes bado aligombea wakati mgombea mwingine alijitoea kama nakumbuka vizuri?
 
Mkuu Mzee Mwanakijiji, sisi ambao hatukuwepo, tunajikuta tukiendelea kudanganywa na simulizi kama hizi za Maalim, Mohamed Said simply kwa sababu yeye ame document alichosimuliwa!, kama amedangaywa na hao wasimulizi wake, na yeye akaishia kutudanya sisi kwa kuamini uwongo ule kuwa ndio ukweli, historia itakuja kuishia kubaki na records za uwongo huo kuonekana ndio ukweli wenyewe simply because ukweli halisi, "was not told!, was not documented!". Ikumbukwe tuu kuwa "half truth" huonekana kama ndio "full truth" as long as the other half is never told!, Hiyo half truth can only be defeated if the other half is told and that is the only way of getting "the full truth!". Mohamed Said played his part, got his "half" toka simulizi za babu zake, lets get the other "half" from other nayo iwe compiled, vinginevyo hiyo "half" ya wazee wake Mohamed Said ndio itakayokuja kuishia kuonekana kama ndio the only "full truth!".

Nakumbuka kuna wakati mwandishi Kanyama Chiume (Rip). alipewa kazi ya kuandika historia ya Tanu, sijui iliishia wapi maana hata historia yetu tuu, tulimtegemea Mmalawi!. Kwa nini waandishi kama nyinyi, msijitolee kui compile historia ya mapambao toka machapisho mbalimbali, ikaandikwa kwenye kitabu na kitabu hicho kichapishwe ili ku defeat upotoshwaji kama huu unaofanywa na Maalim Mohamed Said, as of now, Maalim yuko right ku preserve historia ya Wazazi wake kama alivyosimuliwa, na mimi naendelea kukiri wazi kuwa kwa vile napenda simulizi za hadithi, naendelea ku enjoy simulizi za hadithi za Mohamed Said.
Pasco.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…