Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

Picha ya Waasisi wa TANU ndiyo hiyo lakini hii imechakachuliwa.
Kisa chake nitakieleza Insha Allah siku nyingine.

Kassela Bantu amepachika picha yake kati ya Abdu na Chief Kunambi.

Hiyo ofisi ya TAA ndiyo hilo jengo lililojengwa na baba yake Abdu Sykes Mzee Kleist.


View attachment 79966

Kumbukumbu nzuri masiku yamepita mengi hebu tutajie majina ya hao viongozi wa TANU.
 
Naona ujanja wako ni kum frustrate mtu unapojibu hoja zake ili asikuulize tena. Jaribu kukaa chini basi ujibu kiutu uzima kama ulivyomuamba aandike maswali yake. Nimesikia uzee ukishika kasi saa nyingine akili zinakuwa kama za kitotokitoto hivi.

Kaka! Ulichoandika ni tusi hata kwa wazee wako.
 
Wanajamvi, hapo nyuma kidogo nimechokoza tu mjadala kwa kuuliza maswali mawili nayo ni;


Kama kawaida bingwa wa hadithi anayejulikana kama Mohamed Said, haraka haraka, akadakia kwa kutoa majibu na nanukuu tu sehemu ya simulizi ambazo anadai alipewa na wazee wake wa Gerezani.


Hilo hapo juu ndilo jibu la Mohamed Said kuhusu viongozi wakuu walioiongoza AA toka kuasisiwa kwake mwaka 1929 hadi ilipobadilika na kuwa TAA na badaye kuundwa TANU mwaka 1954. Kwa hilo jibu peke yake Mohamed Said anathibitisha hila zake za kichochezi na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika (na Zanzibar?) kama mtoa hii mada alivyoainisha.

Je ni kitu gani kimejificha katika hili jibu la Mohamed Said? Ukilisoma hili jibu kwa haraka haraka utadhani AA haikuwa na Kiongozi Mkuu. Kwa nini hataji kuwa AA ilikuwa na Raisi aliyeiongoza? AA haikuwa kikao kama cha wanywa kahawa ambapo watu wanapasishana kikombe bila kujali "protocol" yoyote. Je huyo Kleist anayetajwa mara mbili, ndiye alikuwa kiongozi mkuu wa AA?

Mwalimu Cecil Matola, myao ambaye nyumbani kwake ndiko kulikofanyika mkutano wa kwanza wa TAA yeye akiwa ndiye Raisi wa kwanza, mbona anatajwa mwisho kama vile hana umuhimu wowote? Je baada ya kufariki kwake mwaka 1933, kwa nini AA ilizorota na hakuweza kupatikana kiongozi mwingine wa kuiongoza AA hadi alipoingia kijana msomi kutoka Makerere, Dr. Vedasto Kyaruzi, Raisi wa kwanza wa TAA?

Dr. Kyaruzi aliiongoza TAA kwa miaka miwili hadi 1951 na hata alipohamishiwa mikoani na kushindwa kumudu kuiongoza TAA kwa nini hakupatikana Kiongozi mwingine hadi mwaka 1953 alipoingia kijana mwingine msomi kutoka Edinburgh, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere? Kwa nini wazee wa Mohamed ambao anadai ndio walikuwa vinara wa mwamko wasimchague mmoja wao kuwa Raisi?

Je ni kweli kuwa chombo cha kwanza kilichowaunganisha waafrika kilianzia Dar es Salaam? Vipi Msomi Martin Kayamba aliyeanzisha TTACSA (Tanganyika Territory African Civil Service Association) huko Tanga mwaka 1922? Je si kweli kuwa TAA iliasisiwa kwa kufuata unyayo na misingi iliyoanzishwa na TTACSA? Ni TTACSA iliyowawezesha wafanya kazi kukutana pamoja bila kubaguana kikabila, kirangi wala kidini.

Tuendelee na mjadala...

Ukweli ni kitu kizuri sana hasa katika historia,

Mohamed Said ameukwepa ukweli katika kitabu chake,

Nimejaribu kueleza kwakifupi tu pale juu kuwa kundi la wale vijana wakariakoo lilikabiliwa na changamoto kadhaa, Elimu na Woga.

Dr Kyaruzi aliisimamia TAA kwa weledi sana, lakini baada ya kuondoka iliyumba yaani waliokuwepo hawakuwa na uwezo wakuongoza mpaka mpigania ukombozi mwingine Julius Nyerere alipokuja kushika hatamu
 
Wanajamvi, hapo nyuma kidogo nimechokoza tu mjadala kwa kuuliza maswali mawili nayo ni;


Kama kawaida bingwa wa hadithi anayejulikana kama Mohamed Said, haraka haraka, akadakia kwa kutoa majibu na nanukuu tu sehemu ya simulizi ambazo anadai alipewa na wazee wake wa Gerezani.


Hilo hapo juu ndilo jibu la Mohamed Said kuhusu viongozi wakuu walioiongoza AA toka kuasisiwa kwake mwaka 1929 hadi ilipobadilika na kuwa TAA na badaye kuundwa TANU mwaka 1954. Kwa hilo jibu peke yake Mohamed Said anathibitisha hila zake za kichochezi na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika (na Zanzibar?) kama mtoa hii mada alivyoainisha.

Je ni kitu gani kimejificha katika hili jibu la Mohamed Said? Ukilisoma hili jibu kwa haraka haraka utadhani AA haikuwa na Kiongozi Mkuu. Kwa nini hataji kuwa AA ilikuwa na Raisi aliyeiongoza? AA haikuwa kikao kama cha wanywa kahawa ambapo watu wanapasishana kikombe bila kujali "protocol" yoyote. Je huyo Kleist anayetajwa mara mbili, ndiye alikuwa kiongozi mkuu wa AA?

Mwalimu Cecil Matola, myao ambaye nyumbani kwake ndiko kulikofanyika mkutano wa kwanza wa TAA yeye akiwa ndiye Raisi wa kwanza, mbona anatajwa mwisho kama vile hana umuhimu wowote? Je baada ya kufariki kwake mwaka 1933, kwa nini AA ilizorota na hakuweza kupatikana kiongozi mwingine wa kuiongoza AA hadi alipoingia kijana msomi kutoka Makerere, Dr. Vedasto Kyaruzi, Raisi wa kwanza wa TAA?

Dr. Kyaruzi aliiongoza TAA kwa miaka miwili hadi 1951 na hata alipohamishiwa mikoani na kushindwa kumudu kuiongoza TAA kwa nini hakupatikana Kiongozi mwingine hadi mwaka 1953 alipoingia kijana mwingine msomi kutoka Edinburgh, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere? Kwa nini wazee wa Mohamed ambao anadai ndio walikuwa vinara wa mwamko wasimchague mmoja wao kuwa Raisi?

Je ni kweli kuwa chombo cha kwanza kilichowaunganisha waafrika kilianzia Dar es Salaam? Vipi Msomi Martin Kayamba aliyeanzisha TTACSA (Tanganyika Territory African Civil Service Association) huko Tanga mwaka 1922? Je si kweli kuwa TAA iliasisiwa kwa kufuata unyayo na misingi iliyoanzishwa na TTACSA? Ni TTACSA iliyowawezesha wafanya kazi kukutana pamoja bila kubaguana kikabila, kirangi wala kidini.

Tuendelee na mjadala...

Unachanganya habari.
Unaandika na hamaki.

Hapo ndipo zinaingia kejeli za kahawa nk. nk.
Huu ni mjadala tu kama nimekosea mahali unasema tu kiungwana.

Kleist alikuwa na kipaji cha hali ya juu katika uongozi.

Licha ya kuwa katibu muasisi wa AA mkwaka 1933 alikuwa katibu muasisi
wa Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika (Umoja wa Waislam wa Tanganyika)
Mzee bin Sudi akiwa rais.

Matola alikuwa rais kweli lakini mambo yote akifanya Kleist kwa kuwa Kleist
alikuwa kijana tajiri.

Hii ilimwezesha kufanya mambo mengi sana kwa urahisi.

Cecil Matola alikuwa kiongozi wa African Association na alipoondoka akaingia
Mzee bin Sudi kama rais.

African Association ilizorota mwaka 1933 baada ya kutokea ugomvi kati ya Erika Fiah
na Kleist.

Kleist alijitoa katika uongozi.

Ipo barua aliyoandika Mzee bin Sudi aliyoanza kwa Bismillah Rahman Rahim.

Barua hii Mzee bin Sudi alimwandikia Kleist kumbembeleza arudi AA wakiongoze
chama.

Habari hizi zipo katika mswada wa maisha ya Kleist.

Habari hii inaweza halikadhalika kupatika katika Illife (Modern Tanzanians)
''The Townsman Kleist'' Sykes kama alivyoandika mjukuu wake.

Dr. Kyaruzi aliingia TAA na Abdu Sykes 1950 na hakumaliza hata mwaka
Waingereza wakampa uhamisho Kingolwira Prison kisha Nzega.

Sababu ya uhamisho wa Dr. Kyaruzi ni ile TAA Political Sub Commttee waliyounda
wajumbe wakiwa Sheikh Hassan bin Amir, Abdu Sykes, Dr Kyaruzi, Said Chaurembo,
John Rupia, Hamza Mwapachu na Steven Mhando.

Kamati hii ilimchukua mwanasheria wa Kibyamuda Earle Seaton kama mshauri.
Seaton alikuwa rafiki yake Abdu Sykes.

Habari ni nyingi nisimame hapa kwa sasa.
Kwa ufupi TAA ikawa inafanya kazi kama chama cha siasa halisi.

Huo ndiyo ukawa ndiyo mwisho wake wa uongozi wake kama rais wa TAA.
kuanzia 1951 Abdu Sykes akawa Acting President na Secretary na 1952
Abdu akawa rais wa TAA.

Kuhusu Martin Kayamba nakusihi tufanye subra tutamzungumza.
Kwanza hebu linganisha haya niliyoandika hapa na hayo uliyoandika wewe.

Tukimaliza Insha Allah tutakuja kwa Martin Kayamba Mdumi.

Tuendelee Insha Allah na mjadala.
 
Naona ujanja wako ni kum frustrate mtu unapojibu hoja zake ili asikuulize tena. Jaribu kukaa chini basi ujibu kiutu uzima kama ulivyomuamba aandike maswali yake. Nimesikia uzee ukishika kasi saa nyingine akili zinakuwa kama za kitotokitoto hivi.

Hapana mkuu, punguza jazba twende taratibu.

Tujadiliane kwakuheshimiana sisi sote ni watanzania jamani.
 
Ukweli ni kitu kizuri sana hasa katika historia,

Mohamed Said ameukwepa ukweli katika kitabu chake,

Nimejaribu kueleza kwakifupi tu pale juu kuwa kundi la wale vijana wakariakoo lilikabiliwa na changamoto kadhaa, Elimu na Woga.

Dr Kyaruzi aliisimamia TAA kwa weledi sana, lakini baada ya kuondoka iliyumba yaani waliokuwepo hawakuwa na uwezo wakuongoza mpaka mpigania ukombozi mwingine Julius Nyerere alipokuja kushika hatamu

Hapana TAA baada ya 1950 haikupata kusinzia.
Nakuwekea kitu hapa kutoka kitabu changu ''The Life and Times of Abdulwahid Sykes...'':

[TABLE="class: MsoNormalTable"]
[TR]
[TD] TAA Political Subcommittee, 1950
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD] No records exist which show that the African Association had a clear official policy or programme on the country's political situation.

To understand the direction of African politics as they appeared at that time one need to observe the behaviour of the leadership and its reaction to different African problems.

Abdulwahid's first move was to form what was known as TAA Political Subcommittee [1] comprising himself as secretary; Sheikh Hassan bin Amir as the Mufti of Tanganyika; Dr Kyaruzi; Mwapachu; Said Chaurembo who was the liwali at Kariakoo local court; John Rupia and Stephen Mhando. The task given to this committee was to deal with political issues in the country.

The creation of this committee was a turning point in the history of organised politics in colonial Tanganyika.

Throughout the entire twenty-five years of its existence, the African Association had functioned under a non-political constitution. For the first time, in 1950, TAA under new leadership gave itself political status, not by changing the existing constitution, but by forming a political committee within the Association.
[/TD]
[/TR]
[/TABLE]


[1] Annual Report of the Secretary of Tanganyika African Association, 7 January, 1951. Sykes' Papers.

Hayo unayosema ya kuwabeza wazee wangu ni historia hiyo ya Kivukoni iliyoanza na kumalizikia na Nyerere na wakija wengine kuandika ukweli magazeti yanakusanywa na kuchomwa moto. Haya ninayosema mimi ndivyo mambo yalivyokuwa lakini simlazimishi mtu aniamini. Wanaukumbi nawaachia wasome na waamue nani mkweli. Hapo juu nimeandika kwa mukhtasari tu yaliyofanywa na TAA katika uongozi wa Abdu Sykes.
 
Naona ujanja wako ni kum frustrate mtu unapojibu hoja zake ili asikuulize tena. Jaribu kukaa chini basi ujibu kiutu uzima kama ulivyomuamba aandike maswali yake. Nimesikia uzee ukishika kasi saa nyingine akili zinakuwa kama za kitotokitoto hivi.
Sweke 34, wala usiwe na wasi wasi ndugu yangu.
Baada ya kuondoa vikwazo vyote hiyo ndiyo silaha aliyo nayo katika majadiliano.
Tunafahamu weakness yake ni kudai heshima bila yeye kuwa tayari kutoa.
Tutamvumilia ili taifa lisijetumbukia kule anakotaka lielekee. Tutasimama kidete kuonyesha umma wapi script ilipotofautina na ngano kamili.
Mohamed anafaham kuwa kuna hoja nzito zitakazo mwacha wazi katika maswali.

Kwa faida ya wanajamvi na wale wanaodhani anaonewa, nitarejea swali moja baada ya jingine kwa kutumia kitabu chake na maoni yake hapa ili kila mtu achague ''nafaka'' aitakayo.
 
Hapana mkuu, punguza jazba twende taratibu.

Tujadiliane kwakuheshimiana sisi sote ni watanzania jamani.

Haya maneno ikiwa umenikusudia mimi unanionea.

Hakika mimi ni mzee lakini sijaonyesha athari zozote za umri.

Mnaoandika matusi na kejeli ni nyie vijana.

Nimo katika jamvi Bwana Nyerere nisome umjue mzee wetu Mwalimu Julius Kambarage
Nyerere.
 
Sweke 34, wala usiwe na wasi wasi ndugu yangu.
Baada ya kuondoa vikwazo vyote hiyo ndiyo silaha aliyo nayo katika majadiliano.
Tunafahamu weakness yake ni kudai heshima bila yeye kuwa tayari kutoa.
Tutamvumilia ili taifa lisijetumbukia kule anakotaka lielekee. Tutasimama kidete kuonyesha umma wapi script ilipotofautina na ngano kamili.
Mohamed anafaham kuwa kuna hoja nzito zitakazo mwacha wazi katika maswali.

Kwa faida ya wanajamvi na wale wanaodhani anaonewa, nitarejea swali moja baada ya jingine kwa kutumia kitabu chake na maoni yake hapa ili kila mtu achague ''nafaka'' aitakayo.

Unanionea kusema unanivumilia.
Mie sijatukana mtu.

Labda kama umekusudia unanivumilia kwa haya
ninayoandika.

Huenda yanachoma kwa kuwa takriban mengi hamkuwa
mnayajua.
 
Haya maneno ikiwa umenikusudia mimi unanionea.

Hakika mimi ni mzee lakini sijaonyesha athari zozote za umri.

Mnaoandika matusi na kejeli ni nyie vijana.

Nimo katika jamvi Bwana Nyerere nisome umjue mzee wetu Mwalimu Julius Kambarage
Nyerere.

Maneno hayo nilikuwa namwambia mdau mmoja hapo aliyekuwa amekujbu kwa lugha kali zaidi!
 
Haya maneno ikiwa umenikusudia mimi unanionea.

Hakika mimi ni mzee lakini sijaonyesha athari zozote za umri.

Mnaoandika matusi na kejeli ni nyie vijana.

Nimo katika jamvi Bwana Nyerere nisome umjue mzee wetu Mwalimu Julius Kambarage
Nyerere.

Kumjua baba yangu mzazi mzee Julius Nyerere kupitia wewe bila shaka huko aliko anaweza kunipa laani ya milele!

Nitakuwa simtendei haki kabisa tena ni dhihaka,

Yeye anizae mimi kisha nije nimjulie kwa Mohamed Said?? Hahaa hebu nitake radhi ya kikombe cha gahawa mzee Said.

Nilikuuliza maswali juu ya siasa za Mwalimu akiwa Makerere University na akiwa Misheni Pungu nilikuwa na maana kubwa sana, hasa nikizingatia maelezo yako ya awali kuwa Abdulwakil Sykes ndie aliyemwingiza katika siasa jambo ambalo sio kweli!
 
Kumjua baba yangu mzazi mzee Julius Nyerere kupitia wewe bila shaka huko aliko anaweza kunipa laani ya milele!

Nitakuwa simtendei haki kabisa tena ni dhihaka,

Yeye anizae mimi kisha nije nimjulie kwa Mohamed Said?? Hahaa hebu nitake radhi ya kikombe cha gahawa mzee Said.

Nilikuuliza maswali juu ya siasa za Mwalimu akiwa Makerere University na akiwa Misheni Pungu nilikuwa na maana kubwa sana, hasa nikizingatia maelezo yako ya awali kuwa Abdulwakil Sykes ndie aliyemwingiza katika siasa jambo ambalo sio kweli!

Kwa hapa Dar es Salaam baba yako wengi wamemjua kupita kwa Abdu Sykes.
Usikatae hilo nakusihi sana.

Bibi yako Bi Muyuga (sijui kama napatia sawa jina) alikuwa akishinda nyumbani
kwa Bi Mluguru biti Mussa mama yake Abdu.

Umepata kusikia ile "scare" iliyotokea nyumbani kwa Abdu Sykes Nyerere alipougua
ghafla baada ya kula chakula kwa Abdu?

Ikadhaniwa Nyerere kalishwa sumu?

Muulize mama kizaazaa cha siku hiyo.
Bibi yako hakamatiki analia mikono kichwani anazunguka nyumba
nzima.

Hii ilikuwa pale Aggrey Street.
Wazee wetu wana hisani kubwa baina yao.

Ninaposema kumjua ni kule kumjua katika wakati ule
wa kupigania uhuru.

Huko Ikulu na Msasani wazee wetu hawakuwapo.
Walibakia kule kule Kariakoo.
 
Kwa hapa Dar es Salaam baba yako wengi wamemjua kupita kwa Abdu Sykes.
Usikatae hilo nakusihi sana.

Bibi yako Bi Muyuga (sijui kama napatia sawa jina) alikuwa akishinda nyumbani
kwa Bi Mluguru biti Mussa mama yake Abdu.

Umepata kusikia ile "scare" iliyotokea nyumbani kwa Abdu Sykes Nyerere alipougua
ghafla baada ya kula chakula kwa Abdu?

Ikadhaniwa Nyerere kalishwa sumu?

Muulize mama kizaazaa cha siku hiyo.
Bibi yako hakamatiki analia mikono kichwani anazunguka nyumba
nzima.

Hii ilikuwa pale Aggrey Street.
Wazee wetu wana hisani kubwa baina yao.

Ninaposema kumjua ni kule kumjua katika wakati ule
wa kupigania uhuru.

Huko Ikulu na Msasani wazee wetu hawakuwapo.
Walibakia kule kule Kariakoo.

Heheehee umenikumbusha jambo muhimu sana,

Kisa hicho cha kuugua ghafla kwa Mzee Nyerere baada ya kula chakula kwa Abdu, kilidakwa na wapinzani wake kisiasa na kugeuza kuwa propagana ya eti mama alirubuniwa na wakoloni amlishe sumu Mwalimu Nyerere, kwakweli watanzania uongo haukuanza leo au jana, ni wa karne na karne!
 
Hapana TAA baada ya 1950 haikupata kusinzia...
Abdulwahid's first move was to form what was known as TAA Political Subcommittee [1] comprising himself as secretary; Sheikh Hassan bin Amir as the Mufti of Tanganyika; Dr Kyaruzi; Mwapachu; Said Chaurembo who was the liwali at Kariakoo local court; John Rupia and Stephen Mhando. The task given to this committee was to deal with political issues in the country.
Hapana Mohamed Said, hapa unachombeza tu katika jitihada za kutaka kuwakweza wazee wako...mwaka 1950 Raisi na kiongozi Mkuu wa TAA alikuwa Dr. Kyaruzi, sasa inaingia vipi akilini unapodai hivi;
Abdulwahid's first move was to form what was known as TAA Political Subcommittee comprising himself as secretary; Sheikh Hassan bin Amir as the Mufti of Tanganyika; Dr Kyaruzi; Mwapachu; Said Chaurembo who was the liwali at Kariakoo local court; John Rupia and Stephen Mhando.
Yaani juhudi zote za Dr. Kyaruzi ambazo ndizo zilisababisha hadi akapewa uhamisho huzitaji na badala yake sifa zote unazielekeza kwa katibu wake, Abdul. Hilo moja lakini la kushangaza zaidi ni pale unapotoa dai la huyo huyo katibu kumteua Raisi wake kwenye kamati, duh!
UQAAAABJRU5ErkJggg==


Tuendelee...
 
Kumjua baba yangu mzazi mzee Julius Nyerere kupitia wewe bila shaka huko aliko anaweza kunipa laani ya milele!

Nitakuwa simtendei haki kabisa tena ni dhihaka,

Yeye anizae mimi kisha nije nimjulie kwa Mohamed Said?
Mkuu Yericko, nimekuwa nikilisoma tuu hili jina humu jf, nikijua ni ni jina tuu la Nyerere kama mwanaukoo tuu, sikuwahi kumsikia mtoto yoyote wa Kambarage kwa jina hili, kama hutajali, na sio kwa kuingilia your "right to privacy", unaweza kutuliza kiu yangu?.
Pasco.
 
Bibi yako Bi Muyuga (sijui kama napatia sawa jina) alikuwa akishinda nyumbani
kwa Bi Mluguru biti Mussa mama yake Abdu.

Umepata kusikia ile "scare" iliyotokea nyumbani kwa Abdu Sykes Nyerere alipougua
ghafla baada ya kula chakula kwa Abdu?

Ikadhaniwa Nyerere kalishwa sumu?

Muulize mama kizaazaa cha siku hiyo.
Bibi yako hakamatiki analia mikono kichwani anazunguka nyumba
nzima.

Hii ilikuwa pale Aggrey Street.
Wazee wetu wana hisani kubwa baina yao.
Mzee Mohamed Said, jee huyu Bi Mluguru biti Mussa mama yake Abdu, ndiye huyu aliyekuwa akiiishi pale Upanga, opposite Califonia Dreamer?.

Naomba utuhadithie hicho kisa cha Nyerere "kulishwa sumu!".
Pasco.
 
Ungesoma kitabu changu usingesema, ''Sykes alikataliwa na wazee wenzake.''
Kwanza Abdu hakuwa mzee alikuwa na umri wa miaka 29 na Nyerere alikuwa
na miaka 31.

Uongozi wa ndani wa TAA uliamua kumpa uongozi Nyerere na aliyeongoza kampeni
ya kuchaguliwa Nyerere ni Abdu.

Hili ndilo tatizo la maandishi yako mzee mwenzangu; unatutaka tuamini maneno yako kwa vile umeyasema hata kama hakuna ushahidi wowote. Kwamba tukitaka ushahidi hasa wa kihistoria utasema "amini kama hutaki basi". Sasa hiyo siyo historia. Unapoandika historia you only write on that which you have evidence of.

Kwa kweli ni bahati mbaya sana Nyerere hakupata kueleza vipi aliingia TAA Dar es
Salaam na ndiyo maana nyie wenzangu msiojua historia ya TANU mnababaika na
mengi ambayo hamkupata kuyasikia wala kuyasoma kabla.

Lakini hili si kweli; katika kitabu cha aliyekuwa mke wa Du Bois (ambaye alimhoji Nyerere mwanzoni mwa miaka ya sitini pale Dar) aliandika hili. Na katika kitabu cha We Must Run While They Walk cha William Edget Smith Nyerere ameeleza kwa kirefu sana jinsi alivyoingia kwenye TAA.


Hebu soma hapa chini kisha tuendelee na mjadala:

Nilishasoma haya kwenye kitabu chako; unachotoa hapa kama ushahidi ni maandishi yako wewe na madai (assertions) zako wewe. Unataka tukubali kwa vile umezisema hata kama ulichoandika hakina ushahidi.
''Uchaguzi baina ya aliyekuwa rais wa TAA, Abdulwahid na mwalimu wa shule asiyefahamika vyema pale mjini, Julius Nyerere,
ulifanyika kwenye Ukumbi wa Arnatouglo tarehe 17 Aprili, 1953.

Nje ya uongozi wa TAA ambao ulimpendekeza kugombea nafasi hiyo, Nyerere alikuwa mgeni kabisa kwa wote aliokuwa akiwaomba
kura zao.

Sawa
Maisha ya Nyerere katika siasa yalianza hapo.

Lakini hili si kweli. Nyerere alianza siasa akiwa Makerere siyo Dar. Hata kusema 'uongozi wa kisiasa" Nyerere hakuanzia Dar.


Nyerere alikuwa mgeni na alikuwa hana historia ya kuongoza mapambano ya umma dhidi ya serikali ya kikoloni.

Hili pia si la kweli kwani alishaanza harakati hizi tangu akiwa shuleni (Tabora) mwanafunzi.

Ukoo wa Sykes ulikuwa unatambulikana katika siasa za Dar es Salaam kwa takriban robo karne.

Ndio lakini walikuwa wanafahamika kwa sababu kwanza walikuwa ni mamluki wa Ujerumani ambao walikuja kkupigana na watu weusi ili kumtetea Mjerumani na hawakuwa very fond na Waingereza. Na katika maandishi yako unaonesha kuwa kina Sykes walikuwa na resentment kukbwa sana kwa Waingereza hasa kwa vile Uingereza haikufanya kile kilichotarajiwa kwa ex German Soldiers.

Wengine (kama mimi) wanaweza kusema kuwa Abdule Sykes alimpinga Muingereza sana si kwa sababu ya maslahi ya Watu weusi wengine au Tanganyika bali zaidi wa sababu ya walivyomfanyia baba yake. Unaweza kulielewa hili katika maandishi yako kumhusu Sykes.


Ukoo huu ndiyo ulioanzisha na kuongoza vyama vyote viwili, African Association na Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika.

Ukoo wa Abdulwahid, mtoto wa Kleist Sykes ulikuwa unafahamika kwa kuongoza mapambano dhidi ya serikali.

Ushahidi wa haya ulikuwa unapatikana katika nyaraka kati ya ukoo huu na serikali ya kikoloni.

Katika kipindi cha miaka zaidi ya ishirini, serikali kwa nyakati tofauti, kati ya mwaka 1929 hadi 1953 ilikuwa na barua za Kleist Sykes na
za mwanae Abdulwahid wakiwa viongozi wa African Association kuhusu madhila tofauti yaliyokuwa yakiwakabili wananchi. [1]

Tukubali kwa sekunde kuwa ni kweli waliongoza harakati dhidi ya ukoloni. Je ni ushahidi gani ulio nao ambapo kina Sykes waliongoza harakati dhidi ya Mjerumani? Au Mjerumani hakuwa Mkoloni?


Uongozi wa ndani wa TAA wa Abdulwahid, Ally, Dossa Aziz na Rupia ulikuwa tayari
umekwishaamua kumpa Nyerere urais wa chama.''

Once again ni madai yako haya (assertion) lakini nikiuliza kuna ushahidi gani kukwa kina Abdulwahid na wenzie walikuwa tayari wameshaamua kumpa Nyerere urais? utasema ni maneno uliyosimuliwa. Maana kama walikuwa tayari wamekubali kumpa kwanini Sykes bado aligombea wakati mgombea mwingine alijitoea kama nakumbuka vizuri?
 
Hili ndilo tatizo la maandishi yako mzee mwenzangu; unatutaka tuamini maneno yako kwa vile umeyasema hata kama hakuna ushahidi wowote. Kwamba tukitaka ushahidi hasa wa kihistoria utasema "amini kama hutaki basi". Sasa hiyo siyo historia. Unapoandika historia you only write on that which you have evidence of.
Lakini hili si kweli; katika kitabu cha aliyekuwa mke wa Du Bois (ambaye alimhoji Nyerere mwanzoni mwa miaka ya sitini pale Dar) aliandika hili. Na katika kitabu cha We Must Run While They Walk cha William Edget Smith Nyerere ameeleza kwa kirefu sana jinsi alivyoingia kwenye TAA.
Mkuu Mzee Mwanakijiji, sisi ambao hatukuwepo, tunajikuta tukiendelea kudanganywa na simulizi kama hizi za Maalim, Mohamed Said simply kwa sababu yeye ame document alichosimuliwa!, kama amedangaywa na hao wasimulizi wake, na yeye akaishia kutudanya sisi kwa kuamini uwongo ule kuwa ndio ukweli, historia itakuja kuishia kubaki na records za uwongo huo kuonekana ndio ukweli wenyewe simply because ukweli halisi, "was not told!, was not documented!". Ikumbukwe tuu kuwa "half truth" huonekana kama ndio "full truth" as long as the other half is never told!, Hiyo half truth can only be defeated if the other half is told and that is the only way of getting "the full truth!". Mohamed Said played his part, got his "half" toka simulizi za babu zake, lets get the other "half" from other nayo iwe compiled, vinginevyo hiyo "half" ya wazee wake Mohamed Said ndio itakayokuja kuishia kuonekana kama ndio the only "full truth!".

Nakumbuka kuna wakati mwandishi Kanyama Chiume (Rip). alipewa kazi ya kuandika historia ya Tanu, sijui iliishia wapi maana hata historia yetu tuu, tulimtegemea Mmalawi!. Kwa nini waandishi kama nyinyi, msijitolee kui compile historia ya mapambao toka machapisho mbalimbali, ikaandikwa kwenye kitabu na kitabu hicho kichapishwe ili ku defeat upotoshwaji kama huu unaofanywa na Maalim Mohamed Said, as of now, Maalim yuko right ku preserve historia ya Wazazi wake kama alivyosimuliwa, na mimi naendelea kukiri wazi kuwa kwa vile napenda simulizi za hadithi, naendelea ku enjoy simulizi za hadithi za Mohamed Said.
Pasco.
 
Back
Top Bottom