Barubaru
JF-Expert Member
- Apr 6, 2009
- 7,161
- 2,324
Jasusi,
Tanzania ndipo ilipo hapo hivi sasa.
Hakuna anaemtakia kheri mwenzake.
Tunatazamana kwa jicho baya sana.
Inatisha na inasikitisha.
Al akhiy Mohamed Said.
kama wiki iliyopita ungetazama BBC walionyesha live makadinari wa Kikatoliki wakiingia vatican na kuanza kwa zoezi lao la kumchagua kiongozi wao ambaye ni Papa.
kabla kuanza kwa Zoezi hilo walianza na majadiliano maalum ya ya kUJADILI MAHUSIANO YAO YA KANISA NA WAISLAM. Lakin hilo huko Tanzania hususan wenzenu wa upande wa pili hawalioni hilo na kutaka kuendeleza dhulma kama walivyozoea na kuzoeshwa na Serikali.
jiulize suala dogo tu. Kwanini kuuwawa padri Znz wameleta FBI , kwanini kuteswa kwa mwandishi wa habari KIBANDA na wengi wengi wengine wasiojulikana na wanaojulikana kama Dr Ulimboka wasilete FBI kuchunguza pia?