Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

Nimeziona,hata hivyo hili lisiwe nongwa.Unajuwa Mohammed Said ni binadamu hivyo hata angekuwa madhubuti kiasi gani hawezi kufanya kazi isiyokuwa na kasoro za hapa na pale.

Pamoja na hivyo hizi data alizotoa ilikuwa ni kisaidizi tu ya historia aliyokuwa anaandika.Maudhui makuu ni matukio ya kihistoria yaliyokuwa yametokea kabla na baada ya uhuru.Wahusika wakuu walikuwa ni Nyerere na wapigania uhuru aliokuja kuwapiga teke.Ukirudi kwenye msingi wa uzi huu na historia basi hata kama ukikutana na kasoro za hapa na pale atakuwa ametoa source za kutosha ambazo atakayeita ni ngano au ni uchochezi basi huyo ni mpuuzi wa mwisho.Upuuzi wake wala hautozuia wasomaji wengine kuamini historia hiyo iliyokuwa haikujulikana kabla.
Huu utiiifu wa kanuni za kitafiti naona mmezifanya kuwa ni jambo kubwa sana kiasi ya kutaka kututoa kwenye ajenda.

Well hatutakiwi kuexcuse makosa hata kidogo. Kwenye madai makubwa no room for mistakes....

Anyway mi nasubiria official jibu (kwenye Hili) kutoka kwa muhusika......
 
Naam ndugu yangu! Lakini ngoja tuwasaidie wale ambao wameakuwa wakiamini huu utafiti uchwara wa WARSHA mbele kidogo:

Hoja nzima ya "dhulma" katika elimu inatokana na "utafiti" wa chuo kikuu kimoja tu katika Tanzania nzima. Na katika hicho chuo ni baadhi ya faculties tu zimeangaliwa. Na katika hizo ambazo hazikuangaliwa ni zile ambazo ni muhimu kwa namna ya pekee - Medicine, Kilimo na Veterinary Science. Na ikumbukwe huko kote kilichoangaliwa na majina tu. Yaani, "watafiti" wakachukua kitabu cha majina wakaanza kuangalia nani ana jina la Kikristu na nani ana jina la Kiislamu. Ambaye hakuwa na jina linaloashiria dini yake basi aliwekwa kwenye "wengine" na hata wale ambao wenye majina 'neutral' nao waliwekwa pembeni. Majina kama "Neema, Baraka, Furaha, Daudi" yanawekwa pembeni. Hili tatizo la kwanza - na ni dogo.

Tatizo la pili la "utafiti" wakina Mohammed Said na kundi lake ni kuwa unajaribu kuonesha 'systematic discrimination" katika mfumo wa elimu. Bw. Said hapo nyuma akijinukuu mwenyewe anasema hivi-kwa ujasiri wa kisomi:



Kimsingi anadai kuwa kwa kuangalia 'utafiti' wao huo walifikia hitimisho kuwa kulikuwa na 'sytem' ambayo ilikuwa 'discriminatory to Muslim Youths'. Sasa mtu anaweza kufikia hitimisho hilo kama amefanya utafiti wakutosha - wenye kuhusisha sample ya kutosha na yenye perimeters zinazoeleweka. Kwa kuangalia majina kwenye kitabu peke yake inatosha kweli?

Lakini zaidi la kuudhi ni kweli kwa kuangalia UDSM peke yake tu anaweza kufikia hitimisho la kuweza kuextrapolate his findings to the nation as a whole starting with Ministry of Education?

Mtu yeyote anayesoma takwimu na hata wanaojifunza Research 101 cha kwanza kabisa ni kuwa na sample ya kutosha. Lakini siyo sample tu bali kuna kitu muhimu sana ambacho ni "random sample". Ili uweze kupata matokeo ya kutosha katika utafiti wenye lengo la kupata takwimu fulani basi sample yako ni lazima iwe representative ya general population lakini pia iwe as random as possible. Na pale ambapo unataka kuonesha 'systematic discrimination' kama watu wa WARSHA walivyotaka kufanya basi huwezi kutumia chuo cha elimu ya juu kimoja.

Ili angalau tuweze kupima matokeo yale ni vizuri tungejua mgawanyo (distribution) ya Wakristu, Waislamu na Wengine katika elimu ya juu katika miaka hiyo ilikuwaje:

Chuo cha Uongozi Mzumbe - kilikuwa na intake ya WWW wangapi?
Chuo cha Kilimo Uyole -
Chuo cha Kilimo Morogoro (baadaye Sokoine)
Chuo cha Mifugo Tengeru
Chuo cha Mifugo Mpwapwa
Chuo cha Sanaa Bagamoyo
Taasisi ya Uvuvi Nyegezi
N.k

Na hapo hatujagusa vyuo vya Ualimu, na vyuo vingine vya elimu ya juu vya wakati huo hadi hivi vya sasa. Sasa ni akili gani inamfanya mtu achukue 'matokeo' ya chuo kimoja na kuyafanya yawe ya nchi nzima? HHivi kweli hakuna watu wenye uwezo wa kuwauliza hawa kina Mohammed Said na Warsha validity ya 'utafiti' wao? Hivi kweli hakuna wasomi Tanzania wanaoweza kudebunk this pseudo-research?

Na kweli wapo Waislamu wasomi wenye kuamini 'utafiti' huu? Msingi wa imani yao kwenye utafiti huu ni nini? NI kwa vile wamesema imefanywa na Waislamu? is that enough?

Mwisho wasiku wanasimama na kuitangazia dunia kuwa "waislamu wanadhulmiwa" ukiwauliza ipu hasa dhulma hakuna jibu mtawalia zaidi ya ngano tu.
 
Well hatutakiwi kuexcuse makosa hata kidogo. Kwenye madai makubwa no room for mistakes....

Anyway mi nasubiria official jibu (kwenye Hili) kutoka kwa muhusika......

MF,

Kufanya makosa ndiyo ubinadamu.
Ikiwa umeliona kosa nieleze na tufanya masahihisho.
 
unathibitisha tu hoja yangu; nyie vijana endeleeni kuamini haya masimulizi ambayo mwanzoni wengine waliyapa heshima kidogo kuyaita "ngano" lakini kwa kweli ni porojo nyingi za kufurahisha baraza...
Hata kama upo kazini kuifanyia uadui historia halisi ya Tanzania na mchango wa waislamu kutafuta uhuru lakini unapoita si ngano bali ni porojo unajitangaza ujinga na upuuzi wako.Kwa kauli hii inakutoa kwenye mchangiaji wa mjadala na kukuingia kwenye mpayukaji ambayo ni sifa ya wendawazimu na walevi wa gongo.
 
Mzee Mohamed Said wapigania uhuru toka Afrika kusini waliingiaje Tanzania, au unakataa hapakuwa na kambi zao Morogoro Mazimbu.Kuna yule dereva Dumisani alisababisha kifo cha Sokoine alishi vipi Tanzania ?.

Ngongo,
Hivi ulitakaje?

Unajua kitu kinachoitwa ''the standard of the resoanable man?''

Ikiwa hufahamu muonyeshe mjuzi haya majadiliano kuhusu kuingia
Tanzania na muulize mawazo yake.

Ningeweza kukupa jibu lakini nataka nawewe ushughulishe ubongo
wako.
 
MF,

Nieleze kipi unachotaka ufafanuzi Insha Allah nitajaribu kutoa maelezo
ikiwa ninayo.

wewe umesema

In 1981 BAKWATA had ceased to be an arm of the Christian Lobby. Theorganisation was under the tutelage of Warsha. The letter was ignored.

When Sheikh Deedat went to pay courtesy call to the Vice-President Aboud Jumbe athis official residence, the subject of the letter from the Church requestingfor Sheikh Deedat to be restrained was brought up.
manake 1981 vice president alikuwa Aboud Jumbe...

Mzee Mwanakijiji alisema

Aliyekuwa Waziri Mkuu na Makamu wa Pili wa Rais 1982 alikuwa ni Cleope D. Msuya... endelea kuwapata hawa wadogo zetu tu...

sasa nimejaribu kufukunyua data nashindwa kujua nani yuko sawa katika hili....
 
Kumbe Sheikh Deedat naye alikuwa kaburu?

N,

Hapakuwa na kifungu kilichosema kuwa mtu yoyote kutoka Afrika Kusini angeliweza
kuingia Tanzania.

Na Deedat alikuwa sheikh si mpigania uhuru kwa maana ya vyama vya ukombozi
vilivyokuwapo.

Hili lisitutoe katika picha kubwa.
 
Well hatutakiwi kuexcuse makosa hata kidogo. Kwenye madai makubwa no room for mistakes....

Anyway mi nasubiria official jibu (kwenye Hili) kutoka kwa muhusika......
Yaani kazi ya Mohammed ya historia ya Tanzania ni kubwa na muhimu kuliko Biblia?.
 
wewe umesema

manake 1981 vice president alikuwa Aboud Jumbe...

Mzee Mwanakijiji alisema



sasa nimejaribu kufukunyua data nashindwa kujua nani yuko sawa katika hili....

MF,

Ikiwa kuna mahali nimekosea fanya masahihiso hapana haja ya kuvutana katika
kosa.

Huo ndiyo usomi na uungwana.
 
Hata kama upo kazini kuifanyia uadui historia halisi ya Tanzania na mchango wa waislamu kutafuta uhuru lakini unapoita si ngano bali ni porojo unajitangaza ujinga na upuuzi wako.Kwa kauli hii inakutoa kwenye mchangiaji wa mjadala na kukuingia kwenye mpayukaji ambayo ni sifa ya wendawazimu na walevi wa gongo.
Tusonge kwa busara na adabu, punguza jazba mkuu.

Tuvumiliane mkuu.
 
MF,

Kufanya makosa ndiyo ubinadamu.
Ikiwa umeliona kosa nieleze na tufanya masahihisho.

amechambua vizuri tena kitaalamu Takwimu za Warsha kutoka UDSM zinazo onesha uwiano wa Waislamu na Wakristu katika intake... na ameonesha makosa ya research hiyo vizuri, sasa ilitakiwa mtu aje kujibu na kumuonesha (kitaalamu) kuwa Nguruvi nae amekosea kuichambua....

sasa Ami yeye akasema
Unajuwa Mohammed Said ni binadamu hivyo hata angekuwa madhubuti kiasi gani hawezi kufanya kazi isiyokuwa na kasoro za hapa na pale.

Pamoja na hivyo hizi data alizotoa ilikuwa ni kisaidizi tu ya historia aliyokuwa anaandika.

Huu utiiifu wa kanuni za kitafiti naona mmezifanya kuwa ni jambo kubwa sana kiasi ya kutaka kututoa kwenye ajenda.

na mimi nikamwambia asi excuse makosa, kama kweli kuna makosa basi then You should declare kwamba the Statistical Data au research iko in accurate na isitumike tena kama reference ya kuaminika.
 
Mpaka kufikia hapa wazee wa Gerezani chaliiii....wapo hapa kwa kuendeleza mipasho na ubishi tu na siyo hoja.

Ukweli ni kwamba kupitia mtanange huu wazee wa Gerezani mmeshindwa vibaya sana na mnahaibika vibaya sana.

Yaani kila muulizwapo maswali magumu mnaleta majibu mepesi yenye mipasho na kejeli juu. Poleni sana wafia dini wa Gerezani.
 
Yaani kazi ya Mohammed ya historia ya Tanzania ni kubwa na muhimu kuliko Biblia?.

unajua Ami unashindwa kuelewa kitu, madai yalileta humu ndani kuhusu Mzee Mohamed ni makubwa, Kwamba yeye ni mchochezi na Yeye akaja kujibu kudhibitisha kuwa yeye wala si mchochezi ila historia anayoeleza ni ya ukweli kabisa.

Na katika hilo, kuu zaidi ni dailake kuwa Waislamu wamedhulumiwa au wamekuwa kwenye ''dhulma'' kutoka na Mfumo kristo. Sasa hili si dai dogo hata kidogo, hili dai ni kubwa kuliko unavyofikiria.

Kama kweli Waislamu wamedhulumiwa wanahitaji kujidhatiti kweli na kama vipi tuangalie jinsi ya kulisahihisha ilo kosa na iwe katika kumbukumbu kama taifa na sio tu madai yalio kosa mashiko,

na kama wakristu wanasingiziwa kuwa wanadhulmu waislamu pia tunatakiwa kujua ili basi waombwe msamaha au madai hayo yaishie hapo.

sisi wengine tupo hapa kuangalia nani anasema nini na wapi kuna kunahitaji majibu na ufafanuzi na tunaweka maswali yanayohitaji majibu kila mtu apate nafasi ya kujibu, tujue kweli...
 
MF,

Ikiwa kuna mahali nimekosea na fanya masahihiso hapana haja ya kuvutana katika
kosa.

Huo ndiyo usomi na uungwana.

Kwenye hili Mzee MS mi nlikuwa nataka kujua nani kasema ukweli kati yako na Mzee Mwanakijji

Wewe umesema 1981 Vice President alikuwa Aboud Jumbe na mzee Mwanakijiji kasema 1982 Prime Minister na Vice President (ila yeye alitumia Makamu wa Raisi wa Pili) alikuwa Cleopa Msuya... Sasa wengine Historia sio wazuri kiivyo...

kwenye hili nani yuko sawa... au historia inasemaje
 
Nimeziona,hata hivyo hili lisiwe nongwa.Unajuwa Mohammed Said ni binadamu hivyo hata angekuwa madhubuti kiasi gani hawezi kufanya kazi isiyokuwa na kasoro za hapa na pale.
Pamoja na hivyo hizi data alizotoa ilikuwa ni kisaidizi tu ya historia aliyokuwa anaandika.Maudhui makuu ni matukio ya kihistoria yaliyokuwa yametokea kabla na baada ya uhuru.Wahusika wakuu walikuwa ni Nyerere na wapigania uhuru aliokuja kuwapiga teke.Ukirudi kwenye msingi wa uzi huu na historia basi hata kama ukikutana na kasoro za hapa na pale atakuwa ametoa source za kutosha ambazo atakayeita ni ngano au ni uchochezi basi huyo ni mpuuzi wa mwisho.Upuuzi wake wala hautozuia wasomaji wengine kuamini historia hiyo iliyokuwa haikujulikana kabla.
Huu utiiifu wa kanuni za kitafiti naona mmezifanya kuwa ni jambo kubwa sana kiasi ya kutaka kututoa kwenye ajenda.Kumbuka hakuwa amefanya utafiti wa mfano kutoa kifaa bora cha kuingizwa kwenye injini za ndege za abiria kiasi kwamba kutowiana takwimu kidogo tu au kujitokeza kasoro baadae basi hakuvumiliki na inabidi ndege zote zishushwe chini kwanza kufanyiwa uchunguzi.
Zaidi ya hivyo ni kuwa yapo maandishi ambayo yalipaswa yawe makubwa zaidi kuliko kazi ya historia ya Mohammed Said na ambayo ukifuatilia tofauti zilizomo basi wala huwezi kuiweka nyumbani kwako.Naamini Nguruvi na Mwanakijiji mnazo Biblia zenu majumbani hebu jaribuni kufuatilia tofauti za aina hiyo.

Hayo makosa unayaona madogo kwako! Wonder shall never end.
Hivi unajua kwamba huo utafiti wake anautumia kama sehemu ya malalamiko yake?

Ikiwa kwenye utafiti wa Kitaalam amefanya makosa makubwa kama haya vipi kwenye
ngano zake tusitie mashaka.

Tunakubali kila binadamu hajakamilika 100%, lakini itoshe na aseme kwamba kuna walakin
kwenye data zake na tutamwona muungwana,. Lakini si abwage maandishi yenye makosa
halafu atumie kama reference tena na tena na wewe unameza kama kinda.

Mtu mwenye akili timam akikwambia jambo la uongo na wewe ukajua ni uongo lakini ukakubali atakudharau.
 
Hapo kwenye mstari, Mzee bin Sudi Manyema na Ibrahim Hamis Nubi.
Kuna wakati Nguruvi alikuuliza vipi wengine watiwe kabila zao na wengine waachwe hivyohivyo
kama si hila ya kuonyesha Wamanyema, Wazulu na Wanubi walikuwa superior kuliko wengine,
uliruka kimanga ukasema hujaandika hivyo!

Licha ya chuki za Kidini kuna kingine tumepata "Ilm" kutoka kwako, mbaguzi.

Platozoom,

Sina haja ya kuvutana lakini ningeweza kukuuliza kweli wewe unachukia ubaguzi?
Ningeweza nikaweka ushahidi mwingi tu hapa.

Lakini ya nini yote haya?
 
Hayo makosa unayaona madogo kwako! Wonder shall never end.
Hivi unajua kwamba huo utafiti wake anautumia kama sehemu ya malalamiko yake?

Ikiwa kwenye utafiti wa Kitaalam amefanya makosa makubwa kama haya vipi kwenye
ngano zake tusitie mashaka.

Tunakubali kila binadamu hajakamilika 100%, lakini itoshe na aseme kwamba kuna walakin
kwenye data zake na tutamwona muungwana,. Lakini si abwage maandishi yenye makosa
halafu atumie kama reference tena na tena na wewe unameza kama kinda.

Mtu mwenye akili timam akikwambia jambo la uongo na wewe ukajua ni uongo lakini ukakubali atakudharau.

Platozoom,

Hivi yote yamekupita hayana umuhimu ila kosa langu.
Intrigues zote nilizoeleza mle zote zimekupita hazina
maana ila kosa langu.

Kisa cha Shylock na madai ya kilo moja yake ya nyama.
 
Kwenye hili Mzee MS mi nlikuwa nataka kujua nani kasema ukweli kati yako na Mzee Mwanakijji

Wewe umesema 1981 Vice President alikuwa Aboud Jumbe na mzee Mwanakijiji kasema 1982 Prime Minister na Vice President (ila yeye alitumia Makamu wa Raisi wa Pili) alikuwa Cleopa Msuya... Sasa wengine Historia sio wazuri kiivyo...

kwenye hili nani yuko sawa... au historia inasemaje

MF,

Mbona mimi ushanisoma kuwa nimesema Kawawa?
Ikiwa ni kosa basi linasahihishwa.

Si suala la kuvutana kwenye kitu kilichokosewa.
 
Back
Top Bottom