Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar


Hiki ni kituko cha mwaka hivi Mohamed Said na Philemon Andrew K Mushi nani anajua habari za Mwambao.

Hizi ngano walishe wenzako Mushi na Pwani wapi na wapi.

Chukuwa maneno ya hotuba ya Nyerere hapo kuhusu Wazee wa Dar es Salaam kisha mpelekee Mushi, muulize Mushi kuwa Nyerere naye alipata upinzani wakati anakwenda Mwambao.

Mwambie Mushi ajikite kuelezea habari za Machame, Kibosho, Rombo, Kishumundu, lakini siyo Mwambao.

Endelea kumeza ngano za nazi kutoka kwa Mushi.
 
Last edited by a moderator:
Mwambie Mushi ajikite kuelezea habari za Machame, Kibosho, Rombo, Kishumundu, lakini siyo Mwambao. Endelea kumeza ngano za nazi kutoka kwa Mushi.
Hii ndiyo tofauti kubwa kati yetu hapa ukumbini...wako ambao kwao huo mwambao ndio Tanganyika, Gerezani Dar es Salaam ndio Tanganyika na Wazee wa Mohamed Said ndio Watanganyika! Hamna habari kabisa kwamba;

  • katika miaka ya 1930s wakazi wote wa Dar es Salaam wakiwa hawafiki 15,000 Tanganyika ilikuwa na mamilioni ya watu,
  • miaka ya 1940s Dar es Salaam ikiwa na watu chini ya 50,000, Tanganyika ilikuwa na mamilioni ya watu,
  • miaka ya 1950s Dar es Salaam ikiwa na watu chini ya 100,000 Tanganyika ilikuwa na mamilioni ya watu
  • na wakati tunapata uhuru mwaka 1961 Dar es Salaam ikiwa na watu laki moja na nusu Tanganyika ilikuwa na watu zaidi ya milioni nane.
Ritz wewe baki hapo hapo ukiongelea mwambao jinsi mwalimu wako Mohamed Said naye alivyojikita katika kuongelea wazee wake wa Gerezani, Mushi hapo anaongelea Tanganyika nzima. Wakati dunia yako wewe huenda ikawa ni hapo hapo ulipo, Mushi anatazama ulimwengu mzima, kalaghabaho!
 
Duh, tuna safari ndefu...ni asilimia ndiyo inaongelewa hapa, upo? Kuna watu kweli wanahitaji darasa.
Darsa gani?.Toa basi.
Inayoongelewa ni asilimia...............

Hujajibu kitu na hujaeleweka.
 
mkuu huu unabii una ukweli kabisa, loh!
 
Umejuaje kama Nyerere alisema hicho anachodaiwa kusema kwenye kitabu cha Bergen?
Wee Mzee umechanganyikiwa na huu mjadala.
Kila kitu huamini kilichoandikwa huamini.Mwanzo ilikuwa ni yale yaliyomo kwenye historia ya Mohammed Said.Sasa waandishi wote wakiwa ni pamoja na wa kanisani kwako huwaamini.
Unachoamini ni ngano zako pekee.Unapoteza muda bure.
Mbali na hayo hujajibu kuhusu udugunization uliotokeaje?.
 
Hapa sasa mumekubali ya kwambaa hamkuweza kuleta ushahidi kuwa kweli Mohammed Said alifanya uchochezi kwa kuandika historia ya kupatikana kwa uhuru na vituko vya Nyerere kwa waislamu.
Mpaka mjadala unakwisha na Mohammed kujiandaa kutoa tolea jengine la kitabu chake watetezi wakuu wa Nyerere Aakina Nyambala,Jasusi,Mwanakijiji na Nguruvi wameshindwa hiyo kazi.Mwishowe wamekuwa wakitoa ngano na kutaka eti watu wachukue ushahidi mitaani badala ya kwenye vitabu vya historia.
Wengi wa watetezi wa Nyerere akiwemo mtoto wake Yerico na wengi walioanza hii kazi wamekimbia na hawaonekani tena.Wa mwisho amebaki Nguruvi aliyekuja na hekaya ya sensa,Mwanakijini na ngano ya Udugunization.
Wakipewa majibu wanakuja na swali
 
Darsa gani?.Toa basi.
Inayoongelewa ni asilimia...............

Hujajibu kitu na hujaeleweka.
Sasa population inapungua vipi hadi kufikia 40% from 67%??

kilitokea nini??NUNGWI zilikua nyingi sana nin??

naona NGURUVI'S HISTOHISIA BADO ZINAENDELEA..

poleni sana..
nyie people mnatia aibu sana,
swala la % kwenye population mbona mnalichukulia kimasiala masiala sana aisee? kumbe ndo maana mnafeli shuleni..
nawapa mfano hapa...
''ufaulu wa wanafunzi wa kidato cha nne mwaka 1999 kwa kiwango cha division one ulikuwa juu kulinganisha na wa mwaka 2012, lakini idadi ya waliomaliza mwaka 1999 ni ndogo sana kulinganisha na mwaka 2012''
hapo mmeelewa calculation za % au bado?
halafu hiyo sensa ya mwaka 1967 kuhusu idadi ya waislam ina walakini maana ilijumlisha na wapagani ambao wakati huo walikuwa wengi kuliko waislam na wakristo, sasa kama wakristo waliwazidi waislam ujanja kuwabadili wapagani kuingia kwenye dini zao ulitegemea muujiza gani?
 
Hiyo darsa yako ovyo kabisa!.Mwalimu gani unayetoa somo la ubabaishaji.
Sensa ni kitu tofauti na ufaulu wa mitihani.
Kitu gani kinakupa uhakika kuwa wapagani wakati huo walikuwa ni wengi kuliko waislamu na wakristo?.
 
Ajabu iko wapi akijibu Amiri Jamal.Kwani mara ngapi maraisi wanapeleka wawakilishi wao kufanya mambo kwa majina yao.
 
Mfumo kristo upo Dunia nzima (Haukuanzia nchini kwetu) ukitoa nchi zenye mfumo Islam. Hii inatokana na uenezaji wa hizi dini kati ya wakoloni ((Waislamu (Waarabu)) na Wakristo ((Wamagharibu)). Wakristo walieneza dini kwa kujenga mashule, mahospitali na kadha wa kadha kuelimisha jamii husika, Wailsam walisisitiza dini zaidi. Matokeo yake ndiyo tunaendelea kutofautaina LEO MPAKA KESHO.
 
Hiyo darsa yako ovyo kabisa!.Mwalimu gani unayetoa somo la ubabaishaji.
Sensa ni kitu tofauti na ufaulu wa mitihani.
Kitu gani kinakupa uhakika kuwa wapagani wakati huo walikuwa ni wengi kuliko waislamu na wakristo?.
poor you!
kwa hiyo mnataka kulazimisha kuwa kupungua kwa 67% to 40% ni kupungua kwa population?
 
poor you!
kwa hiyo mnataka kulazimisha kuwa kupungua kwa 67% to 40% ni kupungua kwa population?
Nani aliyepungua kutoka 67% mpaka 40%?.
Bila kuwepo sensa nyengine baada ya hiyo na bila kuwepo sababu maalum basi tunaamini waislamu ama wamebaki hapo au wameongezeka.
Kwa maana hiyo kuwepo kwa ufaulu wa 17% kwa waislamu daima ni jambo la kupikwa kwa mfano kukata wanafunzi wanaofaulu kuendelea na masomo.Ushahidi huu umetolewa mara kadhaa.
 
Duh ha ha ha ha Nyambala huyu Mzee wa Gerezani hashindwi kunogesha ngano zake ila atakuwa amewapaisha Mag3 Nguruvi3 & Mzee Mwanakijiji natamani angenitia na mimi katika daraja la Paroko ha ha ha ha.


 
Last edited by a moderator:
Mohamed Saidi kala chocho...kawaacha wafia dini wenzake (wanafunzi wake) wanadanki danki kwa hoja mfu na nyepesi.
 
Kama viongozi wa CCM wamepita hapa na kusoma mjadala huu,basi sina shaka wameona na kuamini kuwa ile propaganda yenye sumu kali ya udini na ukabila wanayoihubiri kila siku ili waendelee kukaa madarakani basi sasa imetunga mimba na
siku siyo ndefu mtoto wake atazaliwa kwa tumbo la mama kupasuka.

Yaani kupitia mjadala huu,CCM kuna kitu mnatakiwa kujifunza. Tumefika sehemu mbaya sana.
 
Mohamed Saidi kala chocho...kawaacha wafia dini wenzake (wanafunzi wake) wanadanki danki kwa hoja mfu na nyepesi.
Mohammed kaa upumzike kazi imeisha.Kila nikiingia hata usiku wa manane nakuta upo.
Hakuna haja tena kujibizana na watu walioshindwa mjadala.Sisi wanafunzi wako tumetosha kuwanyamazisha watu wa mfumo wa kidhalimu.Ukiona tumekosea sahihisha.
Najua unacheka unapoona Mwanakijiji anapokuja na udugunization baada ya miezi yote hiyo kushindwa kutoa hoja ya kuonesha uchochezi.
NASAHA KWAKO Mwl. MOHAMMED SAID.

Hapa tulipofika na mafanikio yaliyopatikana kutokana na kazi yako omba dua ya nabii Suleiman ya kumshukuru ALLAH s.w.

Swali sana usiku na mchana na mswalie Mtume Muhammad S.A.W.
 

Hivi kwa akili yako Mushi anaweza kuandika historia ya Tanganyika kwanza ataanzia wapi.

Msalimie sana Mushi, muulize anawafahamu Waswahili ya Kariakoo wanywa kahawa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…