Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

Ndio maana tuko hapa kuwaonyesheni kuwa ushahidi wenu ni magumashi tu. Mohamed ameshindwa kunijibu swali la Nyerere kutaifisha shule za misheni ili waislamu wapate fursa ya kusoma. Yeye hilo kwake halizungumzii kabisa. Wala hazungumzii kuwa elimu yake ameipata St. Joseph, shule ya wakatoliki. Hayo kwake hayagusi. Ukimlaumu Nyerere basi angalau mpe sifa kuwa alijitahidi kutoa fursa sawa za masomo kwa waislamu. Lakini hilo katu hamtasema kwa sababu mkisema hivyo mnamwagia maji theory yenu ya Nyerere kuwa mbaguzi wa Waislamu.
Na hakuna mahali ambapo Mohamed amesema kuwa alipokuwa st Joseph mfumokristo school aliwahi kubaguliwa.

Sasa hivi yupo mstari wa mbele kuelezea mfumokristo ambao yeye mwenyewe kwa experience yake st Joseph hajathubutu kuandika hata nusu mstari wa ubaguzi aliouona.

Hataki kuongelea st Joseph maana vijana watamuuliza kwanini mtoto wa ''wazee wa Dar es Salaam'' alikwenda kusoma katika shule ya ''makafir''

Yeye yupo bize kuwakataza wenzake wasipeleke watoto kutafuta elimu inapopatikana.
 
Mkuu Ritz hapo umeteleza kidogo.Padre ni kiongozi wa kiroho wa kanisa Katoliki.Mpake ufikie daraja la upadre kuna ngazi mbali mbali za kiimani utatakiwa kuzipitia.Mchungaji au wachungaji (wingi) ni viongozi wa makanisa (Protestant) Lutheran,Anglican,AIC na nk.Kufikia daraja la uchungaji kuna taratbu za mafunzo ya kiroho.Makanisa kama pentecoste/Assembly na mengine ya kiroho mchungaji si lazima usomee unaweza kukuta mtu ni mhandisi akaanzisha kanisa lake akajiita mchungaji au Askofu au Nabii/Mtume.Hizi title huwezi kuzikuta Lutheran,Catholic au Anglican.Nadhani umenielewa turejee kwenye mada.


Padre na Mchungaji ni sawa sawa jiwe na stone.
 
Inahuzunisha kuona kuwa mtu anaemwamini na kuamini kuwa ana kichwa kizuri akatokea akafanya mambo bila tafakuri kwa vile tu amebebwa na mhemuko au amekuwa 'fanatic'. Katika hotuba yake ya kwanza kabisa kama rais wa nchi akihutubia bunge Nyerere alikiri kuwepo tatizo. Nyerere alipojiunga TAA na badae TANU akakuta kuwa lengo kuu la vyama hivyo ni kuondoa tatizo la kubaguliwa kielimu na kutokuwa na taasisi imara za kiisalmu kwa kuwa mfumo wa kikoloni ulikuwa wa kikristo, wale wazee lengo alo lilikuwa ni kubadili hali ile. Wale wazee ambao walikuwa viongozi wa EAMWS ndio hao hao walikuwa viongozi wa TANU kupitia kamati ya wazee wa TANU. Walisimama kidete kuhakikisha Chuo Kikuu kinajengwa. Harakati zilipofikia hatua ya kuingia mkataba, kamati ile ikavunjwa na wazee wote wakaondolewa katika TANU na kundi kubwa la waislamu imara walioshirikiana na Nyerere katika kufikia hapo wakawekwa kizuizini na kukafuatiwa kuvunjwa kwa EAMWS.Kutaifisha shule hakukuendana na progamu yeyote ya kuwasaidi wale walioachwa nyuma kielimu, ilikuwa hatua ya kisiasa tu kama vile ujenzi wa sasa wa shule za kata. Mohamed Said kusoma St. Joseph hakuondoi ukweli wa mambo yaliyofanyika kuwadhulumu waislamu. Mohamed Said kusoma St Joseph kunaonesha jinsi gani wazee wake walivyothamini elimu na inadhihirisha nafasi waliyokuwa nayo katika nchi hii lakini kwa uungwana wao wakaona kupata elimu kwa mtoto wao tu hakutoshi bali kundi kubwa la waislamu waliokosa mtetezi nao wapate fursa ya elimu. Si zama zile tu hata sasa, sehemu ambazo wanaishi waislamu wengi muamko wa elimu ni mdogo kama ilvyo kwa wafugaji. Serikali yetu leo ipo tayari kuwahamasisha wafugaji kwa mabilioni ya pesa waende shule lakini hawafanyi hivyo katika jamii za kiislamu ingawa wote ni raia wa nchi hii na wana haki sawa kuhudumiwa na kushughulikiwa na serikali yao. Kam kukosa muamko wa elimu kwa waislamu ni tatizo, mbona tatizo hili halishughulikiwi basi
Nani ana wajibu wa kushughulikia tatizo la ukosefu wa mwamko wa elimu miongoni mwa Waislamu? Ni wote. Wazazi, viongozi wa dini na viongozi wa jamii za Kiislamu. Mohamed angekuwa anapita mitaani anahubiri umuhimu wa watoto wa waislamu kujiunga mashuleni ningefuatana naye. Mbona wachaga hawahitaji uamsho huo? Hii ya EAMWS ni kisingizio tu. Kulikuwepo mfarakano wa ndani ya kundi hilo. Mbona hatujaona wakifanya maajabu Kenya ambako pia walikuwepo?
 
Na hakuna mahali ambapo Mohamed amesema kuwa alipokuwa st Joseph mfumokristo school aliwahi kubaguliwa.

Sasa hivi yupo mstari wa mbele kuelezea mfumokristo ambao yeye mwenyewe kwa experience yake st Joseph hajathubutu kuandika hata nusu mstari wa ubaguzi aliouona.

Hataki kuongelea st Joseph maana vijana watamuuliza kwanini mtoto wa ''wazee wa Dar es Salaam'' alikwenda kusoma katika shule ya ''makafir''

Yeye yupo bize kuwakataza wenzake wasipeleke watoto kutafuta elimu inapopatikana.

kumbe mo said alisoma misheni...hapa Dodoma hiki ni kipindi cha shule lakini madrasa za bweni zimejaza watoto wa umri wa kwenda shule na zipo kila kona, sijui wahusika hili wanalitazamaje, kesho hawa watoto watakuwa nani kwa elimu ya dini peke yake.
 
Mkuu Ritz hapo umeteleza kidogo.Padre ni kiongozi wa kiroho wa kanisa Katoliki.Mpake ufikie daraja la upadre kuna ngazi mbali mbali za kiimani utatakiwa kuzipitia.Mchungaji au wachungaji (wingi) ni viongozi wa makanisa (Protestant) Lutheran,Anglican,AIC na nk.Kufikia daraja la uchungaji kuna taratbu za mafunzo ya kiroho.Makanisa kama pentecoste/Assembly na mengine ya kiroho mchungaji si lazima usomee unaweza kukuta mtu ni mhandisi akaanzisha kanisa lake akajiita mchungaji au Askofu au Nabii/Mtume.Hizi title huwezi kuzikuta Lutheran,Catholic au Anglican.Nadhani umenielewa turejee kwenye mada.

Mkuu Ngongo,

Nashukuru kwa kunipa darsa nimekuelewa takuwa mchoyo wa Fadhwila kutokushukuru.
 
Last edited by a moderator:
Hebu rudi usome post yangu kwa umakini na ukiwa umetuliza akili tena sehemu uliyokazia kwa rangi ya zambarau

Nimesema hivi ''Mohamed anatakiwa afahamu kuwa population ni ''variable value'' kwamba si lazima asilimia 67 ya mwaka 1967 ibaki kama ilivyo.Kuna uwezekano iliongezeka na kufikia 80 au kupungua na kufikia 40 kwahiyo alitakiwa kwanza apate the most recent stats.
Kufanya extrapolation ya mwaka 1967 ni sawa na mtu kupanga mipango ya maendeleo ya nchi kwa kutumia stats za 1967. Huku ni kupotosha vijana kusikoweza kuvumilika hata kidogo. Wrong! Mohamed denounce this ASAP!''

Sikuwahi kusema kuwa population imepungua hadi 40%. Narudia tena population ni variable value. Kuna uwezekano kuwa wakati Mohamed anaandika kitabu population ua waislam ya mwaka 1967 iliongezeka na kufikia 80% au ilipungua na kufikia 40%.

Ukisoma maandishi usisome ukiwa na dhana tayari, hayo ndiyo matatizo yanayomkumba Mo. Naona karithisha vijana wake.
Usipindishe jawabu!.
Unatumia kanuni ya mtafiti gani anayekubaliana na hoja yako?.
Nakuuliza tena ikiwa ni kupanda au kushuka kwa population jee inakubalika kushuka kwa kiasi hicho bila kuwepo sababu maalum?,
Bila sababu maalum kuwepo.Kushuka au kupanda huoni kwamba hiyo ni mbinu ya kimfumo ili kuleta manufaa fulani?.
Kwanini serikali ikatae kata kata kuingiza kipengele cha dini ili kujua idadi halisi ya watanzania na dini zao?.Huoni kuwa huo ni ushahidi wa kuficha ukweli wa hizo takwimu za 83/17 ?.
 
Rejea darsa tulilokupa kuhusu hiyo namba katika nyuzi za Mohamed Said zilizopita.

Hapa, pata darsa kwa Mohamed Said la historia ya wazee wake.

Umekisoma kichwa cha mada? Jee, umekuja na lolote? au bado mpo katika kujipiga chenga za mwili wenyewe kwa wenyewe?

umeshindwa kutoa darasa nilidhani tungeweza kujadiliana na badala yake unanirudisha nyuma tena..
 
Ukisikia ngano basi ndiyo hiyo hapo juu.Angalia Nguruvi alivyoandika

Mimi nikamuahidi Nguruvi kama hivi


Jibu la ngano ya Mwanakijiji lipo kwenye paragraph chache alizozinakili Mohammed Said katika kitabu chake kama hivi
Kwenye kitabu cha Developement and religion in Tanzaia cha Bergen uk365 alimnukuu mwalimu Nyerere akisema
" I am a layman but I try to do what I can and will not go against my own church.I want to give the church a better chance here.Tell the bishops that I have established in TANU a department of political education and have put a Lutheran minister in charge;he was not a greater politician. I selected him because of his strong faith"

Sasa hiyo ngano yako Mwanakijiji ya udugunization imeanzaje?.

Sijui ni kwa kiasi gani unaamini kauli hiyo; ndani ya hiyo sentensi sijui hata kama umeona contradictions. Unasema Nyerere hatoenda kinyume na Kanisa lake halafu anasema awaambie maaskofu kuwa amemuweka Mlutheri kwa sababu ya imani yake? Walutheri na Wakatoliki? kwa kumuweka Mlutheri anaendeleza vipi Kanisa Katoliki? It just doesn't make any sense..
 
ami
Nitakujibu maswali yako kwa maswali:Je huo ni ushahidi wa dhulma ya ukristo dhidi ya uislam? DPP sio ukristo. Na je ni Ponda peke yake ambaye amewahi kukataliwa dhamana na DPP?Je huo ni ushahidi wa dhulma ya ukristo dhidi ya uislam? Kama serikali ndiyo imewalaumu, je maana yake muislam kalaumiwa na mkristo? Na je kuhusiana na hizo vurugu, hakukuwa na lawama zilizopelekwa kwa wakristo?Je huo ni ushahidi wa dhulma ya ukristo dhidi ya uislam? Je NECTA ni synonymous na ukristo? Na una uhakika gani kuwa hamna wasio waislam ambao walikuwa affected na ile computer glitch?Je huo ni ushahidi wa dhulma ya ukristo dhidi ya uislam?, Radio ya kwa Neema, nayo imefungiwa, je ni dhulma ya ukristo dhidi ya uislam?Je huo ni ushahidi wa dhulma ya ukristo dhidi ya uislam?,
Katika vyote hapo juu kwanini waathirika wakubwa wawe ni waislamu tu.Huoni kuwa huo ni ushahidi wa makusudi.computer gani yenye chuki na waislamu tu?.Mwenye chuki atakuwa ni mtu wa kimfumo aliyeiongoza hiyo comyuter.
Vipi ukilinganisha na mauaji ya mwandishi Mwangosi? Ni ukristo huo?Siogopi kutajwa kwa hao waandishi.
Mwangosi pamoja na kuwa hawakilishi malalamiko ya kundi maalum lakini tume si iliundwa?.Kwanini masuala yote yanayowahusu waislamu hakuna haja ya kuundiwa tume?.
Niliomba usirejee vitabu hivyo kwasababu, wote tumeishaviona. Wewe unakubaliana navyo, mimi sikubaliani navyo, hasa hasa zile hisia zilizopandikizwa kuwa kuna watu wa dini fulani ndio wanaonewa na wa dini nyingine. Lakini kikubwa ni kwamba, penye dhulma, mara nyingi huwa kuna ushahidi wa wazi, Ndio maana nikasema, hivi kwa mtu ambaye hajawa-influenced na hisia za kwenye hivyo vitabu, je anaweza akatoa ushahidi ulio wazi na usiopingika, kuonesha kuwa waislam wanadhulmiwa na wakristo? Au ushahidi ndio hayo maswali uliyoniuliza hapo juu???
Ikiwa hutaki kuamini vitu vilivyoandikwa baada ya utafiti basi hakuna sababu ya kuamini mambo ya mitaani.Nakuonya usiendelee na utovu wa nidhamu kama huu.
Wewe vipi?.Unakimbilia ushahidi wa mitaani wakati watafiti waislamu kwa wakristo wamethibitisha kuwepo dhulma.
 
Sijui ni kwa kiasi gani unaamini kauli hiyo; ndani ya hiyo sentensi sijui hata kama umeona contradictions. Unasema Nyerere hatoenda kinyume na Kanisa lake halafu anasema awaambie maaskofu kuwa amemuweka Mlutheri kwa sababu ya imani yake? Walutheri na Wakatoliki? kwa kumuweka Mlutheri anaendeleza vipi Kanisa Katoliki? It just doesn't make any sense..
Kabla kuja kwa walutheri na wakatoliki kwanza ulipaswa ujibu jee kwa Nyerere kusema amemuweka aliyemuweka kutokana na imani yake ni Udugunization au la.
Hii ndio tabia yako unapokosa jibu unauliza swali.
 
Kwa vijana wadogo ni vigumu sana kuelewa mambo yalivyokuwa huko nyuma na hivyo wanakuwa wepesi mno kumeza ngano wanazolishwa na Mohamed Said...kwa mfano, je wanajua, wakati wa mkoloni, ushindani uliokuwapo baina ya dhehebu mbali mbali za Kikristo na hasa Wakatoliki, Walutheri na Waprotestant ndio chachu iliyowezesha maendeleo makubwa kupatikana sehemu zote walizopiga kambi.

Kulikuwa na ushindani katika utoaji wa huduma za kiroho, hospitali na shule...hivyo mathalani kila moja wao alipofungua shule eneo fulani na mwenziwe alifanya hivyo hivyo kwa lengo la kutoa huduma bora zaidi. Bahati mbaya kwenye mikoa ya mwambao yenye Waislaam wengi walipata upinzani mkali kupokewa kama inavyosimuliwa hapa na Mwandishi wa historia Philemon Andrew K Mushi katika kitabu chake History and Development of Education in Tanzania, nanukuu;
Although variations in access to education developed among Africans of various beliefs, a more significant distinction evolved between Christians and Muslims. The early missionaries encountered considerable hostility from the population of the predominantly Muslim coastal belt; as a result they had to concentrate their operations inland among people who held traditional African beliefs.

Even when German and British government educators took special interest in Muslim education, their sheikhs (the spiritual leaders of the Muslim community) and many parents viewed Western-inspired schools , even when government run, as a threat to their authority. Consequently, most sheikhs restricted the children under their charge to Quranic schools (madrasa) that taught religion and Arabic.
Mwandishi na mtafiti Philemon Andrew K Mushi, anaendelea;
In 1956, 711 government and native authority and 27 Muslim Agency institutions catered for 97, 917 children, while 1,846 mission schools provided 237,669 places. Assuming that most mission educated school leavers were nominal Christians, one can see that this group had proportionally greater chances of advancing to higher levels of education.

One of the features of the mission activity was diversity, with important consequence. There were some 21 missions by 1933 and more than two thirds of these were not British. The intense competition for converts and local power, especially between Catholic and Protestant missions, led to concentration of mission and schools in the same areas.
Je, Mwalimu Nyerere alirithi nini mwaka 1961 tukipata uhuru, Mwandishi na mtafiti anaendelea kutoa darasa;
At the time of independence, in 1961, the inheritance was an economically poor and illiterate society; about 85% of the population (80% men and 89% women) was illiterate. Primary School enrolment was less than 30% of the school age population. There were only 11,832 students in the secondary school, and only 176 of these in the sixth form.
After independence the new government under its leader Mwalimu Nyerere was committed to educational policies and strategies aimed at addressing the observed inequalities in education provision. The first thing Mwalimu did was to address the issue by nationalizing all mission schools to give equal opportunity to all Tanganyikans/Tanzanians and this made it possible for people like Mohamed Said to see the inside of a classroom at St Josephs...sasa shuhudieni kejeli na dhihaka zake kwa Mwalimu, kweli shukhrani ya punda ni mateke.
 
Last edited by a moderator:
Hebu rudi usome post yangu kwa umakini na ukiwa umetuliza akili tena sehemu uliyokazia kwa rangi ya zambarau

Nimesema hivi ''Mohamed anatakiwa afahamu kuwa population ni ''variable value'' kwamba si lazima asilimia 67 ya mwaka 1967 ibaki kama ilivyo.Kuna uwezekano iliongezeka na kufikia 80 au kupungua na kufikia 40 kwahiyo alitakiwa kwanza apate the most recent stats.
Kufanya extrapolation ya mwaka 1967 ni sawa na mtu kupanga mipango ya maendeleo ya nchi kwa kutumia stats za 1967. Huku ni kupotosha vijana kusikoweza kuvumilika hata kidogo. Wrong! Mohamed denounce this ASAP!''

Sikuwahi kusema kuwa population imepungua hadi 40%. Narudia tena population ni variable value. Kuna uwezekano kuwa wakati Mohamed anaandika kitabu population ua waislam ya mwaka 1967 iliongezeka na kufikia 80% au ilipungua na kufikia 40%.

Ukisoma maandishi usisome ukiwa na dhana tayari, hayo ndiyo matatizo yanayomkumba Mo. Naona karithisha vijana wake.


Sasa population inapungua vipi hadi kufikia 40% from 67%??

kilitokea nini??NUNGWI zilikua nyingi sana nin??

naona NGURUVI'S HISTOHISIA BADO ZINAENDELEA..

poleni sana..
 
  • Thanks
Reactions: Ami
Kabla kuja kwa walutheri na wakatoliki kwanza ulipaswa ujibu jee kwa Nyerere kusema amemuweka aliyemuweka kutokana na imani yake ni Udugunization au la.
Hii ndio tabia yako unapokosa jibu unauliza swali.

Umejuaje kama Nyerere alisema hicho anachodaiwa kusema kwenye kitabu cha Bergen?
 
Umejuaje kama Nyerere alisema hicho anachodaiwa kusema kwenye kitabu cha Bergen?

Kwa kuwa yeye mwenyewe hakukanusha kilichoandikwa dhidi yake! wakati akiwa hai kitabu kinasomwa inakuwaje wewe unakanusha baada ya mhusika kufa? Nyerere akisingiziwa mara moja hukanusha ndio maana mwaka 1992 alikanusha madai ya Kambona kuwa anamiliki mali kibao na ameweka fedha nyingi ktk benki ya Uswissi yeye na Amir Jamal na Kawawa! madai haya ya Kambona alitoa wakati akihutubia mkutano wa hadhara uwanja wa Jangwani!
 
  • Thanks
Reactions: Ami
Ma3, I was there and as a Moslem I benefited from Nyerere's decision to nationalize mission schools.
Kwa vijana wadogo ni vigumu sana kuelewa mambo yalivyokuwa huko nyuma na hivyo wanakuwa wepesi mno kumeza ngano wanazolishwa na Mohamed Said...kwa mfano, je wanajua, wakati wa mkoloni, ushindani uliokuwapo baina ya dhehebu mbali mbali za Kikristo na hasa Wakatoliki, Walutheri na Waprotestant ndio chachu iliyowezesha maendeleo makubwa kupatikana sehemu zote walizopiga kambi.

Kulikuwa na ushindani katika utoaji wa huduma za kiroho, hospitali na shule...hivyo mathalani kila moja wao alipofungua shule eneo fulani na mwenziwe alifanya hivyo hivyo kwa lengo la kutoa huduma bora zaidi. Bahati mbaya kwenye mikoa ya mwambao yenye Waislaam wengi walipata upinzani mkali kupokewa kama inavyosimuliwa hapa na Mwandishi wa historia Philemon Andrew K Mushi katika kitabu chake History and Development of Education in Tanzania, nanukuu;

Mwandishi na mtafiti Philemon Andrew K Mushi, anaendelea;

Je, Mwalimu Nyerere alirithi nini mwaka 1961 tukipata uhuru, Mwandishi na mtafiti anaendelea kutoa darasa;

After independence the new government under its leader Mwalimu Nyerere was committed to educational policies and strategies aimed at addressing the observed inequalities in education provision. The first thing Mwalimu did was to address the issue by nationalizing all mission schools to give equal opportunity to all Tanganyikans/Tanzanians and this made it possible for people like Mohamed Said to see the inside of a classroom at St Josephs...sasa shuhudieni kejeli na dhihaka zake kwa Mwalimu, kweli shukhrani ya punda ni mateke.
 
Kwa namna huu mjadala unavyoendelea Mag3, Nguruvi, Mwanakijiji, Jasusi etc. mjiandae pale toleo la tano la kitabu cha Mzee Saidi litakapokuja na madai:

"In between 2010 - 2013, a huge discussion regarding the church and its efforts to suppress the rights of muslim emerged in a forum called Jamii Forum, also part of the christian lobby. The church was quick to dispatch four prominent bishops under pseudo names like Mag3, Nguruvi, Jasusi and Mwanakijiji to ensure church's manipulation interests and its long arm were not exposed."

Hahahaha ahahahaha ahaha!!!!!!

Please haya ni maoni yangu and I responsibly own them.


Isn't this what we see on things we know, stuff that we saw, lived and experienced ndani ya simulizi za MS?
 
Kwa kuwa yeye mwenyewe hakukanusha kilichoandikwa dhidi yake! wakati akiwa hai kitabu kinasomwa inakuwaje wewe unakanusha baada ya mhusika kufa? Nyerere akisingiziwa mara moja hukanusha ndio maana mwaka 1992 alikanusha madai ya Kambona kuwa anamiliki mali kibao na ameweka fedha nyingi ktk benki ya Uswissi yeye na Amir Jamal na Kawawa! madai haya ya Kambona alitoa wakati akihutubia mkutano wa hadhara uwanja wa Jangwani!
Kuna vitu vingi sana ambavyo Nyerere hakukanusha. Yaani mlitaka wakati wote kunapotokea kitabu Nyerere akanushe hadharani? Angefanya kazi yake saa ngapi? Unakumbuka alivyowajibu waandishi habari wa Kenya wakati mmoja kuhusu kuzaa na mama zao? Alitaka watumie akili zao. Nyerere hakujibu madai ya Kambona kuhusu kuwa na fedha katika benki ya Uswiss. Aliyejibu ni Amir Jamal katika interview niliyofanya naye wakati huo natumikia shirika moja la redio ya kimataifa.
 
Kwa kuwa yeye mwenyewe hakukanusha kilichoandikwa dhidi yake! wakati akiwa hai kitabu kinasomwa inakuwaje wewe unakanusha baada ya mhusika kufa? Nyerere akisingiziwa mara moja hukanusha ndio maana mwaka 1992 alikanusha madai ya Kambona kuwa anamiliki mali kibao na ameweka fedha nyingi ktk benki ya Uswissi yeye na Amir Jamal na Kawawa! madai haya ya Kambona alitoa wakati akihutubia mkutano wa hadhara uwanja wa Jangwani!

Una uhakika alikanusha au unafikiria alikanusha; mtawapata hawa wadogo na watoto zetu na hii historia mpya.
 
Back
Top Bottom