Inawezekana kitabu changu umekisoma zamani.
Kipitie tena uangalie nilivyoieleza AMNUT.
Nimesema Waislam waliikataa.
Kuhusu Mwinyi hujui.
Niliwasilisha mada Kenyatta University mwaka 2006 "Al Marhum Sheikh Kassim Juma and the Pork Riots of 1993""
Wanaukumbi wakipenda nitaiweka humu wasome wenyewe washuhudie fikra zangu kuhusu Mwinyi.
Ama hayo mengine uliyosema ni mengi siwezi kujibu yote.
Sawa lakini hujawahi kumhoji; na leo mzee bado yupo hujawahi kujaribu kutafuta mawazo yake juu ya Nyerere na udini. Ila akija kututangulia sitoshangaa utaanza kutumia maneno mbalimbali kuelezea msimamo wake.
Mimi nimeingia humu kuja kueleza historia ya kweli ya uhuru wa Tanganyika.
Nimeingia humu kurejesha hadhi na heshima ya wazee wangu.
Lakini hili hujajaribu kulifanya na kama umejaribu basi ndugu yangu umeshindwa kwa kiasi kikubwa. Hujathubutu kuelezea historia ya 'kweli ya uhuru wa Tanganyika'. Utafanya hivyo vipi wakati unafanya kile kile unachowatuhumu kuwa Nyerere alikifanya? Unaweza kudai kuwa umejaribu kuelezea 'sehemu' ya historia ya kupigania uhuru na hapo utakuwa umekaribia kwa usahihi sana kuelezea kile unachokifanya lakini kudai umeelezea historia ya 'kweli' la hasha mkuu wangu.
Waulize Waislam.
Tunajua nini maana ya kudhulumiwa.
Tatizo ni kuwa unataka watu waamini kuwa Wakristu wa Tanzania hawajui dhulma vile vile. Unataka watu waamini kuwa Wakristu wa Tanzania wanafurahia maisha ya raha tofauti na Waislamu. Huwezi kuamini kuwa wapo Wakristu ambao hawajapata elimu, wamenyang'anywa ardhi, wamehamishwa kwa nguvu n.k chini ya utawala huu huu ambao nyie mnaulalamikia. Wakristu hawa hata hivyo yawezekana hawaoni kuwa ni ktokana na mfumo Kristu bali wanaona ni matokeo ya mfumo mbovu wa kisiasa uliojengwa kutokana na kutamalaki kwa ufisadi.
Mgogoro wa Ardhi Meru, Mgogoro wa Ardhi Usukumani, au suala la Kodi kule Upareni wakati wa Uhuru liligusa watu ambao miongoni mwao walikuwa ni Wakristu wengi tu. Na hata leo tumeshuhudia maeneo yenye Wakristu wengi - Kyela kwa mfano watu wakijiona wanadhulumiwa. Tumeshuhudia wananchi wa Rukwa huko wakilalamikia ardhi yao kuuzwa kwa wageni, tumeshuhudia Kilombero huko na sehemu nyingine nyingi tu ambapo wananchi - wakiwemo Wakristu wengi tu - wamejikuta wakihisi dhulma chini ya serikali yao lakini hawaioni hiyo kama wamelengwa wao kwa sababu ya Ukristu wao.
Utaona hata kwenye matokeo ya mitihani watoto wa Kikristu wanaofeli katika shule za Kikristu (au zenye majina ya Kikristu) hawaangalii au kudhania kuwa wamefelishwa kwa sababu ni Wakristu. Kuna vituo vya mitihani kama Dar-es-Salaam Christian Seminary ambayo mwaka 2011 ilikuwa na watoto 66 waliofeli na 24 wakiwa na Div 4, mmoja Div 2 na 3 Div 3; lakini huwezi kuwaambia watoto hawa ambao labda ni Wakristu kuwa mfumo wa elimu haujawadhulmu na kuwa wazazi wao hawajui madhara ya mfumo wa ufisadi!
Unavyozungumzia dhulma kwa Waislamu ni kana kwamba Waislamu wanaishi kwenye jamii nje ya jamii ya Watanzania. Kwamba ipo miji au mitaa ya Waislamu ambapo WAkristu hawaishi na hivyo madhara ya utawala yanawalenga Waislamu kwenye miji na mitaa hiyo. Mtaa ambao hauna maji madhara yake ni sawa sawa kwa Wakristu na Waislam wanaoishi katika mtaa huo.
Hakuna lolote ambalo unaweza kudai Waislamu wamepata katika mfumo huu wa utawala wa kifisadi ambao WAkristu hawajapata madhara yake vile vile. Madhara ya mfumo huu yanaathiri Watanzania wote bila kujali dini, rangi, jamii, au mahali. Ndio maana wengine tumeamua kupambana na mfumo huu wa kifisadi badala ya kukumbatia adui hewa wa Mfumo Kristu.
Ndio maana leo Wananchi wa Mtwara ambao walikuwa ni wapenzi wakubwa wa CCM na wengi wao wakiwa ni Waislamu wamefunguka na wanatambua mara moja kuwa adui yao siyo kanisa au Ukristu bali mfumo wa utawala wa Chama ambacho kimekuwa kipenzi kikubwa cha WAislamu. Wameanza kufunguka.