MS anaamini kuwa Ditopile anaweza kuwa alitendewa vibaya na magazeti yanayosimamiwa na wakristo lakini yeye na kundi lake wana haki ya kuaminiwa kuwa hakuna upotoshaji hata pale ambapo imedhihirika kuwa kulikuwa na upotoshaji wa hali ya juu. 1. Kuhusu namba za mitihani, 2. Kuhusu kupigwa marufuku kitabu chake UDSM ''by Christian lecturers'' n.k. Anachotaka ni ku-provoke mtafaruku kama alivyowahi kuwataka maaskofu wajibu hoja za kitabu pengine kulenga kuamsha hisia na kuchochea vurugu kwa uwazi kwasababu Ponda si peke yake. Hapa anatupa ushahidi kuwa hana uthibitisho bali hisia zake zinamtuma kusema hivyo. Tena bila haya MS amekua akitumia neno ''huo ni ukweli'' sidhani kama kuna ukweli usiothibitika. Tunaposema historia asemayo imejengwa katika hisia, ushihidi ni kama huo.Hata kama maandishi yake yanaweza kuleta vurugu, MS yupo bize na toleo la tatu, take care of today, tommorrow will take care of itself.
Waliobadili majina ya mitaa ni madiwani wa Dar es salaam. Walioshindwa kuwaenzi wakazi na wanaharakati ni madiwani na wananchi wa Dar es salaam. Kuna nyakati Mwenyekiti wa CCM mkoa, Wilaya, Mkurugenzi, Meya na Madiwani wote walikuwa wazee wake. Anajua fika kuwa kosa si la Nyerere ni la wazee wake kama akina tambalizeni ambao badala ya kufikiria namna ya kuboresha maisha ya wakazi na wenyeji wamebaki kuandika ngonjera kama hizi tunazoziona.
MS hapaswi kutumia muda mwingi kumhukumu Nyerere kwa jina la mtaa mmoja ambao mtendaji wa kata angeweza kukaa na wananchi na madiwani wao wakafanya hivyo.
MS anapaswa aangalie picha kubwa zaidi. Je,kuna kitu gani cha kumbu kumbu ya Mzizima walikoishi wenyeji wetu?
Je, kiwanja cha Chang'ombe kiendelezwe vipi kwa faida ya wakazi wa jiji.
Je, kifanyike nini wakazi wa kariakoo-mzizima wanufaike na ardhi na rasilimali zilizopiganiwa na akina Abdul Sykes na Kiyate. Kwanini wahamishwe kwa kupewa milioni 15 kwa kitu chenye thamani ya milioni 400 n.k.
Kufikiria street moja tu ni tatizo kabla ya tatizo.
Walioifikisha Dar hapo ilipo ni wazee wako, Nyerere anafanywa Bangusilo tena kwasababu tu ya jina Julius.
Anahukumiwa kwa uzembe, ujinga na ututusa usiomhusu.
Nyerere hakuwa diwani Moshi, Mwanza au Mbeya! kimeshindikana nini Dar!
MS warithishe watoto werevu na kujitambua kwasababu dunia ya leo majungu haujawa mtaji wa maana the least to say
Sasa kama unajua hujui na huna majibu, kwanini ujihusishe na kuwa msemaji wa waislam?
Ukweli ni kuwa unaogopa kusema Mwinyi, Mkapa au Kikwete kwasababu kufanya hivyo utagusa wazee wako.
Tunarudi nyuma kuwa tuhuma dhidi ya Nyerere ni za kupikwa kwasababu historia inamsuta MS.
Huwezi ukawa na tukio moja katika historia ukachagua namna ya kulijadili au kuliandika kwa nyakati tofauti.
Chuki dhidi ya Nyerere ni kwasababu tu ya kumhusisha na dini yake.
MS unapaswa kwenda kujadiliana na Kikwete kwanza, kwasababu Nyerere ni marehemu. Kuendelea kumsukumia lawama hakumdhuru bali kunaidhuru jamii yako. Kumzushia yaliyomshinda Mwinyi na Kikwete ni ubaguzi wa ajabu sana.
Ubaguzi ni dhambi mbaya sana na humdhalilisha awayeNyerere aliwahi kulieleza na maandishi yapo. Mkapa kalizungumzia hotuba ipo.
Kikwete hajawahi kulizungumzia. Tatizo lipo lakini si kwa namna unayoielewa wewe na kundi lenu.
Kwanza hamtafuti suluhu mnachotaka ni kuvuruga nchi. Mtu mwenye suluhu hawezi kuwa anapiga mdomo na ikifika mahali anaulizwa tufanye nini anajibu haya
MS anachotaka ni kuita majina na kuwapa watu madaraka. Kuita majina na kuwapa watu kazi za taaluma.
Kwamba kwake Daktari anaweza patikana kwa uwiano au kupiga kura!!!
Kibaya zaidi MS anaamini kuwa mtu anayeitwa Abdallah Husein Bin Suein au John William Walace basi huyo ni muumini wa dini. Tatizo la watu kama akina MS ni kutochukua kioo na kujiangalia!Ni kunajisiwa fikra zao na ukoloni wakidhsni kuwa dini ni jina hata kama awaye ni mzushi, jambazi, muongo.
Hivi unapata wapi mtaalam au kiongozi kutoka Kilwa kama shule zinafungwa kwa kukosa wanafunzi.
Shule ifungwe kwenda kusikiliza kesi ya Ponda!! Hayo si tatizo kwa MS,tatizo ni Nyerere!
MS waambie watu wako ukweli acha kuwadanganya ili uuze nakala za vitabu, unawapotezea muda wa kusonga mbele.
MS hana ushahidi wa maswali yote mawili, bado anasema alichoandika ndio ukweli. Huu ni ushahidi kuwa sehemu kubwa ya ngano hii imejengwa kwa fikra zake binafsi zikichagizwa na uzushi.
Mwanafunzi hawezi kuja kusema na mtafiti akakubali tu kwasababu ni mwanafunzi huyo ni Mwislam.
Hili kama si majungu ni nini. Uliposema ndani ya kitabu kuwa christian lecturers at UDSM... ulichotaka ni kujenga chuki tu.
Huko Ulaya wasikojua hali ya Tanzania hawawezi kukuuliza uwape ushahidi. Ndio maana tunasema MS ni mpotoshaji, mzushi na mjenzi wa historia kwa kutumia majina na matukio huku akichomeka mbegu yake ya chuki miongoni mwa jamii.
Kusema jambo usilo na uhakika nalo ni uzushi na ni uongo. Dini ya kiislam haitaki hivyo na imekataza.
Unapaswa umuogope mwenyezi mungu kwanza kabla ya mauzo ya kitabu.
Muogope mola wako kabla hujazua balaa maana hilo limekatazwa.
Sasa tuna mambo mengi sana ambayo Mohamed ameyaandikia kurasa na kurasa na ameshindwa kuyatetea kwa mantiki,
hoja na hekima. MS nani asiyejua kwanini unakimbia hoja na maswali na umebaki kukata vipande vya kitabu.
Ninafikiria hivi kama kuna mwanafunzi anaandika thesis na amefanyia reference kitabu hiki, atawezaje kuitetea thesis yake kama mwandishi hawezi kutetea maandiko yake. Sad!