Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar


Nguruvi3 ni kichwa ana uwezo mkubwa wa kujenga hoja sana, ukimsoma unavutiwa na hoja zake

lakini pia masimulizi ya Mohamed Said yanavutia sana kuna baadhi ya vitu nilikuwa sifahamu lakini kupitia masimulizi yake nimepata vitu

lakini hawa kina Boko haram naona mipasho ndio imejaa Ritz naona sikuhizi amestaarabika sana

mnakasha naona ni mzuri sana maana tunapata vitu vingi sana nilikuwa sivifahamu pamoja na stori za kuvutia

yaani huwezi kuchoka kusoma...
 
Last edited by a moderator:

Bashadido nimekuelewa ngoja nukufundishe kitu kimoja ukituita wafia dini wala hujakosea kwasababu zifuatazo, kwanza kabisa uislamu huwezi kuutenganisha na siasa kwasababu uislamu ni mfumo uliokamilika katika kila kitu. Uislamu unafundisha jinsi ya kuishi na wasio waislamu na haki zao kwetu,hukumu za mirathi,wakfu yani kwenye mambo ya biology huko ndio kwenyewe uislamu umefundisha mwanamke amnyonyeshe mtoto miaka miwili vile vile mimi nakumbuka shuleni tuliambia jua limetulia kwenye mhimili wake yaani jua liko (stationary) sasa tukirudi kwenye QURAN tunaambiwa jua nalo linazunguka kwenye mhimili wake sasa muumba na viumbe walio umbwa nana wa kumfuata baada ya muda hao hao wanasayansi na wao wakasema wamegundua kuwa jua nalo linazunguka kwenye mhimili wake sasa KWANINI NISIWE MFIA DINI KAMA KITABU CHANGU KIMESEMA MAMBO YOTE HAYO NA HAYO MAMBO YAMEANDIKWA MIAKA 1434H ILIYO PITA KWAHIYO IKIMUONA MZEE MS ANAINGIZA MAMBO YA KIIMANI USIMSHANGAE NDIO DINI YAKE ILIVYO IMEKAMILIKA KATIKA KILA KITU MKUU.
 

Mkuu wa Chuo,
Ahsante.

Lakini iko siku na wewe usomeshe humu usichukue jina kubwa bure.
Ahsante sana mkuu.
 

Umesahau na ktk historia ati binaadamu kiasili ni Manyani?
 
Kadogoo,

Nilikuwa naangalia mashindano ya magari Formula 1 Malaysian Grand Prix huku nakunywa gahawa na kashata za Jidah nimesoma post yako nimecheka sana.

RITZ,
hembu nikumbushe ni ipi hiyo?
 

Joka Kuu,
Mbabe wa zamani, Ndava.

Ninajaribu sana kila ninapokwenda kuwahimiza vijana waandike historia za hawa mashujaa.
Mie kuandika kwa sasa nakuachieni vijana.
 
Kwahiyo kauli yake inayochochea mauaji ni kauli mbiu aliyopewa na waislam?

Nguruvi,

Hili nilijibu.

Nikasema kauli ya kisasi kama alivyozungumza Sheikh Ilunga
ni suala la maulamaa watoe fatwa mimi sina ujuzi huo.
 
Kweli ujinga ni mzigo mzito na wahatari sana! nakushauri jaribu kujisomea ili upate maarifa zaidi bwana mdogo.
 
Mohamed Said,

Jana nimeuliza humu kwa yeyote anayefahamu habari za hiki chama United Tanganyika Party (UTP) bahati mbaya hakuna aliyenijibu kama unafahamu chochote basi tupe darsa.
 
Nilikua nimeondoka kama wiki nzima hivi.
Nimeshindwa kupitia post zote.

Swali langu je ile audio imeshawekwa?
 
Mdondoaji
Sina ujuzi wa mengi uliyouliza. Na kwa hiyo siwezi kuyajibu. Ninachojua mimi ni kuwa Vatican ni nchi, solomon Islands, ni nchi, Vanuatu, ni nchi, Guam ni nchi, Western Samoa ni nchi. Nchi zote hizo ukiniambia nitaje majina ya wazawa na wageni wao, kwakweli sijui na siwezi. Ila haibadilishi ukweli kuwa hizo ni nchi.

Si lazima tukubaliane sote katika kila jambo. Hata ujio wa Xi Jinping, Rais wa China, sio wote wameuona ni wa manufaa. Lakini bado, serikali na wananchi wengine wameona ni wa manufaa. Kumbuka Tanzania tunasema Sahara Magharibi ni nchi, lakini Morocco wanasema ni sehemu ya nchi yao. Tofauti zitaendelea kuwepo tu. Kwa hiyo, wewe unaweza ukaendelea tu kuumia kwa mawazo kuwa Vatican sio nchi- utaumia kwa vile ulitaka ndio ujengee hoja ya OIC. Sisi wengine tunasema ni nchi. And life goes on....Tunakubaliana kutokukubaliana. By the way, usije ukafikiri mimi ni mkatoliki, sio. Lakini najitahidi tu kuwa objective.
 
Last edited by a moderator:
Nilikua nimeondoka kama wiki nzima hivi.
Nimeshindwa kupitia post zote.

Swali langu je ile audio imeshawekwa?
Audio haijawekwa. Nimejitolea mimi kuitafuta nitakapokuja Bongo. Maybe April, maybe May. Vuta subira.
 
Mohamed Said,

Jana nimeuliza humu kwa yeyote anayefahamu habari za hiki chama United Tanganyika Party (UTP) bahati mbaya hakuna aliyenijibu kama unafahamu chochote basi tupe darsa.

Ritz,
UTP kilikuwa chama cha Wazungu kiliundwa mwaka 1955 na rais wake alikuwa Ivor Bayldon na makamu wake alikuwa Sheikh Hussein Juma, a prominent Manyema in Dar es Salaam.

Chama hiki kiliundwa na wakoloni makhsusi kuipinga TANU.

Huya Bayldon mwaka 1953 aliwapelekea barua baadhi ya wanasiasa mashuhuri katika TAA akiwaomba waunde chama cha siasa ambacho kitawaunganisha Watanganyika wote - Waafrika, Wazungu na Waasia.

Bayldon alimwandikia Abdu na Ally Sykes, Hamza Mwapachu, Steven Mhando orodha ni ndefu...
Nyerere hakuwamo katika orodha ile.


Nitakuwekea hapa mambo ya Bayldon na UTP Insha Allah.
 
Huyu Nguruvi wenu ni yupi ambaye baada ya kuishiwa hoja nyote mmejenga matumaini naye?.Hata Invisible nae pia.Inaonekana mmeshika kamba mbovu na mkumbuke wako wengi waliokimbia na wengine hupita kuchungulia tu.Jee Nguruvi huyu si ndiye ninayesubiri aje na jibu la kitu alichokiona ni kasoro kubwa katika kitabu cha Mohammed Said na mpaka sasa amebaki kimya.Ukiangalia hiyo post yangu ameweka saini yake kwamba ameiona hivyo kutokujibu ni dalili ya hofu aliyonayo moyoni.Muda mwingi nimebaki kimya nikisubiri jibu lake na nilidhani amejichimbia kutengeneza jawabu yake refu kumbe ni kupotea tu huku akiendelea kuja na maneno yenye lafdhi za kishairi.Ikiwa amekwamba mwengine amsaidie kujibu hilo swali lililomshinda ambalo ni la msingi kwenu kwani ni sehemu muhimu ya pingamizi yenu katika historia ya Mohammed.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…