Remote,
Mimi huwezi kunilinganisha na Sheikh Ilunga.
Ilunga ni alim.Mimi napiga goti nasomeshwa na Sheikh Ilunga.Mimi akiwapo siwezi hata kunyanyua sauti yangu
kunong'ona achilia mbali kusema.Heshima ya Sheikh Ilunga iko juu sana kwa Waislam.
Ndiyo maana umeona yeye ndiye aliyeaminiwa kutembea
nchi nzima kuwazindua Waislam kuhusu mfumokristo.
Mimi siwezi hata kumbebea viatu vyake.
Kwahiyo kauli yake inayochochea mauaji ni kauli mbiu aliyopewa na waislam?
Nina uhakika Mohamed hutajibu swali hilo hapo juu. Utasubiri baada ya post kadha unirushie kombora la matusi.
Kwanza nikuulize, unaposema ameaniwa na waislam ni waislam wapi hao kwa kuzingatia kuwa wapo BAKWATA na makundi mengine kila moja likiwa na agenda yake?
Mohamed Ilm si vitabu, paper au machapisho tu. Ilm ni maarifa aliyo nayo mtu katika kukabiliana na mazingira yake kwa ujumla.
Kitu muhimu sana kwa mwenye Ilm ni mawasiliano.Endapo mtu hana mawasiliano basi hapo Ilm inakosa maana yake halisi.
Sijui Sheikh Ilunga ana Ilm ya kiwango gani katika hii iitwayo elimu dunia hadi kufikia mahali pa kupewa jukumu la kuueleza mfumo nchi nzima.Sijui kama anachokiongea anafahamu madhara na athari zake.
Nisichokubaliana nawe ni hoja ya kumpa wadhifa wa kuongea kwa niaba ya waislam.
Nina uhakika katika waislam wanaomsikiliza na kumfuatilia wapo mamilioni wasiokubaliana na hoja zake.
Hao nao umeamua kuwachanganya na wale wanaokubaliana naye katika chungu kimoja cha waislam ''wamemtuma''
Ukiangalia ile video ni ngumu sana kuamini kuwa bado unaweza kusimama na kusema ametumwa na waislam.
Hata wewe tumekuuliza unakubaliana na video ile? hakika hukujibu kwasababu unafahamu wazi kuwa kile si kitu sahihi kidini, kidunia na kijamii.
Wapo waislam si kuwa wameudhika bali kukirihika sana na maneno ya mentor wako.
Labda utupe Ilm sisi wengine kuhusu Uislam ya kuwa wapi imeelezwa kuwa dini ya uislam itaenezwa kwa chuki na farki?
Je, yale maneno (niwieni radhi kama nitakosea) yanayosema '' walinganieni wasio waislam kuingia katika dini kwa hoja'' yalilenga nini na kwa nani? Na je, ndio hoja za Ilunga azisemazo
Njaribu kufikiri hivi kama yupo aliyetamani kuwa mwislam halafu akaiona ile video, je huyo mtu atakuwa amelinganiwa kuingia katika dini kwa maneno yale? Je, pale kuna ilm ya aina yoyote kweli na kwa msingi huo ilim ya kueleza mfumokristo ipo kwa hoja mantiki na busara!
Mohamed, ifike mahali kila mtu atambue kuwa imani ni suala la mtu binafsi na si chama cha ushirika au cha kisiasa.
Ni makosa kuchukua maneno ya mtu mmoja na kuyafanya ya waislam mamilioni wa Tanzania.
Ningeshauri siku nyingine useme ''ndiyo maana Ilunga ameaminiwa na kundi lenu kueleza mfumokristo'' na wala si waislam.
Unless uniambie anaongea kwa niaba ya waislam gani kauli yangu inabaki kama ilivyo.