Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

sweke.
Kwanini tubishane?

Ikiwa wewe unaona hakuna dhulma na wengine ipo
kuna haja gani tuzunguke katika hilo?

Kila mtu abaki na msimamo wake.
Tuiachie historia pindi mwaka itatuamua.


tupo pamoja ndugu,
tunashukuru kwa darsa hili.
 
Wild Card,

Nina hakika unaazungumzia jambo ambalo wewe huna ujuzi nalo.
Kitabu cha Rushdie ni matusi makubwa sana kwa Mtume Muhammad SAW.

Nakusihi usiguse huko.

Yale aliyoandika mle laiti angelimuhusishanayo Yesu....
Balaa lake lingekuwa kubwa.

Naogopa kutukana lakini ametoa matusi ambayo siwezi kuyaandika hapa.
Ndiyo maana tuliamua auliwe ili jambo lile lisirejewe na yeyote hadi kiama.
 
Huu ndio uthibitisho wa kazi thabiti ya hayati Mwalimu Julius Nyerere aliyoifanya baada tu yakupata uhuru!
usiwe mchache wa fadhwila kuwa mkweli. Hayo ndio mafunzo ambayo Nyerere aliyakuta alipokuja Dar. Watu waungwana na wanapendana kwa dhati swifa kubwa ikiwa ni kuhishimiana na kujaliana. Alikotoka Nyerere nafikiri mpake leo unajua nini kinaendelea kugecha tu na mauaji na kupigana kila wakti. sasa ustaharabu wa Pwani ukisema umeletwa na Nyerere nafikiri utakuwa umekosea. Kwanini usianzie Mara ambako watu wanapigana visu na kuuwana kila siku aje auanzishe Dar?.
 
NAKUSHUKURU SWEKE KWA HOJA ZAKO ZENYE TIJA.
LAKINI NINA UHAKIKA TUPO WOTE KWENYE MWANZO WA MJADALA HADI SASA,MAJIBU YA HOJA ZAKO YAPO HUKO NYUMA,TENA YAMEFAFANULIWA VEMA TUH,JARIBU KUPERUZI NA KUONA UNDANI WA SUALA HILO.,KWANI SISI TUNA SHIDA NA NYERERE?HAPA TUPO KATIKA KUZUNGUMZA YALE YALIYOFANYWA KWA MAKUSUDI NA KUPOTOSHWA,NA SIO KWAMBA TUNA CHUKI BINAFSI NA NYERERE LA HASHA,
HOJA ZETU ZISIHUZUNISHWE NA CHUKI BINAFSI.
Maneno yako hapo kwenye blue yanakinzana na ya Mohamed Said. Mzee wetu tumetoka naye mbali sana tangu zile nyuzi za makala zake za miaka 50 ya uhuru lakini hatupati ufafanuzi na uthibitisho kwenye mambo mengi anayomtuhumu Nyerere badala yake anatupa mabandiko ya vitabu na papers zake.
Mimi kwenye suala la elimu kwa kweli ningependa kupata ufafanuzi zaidi maana mtu akikunyima elimu kwa makusudi ni kwamba amekufanyia dhulma kubwa sana.
Mohamed Said ameendika tangia nchi hii inapata uhuru mpaka pale Kighoma Malima aliteuliwa kuwa waziri wa elimu, wizara hiyo ilikuwa inaongozwa na wakristu tu. Anasema ilifikia mpaka wakati padre/mchunguji aliongoza wizara hiyo. Teuzi hizo za wakristu zilikuwa na lengo la kuwakandamiza waislam kielimu na kuwapendelea wakristu na ndiyo maana (kwa mtazamo wa MS) Kighoma Malima alipoingia wizarani akakutana na madudu mengi.
Kuna siku nimemuuliza hivi hawa mawaziri wote waislam(Juma Kapuya,Maghembe, Shukuru Kawambwa) waliotumikia hiyo wizara ya elimu baada ya Malima hawayaoni hayo madudu tena wakati huu vitu vipo wazi zaidi? Hakunipa jibu la maana. Yeye Mohamedi said anajua dhulma hiyo kushinda waziri muislam anayetumikia wizara hiyo.

Ni huyuhuyu Shukuru Kawambwa aliyeacha kazi zake na kwenda kupokea maandamano yenu(wanafunzi waislam) Kidongo chekundu kuhusiana na ile issue ya wanafunzi wa ndanda. Na aliwaahidi atalishughulikia lile tatizo. Lakini nadhani ni naibu waziri wa elimu wakati huo Kassim Majaliwa(Muislam) ndiye aliyeivalia njuga issue ile na mwisho wake wote tunajua kilichokuja julikana.
Ni huyuhuyu Shukuru Kawambwa aliyetoa ufafanuzi mzuri tu kwenye vyombo vya habari kuhusu majibu ya Islamic Knowledge yaliyokosewa.
Sasa inashindikana vipi kwa huyu muislam kuona dhulma wanayofanyiwa waislam kwenye wizara yake? Anatumikia Kanisa?
Si mnaswali naye misikitini huyu?
Jamani tuwe wakweli. Leo hii ukifeliswa ni rahisi sana kujua umeonewa au la kwa sababu mitihani huwa inabaki pale wizarani kwa muda kuruhusu watu ku appeal na hivyo mitihani yao kuangaliwa upya. Mkuu muulize mohamed said anajua nini kuhusu jinsi mtihani invyosahihiswa mpaka kufikia kutolewa matokeo.

Binafsi kama angeniletea cases za wanafunzi kadhaa za waislam walioonewa na baada ya kuappeal wakapata matokeo mazuri zaidi, ningemuelewa. Au aniletee cases kadhaa za wanafunzi wa kiislam waliofaulu lakini hawakuchaguliwa kuendelea na masomo nitamuelewa.
Lakini asituambie tuamini tu.


quote_icon.png
By Mohamed Said


Sweke.
Kwanini tubishane?

Ikiwa wewe unaona hakuna dhulma na wengine ipo
kuna haja gani tuzunguke katika hilo?

Kila mtu abaki na msimamo wake.
Tuiachie historia pindi mwaka itatuamua.
 
Yericko,

Hakuna anaepinga uwezo wa Nyerere. Nyerere ni kiongozi wa pekee.

Itachuka miaka mingi aje mtu kama yeye. Kaacha nyuma yake mengi ya kuhadithiwa.

Ila hakuasisi harakati za uhuru. Kubwa na hii ndilo doa aloacha nyuma.

Alishirikiana na Kanisa Katoliki kuwakandamiza Waislam.

Hili si kama linakushtueni nyinyi peke yenu.

Nilifanya mhadhara Zentrum Moderner Orient (ZMO) Berlin mwaka 2011.
Niliwasilisha paper ''Christian Hegemony and the Rise of Muslim Militancy in Tanzania.''

Wasikizaji wangu Wajerumani walipata ubaridi nilipokuwa natoa hoja na ushahidi, hoja
na ushahidi, hoja na ushahidi.

Waliloa.

Picha waliyokuwanayo ya Nyerere si ile iliyokuwa inaelezwa pale.

Magazeti yanakusanywa kwa kuwa tu katajwa Abdu Sykes kama muasisi wa TANU na Waislam
wameadhimishwa kwa mchango wao.

Nikawa nawauliza wasikilizaji wangu ni nani alikuwa anatoa maelekezo na amri zile?

Katika wasikilizaji wangu baadae niliarifiwa walikuwa maofisa wa ubalozi na niliarifiwa wataandika
taarifa.

ZMO waliniahidi kuwa watatuma mtu kuja kufanya utafiti zaidi kuhusu Uislam na Siasa Tanzania.

Hakupita hata mwezi nimepokea msichana wa Kijerumani kaja kufanya utafiti ule.

Katembea nchi nzima anafanya utafiti.

Insha Allah tusubiri matokeo.
 
Hilo usemalo ni kweli. Nyerere hapendezi tena kwa Waislam.

Dhulma imetamalaki sana katika nchi yetu. Hii imezaa chuki na uadui.

Prof. Haroub aliliona hili na alimtahadharisha Nyerere kuwa heshima yake
siku za usoni itaingia dosari.

Waislam wana ghadhabu kwa kubaguliwa katika elimu nafasi za kazi nk.

Lakini bado nafasi tunayo ya kukabiliana na hili tatizo.
Wahusika wameshafahamika.

Kilichobaki ni kwa serikali ichukue hatua. Ikubali kuwa lipo tatizo katika nchi.
Mwalimu hapendezi kwa Waislam wepi hao, akina Salim, Jakaya, Bakari Mwapachu Mustafa Nyang'anyi, Ali Hassan Mwinyi, Mufti Simba au akina Ponda, Mohamed Said, Kundecha,...

Serikali kwa kweli ichukue hatua ya kukaa mbali na DINI zote. Ni hatari kwa umoja wa WATANZANIA. Biblia na Quran viondolewe pale IKULU yetu.
 
Yericko,

Hakuna anaepinga uwezo wa Nyerere. Nyerere ni kiongozi wa pekee.

Itachuka miaka mingi aje mtu kama yeye. Kaacha nyuma yake mengi ya kuhadithiwa.

Ila hakuasisi harakati za uhuru. Kubwa na hii ndilo doa aloacha nyuma.

Alishirikiana na Kanisa Katoliki kuwakandamiza Waislam.

Hili si kama linakushtueni nyinyi peke yenu.

Nilifanya mhadhara Zentrum Moderner Orient (ZMO) Berlin mwaka 2011.
Niliwasilisha paper ''Christian Hegemony and the Rise of Muslim Militancy in Tanzania.''

Wasikizaji wangu Wajerumani walipata ubaridi nilipokuwa natoa hoja na ushahidi, hoja
na ushahidi, hoja na ushahidi.

Waliloa.

Picha waliyokuwanayo ya Nyerere si ile iliyokuwa inaelezwa pale.

Magazeti yanakusanywa kwa kuwa tu katajwa Abdu Sykes kama muasisi wa TANU na Waislam
wameadhimishwa kwa mchango wao.

Nikawa nawauliza wasikilizaji wangu ni nani alikuwa anatoa maelekezo na amri zile?

Katika wasikilizaji wangu baadae niliarifiwa walikuwa maofisa wa ubalozi na niliarifiwa wataandika
taarifa.

ZMO waliniahidi kuwa watatuma mtu kuja kufanya utafiti zaidi kuhusu Uislam na Siasa Tanzania.

Hakupita hata mwezi nimepokea msichana wa Kijerumani kaja kufanya utafiti ule.

Katembea nchi nzima anafanya utafiti.

Insha Allah tusubiri matokeo.
Mwalimu asingeweza kuasisi harakati za uhuru wa Tanganyika. Kazaliwa kaikuta ipo nchi inaitwa Tanganyika. Hata hawa wazee wako hawakuasisi harakati hizi kwa kuwa wengi wao NCHI hii sio yao ya asili. Kilichofanya hata wewe ukawasikiliza na kuandika simulizi hizi ni kwa kuwa baba zao walibadili DINI wakawa Waislam. Wakaongea lugha moja na WAMANYEMA waliokuwa wamejikita Kariakoo.

Harakati zenyewe za kudai uhuru UN zilikuwa za kistaarabu sana. Hakuna aliyemwaga damu wala kutiwa misukosuko ya ajabu zaidi wale waliokuwa kwenye ajira zao. Hatukuhitaji bunduki wala mapanga. Hata bila TANU bado nchi hii ingerudishiwa uhuru wake kwani Tanganyika haikuwa koloni la yeyote.
 
usiwe mchache wa fadhwila kuwa mkweli. Hayo ndio mafunzo ambayo Nyerere aliyakuta alipokuja Dar. Watu waungwana na wanapendana kwa dhati swifa kubwa ikiwa ni kuhishimiana na kujaliana. Alikotoka Nyerere nafikiri mpake leo unajua nini kinaendelea kugecha tu na mauaji na kupigana kila wakti. sasa ustaharabu wa Pwani ukisema umeletwa na Nyerere nafikiri utakuwa umekosea. Kwanini usianzie Mara ambako watu wanapigana visu na kuuwana kila siku aje auanzishe Dar?.
Hivi kweli kati ya WAKURYA na WAARABU nani zaidi kwa kuuana? Tena WAARABU wanauana kwa kutumia jina la DINI na MUNGU wetu!
 
Sijui kama hili litakusaidia kujenga fikra zako kwa upana zaidi.

Hao waliotoka nje ya Tanganyika na kuaisisi harakati mathalan
za African Association walikuwa ni kizazi cha kwanza.

Waliokuwa wametoka nje ya Tanganyika walikuwa ni baba zao.

Hawa kama Kleist na babu yangu walikuwa wote wamezaliwa
Tanganyika.

Kleist kazaliwa Pangani babu yangu Salum Abdallah kazaliwa Shirati
na bibi yangu mkuu alikuwa katoka kisiwa cha Ukerewe.

Hilo la ugeni halikuwapo wakati wa kupigania uhuru.

Katika TAA hadi TANU kulikuwa na Dome Okochi Budohi, Patrick Aoko
(Kenya), Denis Phombeah (Nyasaland) na walikuwa viongozi.

Mimi ni kizazi cha tatu cha Kimanyema kuzaliwa Tanganyika.

Nimeona nikuwekee haya huenda ikakuongezea fikra ukaona haya mambo
kwa mtazamo mwingine.

Hayo mengine wala sina haja ya kuyagusa mtu ana haki ya kuamini kama fikra
zake zinavyomwelekeza.
 
Kwa kuondolewa dini tushachelewa.
Mfumokristo unatawala.
Unawatukana ambao wamekuwa maRAIS na VIONGOZI wa nchi hii ambao ni WAISLAM kama wewe. Walikubali vipi kuutumikia mfumo huu? Njaa zao? Au Uislam wao una walakin!
 
Mohamed Said, hivi ni nani aliyesema Kanisa limepewa 91 Billion mwaka 2011? Ni Kikwete au waziri wa fedha?
In 2011 the government provided 91 billion shillings to the Church for its development activities.
 
Yericko Nyerere,

Tunasubiri majibu yako utuambie wale waliosamehewa na Mwalimu Nyerere baada baada ya kushindwa jaribio la mapinduzi mwaka 1982 na wengine kupewa ubalozi kama ulivyotuambia.
 
Last edited by a moderator:
Situkani.

Unastaajabu vipi marais Waislam lakini watumikie mfumo wa dhulma.
Hapa ni padogo mno kuweza kueleza jinsi mfumokristo unavyofanyakazi.

Lakini serikali imeshaelezwa na Waislam wameelezwa.

Mwaka juzi mzima Sheikh Ilunga alipita nchi nzima akifanya mikutano ya
hadhara akieleza vipi mfumokristo unavyokandamiza Waislam na Uislam.

Waislam wanasubiri jibu la serikali.

Lakini katika kitabu changu sehemu ya tatu nimeandika sura mbili nikieleza
tatizo hilo halikadhalika katika paper yangu ''Çhristian Hegemony...''

Serikali inajua kila kitu na tunaamini Kanisa nalo linajua pia.
 
Wild Card,

Nina hakika unaazungumzia jambo ambalo wewe huna ujuzi nalo.
Kitabu cha Rushdie ni matusi makubwa sana kwa Mtume Muhammad SAW.

Nakusihi usiguse huko.

Yale aliyoandika mle laiti angelimuhusishanayo Yesu....
Balaa lake lingekuwa kubwa.

Naogopa kutukana lakini ametoa matusi ambayo siwezi kuyaandika hapa.
Ndiyo maana tuliamua auliwe ili jambo lile lisirejewe na yeyote hadi kiama.
DINI yenu inavumilia kwa taabu sana maoni huru. Salman aliandika "fiction" tu ambayo haina tofauti sana na yule mtoto wa Mbagala aliyekojolea Quran. Adhabu yake afe! DINI yenu hamtaki Mtume Mohamad( S.A.W) aguswe au kama kuna makosa alifanya yasemwe!

Simlinganishi Mwalimu na Mtume wenu, lakini haya uliomsingizia ya kukandamiza Uislam huku misikiti ikiongezeka na Waislam wanaongezeka, tuyaiteje haya.

Yesu katukanwa sana tena sio kwa maandishi tu bali hata filamu kabisa. Tembea hata leo hii mitaa yote ya hapa Dar ukimtukana Yesu, hakuna atakayejali. Jaribu hivo kwa upande mwingine uone. Hautavuka hata nyumba ya tatu!
 
Ni muhimu hapa tulipofika serikali ikachukua hatua.
Na hatua yenyewe ni serikali kutokuwa karibu na DINI kwa lolote labda katika shughuli za kijamii kama kuzikana, ndoa(?). Irudishe kila ilichochukua kwenye makanisa na misikiti. Biblia na Quran viondolewe mara moja pale Ikulu yetu. Watu waape kwa kushika KATIBA yetu.
Serikali iwe makini na sheria kali kabisa dhidi ya watakaoingiza DINI kwenye SIASA na utendaji wake.

Nikuulize swali moja Mzee Mohamed; angalia St Joseph ilivyojengwa tangu miaka hiyo halafu ulinganishe na msikiti wowote uliojengwa enzi hizo au hata baada ya hapo. Unapata picha gani kuhusu elimu?
 
Back
Top Bottom