Hivi kujua wanaokula vizuri keki ya taifa ni Wakirsto ni hisia tu kweli damu nzito...
Angalia "Ratio" ya Waislam na Wakirsto katika idara za serikali zote wizara mashirika ya umma toka kwa mkoloni mpaka leo wamejaa Wakirsto wengi Waislam wachache waliopo huko wanaonekana kama wanafanyiwa hisani tu.
Wewe fikra zako siku zote dhidi Waislam na mtazamo wako ni kuwa hakuna jambo baya lolote ambalo wameishafanyiwa Waislam na serikali dhulma kwako huwa wanafanyiwa Chadema tu pamoja na Maaskofu, mpaka ukafikia wakati ukatoa ushauri kwa Pengo atoe tamko dhidi ya serikali.
Nakuombea dua sana Allah hakupe umri mrefu na muda uandike kitabu cha kumpinga Mohamed Said kama ulivyosema kuwa ni kazi rahisi kuandika kitabu cha kupinga tatizo muda hauna.
Ritz, hayo unayoyasema ni makosa na hakika hakutakuwa na suluhu ya kudumu kwa matatizo hayo kama mtazamo utabaki kama huo.
Huwezi kuniambia kuwa maofisi kuna wakristo wengi ukasahau kuwa vijijini kuna wananchi wengi wanamenyeka sawia.
Sijui kule kijijini Kibuyi karibu na Kinesi ukivuka kutoka Musoma wananchi wana afadhali gani.
Nilifika kule na sidhani kama kulikuwa na waislam zaidi ya kaya 10 katika kaya 300 siku hizo.
Ukiangalia hali za maisha ya watu ni mbaya sana pengine afadhali na kwingine.
Pili, unapoangalia maofisini unaangalia kundi dogo sana. Kwanini udhani kuwa keki ya taifa ipo katika wizara au mashirika 50 usifikirie maeneo mengine? Nimewahi kukuliza vipi mbona hatusikii idadi ya walimu na mabwana shamba, je hao hawafaidi keki ya taifa.
Ni kwa mtazamo kama huo usitegemee kuona watu wakiliangalia tatizo kutoka Magoroto, Kilwa, Mpanda au kule kwa Wamang'ati kwasababu wanadhani kuwa wakurugenzi 20 ni bora sana kuliko jamii ya watu 6,000,000 au zaidi inayomenyeka.
Ningeelewa kama mngeongelea kuwa kwanini kuna idadi kubwa ya mabwana shamba au walimu au madaktari kama siyo wauguzi n.k. Jicho lenu lipo katika ukurugenzi ambao sidhani kama una nafasi zaidi ya 100 nchini.
Kwa maana hiyo mnadhani matatizo ya waislam yataisha automatic kwa kuwa na wakurugenzi na si kuangalia tatizo na kiini chake.
Huko nyuma nimewahi kukuambia kuwa kuna shirika linatafuta Zoologist mtanzania.
Kama yupo naomba tuwasiliane naye haraka hasa akiwa mwislam ili kuhakikisha keki ya taifa inagawana vema.
Hadi leo hakuna aliyejitokeza.Nadhani ujiulize kwanza kwanini hakuna zoologist halafu ndipo ufikirie wakurugenzi.
Nimewahi kumwambia Mohamed alete majina ya Lawyers, Engineers, Doktors, Prodessor n.k.ambao wamefanyiwa hila tu.
Hakuna aliyeleta, lakini bado watu wapo pale pale kwa wakurugenzi.
Tatizo si wakurugenzi, tatizo ni namna gani wanapatikana.
Huwezi kupata wakurugenzi kutoka Kilwa ambako shule imefungwa na huko kuna asilimia 99 ya waislam.
Nadhani kuna umuhimu wa kutafuta taa ya fanusi na kuiwasha mchana ili isiaidane na jua kuangazia watu!!!
Lakini pia lazima watu waangalie mambo kwa upana wake. Hivi Wamang'ati na Wairaq pamoja na wamasai nao watasemeaje kuhusu keki ya taifa?
Tukiendelea na utaratibu huu basi ipo siku wasukuma na wanyamwezi nao watahoji keki ya taifa vipi? Maana wenyewe tu kwa idadi wanahaki ya kudai wakurugenzi na hata mawaziri. Si ndio uwezo wetu wa kufikiri ulipo!
Kitu wanachosahau watu ni kuwa wafanyabiashara wengi waliofanikiwa kwahakika ni jamii ya waislam tangu enzi.
Sijui yule jamaa yangu wa Mtimbira au kule Nyangao naye asemeje kuhusu keki ya taifa.
Keki ya taifa ni Richmond, Radar, Meremeta na dola laki moja na nusu ikwa siku bila malipo za Dowans.
Keki ya taifa ipo Dodoma pale mtu anapolipwa kwa kukaa kwenye kiti achilia mbali mshahara.
Keki ya taifa ni pesa za halamshauri zinazojenga vyumba viwili vya madarasa kwa thamani ya shule kumi.
Labda sielewi maana ya keki ya taifa lakini kama unakula na kusaza, kama unafadhili timu ya mpira huku mwingine akitafuta aspirin ya kupunguza maumivu ya njaa hilo halihusiani na keki ya taifa.
Na je sasa ni wakati watu washikwe mashati ili wasifanye biashara zao kuleta usawa na kugawana keki ya taifa.
Watu wasitafute visingizio, watafute ukweli na wakabiliane nao.Ukweli usikwepwe ueleze na kama ikibidi msaada uombwe lakini ukweli ubaki kuwa ukweli. Tatizo si wakurugenzi, narudia tatizo ni namna gani unamtengeneza mkurugenzi.
Manchester United wana timu hadi za watoto wa miaka 6 hadi 7. Hawa ndio wanaandaa 'wakurugenzi''
Kama kuna mgao wa keki, vipi mgao wa keki ya nafasi za waislam kusoma kwa msaada mbona haufuati utaratibu wa kugawana keki katika jamii hiyo hiyo inayodai keki ya taifa haigawiwi sawa sawa?
Ritz si unafahamu Afircan Muslim Agency, Islamic bank n.k wanatoa nafasi, je hujui kuna ugomvi wa kugawana''keki''
Wale waliotumwa Turkey na kwingineko kutafuta keki wangapi wamerudi na vipande na kugawia wenzao. Please please!
Kuna mahali sielewi naomba msaada, keki ya taifa maana yake nini?